I got it! Mheshimiwa Spika mnataka kutuloga!!?

I got it! Mheshimiwa Spika mnataka kutuloga!!?

...walianza na digitali, wanataka wazime kabisa yanayoendelea mjengoni...subiri M4C na NGOs waingize watu road, Vasco atakimbia nchi...
 
Naunga mkono hoja kwa asilimia zote. Ni kikao tu cha kichawi ndicho kinachofanyika gizani na kwa kuwa dhamira zao zinawasuta kwa ouvu waliokusudia kutenda dhidi ya wengine, hawatataka uovu huo kuwekwa nuruni.

Watanzania kwa sasa tumefunguka na tuna neema ya kuangaziwa nuru. Tutahakikisha kwa namna yoyote ile nuru tulio nayo ndiyo itakayolifukuza giza.

Na Nyongeza kwa watu wa dini tumepewa mamlaka ya kuwakanyaga chini ya miguu yetu nyoka na ng'e na nguvu zote za giza(uchawi) na wala hakuna kitakachotudhuru.

Huu ndio wakati muafaka wa kusimama kiume kukataa dhulma ya aina yoyote kwa ajili ya watoto wetu na vizazi vijavyo.

.
 
Kibaya zaidi wanataka watupe taarifa ambazo zishafanyiwa editing ya kutosha kama ni ile ya kuisulubu serikali yashaondolewa yote tutakuwa tunaletewa taarifa ambazo ni tamu kama peremende kuambiwa kuwa wabunge wetu wanaisifia sana serikali na kuwa serikali iko makini na inafanya kazi na inayafanyia kazi malalamiko yaa wananchi
hatutasikia tena habari za wabunge kutoka nje au sijui kuomba miongozo wala kuwa kuna mbunge alitoa shilingi kwenye budget
tutakuwa tunalishwa habari nzuri tuu za bunge na wala sio kile kinachoendelea bungeni
Hatutajua kama mbunge wa jimbo fulani ni mtoro toka bunge limeanza au hachangii kitu cha maana bungeni zaidi ya pumba

Badala ya kwenda kwenye ulimwengu wa uwazi na uwajibikaji tunarudi nyuma kwenye siri za serikali mambo ya serikali yanafichwa fichwa mambo ya wabunge yanafichwa fichwa as wao ni watakatifu sana
 
Well said Mzee Mwanakijiji.. Hii nchi c yao.. Hatuwezi kuongozwa kama sie ni ng'ombe au mbuzi.. Na wala wacijifanye ati wao ndo wenye akili kuliko sie.. Walivunja kamati ya bunge ya madini na hawajaunda nyingine.. Wamevunja kamati ya mahesabu ya Zitto na wanaleta longo longo.. Sasa wanataka bunge lisionyeshwe live ili wananchi wasione jinci wanavyoibiwa mchana kweupe..
 
Udikteta wa Hitler haukuanza siku mmoja, alianza taratibu kama tunavyoyaona sasa, mwisho ukawa dikteta halisi. Hata kauli ya Rais kwamba Polisi wasiogope Lawama imenisononesha sana. Lazima tuilaani hatua hii ya kuipeleka nchi kwenye udikteta. Nadhani hata baba zao wanaowafadhili (wahisani) hawatakaa kimya ktk hili. Let us see.

WAO wana Bunge, Pesa, TBC na POLICE. Sisi tuna watu na MUNGU. Tuone ni nani atakayeshinda
 
Mie nilijua watarekebisha upuuzi wao kumbe ndio kwanza wana mpango wa kuficha upuuzi wao kwa wananchi?

Hakuna kitu kinachotia hasara nchi yetu kama bunge. Sijaona cha maana wabunnge wa ccm wanajadili zaidi ya kucheka cheka hovyo na kupiga makofi hovyo hovyo.


Bunge lifutwe kabisa halina maana kwenye nchi yetu. Kila kitu cha maana kinapingwa na spika
 
hayo ya kulogana huko huko ! Hapa tunachotaka ni kutazama nini kinaendelea wakati wote wa vikao vya bunge. Na ole wao wapitishe kusudio hili; wajue watakiona cha 'mtema kuni'.
 
