I got it! Mheshimiwa Spika mnataka kutuloga!!?

I got it! Mheshimiwa Spika mnataka kutuloga!!?

Nina pendekezo - kama kweli uamuzi huu utachukuliwa naomba uchukuliwe hadharani angalau mara hiyo moja kabla hawajaacha kurusha matangazo wapigiwe kura ya kuitwa majina (roll call) ili tujue wabunge wetu ambao wanataka kutuficha wanachofanya Bungeni ni kina nani? Na kama kuna wabunge wa upinzani wanaofikiri hili ni jambo jema wasimame na waseme sasa; kama wapo wabunge wa CCM wanaamini kuwa hili ni jambo jema wasimame na wajitaje kwa majina yao Bungeni kuwa wanaunga mkono kuwaficha wananchi waliowaajiri kujua nini wanafanya.

Angalau tutawajua wachawi wetu kwa majina yao!

Na. M. M. Mwanakijiji

Kama kuna dhambi waliwahi kufanya basi dhambii hii itakuwa kubwa mmno na watahitaji hukumu stahiki 2015
Pendekezo lako zuri sana lakini sijui kama watakubali.....
 
Well said Mkuu Mwanakijiji, Hii ni mada pana ambayo viongozi wa upinzani wanapashwa kuileta kwetu ili tuitolee maamuzi sahihi...CCM kwa wingi wao plus upofu ulio watanda watapitisha kila uharo ilimradi wawakomoe Watanzania, hili wamelithibitisha katika kila nyanja na halina mjadala. Muhimu kama ulivyosema tena kwa kurejea maneno ya Mwalimu...Tukatae Kudharauliwa kwa Vitendo, Sisi tuko wengi, kwa NGUVU ya UMMA tutawang'oa tu....
 
Huyu Mama hashauriki, chochote mtakachomshauri ataenda kuuliza kwa mzee wa LIWALO NA LIWE na yeye ataenda kuuliza kwa FASTJET na mwisho wa siku maamuzi ya fastjet ndio yanaongoza bunge. Hakuna bunge hii miaka mi5. I miss u Samwel Sitta, you are Legend

.......

Ni kweli Ms. KIROBOTO anapeleka kwa LIWALO NA LIWE then kwa FASJET then back to Ms. KIROBOTO. Watanzania tuamke na kukataa hawa wabakaji wa demokrasia.

Jirani zetu wa Kenya jamani wanakwenda mbele kwa kasi sisi hawa wabakaji wanafanya kila jitihada ya kuturejesha nyuma.

Miaka 20 ijayo Kenya itakuwa kama Thailand na hapana shaka watoto wetu wanaozaliwa leo watafika makaburini kwetu na kuyachapa fimbo makaburi.
 
Huu ni mpango maalumu wenye malengo mapana kwa minajili ya kuficha udhaifu wa serikali, kuendeleza matumizi ya ubabe na kupitisha maamuzi hovyo yakiwamo ya wabunge kujitengenezea mafao ya kufuru (hefty send-off packages) kwa ajili ya uchaguzi 2015.
Nia hasa ni kutowachonganisha wabunge na wananchi wakati wa kujitengenezea ulaji.. It is simply a disgrace..
 
Wanataka kuficha nini? Si wanachojadili ni kuwawakilisha wananchi? wanataka sisi tuelewe nini, kwani wanataka kunyonyana ndimi huko bungeni? Hii ni dalili ya uchizi kwa hawa viongozi!
 
Nani kawaambia kuwa vikao vitakuwa vya siri? waandishi watakuwapo ndani ya ukumbu as usual mbona mnadanganya watu NINYI?
 
Utawala huu unanikumbusha nyuma sana wakati watanzania hawaijui Televisheni mpaka miaka ya 90' mwanzoni... ni zile enzi za kuambiwa Televisheni ni anasa kuwa na friji nyumbani kwako ni anasa, kununua gari ni ubepari, kujenga nyumba ni ubepari, kujifunza lugha za kigeni ni ulimbukeni, wanakujenga na kukuweka katika hali ya mazingira ya kukufanya udumae...usijue chochote kuhusu dunia hii...uwe mshamba mshamba... exposure haipo kabisa kabisa.... na inasemekana mkubwa mmoja anawaambia watanzania kuwa ameota kuna kitu kitatokea au kimetokea ulaya au nchi nyingine.. kumbe yeye ameona kwenye luninga yake .... dunia ya leo kila kinachotokea duniani kinakuwa wazi tena kwa habari mpasuko..(kiswahili kibovu kidogo) nina maana Breaking news unaona kila kitu... leo wanasema iwe siri.. siri gani hiyo kama sio ulevi wa madaraka na matumizi mabaya ya madaraka? kuzuia bunge kuwa live ni kushindwa kuthibiti nidhamu bungeni ni dhahiri kwamba kuna udhaifu wa uongozi ulioko bungeni wakawti ule... kufanya vikao vya bunge kwa siri pia ni kuwanyima watanzania kutoa mawazo yao juu ya maendeleo ya taifa na mustakabali wake...
 
