Agricultural Reseacher
Member
- Jun 7, 2022
- 14
- 21
1. Afya ya udongo ni nini?
Afya ya udongo ni uwezo wa udongo kukidhi mahitaji ya ukuaji na uzalishaji wa mimea kama vile: virutubisho, maji, hewa pamoja na uwezo wa udongo kushikilia mmea
2.0 Virutubisho 16 muhimu kwa ajili ya ukuaji wa mmea
A. Virutubisho vinavyohitajika na mmea kwa kiasi kikubwa
•C, H, O (carbon, hydrogen na oxygen)
•N, P, K (nitrogen, phosphorus, potassium)
B. Virutubisho vinavyohitajika na mmea kwa kiasi cha wastani
•Ca, Mg, S (calcium, magnesium na sulphur)
C. Virutubisho vinavyohitajika na mmea kwa kiasi kidogo
•B, Cl, Cu, Fe, Mn, Mo, Zn (boron, chlorine, copper, iron, manganese, molybdenum na zinc)
3. Utafahamuje afya ya udongo?
Viashiria katika mimea pia hukufahamisha afya ya udongo
Viashiria katika mkonge vinavyoonyesha upungufu wa Naitrojeni katika udongo
Upungufu wa Calcium Kwenye Mkonge
Ugonjwa wa upungufu wa kirutubisho cha Calcium.
Majani ya mkonge yanakuwa na rangi ya zambarau na majani ya mkonge yanajikunja kuanzia nchani.
Upungufu wa Potasiam (K) katika udongo
•Ni kirutubisho ambacho hutembea katika mmea
•kwa hiyo viashiria huanza kuonekana katika majani ya chini
•Jani huanza kukauka kuanzia kwenye ncha na kingo za jani.
4. Umuhimu wa kupima afya ya Udongo
-Ni muhimu sana kupima afya ya udongo ili kujua kama udongo katika shamba husika unafaa kwa zao husika.
-Kuweza kujua matatizo ya udongo wa shamba husika na kutoa tiba sahihi (mfano matatizo ya tindikali, chumvi, magadi, upungufu wa virutubisho.
-Kuweza kujua aina stahili ya mbolea inayofaa kwa kuzingatia zao na afya ya udongo.
-Kuweza kujua kiwango cha mbolea kinachohitajika kwa zao husika.
-Inaondoa uwezekano wa kuweka mbolea isiyohitajika shambani kwa zao husika.
- Kuweza kujua zana sahihi za kulimia kulingana na aina ya udongo wa shamba husika
5.0 Mbolea ni nini?
-Mbolea ni chakula cha mmea kilichobeba virutubisho ambavyo huhitajika katika ukuaji wa mmea
1. Aina za mbolea
2. Mbolea za viwandani
1. Mbolea za Kiwandani
•Zipo zenye virutubisho zaidi ya kimoja zinaonyeshwa kwa kiwango na aina ya virutubisho vilivyomo,
-17-17-17 ni 17% kwa kila kirutubisho: N, P2O5, na K2O
-Compound fertilizer, e.g. N-P-K-S
-N & P: Diammonium phosphate (DAP), 18-46-0
•Zipo mbolea zenye kirutubisho kimoja kama
-Nitrogen: Urea, 46-0-0
-Phosphorus: Triple Super Phosphate (TSP), 0-46-0
-Muriate of Potash (KCl), 0-0-62
•Aina hizi za mbolea zipo katika hali ya chembechembe, kimiminika/maji, na gesi
Mbolea za Kemikali na Matumizi Yake
-Weka kilo 100 za Diammonium phosphate (DAP) au kilo 121 za Triple Superphosphate (TSP) wakati wa kupanda mkonge shambani ikiwa udongo unaupungufu wa phosphorus (P).
-Madini (Kirutubisho) cha Calcium
Mkonge unahitaji kirutubisho cha calcium kwa wingi ili kuzifanya nyuzi za mkonge ziwe imara na zisikatike hovyo.
Kama shamba lina miamba ya chokaa (lime stone) ni vizuri kwani mkonge utakuwa vizuri na hakutakuwa na haja ya kuongeza kirutubisho cha calcium.
Calcium ni muhimu sana kwa kuwa inauwezo pia wa kupunguza kiwango cha tindikali kwenye udongo na kuufanya udongo uwe na rutuba ya kutosha
-Baada ya mwaka mmoja tangu miche kupandwa shambani
-Weka mbolea ya Calcium ammonium nitrate (CAN) au UREA lakini CAN ni bora zaidi kwa vile mbolea hiyo licha ya Nitrogen pia ina kirutubisho cha Calcium kinachohitajika kwa wingi ili kuboresha nyuzi (fibre) pamoja na kupunguza tindikali kwenye udongo.
