Ifahamu Dodoma

Ifahamu Dodoma

Kuhusu Saba saba, Hazina, Mlezi na hata Kikuyu sio yote

Dodoma barabara zote zinaeleweka na suala la usafi maeneo mengi limezingatiwa labda kama kuna tatizo la uzoaji taka

Dodoma mimi ni home away from home, nimekulia hapo na kusoma hapo na likizo huwa nipo hapo,

Tena hiyo Majengo Sokoni nimekuta na huo mtaro umesafishwa unang'aa kitu ambacho sijawahi kuona kifanye miaka mingi niliyoishi hapo.

Sasa sijui uchafu huo unaoongelea wewe ni upi na sikatai kuna baadhi ya maeneo bado si masafi sana ila asilimia kubwa ya Maeneo uliyoyataja hujawa mkweli
Mchanga umejaa barabarani, lami utaiona sehemu tairi zinapita.
Huwezi fananisha na barabara za Mwanza aisee.
 
Huu mji siuelewagi, mchanga umejaa kwenye lami, yani lami inaonekana maeneo ambayo tairi zinapita tu, na viongozi wapo tu hawalioni hilo.
Kwakwel swala la mchanga kwenye lami hata mi nimeliona sana nikaja kuelewa kuwa Dodoma inavumbi saaana hiyo changamoto ni yakudumu itakua kwa Dodoma watakua wanashindana Nayo tu
 
Mleta mada kakaa wiki mbili tu haijui Dodoma..

Mimi pia nimeshi Dodoma miaka hiyo hiyo na Mzee wangu kajenga hapo Dom japo sio nyumbani ila huwa ninarudi mara kwa mara likizo.

Dom ya sahivi sio ya kipindi kile, hakika sasa hivi kwenye suala la usaf wanajitahidi sana.

NAOMBA KUFAFANUA, KUTOKA KATIKATI YA MJI KWENDA MPAKA;

1. NZUGUNI NA KISASA KWA NJIA YA DAR

2. MAKULU KWA NJIA YA UDOM

3. KIKUYU KWENYE NYUMBA ZA HABITAT KWA NJIA YA IRINGA

4. MNADA MPYA KWA NJIA YA SINGIDA

5. MIPANGO KWA NJIA YA KONDOA

Eneo lote hilo huwezi kuchukua siku zaidi ya sita kulizunguka MTAA KWA MTAA tena kwa baiskeli.

Wiki mbili zinatumika pale unapokuwa na shughuli zingine.

Waliokaa Dodoma wanafahamu. Wiki chache nilizokuwa kule zilitosha kunipa picha halisi.
 
Mleta mada anatembelea masoko anaakuja kuhitimisha Dom chafu

Eti saba saba chafu kisa kapita stand kule nyuma kwa mtu ambaye hajafika Dom anaweza akaamini Saba saba yote chafu

Na hata huko alipopataja ukiachwa uswazi wa 'nyumba' ambazo ni za kawaida, mazingira bado wanajitahidi sana Viongozi wa Serikali za Mitaa Dodoma wako makini sana na suala la usafi...

Nina wasi wasi huyu mleta mada hajakaa Dom au ana tatizo flani na Dom

Zunguka mitaa yote niliyoainisha Mkuu utathibitisha.
 
Kwa bahati mbaya zaidi maeneo uliyotaja ni uswahilini sana tena kwenye idadi kubwa ya watu.

Kwa mfano chang,ombe ni mji mkongwe ambao hauna tofauti na kwa mtogole na maeneo mengi ya Temeke n.k

Unaonesha ww ni mgeni sana tu,dodoma ya jana ni tofauti sana na leo yaani sehemu kubwa ya mji ni safi kuliko hizo sehemu chache ambazo hazifiki 10.
Chukulia mfano:
Area A
Area D
Area C
Chamwino
Mipango
Kisasa
Uzunguni
Kikuyu usalama
Kisasa na maeneo yote kuelekea chuo kikuu
Chinangali.
Ila ninachokushangaa umetaja maeneo ya masoko tu ambapo kwa kawaida maeneo hayo huwa na usafi wa kawaida ama hafifu kabisa.
Ila nikupongeze kwa kuleta changamoto kwa watendaji wa mji wa Dodoma huenda watarekebisha na hizo kasoro chache ulizoziona mwisho wa siku utafurahia maisha.
Narrow mind, HAZINA, MLEZI, KIZOTA, CHANG'OMBE YA CHINI, MAILIMBILI Kuna Masoko?
 
SEHEMU HII YA 1 NITAJIKITA ZAIDI KWENYE SUALA LA USAFI.

Kwa ujumla Dodoma Mjini ni mji mchafu katika maeneo mengi japo baadhi ya maeneo ni masafi


Nilivyoona hayo maneno mekundu nikajua unatiririka na takwimu
 
NAOMBA NITIMIZE AHADI YANGU KUHUSU DODOMA SEHEMU YA 2.

HII ITAHUSISHA MAENEO AMBAYO,
1. Yanauza madawa ya kulevya ikiwemo Bangi.

2.Maeneo yenye vibaka kwa wingi

3. Maeneo ambayo biashara ya ngono inafanyika.

Tafuta topic inayosomeka "IFAHAMU DODOM SEHEMU YA 2"

Asanteni.
 
NAOMBA NITIMIZE AHADI YANGU KUHUSU DODOMA SEHEMU YA 2.

HII ITAHUSISHA MAENEO AMBAYO,
1. Yanauza madawa ya kulevya ikiwemo Bangi.

2.Maeneo yenye vibaka kwa wingi

3. Maeneo ambayo biashara ya ngono inafanyika.

Tafuta topic inayosomeka "IFAHAMU DODOM SEHEMU YA 2"

Asanteni.
 
Ninawasalimu wanajamvi wote.

Naomba nijikite moja kwa moja kwenye dhumuni husika la andishi langu la Leo;

Leo naomba niainishishe maeneo hatarishi kwa Dodoma Mjini katika vipengele vifuatavyo;

1. Maeneo yenye vibaka sana

2. Maeneo maarufu kwa uuzaji wa Dawa za Kulevya ikiwemo Bangi na Mirungi.

3. Maeneo maarufu kwa biashara ya Ngono.

NB: Mtaniwia radhi kwa kutokuwa specific kwa kumtaja mtu au biashara yake.

NAOMBA NIANZE:

1. MAENEO YENYE VIBAKA WENGI
Ukihamia Dodoma kama wewe ni Mchelewaji wa kurudi nyumbani usiishi maeneo yafuatayo;
a. KIKUYU
b. MAJENGO
c. KIZOTA
d. CHANG'OMBE YA CHINI
e. CHADULU
f. MAILI MBILI
g.BAHI ROAD
h. MAKOLE
I. MAKULU

Maeneo haya ni hatari sana kwa kutembea usiku pia kama una vitu vya dhamani ni maeneo hatarishi pia.

2. MAENEO MAARUFU KWA UUZAJI WA MADAWA YA KULEVYA

a.HAZINA AIRPORT na MJI MPYA

√ Haya ni maeneo maarufu sana kwa uuzaji wa Unga "Cocaine n.k". Hazina kuna mfanyabiashata yupo karibu na ofisi nyeti akiendesha hii biashara. Vijana wengi watumia unga huenda maeneo haya kujipatia huduma.

b. MAKOLE AIRPORT NA CHAMWINO

√ Ni maeneo maarufu kwa upatikanaji wa Mirungi. Wahitaji wengi wa Mirungi huipata maeneo haya. Zipo gari binafsi na za-biashara ambazo hutumika kusafirisha Mirungi kuingia Dodoma.

c. HAZINA, MAJENGO, KIKUYU, KIZOTA, CHANG'OMBE YA CHINI, CHADULU, MAILIMBILI, BAHI ROAD, MAKOLE na MAKULU

√Haya ni maeneo ambayo BANGI inauzwa sana na watumiaji wake wapo wengi pia. Mfano, Eneo la MAJENGO kuna Kibanda maalumu cha kuvutia Bangi. Mvutaji hufika hapo na Bangi yake na kiasi kati ya 200 hadi 500 kwa ajili ya kulipia huduma ya kuvutia Bangi kwenye Banda.

√ Maeneo mengine maarufu kwa uuzaji wa Bangi ni Vituo vya Daladala ambavyo kuna wapiga debe, mfano Nkuhungu, Chang'ombe ya Chini, na Jamatini.

3. MAENEO MAARUFU KWA BIASHARA YA NGONO

Ukiwa Dodoma huduma hii inapatikana sana UHINDINI, MAKOLE na AIRPORT. Nyakati za usiku Dada poa wengi wanapatikana maeneo hayo.

Pia wapo ambao huziacha namba zao kwa wahudumu wa Nyumba za Wageni na pindi unapohitaji huduma hupigiwa simu na kuja kukupatia huduma.


Hapo ndipo mwisho wa utafiti wangu.


Nawasilisha.


Moderators msifute Uzi huu tafadhali utawasaidia wengi
 
Aisee wewe hujaishi Dom, yaelekea Chadulu na Makole hata saa Tisa usiku unamove bila shida tena kwa mguu
 
Hapo kwenye vibaka ni kwel kabisa hasa maili mbili na chang'ombe hatari sana
 
Back
Top Bottom