kwani TBC HAIDANGANYI? mimi siliamini habarileo na hata TBC. kwani tangu yule mtoto alietaka kupiga bomu la maji pale ubalozi wa marekani. halafu HABARAILEO likaingiza propaganda yake. kwa hivyo hata TBC inaweza kudanganya
Mkuu ww ndio hujamwelewa huyu Malaria Magamba Sugu, Yaani haamini mtu waliyefunga naye ndoa anaweza kuwafanyia fujo ndio maana anawahi kusema ni CDM, maskini hajui..kikulacho ki nguoni mwako!
Mkuu naona umeanza tena ile tabia yako ya umagamba,siku chache zilizopita ulikuja na post zenye matumaini hapa JF tukadhani akili zako zimepigwa flash!! sasa leo umekuja na uharo hapa...ACHA KUDANGANYA UMMA,HABARI INASEMA SHIGELA NA WATU WAKE NDIO WAMEMFANYIA VURUGU KIONGOZI WA CUF,na huyu Shigela kupitia TBC1 NEWS BULLETIN ameojiwa na kutoa kauli kuwa si yeye wala timu yake wanaohusika na tukio hilo...sasa unapokuja na siasa majitaka na uharo hapa hatukuelewi kabisa mkuu,kajipange vizuri nadhani una matatizo ya ugonjwa wa uzushi...
Ccm na cuf??
Huo ni ugomvi wa wanandoa. Msiingilie?
Mfuasi mmoja wa chama cha siasa( CUF), kavamiwa na vijana waliotambulika ni wa CCM na kumpa kipigo mpaka akapoteza fahamu.
Mfuasi huyo wa CUF alikutwa akipandisha bendera ya chama cha CUF nyumbani kwake, vijana wa CCM walimvamia na kumpa kipigo majeruhi huyo kalazwa hospitali, inasemekana kavunjika mbavu.
SOURCE: TBC HABARI
hahahhah. Naogopa kumwagiwa tindikali? Au hutakuja na chupa hiyo?
Usiumeume mdomo walaani wahuni wenu wa CCM vinginevyo tutolee unafiki wako hapa.Vurugu za aina zote zilaaniwe
mme na mke wagombanapo......
Hawa CCM wanafikiri Tanzania ni mali yao, chama kimepoteza heshima ya zamani ile ya kina Mzee Nauye leo kimekuwa chama cha vurugu.