Iache nyumba yako ipumue

Mshana Jr

Platinum Member
Aug 19, 2012
269,633
697,754
Kuna wakati huwa tunaugua magonjwa yanayosababishwa na sisi wenyewe. Kuna wakati yale tunayoyabeba vichwani mwetu na kushindwa kuyaachilia hivyo hivyo hufanya hivyo kwenye majumba yetu.

Nyumba safi, yenye vitu vichache huchangamsha mwili na kuleta afya ya akili. Si lazima iwe kubwa, hata hiyo ndogo katika udogo wake yaweza kukupa nuru, hewa safi na mwanga mpaka rohoni kama hutaigeuza kuwa ghala.

Hewa safi, nafasi na mwanga wa kutosha ndani ya nyumba/ chumba huufanya mwili kuchangamka na kuwa na siha njema hata kama kula yako ni ya shida.

Nyumba safi iliyopangiliwa vizuri huvutia mahusiano mazuri yenye furaha. Nyumba nayo ina roho hebu ipe nafasi ipumue.

Natambua kuna baadhi yetu kiasili ni wabinafsi na wenye roho ya kukusanya kila kitu lakini kama wakielimishwa wanaweza kubadilika.. Unajua hata hawa wadudu kama kunguni, papasi, chawa mende nk huletwa na nyumba isiyopangiliwa na iliyojazana vitu visivyo na faida tena.

Kuna nyumba makabati ya nguo yamejaa nguo zisizovaliwa tena
Kuna nyumba vyumba na shoes rack vimejaa viatu visivyovaliwa tena
Kuna nyumba chumba cha ghala kimejaa vitu vibovu visivyotumika tena pasi, feni, sufuria viti nknk
Kuna nyumba karibia kila chumba kimejazwa vitu visivyo na faida chini mpaka juu, makawa ya chakula, mapichapicha kutani, vimitomito, vizulia, vipambopambo nknk

Kumbuka kila kimoja kati ya hivyo kimetengenezwa na malighafi tofauti tofauti, kitendo cha kuvirundika vyote sehemu moja husababisha futuko, hewa nzito na harufu za ajabu.

Fanya mambo haya muhimu
Kuwa na tabia ya kugawa vitu usivyotumia tena hasa nguo vyombo na viatu

Vitu vibovu tengeneza, gawa au uza. Kitu kisipotumika muda mrefu huwa mazalia ya wadudu na makao pia
Kuwa na utaratibu wa kuwa na vitu vichache lakini vizuri hata kama thamani yake sio kubwa sana
Fanya kila kitu ndani ya nyumba/chumba chako kiwe na nafasi yake ya kutosha

Usibabanishe vitu, usivipandanishe, usivisokomeze mahali pamoja vitashindwa kupumua

Jaribu kufanya hayo machache utaona hata stress zitakavyokupungua...kuipa nyumba nafasi ya kupumua ni kuupa mwili pia nafasi ya kulerax

Si kila wenye mapepo wametupiwa wengine wameyakaribisha wenyewe kutokana na lifestyle ndani ya sehemu wanazoishi
 
Mshana Jr anena tena ya maana

Kuna aina ya mavazi
Aina ya mapambo.

Aina ya mziki humtambulisha mtu hata anapoishi...! Unakuta mdada ana furushi la nywele kichwani tena bandia, ana hereni mbili mbili masikio yote, ana Kishaufu puani, ana mapete vidoleni mikono yote, ana mabangili, ana cheni shingoni, shanga kiunoni, vikuku miguuni.

Ana nyusi bandia kabandika, ana makeup mpaka hazitoshani usoni...huyu ukimkuta miziki yake anayopenda.... Ukikikuta chumba chake au nyumba yake.

Ukiikuta dressing table yake ni full vurumai
 
Wa aina hii hua nawapenda sana kwa sababu ukikutana nae lazima aku introduce kwenye mkondo wa maji taka
 
Wa aina hii hua nawapenda sana kwa sababu ukikutana nae lazima aku introduce kwenye mkondo wa maji taka
Kuna vitu hata shetani mwenyewe akiviona anatimua mbio..! Shauri yako! Kuna mikondo imejaa matakataka mpaka imebadilika rangi
giphy.gif


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Si kila wenye mapepo wametupiwa wengine wameyakaribisha wenyewe kutokana na lifestyle ndani ya sehemu wanazoishi

Kiongozi, nifafanulie hapa... una maana mapepo yataingia kwenye nyumba iliyo na mlundikano? lifestyle? kwa vip?
 
Umeongea vyema my.

Katika mtu asopenda makorokoro mmoja mie. Siishi kutupa na kugawa mpk wanangu wananambia mama wewe too much.

Nawaambia kukaa na makorokoro ndani unaweka makaazi ya mashetani.

Hapa nisichoweza kutupa au kugawa ni mabuku na vitabu vyao tu ila navyo vinanitia wazim.
 
Si kila wenye mapepo wametupiwa wengine wameyakaribisha wenyewe kutokana na lifestyle ndani ya sehemu wanazoishi

Kiongozi, nifafanulie hapa... una maana mapepo yataingia kwenye nyumba iliyo na mlundikano? lifestyle? kwa vip?
Yeah iliyojaa makorokoro yasiyotumika ni makazi ya wadudu,viumbe kama panya ,nyoka na hata mapepo wachafu.
 
Umeongea vyema my.

Katika mtu asopenda makorokoro mmoja mie. Siishi kutupa na kugawa mpk wanangu wananambia mama wewe too much.

Nawaambia kukaa na makorokoro ndani unaweka makaazi ya mashetani.

Hapa nisichoweza kutupa au kugawa ni mabuku na vitabu vyao tu ila navyo vinanitia wazim.
hayo mabuku yao yatengenezee shelf uyapange vema huko na uwawekee masharti ya kutoa kwa ustaarabu na kurudisha kama kilivyokuwa.
 
Back
Top Bottom