Hata kura ipigwe wanaounga mkono matangazo ya bunge yarushwe live au yasirushwe idadi ya ccm bado ni kubwa na hawaaminiki.
 
Yaani sijui nisemeje,inachosha kwakweli.

Watanzania wenzangu kweli tunaweza kuendeshwa namna hii kama mataahira? Watu wanapata wapi huu ujasiri wa hata kujaribu kutamka haya hadharani alafu tukawaacha?

Hiki ni kiburi na ni dhahiri wapinzani wasipojiandaa sasa CCM hawako tayari kuachia madaraka kwa amani! Tujiandae Watanzania,Maana hii si siasa tena bali uhaini! Bunge kuonyeshwa live imekuwa hisani tena!!!

Nafikiri imetosha sasa!!!!
sikumbuki ni nani lakini ni katika wanamageuzi wa mwanzo hapa Tanzania (90s) aliwahi kuongea kawa uchungu juu ya hii perception ya mzungu wa kwanza kufika hapa aliyoyaona kabla ya kupiga marufuku biashara ya utumwa.

Kwamba waswahili zaidi ya sabini (70) wanaongozwa na mwarabu mmoja mwenye gobole (aina ya bunduki) kutoka Ujiji mpaka Bagamoyo!!! Hakuwahi kuamini kama hawa binadamu walikuwa sawa binadamu wengine au walikuwa na elements za unyama. Maana kuswagwa maili hizo zote bila hata kuhoji........ (nahisi machozi)

Nikiangalia kinachoendelea hapa kwetu hadi sasa nashindwa kutenganisha hii simulizi na hali halisi wakuu!

 
hivi huyo katibu wa bunge nani kamtuma? Nani anampa mamlaka ya kuwaamulia watz? mimi nadhani huu ndio muda wa wabunge kususia bunge kama hili litapitishwa. Wabunge wote wasuse kuingia bungeni kwa sabubu bunge limeenda kinyume na matakwa ya waajiri wao ambao ni wananchi na waseme hawataki kufukuzwa kazi na wananchi kwa ajili ya mawazo ya watu wachache. Kama wanataka pitisha hili likapigiwe kura bungeni tena kwa utaratibu aliousema MM.
WABUNGE HUU NDO MUDA WA KUUNGANA KUTETEA MASLAHI YA MWAJIRI WENU AMBAE NI MWANANCHI WA KAWAIDA. TUTAKUTANA KWENYE INTERVIEW 2015
 
Mie nilijua watarekebisha upuuzi wao kumbe ndio kwanza wana mpango wa kuficha upuuzi wao kwa wananchi?
Hakuna kitu kinachotia hasara nchi yetu kama bunge. Sijaona cha maana wabunnge wa ccm wanajadili zaidi ya kucheka cheka hovyo na kupiga makofi hovyo hovyo.
Bunge lifutwe kabisa halina maana kwenye nchi yetu. Kila kitu cha maana kinapingwa na spika
sasa si ndio vizuri mkuu Oxlade-Chamberlain, wamejitambua kuwa they have nothing to offer to the Tanzanians
 
Udikteta wa Hitler haukuanza siku mmoja, alianza taratibu kama tunavyoyaona sasa, mwisho ukawa dikteta halisi. Hata kauli ya Rais kwamba Polisi wasiogope Lawama imenisononesha sana. Lazima tuilaani hatua hii ya kuipeleka nchi kwenye udikteta. Nadhani hata baba zao wanaowafadhili (wahisani) hawatakaa kimya ktk hili. Let us see.
Kuna wakati niliwahi kuandika humu JF kwamba Kikwete ana element zote za udikteta. Na kwamba kutokana na kukosa uwezo wa kujenga hoja za kushawishi sasa kila mahali anatumia ubabe. Watu wakanikejeli kwamba sijui maana ya dikteta na uchadema unanisumbua. Lakini naona sasa hatimaye niliyosema miaka miwili iliyopita yanaanza kudhihirika. Kikwete yupo tayari kulinda himaya yake kwa gharama yoyote ile ikiwamo ya kumwaga damu ya watanzania na kuwanyima watanzania haki wanazostahili kama binadamu. Mungu atuepushe na hali hii, maana tunakoelekea hatuna miaka mingi kabla hatujauana.
 
