Huyu ndiye mh. Mbowe na hatari ya kujikanyagakanyaga kwenye kauli zake,amekosa msimamo kupita kiasi

kitu unasahau ni kuwa wewe ni mtu ambaye hata bei yako inajulikana nikitaka hata mimi nikuite SAU utakuja provided nina hela sasa wewe na mbowe wapi na wapi? mpaka umjadili ? vijana wa magamba hata sijui kwa nini ni wa kiwango cha chini hivi poor analysis
 
Kitu kinanishangaza,ni the fact that hawa masalia majukumu yao toka walipokuwa chadema hadi walipohamia ccm ni yale yale.

Hili linanipa tabu sana kuhusiana na uwezo wa watu hawa wa kufikiri.

Ina maana ccm ni perfect ama ni kwamba hamna kazi ya kufanya ccm ina wenyewe?

Kama nyie ni wajuzi sana wa kubomoa na si kujenga,basi mtegemee muda mfupi sana ndani ya ccm,yani very soon mtakuwa flushed kama tp.
 
Hivi wewe Ndg Mtela Mwampamba kama bwanahakutaki ya nini umfatefate,yaelekea hata mwanamke akikukataa unapita kutangaza je inakusaidia nini?Kwanini usitumie hiyo nguvu unayoitumia kuwaongelea Chadema ukakijenga chama chako kipya,maana unazidi kujishushia heshima mbele ya jamii au ndio upeo wako wa kisiasa umeishia hapo?Yaelekea bado una mapenzi na Chadema kwa hiyo ina kuuma sana polee weee,ungekuwa mwanamke ningekupeleka kwa kungwi ufanyiwe kitchen party ufundishe jinsi ya kuishi na mwanaume.Am feel soo sorry for you unmatured politician!!!!
 
Ili ku support hii document , Basi ngoja tuseme hivi ' ofisi ndogo oyeee ! Lumumba oyeeee! ' kwa hoja hii dhaifu bini Tepetepe , ile Buku 7 fc yote naona imeingia uwanjani ! Poleni sana aisee !
 
Kila siku zinavyozidi kwenda ndivyo mnavyozidi kugundua kwamba tatizo la TZ SIO CCM, bali ni la Mila Na Desturi zetu!

Huyo ndio Adui namba moja, nasema kila Mtz aliyezaliwa, kulelelwa na kukulia TZ yuko hivyo kama Bw.Mbowe au Bw.Kikwete, na wengi wetu tutafanya hivyo hivyo pindi tupatapo nafasi!
Tutaandika Katiba mpya nzuri tunavyotaka, tutaongea Majukwaani tunavyotaka lkn HAKUNA jipya!

Hakuna Mtanzania ambaye atakuwa tofauti na hao akina Bw.mbowe na Bw. kikwete, labda awe diaspora, yaani Mtanzania aliyelelewa ktk Mila na desturi za Jamii nyingine lkn siyo hii ya kwetu!

ANAYELALAMIKIA UFISADI TZ HAJAPATA NAFASI- Kardinali Pengo (Kiongozi Mkuu wa Kiroho wa Kanisa Katoliki
Tanzania)


Hapo kwenye red, hata masha alikuwa, kipi cha ajabu alichofanya? na wapo wengine kwenye serikali yako, kipi kipya??
 
Kwanza niseme wewe Mtela Mwampamba huna hadhi yoyote ya kujiita mtu makini kwakuwa unasumbuliwa na njaa na hivyo kulazimika kufikiri kwa kutumia tumbo lako. Hii post yako ni kuthibitisha tu kuwa bado sana kisiasa unahitaji muda wa kutosha ili ukue na kukomaa.

