Ifahamu Dodoma

Ifahamu Dodoma

Kuomba ni kero kubwa, yani hata ukikaa zako mahali ujiagizie ka kuku, watakuja tu kukuomba!!!!!!
 
Dodoma mifumo ya maji imefika hadi mkonze kuelekea mbele huko kama utaenda iringa, ukielekea kwa pinda zuzu maji yapo, ukija kizota-nkuhungu maji yapo rudi huku ilazo-kisasa sasa nyie mnaosema maji ya shida au mnamaanisha vijijini huko?...
Chadulu zipo mbili kama ilivyo Makole na hata hiyo Kikuyu zimegawanyika pia!..


Acha uongo bwana wewe, kuna maji?
 
Kapicha tafadhali maneno matupu hayanogi


Napita
Kwa
Majonzi
 
Ni sawa kabisa.. miundo mbinu kama mabomba yapo sehemu kubwa sana, tatizo ni utokaji wa Maji. Fanya utafiti hasa wakati ambao Wakubwa wapo Dodoma utanielewa vizuri.

Watu wanaoishi maeneo kama Kisasa, Area C na D hawawezi kuona shida hii kwa sababu ni maeneo ambayo Wakubwa wanaishi na maji yapo muda wote.
Nimeishi kikuyu ya juu hilo tatizo sijalipata, nikahamia maeneo ya magorofani pia sikukumbana nalo..
 
Mlezi nenda maeneo ya karibu na Daraja la Kigamboni na maeneo ya Mlezi katikati.

Hazina nenda upande wa pili wa Shule ya Mlezi,

Sabasaba nenda yale maeneo yenye soko na stand.

Soko Kuu kila sehemu ni chafu, pitia Eneo la Bustani ya
Mh. Mavunde na pale kwenye kituo cha Tax.

Hiyo ni mifano tu.
mbona ni ya kutafuta tu. tanzania hii kuna sehemu sio pachafu.
 
Nimeishi kikuyu ya juu hilo tatizo sijalipata, nikahamia maeneo ya magorofani pia sikukumbana nalo..
Mkuu Magorofani maarufu kama MAGOROFA YA CDA kuna shida ya maji tangu kitambo. Na nimefanikiwa kufika eneo hilo ambalo kwa sasa Magorofa mengi ni kama Magofu.

Eneo hilo pia lilikuwa na uchafu wa kutosha.
 
Mkuu Magorofani maarufu kama MAGOROFA YA CDA kuna shida ya maji tangu kitambo. Na nimefanikiwa kufika eneo hilo ambalo kwa sasa Magorofa mengi ni kama Magofu.

Eneo hilo pia lilikuwa na uchafu wa kutosha.
Magorofa ya Nhcf umefikaaa
 
Magorofa ya Nhcf umefikaaa
Waliyarekebisha na sasa ni Masafi. Wakati nafanya utafiti wangu kuna mdau alinielekeza maeneo hayo na nilienda face to face.

Yameboreshwa sana.
 
Kapicha tafadhali maneno matupu hayanogi


Napita
Kwa
Majonzi

Nimefika Kituo cha Mabasi yaendayo Mikoa leo. Nilipotaka kupiga picha kuna mdau akanieleza kama nahitaji simu yangu niache hiyo shughuli.


Soko Kuu la Majengo Leo tangu Asubuhi Halmashauri walikuwa wanazoa uchafu.
 
Waliyarekebisha na sasa ni Masafi. Wakati nafanya utafiti wangu kuna mdau alinielekeza maeneo hayo na nilienda face to face.

Yameboreshwa sana.
Ila Kwa usafi 100%
 
Nimefika Kituo cha Mabasi yaendayo Mikoa leo. Nilipotaka kupiga picha kuna mdau akanieleza kama nahitaji simu yangu niache hiyo shughuli.


Soko Kuu la Majengo Leo tangu Asubuhi Halmashauri walikuwa wanazoa uchafu.
Sio uchafu bomoa bomoa imepita hapo unapoongelea uchafu unakosea wakat unaelewa kabisa walichokifanya reli ni nn unazan hapo mpaka stand ihame mambo yatakaa sawaa
 
Mkuu Magorofani maarufu kama MAGOROFA YA CDA kuna shida ya maji tangu kitambo. Na nimefanikiwa kufika eneo hilo ambalo kwa sasa Magorofa mengi ni kama Magofu.

