Huyu ndiye Simon Kisena mnunuzi wa UDA?

Taifaletu

Member
Feb 21, 2011
34
17
SIMON GROUP CO.LTD inayojitambulisha kununua shirika la usafiri Dar es Salaam ni wawakilishi wa viongozi wa Tanzania katika kufisadi mali za Umma.

Anae jitambulisha kama Robert Simon Kisena ambae alisoma Nsumba Sekondari School akijulikana kwa jina JOKALA KISEANA na kumaliza Kidato cha Nne mwaka 1991 baada ya hapo alijiunga na Kidato cha Tano Shule ya Sekondari Mirambo Tabora mwaka 1992, hapa alifukuzwa akiwa Kaka Mkuu baada ya kuwasaliti wanafunzi wenzake aliokuwa kiwachongea kwa mwalimu mkuu na wanafunzi kuungana na kusababisha kusimamishwa, baada ya hapa JOKALA KISENA ambae leo anajulikana kwa majina ya Robert kisena bila kutoa sababu za kubadilisha jina lake la awali alikuwan akikaa na rafiki yake uku akifanya kazi NCU Ushirika kanda ya ziwa-Nyanza,walikosana na rafiki yake aliyekuwa anakaa kwake baada ya kumpa mimba dada wa rafiki yake aliyekuwa akikaa kwake.

Katika Uchaguzi mkuu wa 1995 Kisena alichukuliwa na John Cheyo wakati huo Cheyo akiwa mgombea urais na kumuweka kuwa kama masidizi wa kusimamia mali zake Shinyanga,hapa ndio kisena alipata pesa kidogo isiyoweza kununua UDA.kisena katika kusimamia mali za cheo alifanikiwa kujenga nyumba Tatu zote zipo Nyegezi mwanza eneo lijulikanalo kwa jina la CALIFONIA.

Baada ya hapo ndio akaanzisha SIMON Agency iliyokuwa inajishughulisha na uuzaji wa spare za magari kwa muda na baadae akajiunga na Profesa Juma Kapuya akiwa waziri ambapo walifanikiwa kuanzisha kampunin iliyofahamika kwa jina la ROBASIKA-Robert Simon Kapuya na kufanikiwa kuchota bilioni 13 za wananchi kupitia Benki ya NMB mwanza kwa ushawishi wa kapuya na kuanzisha ginery ya pamba katika jimbo la kapuya .

Ndio maana ukifuatilia pesa zilizolipwa kwenye account ya Iddy Simba imelipwa na Robasika kwa niamba ya Simon Group ili wafanikiwe kuchukua UDA na Kapuya akiwamo uku Simon Group wakidai kuwa ni malipo iliyokuwa ikidaiwa na Simon Group kutoka kwa Robasika kutokana na mkataba kati ya Simon Group na Robasika wa kusafirisha mizigo.Robet kisena ni chambo tu katika kuwafanikishia watu maalum kazi.

Watanzania hapa kuna ujambazi wa mchana, tunaibiwa, Juma Kapuya, Iddy Simba, Didas Masaburi wanahujumu watanzania kupitia UDA.
 
Duh!mkuu nasita kuamini kuwa historia yake kielimu imeishia hapo alipofukuzwa milambo.Kama unajua endelea kutujuza mkuu.
 
hivi viongozi wetu wanaimba kweli zile nyimbo za uzalendo km Tz eeh,tazama ramani,tanzania tanzania nakupenda
 
Maeneo yote uliyobainisha Mkuu kama Historia ya Huyo Bwana ni Muhimu na ya maana;isipokuwa hapo kwenye kubadilisha jina,sababu ya kubadilisha jina si ya Muhimu,swala amefuata utaratibu wa kisheria wa kufanya hivyo na kama ana document za kisheria kuthibitisha hilo!!

Kwenye kubadilisha jina huwa hakuna sehemu ya kujaza sababu ya kubadilisha jina,una apa mahakamani,unapewa document ya kiapo "Deed Poll" inasajiliwa Wizara ya Ardhi na kugongwa Mihuri,mara nyingine mtu hutangaza mabadiliko hayo kwenye Gazeti la Serikali!!

Otherwise nakubaliana na wewe Mkuu hapo wakubwa wamehusika katika Ukwapuaji wa rasilimali za Taifa!!!
 
Hiyo Ginery ya kapuya imejengwa kijiji gani jimboni kwa kapuya? maana jimbo la kapuya mazao makuu ya biashara ni tumaku na yale ya chakula kama karanga, mpunga etc...(i stand to be neutral)
 
Imejengwa KALIUWA...makao makuu ya jimbo la Kapuya,na nyingine amejenga MALAMPAKA...ni tapeli mzuri sana wa PAMBA kanda ya ziwa...waulize wakulima wa pamba kanda ya ziwa watakupa habari!
 
hivi viongozi wetu wanaimba kweli zile nyimbo za uzalendo km Tz eeh,tazama ramani,tanzania tanzania nakupenda

Nina uhakika sio zadi ya 30% y mawaziri wa Tanzania wanaweza kuimba hata wimbo wa taifa bila kukosea.watu wapo ki international inernational.
 