Pili: (1)Nimeona ni vizuri tu nikusaidie kwa kukukumbusha kuwa hata mwenyekiti wako wa ccm Ndugu Kanali Kikwete alikuwa akitoa kauli kama hii ya kwamba Chadema ni chama cha msimu, bila shaka maneno hayo umeyakopa kwake. Sasa nachotaka kukukumbusha ni kwamba chama cha msimu Chadema ndicho sasahivi kinachoset agenda za kisiasa nchini. Chama cha msimu Chadema ndicho kinawanyima usingizi viongozi wa ccm na serikali yake hata wamefikia hatua ya kutaka kutunga sheria ya kuzuia maandamano. Ni chama hiki cha msimu kimeifanya ccm itumie gharama kubwa sana kuitisha mikutano kwa kulazimika kukodishia watu magari na kuwalipa posho ili wahudhurie mikutano yake wakati mikutano ya Chadema inafurika wananchi wakija wenyewe kwa gharama zao.

(2)Nilitaka nikukumbushe kuwa sio lazima kutumia lugha ambayo huna uwezo nayo, lugha ambayo huimudu. Ulitakiwa kuandika attention ili umaanishe ulichokusudia lakini kwakuwa na wewe ndio wale wale wa kawambwa umeandika tentio kwa kujiami lakini kumbe hujui ulichopaswa kuandika. Na wewe ukiwa mhitimu wa shahada ya ualimu ulipaswa kujua lugha unayoitumia kuwasiliana na wadau wengine. Kwa mfano kama huu na kwa kuzingatia hivi karibuni imebainika kuwa hata vitabu vinavyotumia mashuleni vimekosewa sana, hii ni dalili kuwa ccm inawatumia watu vilaza ambao ni wanachama wake kusimamia mfumo wa elimu na matokeo yake ziro zinaongezeka kila uchao na waalimu wanazidi kuwajaza ujinga watoto wetu kwakuwa wao wenyewe ni vilaza.

Kaka Mwita Maranya hizi Kauli za Mbowe mtazamo wako ni upi hasa achana na Mtela! Au ndio mwana siasa anatakiwa awe na kauli za aina hiyo??
 
Last edited by a moderator:
Kumbe si kila umuonaye kwenye jukwaa la siasa ameshika Mic ni Mwanasiasa ! Wengine ni ..............
 
Mtela naona povu linakutoka sanaa bila sababu za msingi.tatizo au ugonjwa unaokusumbua ni personal issues au chuki binafsi ulizonazo juu ya mh.mbowe.

Let me tell you something, huwezi kufanya wananchi wamchukie mbowe kwa chuki zako binafsi zilizojaa utoto.ulifukuzwa chadema sababu ya usaliti...sasa. basi ccm wamekupokea movweon na ccm, nakushangaa kila mara ni kumkashifu na kumtukana mh.mbowe , haikusaidii wala haikujengi kisiasa.hujui maana ya politics ..angalia marekani wanavyoendesha siasa au UK. ..hawasemi ukweli kwasababu ni politics. Sio kila mtu anachosema kwenye siasa anamaanisha...siasa ni kama karata 3.pia huwezi na hautakaa uweze kufikia level aliyonayo mbowe.hizo ni ndoto.na huwezi kumshusha mbowe wewe utatokwa na povi kila siku sababu ya chuki binafsi ni ugonjwa mbaya sana.nq ubunge utaishia kuuuona kwenye TV.maana kama hutabadilika utaishia kuwa mpiga debe wa kunadi wagombea wa ccm.sasa hayo ni maisja gani? Jirekebisha wewe achana na mh.mbowe..mara billicanas ni danguro, mara sijui kampa mtu mimba haikusaidii utaishia kupuuuzwa.
 
Bw Mtela hebu onesha watu umekuwa kiakili na kimtazamo, cdm ulifuata nini na ccm umefuata nini? siasa hizi za ajabu!


Ngoja nimsaidie kujibu. Alidhani kule CDM kuna fedha za kifisadi. Alipoonekana lengo lake ni hilo akatimuliwa. CCM sasa anaganga njaa kwa kuwa hana pa kwenda. Jambo baya sana ni kwamba hajui anatumika. Anadhani anaweza kubahatisha viti maalum kwama Mbatia. Amechelewa. Too bad!
 
