Gift mzalendo
JF-Expert Member
- Dec 13, 2019
- 4,436
- 5,997
Nimekufuatilia muda mrefu nimeona wewe ni miongoni mwa wale wapambavu ambao wanasema hakuna MunguMungu muweza wa yote, mwenye ujuzi wa yote na upendo wote angekuwepo, mabaya yasingeweza kuwepo.
Kuwezekana kuwepo kwa mabaya, pamoja na hiyo dhana ya kukataa kumheshimu Mungu, ni ushahidi kwamba huyo Mungu hayupo.
Hivi unaelewa kwamba tuna sheria za kutungwa na watu tu zinakataza kumhukumu mtoto kwa kosa la baba?
Sasa, inakuwaje sheria za kutungwa na watu ziwe na rehema kubwa kuliko sheria za Mungu?
Yani sheria za kutungwa na watu zitawezaje kuzipita haki sheria za Mungu?
Huoni hapo huyo Mungu ni kikaragosi katungwa na watu tu, tena katungwa enzi za ujinga?
Mpambuvu hawezi kuelimika hata akijua ukweli hata wewe NDANI yako nafsi yako tu inakushuhudia kwamba Kuna kiumbe kingine chenye nguvu kilichokuumba lakini unakaza kwa sababu hauko tayari kuijua kweli
Vilevile napata mashaka level yako elimu na uelewa wako wa kawaida wa mambo ya kawaida tu kabla hujazungumzia hoja nzito za mambo ya kiroho zilizokuzidi uwezo wako
Watu wenye elimu ,na hekima uwezo mkubwa wanasayansi na watu wenye uwezo mzuri wa akili walikubali kwamba Kuna Mungu ambaye ana nguvu ya asili ambao chanzo Cha Kila kiumbe
Hata shetani anajua uwepo wa Mungu aliye hai
Sasa wewe na elimu yako ya kuunga unga unabisha bila hoja uwepo wa Mungu na matendo yake ya ajabu na kazi zake
Ila Mungu ni wa ajabu amekupa uhuru ufanye maamuzi yako ili MWISHO Kama usipotubu ulipwe sawa sawa na matendo yako