Mimi naona tunatoa hukumu mapema angekuwa mgeni kutoka nje ya nchi nadhani mambo yote haya yasingetokea angalieni mambo mengine yanayotokea watu wanachukua kilaini mfano angalieni madini hakuna hata faida kwa waTz.

Huyu ni kijana wa TZ kama ana nia njema ya kufufua UDA mimi sioni tatizo. Pia kunasehemu ya historia yake umekosea siyo kwamba alikuwa kaka mkuu wakati akiwa Mirambo Sekondari bali alikuwa mwanafunzi wa kawaida na alimaliza form six kwa kufanyia mtihani Pugu sekondari baada ya usaliti kwa wanafunzi.
 
Hawa wazawa ndo wametufkisha hapa, tuanze na hawa kwanza ili waumbuke ndo washike adabu, hao wazungu wa migodini wamewekwa na hawahawa wazawa kwa mda mrefu... Tukianza na hawa na serikali, nao wataamka huko migodini...subiri data za KISENA zinakuja ndo mtajua...fisad hana rangi
 
Mimi naona tunatoa hukumu mapema angekuwa mgeni kutoka nje ya nchi nadhani mambo yote haya yasingetokea angalieni mambo mengine yanayotokea watu wanachukua kilaini mfano angalieni madini hakuna hata faida kwa waTz.

Huyu ni kijana wa TZ kama ana nia njema ya kufufua UDA mimi sioni tatizo. Pia kunasehemu ya historia yake umekosea siyo kwamba alikuwa kaka mkuu wakati akiwa Mirambo Sekondari bali alikuwa mwanafunzi wa kawaida na alimaliza form six kwa kufanyia mtihani Pugu sekondari baada ya usaliti kwa wanafunzi.

Thanx mkuu.

Baada ya hapo historia yake kielimu imekaaje?
 
Tanzania shamba la bibi, watu wanajicumia tu, wala hawaogopi, nadhani maelezo yako yana ukweli fulani nikilinganisha na alivyokuwa anajibu maswali kwenye mdahalo jana na Star tv, japo alikuwa anakanusha kuhusu kuhusiana na vigogo na alikuwa akitetea kuwa SIMON GROUP ni ya familia 2 tu, ya kwake na ya rafiki yake, lakini kila alivyokuwa anajitetea kulikuwa na kila dalili ya kuonesha kuwa yule jamaa ni tapeli.
 
pale UDA jamaa waliingia kwa mkwala mzito wakavunja uzio,wakageuza garage kuwa warehouse na wakawafukuza na kuwanjia mikataba wapangaji wote wa zamani.Hakika watz tumebweteka mno
 
Jamani hivi huyu siyo mtoto Wa ****** kweli! Mimi nimuangalia kwa makini jana nashawishika kuamini kuwa ni mbegu za mkuu!
 
Mimi naona tunatoa hukumu mapema angekuwa mgeni kutoka nje ya nchi nadhani mambo yote haya yasingetokea angalieni mambo mengine yanayotokea watu wanachukua kilaini mfano angalieni madini hakuna hata faida kwa waTz.

Huyu ni kijana wa TZ kama ana nia njema ya kufufua UDA mimi sioni tatizo. Pia kunasehemu ya historia yake umekosea siyo kwamba alikuwa kaka mkuu wakati akiwa Mirambo Sekondari bali alikuwa mwanafunzi wa kawaida na alimaliza form six kwa kufanyia mtihani Pugu sekondari baada ya usaliti kwa wanafunzi.
Mkuu kumiliki kampuni yenye manufaa kwa wananchi inabidi tuangalie historia ya mtu ili tuone kama ataweza kuongoza hiyo kampuni.

Sasa kama wewe unaona anahukumiwa mapema na unazo data za kuonyesha kwamba hizo shutuma za usaliti wa wanafunzi; utapeli kwa wakulima wa pamba na utapeli katika benki ya NMB na kutumiwa na vigogo kuiba tunaomba utueleze ukweli ili tusiendelee kumuhukumu
 
Nadhani hii issue kaisuka Manji(mhindi) hasa baada ya Simon Group kuhoji kulikoni milioni 20 kwa mwaka kwa heka zaidi ya 12 kapangishwa manji hali yakuwa wao wanalipa 200 kwa robo tatu ya Heka.

Manji akadai wao ni nani kuhoji hili,na hiyo UDA hawataichukua.Habari ndiyo hiyo Mhindi anachomeka watanzania wachang'anyikiwe kisha baadae achukue kiulaini kupitia mlango wa nyuma.
 
Back
Top Bottom