Ili uweze kuchangia vizuri mada yoyote ile ni vizuri kusikiliza na kuelewa vizuri kinachojadiliwa. Hoja ya msingi ya madai ya CHADEMA ilikuwa kuingiliwa kwa mchakato wa Tume ya kukusanya maoni ya Katiba mpya. Jibu hapa linapaswa kuwa Tume imeingiliwa au la haikuingiliwa. Hoja ya pili ni kukubaliana na mapendekezo ya Tume ya kukusanya maoni ya Katiba. Hizi ni hoja mbili tofauti yaani kuingiliwa kwa mchakato na mapendekezo ya Katiba. Kama CHADEMA wangesema wanaukubali mchakato lingekuwa jambo jingine lakini wanayakubali mapendekezo na sio mchakato.
Kwa mtu mweledi anaweza kusema kama chadema wanayakubali mapendekezo ya yaliyo kwenye Rasimu ya Katiba Mpya ni sawa na kuukubali mchakato mzima. Lakini huu unaweza kuwa ni mtazamo tu sio lazima uwe ndiyo ukweli wa mambo.
Mtu mwingine anaweza akaona hofu ya CHADEMA kuwa Tume ingependelea CCM ilikuwa hofu ya bure isiyokuwa na ukweli wowote. Tume itakuwa imejipambanua ( has proved chadema to be completely wrong) haiko kiitikadi au kichama kama walivyodhani CHADEMA iko kiuzalendo na kiinchi zaidi. CHADEMA, wangalikuwa waungwana walipaswa kuiomba radhi Tume kwa kuwa walivyowafikiria sivyo.
Hii pia haifuti ukweli kuwa mchakato iliingiliwa. Mchakato umeingiliwa, lakini Tume imeonyesha UKOMAVU zaidi kwa kusimamia ukweli. Wanataaluma walioko kwenye taaluma wameheshimu taaluma zao zaidi kuliko kuheshimu matakwa ya walioko kwenye madaraka ya kisiasa au kichama. Katika nchi ya Tanzania, mahali amapo wanataluma wengi wanauza taaluma zao kwa bei ya posho, cheo au kukubalika katika chama tawala, hakika wajumbe hawa wanapaswa kupewa Tuzo ya Nobel.
Lakini pia upinzani sio kupinga kila kitu hata kizuri. Mtu makini hawezi kupinga jambo kwa sababu tu jana alipinga hata pale ambapo mazingira,yamebadilika. Ukifanya hivyo utakuwa hujui ulikuwa unapinga nini hasa.
mbowe mimi sishangai anavyofanya mbowe simshangai yeye hufanya siasa za kuvizia na kuangalia aegemee wapi ila hana uwezo wa kuanziha hoja na akaitetea kwa mifano yenye mashiko.
 
mbowe mimi sishangai anavyofanya mbowe simshangai yeye hufanya siasa za kuvizia na kuangalia aegemee wapi ila hana uwezo wa kuanziha hoja na akaitetea kwa mifano yenye mashiko.

Inawezekana ukawa sahihi. Ila mimi ninachoamini, Mbowe ni kiongozi aliyeweza kukijenga na kukiimarisha chama chake kuliko viongozi wote katika uhai wa siasa za vyama vingi Tanzania. Nadhani ni fursa ya Mwampamba nae kujipanga huko aliko kukijenga chama chake kipya
 
Wana-Jukwa,
Mh.Freeman Mbowe jikague hapo ulipo,Safisha ubongo wako kwanza ndipo usimame kuongea.Ninachojua sio ujinga kuuliza,Mbowe unanafasi ya kujiuliza kwa viongozi wenzako wa kisiasa na hata wale wasio wa kisiasa namna ya kuchambua mambo na kuja na kauli moja ya kusimamia. Bila kufanya hivyo ipo siku Mh.Freema Mbowe utajikuta mtupu mbele ya haraiki ya watanzani,ikumbukwe njia ya Muongo ni fupi.