Mkuu Mwanakijiji, naona Madame Spika anataka kulivunja Bunge kabisaaaa. Ameshaanza na Kamati, kinachofuata ni kulivunja lote. Sasa uamuzi kama huu nadhani haoni sababu ya kuupeleka hewani moja kwa moja (live), badala yake ameona kiporo ndio kinatufaa sisi Watz. Na amini usiamini watakaosema Ndiyooooooooo watashinda kwa kishindo.
Mi ningependa ujue kuwa Makinda peke yake na uwezo wake hawezi kuamua hili. This issue has Sekretari Kuu ya CCM (The Presedent in it) all over it. Makinda Kashilila ni Agents tu, Divide and Rule.
 
Well said brother!! Matendo ya CCM yanaashiria kifo chake 2015! Leo ujifiche nisikuone 2015 uje uniombe kura nikiwa nakuona sio? Watanzania tutakuwa taifa la Wapuuzi kama hatutawaondoa hawa magamba madarakani kama watatekeleza hili. Hii nchi ni yetu sote, imefika mahali wao wanaona watakaloamua wao ndio mwisho,as if sisi ni sote ni mbuzi wametufunga kamba wanatuvuta kuelekea wanakotaka wao!Kwa kweli ni aibu sana kwa nchi yetu kuongozwa na watu wenye upeo mdogo na walioweka maslahi yao mbele kuliko ya wananchi wanaowatawala. Sasa wanakoelekea siko,na wakae wakiendelea kufikiri polisi,jeshi ni mali yao na ndio silaha yao kukandamiza wananchi na kufanya watakayo,ipo siku polisi,jeshi havitatosha kuzima hasira za watanzania na wote wanaofanya ushenzi huu watakuwa victim wa kwanza!!
 
Huu ni mpango maalumu wenye malengo mapana kwa minajili ya kuficha udhaifu wa serikali, kuendeleza matumizi ya ubabe na kupitisha maamuzi hovyo yakiwamo ya wabunge kujitengenezea mafao ya kufuru (hefty send-off packages) kwa ajili ya uchaguzi 2015.
Nia hasa ni kutowachonganisha wabunge na wananchi wakati wa kujitengenezea ulaji..

Hizi ndio move za akina Mangula wao ni umafia tu kwani wanajua siasa imeshawashinda,Kuna mengi yanakuja chini ya uongozi mpya wa CCM.

Nia yao kubwa na ya kwanza kupunguza public consumption!
 
yaani sijui nisemeje,inachosha kwakweli.

Watanzania wenzangu kweli tunaweza kuendeshwa namna hii kama mataahira? Watu wanapata wapi huu ujasiri wa hata kujaribu kutamka haya hadharani alafu tukawaacha?

Hiki ni kiburi na ni dhahiri wapinzani wasipojiandaa sasa ccm hawako tayari kuachia madaraka kwa amani! Tujiandae watanzania,maana hii si siasa tena bali uhaini! Bunge kuonyeshwa live imekuwa hisani tena!!!

Nafikiri imetosha sasa!!!!

kusema kweli ni aibu watu wazima kuna na hoja kama hii.wenzetu mahakama ina kuwa live wao eti bunge lisionyeshwe.hawa wenzetu wa kijani sijui wanatumia akili gani kufikiri-ofisi za siri -kali bado haijawatosha tu.

naona ni dalili ya kufanikisha ufalme wa bagamoyo. "urais ni wa familia'' jk
 
Wananchi wa Mtwara wametuonyesha njia ya kusema "HAPANA" badala ya kulaumu au kunug'unika. Ni juu yetu wananchi kusema HAPANA kwa kutoonyesha 'live' bunge. Chanzo cha utumwa, ni mtumwa mwenyewe!
  1. yaitishwa maandamano nchi nzima kupinga upuuzi huo?
  2. tushawishi upinzani kugomea vikao vyote vya bunge ambavyo haviendi hewani live?
Nafikiri sote tujadili nini kifanyike ili tuendelee kuona bunge live!
 
hili likifanikiwa kupita wananchi tuungane kulichoma moto hilo jengo maana halitaitwa tena bunge,litakua pango kama nyumba zingine.Hatutajali lilijengwa na nani
 
Vitabu vitakatifu vinasema. Adam na Eva walikuwa wanaonekana kwa Mungu na Malaika "LIVE" ila walipofanya dhambi walijificha hawakutaka kuwa LIVE tena.
SASA HILI BUNGE KUNA DHAMBI WAMEFANYA AU WANATAKA KUFANYA HIVYO HAWATAKI KUWA LIVE TENA.
 
