Shunie
JF-Expert Member
- Aug 14, 2016
- 157,081
- 464,065
- Thread starter
- #141
SEHEMU YA 40...
Saa tisa ya usiku bibi Nyanjige akikimbia uchi wa mnyama katikati ya pori kuelekea asikokujua, alishangaa kuona helkopta tatu zikitokea juu yake “Mungu wangu wamekuja tena?”
Bibi Nyanjige aliziona helkopta za jeshi zikielekea upande wake bila shaka alijua zilikuwa zikimfuata yeye!
“Hawaniwezi na nitawamaliza mpaka wajute kwanini walimuua mama yangu!”Aliwaza bibi Nyanjige.
Alikitupa kichwa cha mtu alichokuwa nacho na kuinama akaweka mikono yake chini akaanza kutembea kama Sokwe kwa miaka mingi aliyoishi porini na wanyama alijua muondoko wa kila mnyama! Ilikuwa si rahisi kumtofautisha na Sokwe halisi.
Alizidi kutokomea katikati ya vichaka huku helkopta zikimmulika kwa mwanga mkali wa taa uliofanya usiku porini kuonekana kama mchana, mwanga huo ulimtia hofu na kumfanya aamue kujiangusha ardhini na kunyooka wima kama mti.
Marubani walipomulika na taa zao walimwona kama kipande cha mti kilichounguzwa na moto! Ilikuwa si rahisi hata kidogo kuamini walichokiona ardhini kilikuwa binadamu! “Najipumzisha ila hali ikitulia nitaendelea!” Aliwaza bibi Nyanjige.
Alibaki amelala eneo hilo kwa muda wa masaa zaidi ya mawili, hali ilipotulia alinyanyuka na kuanza kutembea taratibu akisonga mbele kwenda mahali kusikojulikana, lengo lake likiwa kufika Serengeti.
Alitembea kwa usiku mzima bila kufika au kutokezea barabarani,kulipokucha alishindwa kuendelea na safari yake kwa kuhofia kukamatwa na kuamua kujificha chini ya kichaka akisubiri usiku mwingine uingie ndio aendelee.
“Nitatembea kila siku usiku kama Bundi na asubuhi nitajificha vichakani hadi nifike ninakokwenda, ninajua ninasakwa sana lakini hawatanikamata hata siku moja!” Bibi Nyanjige aliongea peke yake huku akitetemeka kwa baridi ndani ya kichaka alichojificha.
Alikuwa bado hajakata tamaa na hakutaka kufanya hivyo, alikuwa na matumaini ya kujinasua kutoka mikononi mwa kifo kilichokuwa kimemzunguka! Usiku ulipoingia alitoka kichakani na kuendelea na safari yake, hiyo ndiyo ikawa staili yake ya safari!
Kwa siku kama tatu alitembea usiku na mchana alijificha kichakani.Njaa haikumsumbua sana kwani alishazoea maisha ya porini, alikula matunda na majani ya miti.
Saa tisa ya usiku bibi Nyanjige akikimbia uchi wa mnyama katikati ya pori kuelekea asikokujua, alishangaa kuona helkopta tatu zikitokea juu yake “Mungu wangu wamekuja tena?”
Bibi Nyanjige aliziona helkopta za jeshi zikielekea upande wake bila shaka alijua zilikuwa zikimfuata yeye!
“Hawaniwezi na nitawamaliza mpaka wajute kwanini walimuua mama yangu!”Aliwaza bibi Nyanjige.
Alikitupa kichwa cha mtu alichokuwa nacho na kuinama akaweka mikono yake chini akaanza kutembea kama Sokwe kwa miaka mingi aliyoishi porini na wanyama alijua muondoko wa kila mnyama! Ilikuwa si rahisi kumtofautisha na Sokwe halisi.
Alizidi kutokomea katikati ya vichaka huku helkopta zikimmulika kwa mwanga mkali wa taa uliofanya usiku porini kuonekana kama mchana, mwanga huo ulimtia hofu na kumfanya aamue kujiangusha ardhini na kunyooka wima kama mti.
Marubani walipomulika na taa zao walimwona kama kipande cha mti kilichounguzwa na moto! Ilikuwa si rahisi hata kidogo kuamini walichokiona ardhini kilikuwa binadamu! “Najipumzisha ila hali ikitulia nitaendelea!” Aliwaza bibi Nyanjige.
Alibaki amelala eneo hilo kwa muda wa masaa zaidi ya mawili, hali ilipotulia alinyanyuka na kuanza kutembea taratibu akisonga mbele kwenda mahali kusikojulikana, lengo lake likiwa kufika Serengeti.
Alitembea kwa usiku mzima bila kufika au kutokezea barabarani,kulipokucha alishindwa kuendelea na safari yake kwa kuhofia kukamatwa na kuamua kujificha chini ya kichaka akisubiri usiku mwingine uingie ndio aendelee.
“Nitatembea kila siku usiku kama Bundi na asubuhi nitajificha vichakani hadi nifike ninakokwenda, ninajua ninasakwa sana lakini hawatanikamata hata siku moja!” Bibi Nyanjige aliongea peke yake huku akitetemeka kwa baridi ndani ya kichaka alichojificha.
Alikuwa bado hajakata tamaa na hakutaka kufanya hivyo, alikuwa na matumaini ya kujinasua kutoka mikononi mwa kifo kilichokuwa kimemzunguka! Usiku ulipoingia alitoka kichakani na kuendelea na safari yake, hiyo ndiyo ikawa staili yake ya safari!
Kwa siku kama tatu alitembea usiku na mchana alijificha kichakani.Njaa haikumsumbua sana kwani alishazoea maisha ya porini, alikula matunda na majani ya miti.