Udikteta wa Hitler haukuanza siku mmoja, alianza taratibu kama tunavyoyaona sasa, mwisho ukawa dikteta halisi. Hata kauli ya Rais kwamba Polisi wasiogope Lawama imenisononesha sana. Lazima tuilaani hatua hii ya kuipeleka nchi kwenye udikteta. Nadhani hata baba zao wanaowafadhili (wahisani) hawatakaa kimya ktk hili. Let us see.
Hakuna cha baba zao! Hao wafadhili wao huagalia vitu vinavyowafaidisha wao, usitegemee hata siku moja tukapata maendeleo kwa kuwategemea wafadhili. Tunatakiwa ni sisi tuungane kwa kuondoa tofauti zetu, tusifitiane.
 
Watafanya kila wanalolijua, mwisho wa siku ni sauti yako wewe, yule na mimi ndiyo itakayoamua. Inapaswa sasa kila mmoja wetu apeleke ujumbe kwa ndugu, jamaa, marafiki na majirani. Tujitolee kutoa elimu ya umma kila tunapopata nafasi. Ikifika 2015 iwe mwisho wa wachawi hawa na tuone hivyo vikao vyao kama vitawasaidia kitu.

Mbio za sakafuni huishia ukingoni!

Mungu Ibariki Tanzania.
 
Yaani sijui nisemeje,inachosha kwakweli.

Watanzania wenzangu kweli tunaweza kuendeshwa namna hii kama mataahira? Watu wanapata wapi huu ujasiri wa hata kujaribu kutamka haya hadharani alafu tukawaacha?

Hiki ni kiburi na ni dhahiri wapinzani wasipojiandaa sasa CCM hawako tayari kuachia madaraka kwa amani! Tujiandae Watanzania,Maana hii si siasa tena bali uhaini! Bunge kuonyeshwa live imekuwa hisani tena!!!

Nafikiri imetosha sasa!!!!

Kwakweli,bora umesema,mi nimechoka kabisa!wa tz tumezidi kukaa kimya!
 
Walipo fikia watawala wetu ni pabaya!!
Wanaamini wao wana akili kuliko watu wote,na wao wanaweza kuchagua lipi wananchi wanataka,na lipi hawataki!
Huku ni kutufanya mazumbukuku;lazima tukatae kama taifa!
 
CCM haina mpango wa kuachia hatamu hapa Tz na hili walilisema wazi and they mean it. Wameweka mamluki wao katika vyama vya upinzani ndio maana unaona vyama havitulii. CCM imefunga ndoa na CUF baada ya kuona moto wao huko Znz. Baada ya ndoa sasa CUF wamekuwa toothless bull dogs, wako kimyaaa!! Sasa hivi CCM wamekuja na strategy hii ya kuzuia umma usione madudu ya wabunge kwa kukaba live broadcast. Kama kweli Dk Kashilila ana nia nzuri basi angalau waruhusu redio zirushe live matangazo yao sababu wabunge wanaovaa au kulala hawataonekana. Shame on Kashilila kwa kukubali kuburuzwa na serikali, shame on Makinda kwa kuonyesha udhaifu ilhali alitakiwa aoneshe kwamba wanawake wanaweza!! Wataendelea kufanya kila wawezalo lakini ipo siku watz tutatoka tu kwenye kibano chao CCM
 
Ninakuunga mkono kwa maono yako ya kwamba CCM hawako tayari kuachia madaraka kwa amani.
yaani sijui nisemeje,inachosha kwakweli.

Watanzania wenzangu kweli tunaweza kuendeshwa namna hii kama mataahira? Watu wanapata wapi huu ujasiri wa hata kujaribu kutamka haya hadharani alafu tukawaacha?

Hiki ni kiburi na ni dhahiri wapinzani wasipojiandaa sasa ccm hawako tayari kuachia madaraka kwa amani! Tujiandae watanzania,maana hii si siasa tena bali uhaini! Bunge kuonyeshwa live imekuwa hisani tena!!!

Nafikiri imetosha sasa!!!!
 
Back
Top Bottom