Wakati mwingine ni kheri kuachwa kuliko kuacha. Kama atarudisha pesa zako basi kweli atakuwa amekuchoka, lakini kama atapiga kimya kujifanya amekuacha ha ha ha ha huyo atarudi tu nakuhakikishia atarudi tu! Wakati mwingine tamaa za kutaka vitu vidogo kwa muda mfupi siku zote huwa zinawafanya watu wakose vitu vingi. Me nimekuwa na mahusiano na mwanamke mmoja hivi; ameniacha kwa style kama hiyo hiyo baada tu ya kumpa kiasi fulani cha pesa maana kuna mipango tulikuwa tumeipanga. Aisee chukua tahadhari hawa watu wakiamua kukuacha wanasahau yote na huwa wanajiona wajanja sana, ukipiga simu hazipokelewi wala messages hazijibiwi. Me baada ya siku 2 kupita nilimtumia meseji moja kali ikamchoma, siku hiyo alinijibu kwa ufupi tu "sikutaki". Nilikubaliana na majibu yake japo maumivu makubwa yalikuwa kwenye pesa zangu tu, nimetapeliwa... Kwa kweli sikuweza kukaa kimya nilimchana ukweli najua ulikuwa unamuingia, basi akajidai eti pesa zako nitakutumia ila mpaka leo kimya na mimi wala sijamtafuta tena nimesamehe!