Ninawasalimu wanajamvi wote.
Naomba nijikite moja kwa moja kwenye dhumuni husika la andishi langu la Leo;
Leo naomba niainishishe maeneo hatarishi kwa Dodoma Mjini katika vipengele vifuatavyo;
1. Maeneo yenye vibaka sana
2. Maeneo maarufu kwa uuzaji wa Dawa za Kulevya ikiwemo Bangi na Mirungi.
3. Maeneo maarufu kwa biashara ya Ngono.
NB: Mtaniwia radhi kwa kutokuwa specific kwa kumtaja mtu au biashara yake.
NAOMBA NIANZE:
1. MAENEO YENYE VIBAKA WENGI
Ukihamia Dodoma kama wewe ni Mchelewaji wa kurudi nyumbani usiishi maeneo yafuatayo;
a. KIKUYU
b. MAJENGO
c. KIZOTA
d. CHANG'OMBE YA CHINI
e. CHADULU
f. MAILI MBILI
g.BAHI ROAD
h. MAKOLE
I. MAKULU
Maeneo haya ni hatari sana kwa kutembea usiku pia kama una vitu vya dhamani ni maeneo hatarishi pia.
2. MAENEO MAARUFU KWA UUZAJI WA MADAWA YA KULEVYA
a.HAZINA AIRPORT na MJI MPYA
√ Haya ni maeneo maarufu sana kwa uuzaji wa Unga "Cocaine n.k". Hazina kuna mfanyabiashata yupo karibu na ofisi nyeti akiendesha hii biashara. Vijana wengi watumia unga huenda maeneo haya kujipatia huduma.
b. MAKOLE AIRPORT NA CHAMWINO
√ Ni maeneo maarufu kwa upatikanaji wa Mirungi. Wahitaji wengi wa Mirungi huipata maeneo haya. Zipo gari binafsi na za-biashara ambazo hutumika kusafirisha Mirungi kuingia Dodoma.
c. HAZINA, MAJENGO, KIKUYU, KIZOTA, CHANG'OMBE YA CHINI, CHADULU, MAILIMBILI, BAHI ROAD, MAKOLE na MAKULU
√Haya ni maeneo ambayo BANGI inauzwa sana na watumiaji wake wapo wengi pia. Mfano, Eneo la MAJENGO kuna Kibanda maalumu cha kuvutia Bangi. Mvutaji hufika hapo na Bangi yake na kiasi kati ya 200 hadi 500 kwa ajili ya kulipia huduma ya kuvutia Bangi kwenye Banda.
√ Maeneo mengine maarufu kwa uuzaji wa Bangi ni Vituo vya Daladala ambavyo kuna wapiga debe, mfano Nkuhungu, Chang'ombe ya Chini, na Jamatini.
3. MAENEO MAARUFU KWA BIASHARA YA NGONO
Ukiwa Dodoma huduma hii inapatikana sana UHINDINI, MAKOLE na AIRPORT. Nyakati za usiku Dada poa wengi wanapatikana maeneo hayo.
Pia wapo ambao huziacha namba zao kwa wahudumu wa Nyumba za Wageni na pindi unapohitaji huduma hupigiwa simu na kuja kukupatia huduma.
Hapo ndipo mwisho wa utafiti wangu.
Nawasilisha.
Moderators msifute Uzi huu tafadhali utawasaidia wengi