Ifahamu Dodoma

Ifahamu Dodoma

dodoma ni mji mzuri, ila shida yake ni maji. maji yake ni ya chumvi na ni ya shida sana. hilo tu. siku maji ya victoria yakifika pale huo mji utakuwa bora sana. pia uchawi, warangi wengi, waswahili wamejaa pale kati.
 
watanzania kila kitu mnataka mashindano ya ubishi ,changamoto haibishiwi kwahiyo nyie mnataka yatajwe mazuri tu na mabaya yenu mtayajuaje ili mlekebishe!Dodoma ni mji mzuri sana ila unanapungufu kadhaa ambayo inahitajika kurekebishwa ikiwepo wa uchafu kwa baadhi ya maeneo kama mtoa mada alivyo alezea.

Asante kwa kunielewa,..

Ukiondoa kasoro ya uchafu na shida ya Maji Dodoma ni Mji Mzuri sana.
 
CCM hata kusimamia usafi wa mji mkuu wa nchi hawawezi. Sijui wanaweza nini hawa walaghai
 
Shida ya maji? Wapi? Au uchumvi iliopo kwenye maji.

Wakati ambao viongozi Wakuu wakiwa Dodoma kuna baadhi ya maeneo hukumbwa na shida ya maji. Maji yanaweza yasitoke kwa siku hata tatu. Mfano, Chang'ombe, Kikuyu, Chadulu.

Hii inaonyesha kuwa miundo mbinu ya maji haitatosheleza pindi Wakuu na watu wengine wakihamia Dodoma.
 
Unaweza ku - "SUBSCRIBE " Topic hii ili nitakapo andika SEHEMU YA 2 tuweze kuwa pamoja.
 
Wakati ambao viongozi Wakuu wakiwa Dodoma kuna baadhi ya maeneo hukumbwa na shida ya maji. Maji yanaweza yasitoke kwa siku hata tatu. Mfano, Chang'ombe, Kikuyu, Chadulu.

Hii inaonyesha kuwa miundo mbinu ya maji haitatosheleza pindi Wakuu na watu wengine wakihamia Dodoma.
Huu ni uongo ulio wazi dodoma haina shida ya maji nimekaa miaka 2 hapo!!..
Labda uniambie kikuyu ipi, chadulu ipi zenye hilo tatizo!?..hayo maeneo ni makubwa sawa na kusema temeke/ubungo/tabata
 
Dodoma mifumo ya maji imefika hadi mkonze kuelekea mbele huko kama utaenda iringa, ukielekea kwa pinda zuzu maji yapo, ukija kizota-nkuhungu maji yapo rudi huku ilazo-kisasa sasa nyie mnaosema maji ya shida au mnamaanisha vijijini huko?...
Chadulu zipo mbili kama ilivyo Makole na hata hiyo Kikuyu zimegawanyika pia!..
 
Dodoma mifumo ya maji imefika hadi mkonze kuelekea mbele huko kama utaenda iringa, ukielekea kwa pinda zuzu maji yapo, ukija kizota-nkuhungu maji yapo rudi huku ilazo-kisasa sasa nyie mnaosema maji ya shida au mnamaanisha vijijini huko?...
Chadulu zipo mbili kama ilivyo Makole na hata hiyo Kikuyu zimegawanyika pia!..

Ni sawa kabisa.. miundo mbinu kama mabomba yapo sehemu kubwa sana, tatizo ni utokaji wa Maji. Fanya utafiti hasa wakati ambao Wakubwa wapo Dodoma utanielewa vizuri.

Watu wanaoishi maeneo kama Kisasa, Area C na D hawawezi kuona shida hii kwa sababu ni maeneo ambayo Wakubwa wanaishi na maji yapo muda wote.
 
Ni sawa kabisa.. miundo mbinu kama mabomba yapo sehemu kubwa sana, tatizo ni utokaji wa Maji. Fanya utafiti hasa wakati ambao Wakubwa wapo Dodoma utanielewa vizuri.

Watu wanaoishi maeneo kama Kisasa, Area C na D hawawezi kuona shida hii kwa sababu ni maeneo ambayo Wakubwa wanaishi na maji yapo muda wote.
Dodoma hakuna shida ya maji, hiyo ya maji kukatika huwa Ni dharura tu
 
na vipofu wapo wengi sana, malaya ndo usiseme fika hapo tanzania guest, chako ni chako, club la aziz, 84club, kilima, ndo utaifurahia dodoma, ukitaka kuichukia, nenda kwa wahuni kama gwasa, chadulu, chang'ombe, maili mbili, njedengwa, makulu,kizota, huko utakimbizwa, mpaka utaona bora ukate mambupu uyatupe kwamba yanakuongezea uzito
 
Kuhusu Saba saba, Hazina, Mlezi na hata Kikuyu sio yote

Dodoma barabara zote zinaeleweka na suala la usafi maeneo mengi limezingatiwa labda kama kuna tatizo la uzoaji taka

Dodoma mimi ni home away from home, nimekulia hapo na kusoma hapo na likizo huwa nipo hapo,

Tena hiyo Majengo Sokoni nimekuta na huo mtaro umesafishwa unang'aa kitu ambacho sijawahi kuona kifanye miaka mingi niliyoishi hapo.

Sasa sijui uchafu huo unaoongelea wewe ni upi na sikatai kuna baadhi ya maeneo bado si masafi sana ila asilimia kubwa ya Maeneo uliyoyataja hujawa mkweli
Hayo unayosema yanaweza kuwa kweli. Ila kwa faida ya wanajukwaa ungeweka picha za kuthibitisha hicho anachoongea ingekuwa vema sana. Hapo ungalitenganisha mafuta na maji kiulaiiinii
 
na vipofu wapo wengi sana, malaya ndo usiseme fika hapo tanzania guest, chako ni chako, club la aziz, 84club, kilima, ndo utaifurahia dodoma, ukitaka kuichukia, nenda kwa wahuni kama gwasa, chadulu, chang'ombe, maili mbili, njedengwa, makulu,kizota, huko utakimbizwa, mpaka utaona bora ukate mambupu uyatupe kwamba yanakuongezea uzito
Mkuu club84 hivi bado kuna watu wanaendaga?? Wewe utakuwa unaongelea Dodoma ya zamani. Sasa hivi Malaya wote utawakuta malaika
 
Back
Top Bottom