Kama bunge linataka kufanya mapenzi basi ni sawa wanaweza kujifungia na kufanya mapenzi yao na nashauri ikiwezekana lifanyike usiku ili mapenzi yao yanoge zaidi...

Lakini kama bunge linataka kujadili mustakabali wa nchi hii basi hapa hakuna hisani tena ... wananchi ambao ndio tumewapeleka bungeni tunayo haki ya kujuwa ni nini kinajadiliwa kwa mustakabali wa nchi yetu.

kama wabunge wataongea pumba - tutajua, watakaosigina demokrsia-tutajua .. mwisho wa siku tutaamua mbivu na mbichi...

spika na naibu wake wasikimbie vivuli vyao....

Da mkuu,wametumwa na macd hawa ili wanapofanya mavituz tusiwaone, ila punguza hasira mkuu.
 
This is the only country where you can expect the unexpected to happen.
 
Viongozi wa CDM waweke wazi msimamo wa chama na kila mbunge ausimamie bungeni then mkaidi tumtoe hili halhtaji mjadala Bunge linawakilisha wananchi.
 
CCM wanajisahau wanadhani hivi ni vikao vya ccm. na vyama vingine ni vyama alikwa tu, kwahiyo wanajipangia wanavyofiri. Hawa wachawi wanataka kuuza nchi hii. wanajua fika watawafanyia fujo wapinzani kisha wanawatoa nje kinachofuta ni kupitisha mambo yao ya kuuza nchi hii. Wapinzani watuandalie maandamano mpaka bungeni tukawavamie kupinga jambo hili. ndo hayo ya mikataba ya madini kuwa siri.
 
42470281_bbc72ccff5_o.jpg


Vikao vya wachawi hufanyika kwa siri. Sasa sijui kama uchawi upo na una nguvu au ni imani tu lakini ukweli ni kuwa wapo watu wanaamini katika nguvu za uchawi. Vikao vya wachawi hawaalikwi waandishi wa habari. Sababu kubwa ni kuwa vikao hivyo vinahusiana na mambo ya kudhuru zaidi kuliko kitu kingine chochote. Wachawi basi hupenda mambo yao yawe ya siri sana.


Angalau tutawajua wachawi wetu kwa majina yao!

Na. M. M. Mwanakijiji

........

Mzee Mwanakijiji, just to keep the record clear, aliyeitoa hii hoja ni Katibu wa bunge Dokta Kashiririka na sio speaker. Inapaswa sasa waandishi wa habari wamuulize speaker ni nini maoni yake juu ya pendekezo hili la katibu wa bunge.

Binafsi nimeshasema huu ni ujuha wa kizamani na umeelezea vizuri kuwa ni uchawi. Dunia ya leo huu ni mtazamo finyu sana.

Embu tujaribu kusema sawa, tunakubari bunge lisioneshwe, kesho atakuja Jaji Mkuu na kusema kutokana na vurugu zinazojitokeza sasa kuanzia leo ni marufuku waandishi wa habari kugusa maeneo ya mahamakama.

Na kwa kuwa mahakama wanarungu palepale wataweza kusema hivi, kwa mtu yeyote atakayeonekana na simu au camera au kalamu na karatasi katika maeneo ya mahakama adhabu yake kifuno cha ni miezi sita na kunyang'anywa hicho chombo chako kama ni camera au simu au pen na karatasi, waandishi watatii sheria na kutogusa mahakamani.

Kinachoendelea mahakamani itakuwa ni siri ya hakimu na wenye kesi. Atakuja mkuu wa polisi naye atasema hivyo hivyo kwani kuna watu wanawapiga picha traffic wakiwa "KAZINI", na baadaye ataibuka waziri mkuu na kusema tabia ya waandishi kwenda kwenye maofisi ya serikali muda wa kazi ni marufuku kwani mnaleta umbea na majungu na watu hawafanyi kazi kwa kujiamini kwani wanawaogopa nyie waandishi.

Tutakuwa ni nchi au falme ya kishetani? Kwahili jamani tusikubali na tujiandae kwenda Dodoma mwezi wa nne TUKAANDAMANE endapo upuuzi huu utakubalika.
 
Back
Top Bottom