-Weka kilo 100 – 150 (mifuko 2-3 ya mbolea) kwa hekta mwaka mmoja baada ya kupanda mkonge shambani
-Weka muriate of potash (MOP) kilo 100 kwa hekta mwaka mmoja baada ya miche ya mkonge kupandwa shambani.
-Kama mkonge umeonesha upungufu wa potassium (K) weka kilo 100 kwa hekta kila mwaka kwa muda wa miaka mitano au mpaka ugonjwa utakapotoweka.
2. Mbolea ya asili: Mabaki ya mimea, Samadi mboji n.k
Mimea ya mikundekunde (kunde, maharage mbaazi n.k inatengeneza N)
6.0 Uhusiano wa afya ya udongo na matumizi ya mbolea katika kilimo
•Udongo unapokuwa na afya nzuri mkulima hahitaji kutumia mbolea.
•Lakini udongo ukiwa na afya mbaya /virutubisho kidogo ni muhimu kutumia mbolea.
•TARI Mlingano kwa kushirikiana na Wadau hufanya tathimini na utafiti kujua aina na viwango sahihi vya mbolea.
•Kujua ni wakati na sehemu gani mbolea itawekwa kwenye udongo kulingana na aina ya zao.
7.0 Hitimisho na Mapendekezo
a)Ukifahamu afya ya udongo /rutuba katika shamba lako utapata ushauri sahihi wa kutumia mbolea.
b)Ukitumia mbolea, viwango sahihi na kuweka mbolea ilivyoshauriwa utazalisha mazao kwa tija na utakuwa na uzalishaji endelevu
c)Ni muhimu wakulima na maafisa ugani kuelimishwa kuhusu afya ya udongo na matumizi sahihi ya mbolea
d)Matumizi ya mbegu bora na utunzaji wa mazao shambani ni lazima ili kuleta tija katika uzalishaji.
e)Mbolea haiwezi kuleta tija kama hakuna utunzaji wa mazao shambani.
Mbolea haiharibu udongo kama ikitumiwa
Afya ya udongo ni uwezo wa udongo kukidhi mahitaji ya ukuaji na uzalishaji wa mimea kama vile: virutubisho, maji, hewa pamoja na uwezo wa udongo kushikilia mmea
2.0 Virutubisho 16 muhimu kwa ajili ya ukuaji wa mmea
A. Virutubisho vinavyohitajika na mmea kwa kiasi kikubwa
•C, H, O (carbon, hydrogen na oxygen)
•N, P, K (nitrogen, phosphorus, potassium)
B. Virutubisho vinavyohitajika na mmea kwa kiasi cha wastani
•Ca, Mg, S (calcium, magnesium na sulphur)
C. Virutubisho vinavyohitajika na mmea kwa kiasi kidogo
•B, Cl, Cu, Fe, Mn, Mo, Zn (boron, chlorine, copper, iron, manganese, molybdenum na zinc)
3. Utafahamuje afya ya udongo?
Viashiria katika mimea pia hukufahamisha afya ya udongo
Viashiria katika mkonge vinavyoonyesha upungufu wa Naitrojeni katika udongo
Upungufu wa Calcium Kwenye Mkonge
Ugonjwa wa upungufu wa kirutubisho cha Calcium.
Majani ya mkonge yanakuwa na rangi ya zambarau na majani ya mkonge yanajikunja kuanzia nchani.
Upungufu wa Potasiam (K) katika udongo
•Ni kirutubisho ambacho hutembea katika mmea
•kwa hiyo viashiria huanza kuonekana katika majani ya chini
•Jani huanza kukauka kuanzia kwenye ncha na kingo za jani.
4. Umuhimu wa kupima afya ya Udongo
-Ni muhimu sana kupima afya ya udongo ili kujua kama udongo katika shamba husika unafaa kwa zao husika.
-Kuweza kujua matatizo ya udongo wa shamba husika na kutoa tiba sahihi (mfano matatizo ya tindikali, chumvi, magadi, upungufu wa virutubisho.
-Kuweza kujua aina stahili ya mbolea inayofaa kwa kuzingatia zao na afya ya udongo.
-Kuweza kujua kiwango cha mbolea kinachohitajika kwa zao husika.