Ni maono yako. Nakushauri ungafikiria jinsi ya kujenga chama chako na wala sio kuijenga chadema ambayo kwa sasa haikuhusu
 
umenena mtoa mada nami naongeza ni Mbowe huyu huyu nje ya jimbo lake hai anawakataza wananchi kuchangia shughuli za maendeleo kama madawati,kujenga madarasa nk.lakini akiwa hai ndiye anaongoza kuchangia na ubambuaji(kuwachukulia mali wasio shiriki) huyo ndiye mbowe tajiri anajita masikini adharani bila aibu,zama zako kuumbuka zaja
 
Kwani chadema ni chama chake au cha wnanchi...sasa kama wananchi wanataka mchakato wa katiba uendelee yeye atasusia nini....Alafu wewe ni mjinga hatakama unahoja ujifunze kuandika kwa heshima sio kwa dharau....wewe unamalezi gani wewe...?
 
ALICHOKUA ANAKIPINGA Mh. Mbowe ni MCHAKATO wa katiba hasahasa uchaguzi wa mabalaza ya katiba, kitu ambacho si mbowe tu anakipinga ila hata wanaharakati na watanzania wengi pia tulikipinga!,

ANACHOKIUNGA MKONO mheshimiwa mbowe ni RASIMU ya katiba kwa kuwa maoni mengi waliyoyapendekeza kama CDM yamejumuishwa kitu ambacho hata watanzania wengi wakiwemo wanaharakati pia wanakiunga mkono!,.

Mh. Mbowe asingekua na sababu ya kupinga rasimu ya katiba kwa sababu tu alipinga mchakato wake!, sometimes what matters is not the PROCESS but the OUTPUT.
 
Hakuna hoja hapo ni majungu tu, hivi kusema kuwa chadema hawataunga mkono mchakato wa katiba usipoenda sawa ni kosa? Ina maana ulitaka waendelee na msimamo wa awali hata kama mambo yalirekebishwa? Hata ile issue ya mbowe na chadema kupinga posho na baada ya kukataliwa na wabunge wa ccm kuunga mkono hoja sio kosa la chadema kuendelea kuchukua posho hizo. Ninachoona ni tatizo la mtoa hoja kuonesha chuki ya wazi na chadema pamoja na mbowe! Hoja hii haina tafakuri ya kutosha. Ni vitu vya kuungaunga tu!
 
Kama ungewahi kukumbana na Mbowe enzi zake kwenye mitaa ya London, hata usingepatwa na shock kwa kauli zake na matendo yake.

Mbowe ni mfanyabiashara, Mwelekeo wake kibiashara umempelekea kujikuta yuko kwenye siasa by default.

Kuna kauli aliitoa ambapo amesema hatakuwa mwenyekiti wa CHADEMA next internal election. Hata hivyo, kikikolea, utamuona tena akigombea umwenyekiti wa CDM Taifa.

Huyu ndiye check bob Mbowe wa enzi zake. Ndiyo maana haishangazi kwa wanaomfahamu kwa yeye kuwa form six failure.
 
Today i've passed through a lot of comments from JF members supporting and even writing harsh words to support the views and ideas of CDM chairperson Freeman Mbowe regarding the 3 tier gov't and many other issues as written in the 1st draft of URT constitution of 2013..........the beauty of JF is, if only Mbowe criticized the draft, the picture wud've been very different today, with a lot of JF members criticizing the draft.......with this kind of speed...we'll never build Tanzania we are all dreaming of..........it must reach a point where a Tanzanian whether educated or not, stands for something they believe in and not standing for something that someone else is believing in........the point which people will give out positive comments that will shift Tz from this position to a better one.......viva Tanzania......lets all read the draft, ensure ourselves that we've understood it form line to line....then, we can comment....b'se at the end of the day, it must be our individual ideas that will write the constitution, and not MBOWE'S, KIKWETE'S, MBATIA'S, MREMA'S, LIPUMBA'S OR any other political leader's ideas......its us, present generation that will be accountable for the to be formed and written constitution..........
 
Back
Top Bottom