True story kuhusu multiple IDsp
Kuna mwana hapa jukwaani siwezi kumsahau😂😂🙌🏿 kama anasoma hii post anipe ishara ya 5 tu inatosha..
Huyu jamaa alikuwa na ID kama 10 hivi..! Mimi sikuwahi kujua kabisa
Sasa sijui alijuaje kama kipindi hicho nilikuwa na chenchi kidogo, basi kila week ilikuwa kuna ID ngeni 2 zinaniomba assist PM ya 5 to 10K❗
Mimi bila hiyana wala kinyongo nikawa narusha maana nayajua maisha ya mwanaume kuishiwa
Basi baada ya mwaka nikapata simu ngeni jamaa akanisalimia kwa furaha sana na kunishukuru sana.. Kisha akatuma msg kaka hii
Mshana kuna kipindi nilikuwa nimepigika mno.. Nilikula sana tano tano na kumi kumi zako kupitia ID mbalimbali
Sasa hivi niko Mwanza nataka nikutumie chochote kukushukuru😂😂😂 Je hii number inapokea miamala? Nikamwambia ndio..! Akasema nimpe dakika 5.. !!!
Mpaka Leo nasubiri huo muamala..! Yaani tapeli ni tapeli tuu..! 🙌🏿