-Inaondoa uwezekano wa kuweka mbolea isiyohitajika shambani kwa zao husika.
- Kuweza kujua zana sahihi za kulimia kulingana na aina ya udongo wa shamba husika
5.0 Mbolea ni nini?
-Mbolea ni chakula cha mmea kilichobeba virutubisho ambavyo huhitajika katika ukuaji wa mmea
1. Aina za mbolea
2. Mbolea za viwandani
1. Mbolea za Kiwandani
•Zipo zenye virutubisho zaidi ya kimoja zinaonyeshwa kwa kiwango na aina ya virutubisho vilivyomo,
-17-17-17 ni 17% kwa kila kirutubisho: N, P2O5, na K2O
-Compound fertilizer, e.g. N-P-K-S
-N & P: Diammonium phosphate (DAP), 18-46-0
•Zipo mbolea zenye kirutubisho kimoja kama
-Nitrogen: Urea, 46-0-0
-Phosphorus: Triple Super Phosphate (TSP), 0-46-0
-Muriate of Potash (KCl), 0-0-62
•Aina hizi za mbolea zipo katika hali ya chembechembe, kimiminika/maji, na gesi
Mbolea za Kemikali na Matumizi Yake
-Weka kilo 100 za Diammonium phosphate (DAP) au kilo 121 za Triple Superphosphate (TSP) wakati wa kupanda mkonge shambani ikiwa udongo unaupungufu wa phosphorus (P).
-Madini (Kirutubisho) cha Calcium
Mkonge unahitaji kirutubisho cha calcium kwa wingi ili kuzifanya nyuzi za mkonge ziwe imara na zisikatike hovyo.
Kama shamba lina miamba ya chokaa (lime stone) ni vizuri kwani mkonge utakuwa vizuri na hakutakuwa na haja ya kuongeza kirutubisho cha calcium.
Calcium ni muhimu sana kwa kuwa inauwezo pia wa kupunguza kiwango cha tindikali kwenye udongo na kuufanya udongo uwe na rutuba ya kutosha
-Baada ya mwaka mmoja tangu miche kupandwa shambani
-Weka mbolea ya Calcium ammonium nitrate (CAN) au UREA lakini CAN ni bora zaidi kwa vile mbolea hiyo licha ya Nitrogen pia ina kirutubisho cha Calcium kinachohitajika kwa wingi ili kuboresha nyuzi (fibre) pamoja na kupunguza tindikali kwenye udongo.
-Weka kilo 100 – 150 (mifuko 2-3 ya mbolea) kwa hekta mwaka mmoja baada ya kupanda mkonge shambani
-Weka muriate of potash (MOP) kilo 100 kwa hekta mwaka mmoja baada ya miche ya mkonge kupandwa shambani.
-Kama mkonge umeonesha upungufu wa potassium (K) weka kilo 100 kwa hekta kila mwaka kwa muda wa miaka mitano au mpaka ugonjwa utakapotoweka.
2. Mbolea ya asili: Mabaki ya mimea, Samadi mboji n.k
Mimea ya mikundekunde (kunde, maharage mbaazi n.k inatengeneza N)
6.0 Uhusiano wa afya ya udongo na matumizi ya mbolea katika kilimo
•Udongo unapokuwa na afya nzuri mkulima hahitaji kutumia mbolea.
•Lakini udongo ukiwa na afya mbaya /virutubisho kidogo ni muhimu kutumia mbolea.
•TARI Mlingano kwa kushirikiana na Wadau hufanya tathimini na utafiti kujua aina na viwango sahihi vya mbolea.
•Kujua ni wakati na sehemu gani mbolea itawekwa kwenye udongo kulingana na aina ya zao.
7.0 Hitimisho na Mapendekezo
a)Ukifahamu afya ya udongo /rutuba katika shamba lako utapata ushauri sahihi wa kutumia mbolea.
b)Ukitumia mbolea, viwango sahihi na kuweka mbolea ilivyoshauriwa utazalisha mazao kwa tija na utakuwa na uzalishaji endelevu
c)Ni muhimu wakulima na maafisa ugani kuelimishwa kuhusu afya ya udongo na matumizi sahihi ya mbolea
d)Matumizi ya mbegu bora na utunzaji wa mazao shambani ni lazima ili kuleta tija katika uzalishaji.
e)Mbolea haiwezi kuleta tija kama hakuna utunzaji wa mazao shambani.
Mbolea haiharibu udongo kama ikitumiwa