Eneo hilo pia lilikuwa na uchafu wa kutosha.
sawa
 
Ila Kwa usafi 100%

Hapo Sokoni ni 40% kwa sasa. Maana kuna uchafu bado upo pale chini haujazolewa.

Mvua ikinyesha kuna uchafu wa kutosha eneo zima la soko na harufu Kali pia.

Upande wa karibu na KITUO CHA DALADALA CHA SANGO kuna Mama Lishe wengi sana ambao maji machafu humwaga KORONGONI. Hapo pia kuna uchafu na harufu mbaya.
 
Sio uchafu bomoa bomoa imepita hapo unapoongelea uchafu unakosea wakat unaelewa kabisa walichokifanya reli ni nn unazan hapo mpaka stand ihame mambo yatakaa sawaa

Mkuu Demiss, pale ni pachafu pamoja na kwamba walibomopewa. Vyakula vinauzwa kwenye Mazingira hayo hayo machafu.
 
Habari zenu ndugu zangu,

Kwa muda wa Majuma kadhaa nipo Dodoma Mjini na nimekuwa nikifanya uchunguzi wangu binafsi.

Katika uchunguzi wangu nimegundua mambo kadha wa kadha.

Hapa nitazungumzia mambo makubwa mawili,

1. Usafi na Mazingira Dodoma Mjini

2. Maeneo hatarishi kwa Mkoa wa Dodoma hasa Dodoma Mjini.

SEHEMU HII YA 1 NITAJIKITA ZAIDI KWENYE SUALA LA USAFI.

Kwa ujumla Dodoma Mjini ni mji mchafu katika maeneo mengi japo baadhi ya maeneo ni masafi

Sababu za uchafu huu ni;
1. Mwamko mdogo wa wananchi juu ya usafi.

2. Uwajibikaji mdogo wa mamlaka zinazohusiana na usafi

MAENEO AMBAYO WANANCHI WANA MWAMKO MDOGO WA USAFI;
a. Hazina

b. Mlezi

c. Kikuyu

d. Majengo

e. Kizota

f. Chang'ombe ya chini

g. Chadulu

h. Maili mbili

j. Bahi road

k. Makulu

l. Makole

Kwa wale mnaohamia Dodoma na wapenda Usafi Epukeni sana maeneo haya.

MAENEO AMBAYO MAMLAKA HAZIWAJIBIKI SAWASAWA KATIKA UKUSANYAJI TAKA,

1. Kwenye madampo karibu yote uchafu umejaa hadi kumwagika chini.

2. Masoko yote (Mfano, Bonanza, Soko Kuu la Majengo na Sabasaba) ni machafu sana. Ukifika kwenye masoko haya utajionea mwenyewe.

3. Kituo kikuu cha Mabasi ya Mkoani na Jamatini kuna uchafu wa kutisha. Kwa wale waliopita Dodoma siku za karibuni watakuwa wameshuhudia hali hii ya Uchafu.


BINAFSI SIAMINI KAMA MAMLAKA HUSIKA ZINAJUA HALI YA USAFI KWA MKOA WA DODOMA.

NB:
SEHEMU YA 2 NITAWALETEA MAENEO MAARUFU KWA UUZAJI WA MADAWA NA VIBAKA.


Nawasilisha.

Unaweza ku - "SUBSCRIBE " Topic hii ili nitakapo andika SEHEMU YA 2 tuweze kuwa pamoja. Nitaleta taarifa hapahapa.
Mkuu ulienda kwa shangazi yako au ulitumwa?vp wamekulipa sh.ngap?
 
Mkuu Demiss, pale ni pachafu pamoja na kwamba walibomopewa. Vyakula vinauzwa kwenye Mazingira hayo hayo machafu.
Ndiooooo Nimesema bomoa bomoa imeharibu mazingira
 
Serikali imepanga kuanzisha miji ya Kisasa kuzunguka mkoa wa Dodoma na itapendeza zaidi kuhamia jiji la Wanyakaya
 
Back
Top Bottom