Huyu ni wakuoa kweli?

Huyu ni wakuoa kweli?

Ushasema wa kanda maalumu hiyo romantic utapata wapi? Hapo vita ni vita mura
 
Inataka moyo kuishi na mtu ambae hajui asante nilishawah kuishi na mtu hajui asante samahan wala karibu binafsi niliona kama najipendekeza tu nilishindwa kuishi nae
Sure
Huu usahili wa awali umeisha tumekosa mgombea
 
Habari wakuu

Niko kwenye usahili wa kutafuta mwanamke wa kuoa mnamo mwakani kama Mungu atajaalia.

Sasa kuna binti ambae anaongoza kura za maoni mpaka sasa kukabidhiwa nafasi hiyo,Ila kiukweli ana changamoto kadhaa ambazo naziona kama kikwazo kwangu.

1-Kwa kua amekulia katika mazingira ya utafutaji tangu anakua yani ni kama imempunguzia ule uromantic wa kike+ na asili yao ni watu wa kanda maalumu(Mara).

2-Unaweza mtumia pesa au chochote ila hawezi sema asante au nimeipata mpaka umuulize
mfano leo asubui nimemnunulia kifurushi ila hata kujibu kwamba nimeipata hamna na sio kwamba hanipendi ila tu ndo asili yake.

Binafsi naona kumwambia siwezi ila naona tu nipige chini japo hana sifa zingine mbaya.

Ushauri tafadhali
Mkuu kama ni mjasiria mali mzuri huyo anafaa kuoa.Ukimpa mtaji atahakikisha anaparangana kuzalisha na mwishowe kama familia mnaweza kusonga mbele.Hazo kasoro ulizotaja ni ndogo ndogo zinarekebishika.Songa mbele mkuu umuweke malkia ndani.
 
Kiaje kaka
Mwanamke kama huyo ndio mzuri kuoa, kwa maana inaonekana anabidii kwenye kutafuta, na hata ukimtumia kidogo anaridhika nacho na kushukuru kimya kimya vile vile ni mficha siri, shukuru huyo ambae halopoki mpaka umuulize, kuliko kuja kumpata ambae kidogo umtumiacho atakuja juu na kuropoka badala ya kushukuru au kukaa kimya. Muda mwingine kukaa kimya ni busara.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom