Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,762
- 40,987
Ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano Inasema hivi:
Wazo:
- Je, Mahakama ikisema sheria fulani ni Batili na kinyume cha Katiba sheria hiyo inatenguka mara moja na haina nguvu?
- Je, Neno "badala" linapotumika hapo juu ni sawa au neno "baada" ndilo lingetumika.
- Kama Mahakama inasema sheria fulani ni kinyume na Katiba kwa misingi gani sheria hiyo inaendelea kuwa halali?
(5) Endapo katika shauri lolote inadaiwa kwamba sheria
yoyote iliyotungwa au hatua yoyote iliyochukuliwa na Serikali au
mamlaka nyingine inafuta au inakatiza haki, uhuru na wajibu
muhimu zitokanazo na ibara ya 12 hadi 29 za Katiba hii, na
Mahakama Kuu inaridhika kwamba sheria au hatua inayohusika,
kwa kiwango inachopingana na Katiba ni batili au kinyume cha
Katiba basi Mahakama Kuu ikiona kuwa yafaa au hali au masilahi
ya jamii yahitaji hivyo, badala ya kutamka kuwa sheria au hatua
hiyo ni batili, itakuwa na uwezo wa kuamua kutoa fursa kwa ajili
ya Serikali au mamlaka nyingine yoyote inayohusika kurekebisha
hitilafu iliyopo katika sheria inayotuhumiwa au hatua inayohusika
katika muda na kwa jinsi itakavyotajwa na Mahakama Kuu, na
sheria hiyo au hatua inayohusika itaendelea kuhesabiwa kuwa ni
halali hadi ama marekebisho yatakapofanywa au muda
uliowekwa na Mahakama Kuu utakapokwisha, mradi muda mfupi
zaidi ndio uzingatiwe.
Wazo:
- Je, Mahakama ikisema sheria fulani ni Batili na kinyume cha Katiba sheria hiyo inatenguka mara moja na haina nguvu?
- Je, Neno "badala" linapotumika hapo juu ni sawa au neno "baada" ndilo lingetumika.
- Kama Mahakama inasema sheria fulani ni kinyume na Katiba kwa misingi gani sheria hiyo inaendelea kuwa halali?