Huzuni Nyingine Yaikumba Arusha: Ajali Yachukua Roho Za Watu 15 Jioni Hii

Restless Hustler

JF-Expert Member
Apr 9, 2017
4,742
17,983
Watu 15 wamefariki na wengine kadhaa kujeruhiwa baada ya gari kubwa aina ya Scania kufeli breki na kwenda kuparamia magari mengine katika eneo la Kibaoni Ngaramtoni Wilayani Arumeru Mkoani Arusha.

Ombeni Kirusha ambaye ni Shuhuda wa tukio hilo amesema “Kilichotokea ni ajali, nilikuwa na gari ndogo nikapisha gari iliyobeba cartepilar likaparamia magari hayo kulikuwa na magari matatu moja limebeba Wazungu, nakusababisha vifo vya Watu wengi, tumeokoa waliokuwa wanahema Watu nane, nilioshuhudia wamefariki walikuwa zaidi ya kumi”

Jeshi la polisi Mkoani Arusha kupitia kwa RPC Justine Masejo amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo na kusema Watu 15 wamefariki.

Chanzo: Millard Ayo
 
Watu 15 wamefariki na wengine kadhaa kujeruhiwa baada ya gari kubwa aina ya Scania kufeli breki na kwenda kuparamia magari mengine katika eneo la Kibaoni Ngaramtoni Wilayani Arumeru Mkoani Arusha.

Ombeni Kirusha ambaye ni Shuhuda wa tukio hilo amesema “Kilichotokea ni ajali, nilikuwa na gari ndogo nikapisha gari iliyobeba cartepilar likaparamia magari hayo kulikuwa na magari matatu moja limebeba Wazungu, nakusababisha vifo vya Watu wengi, tumeokoa waliokuwa wanahema Watu nane, nilioshuhudia wamefariki walikuwa zaidi ya kumi”

Jeshi la polisi Mkoani Arusha kupitia kwa RPC Justine Masejo amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo na kusema Watu 15 wamefariki.

Chanzo: Millard Ayo
Nani aliruhusu Malori Kupitia katikati ya Mji wakati Kuna Bypass?

Poleni sana wafiwa na mpumzike Kwa amani marehemu wote
 
Back
Top Bottom