Huwezi Kuua Maiti -Erick Shigongo

Huwezi Kuua Maiti -Erick Shigongo

SEHEMU YA 40...

Saa tisa ya usiku bibi Nyanjige akikimbia uchi wa mnyama katikati ya pori kuelekea asikokujua, alishangaa kuona helkopta tatu zikitokea juu yake “Mungu wangu wamekuja tena?”

Bibi Nyanjige aliziona helkopta za jeshi zikielekea upande wake bila shaka alijua zilikuwa zikimfuata yeye!
“Hawaniwezi na nitawamaliza mpaka wajute kwanini walimuua mama yangu!”Aliwaza bibi Nyanjige.

Alikitupa kichwa cha mtu alichokuwa nacho na kuinama akaweka mikono yake chini akaanza kutembea kama Sokwe kwa miaka mingi aliyoishi porini na wanyama alijua muondoko wa kila mnyama! Ilikuwa si rahisi kumtofautisha na Sokwe halisi.

Alizidi kutokomea katikati ya vichaka huku helkopta zikimmulika kwa mwanga mkali wa taa uliofanya usiku porini kuonekana kama mchana, mwanga huo ulimtia hofu na kumfanya aamue kujiangusha ardhini na kunyooka wima kama mti.

Marubani walipomulika na taa zao walimwona kama kipande cha mti kilichounguzwa na moto! Ilikuwa si rahisi hata kidogo kuamini walichokiona ardhini kilikuwa binadamu! “Najipumzisha ila hali ikitulia nitaendelea!” Aliwaza bibi Nyanjige.

Alibaki amelala eneo hilo kwa muda wa masaa zaidi ya mawili, hali ilipotulia alinyanyuka na kuanza kutembea taratibu akisonga mbele kwenda mahali kusikojulikana, lengo lake likiwa kufika Serengeti.

Alitembea kwa usiku mzima bila kufika au kutokezea barabarani,kulipokucha alishindwa kuendelea na safari yake kwa kuhofia kukamatwa na kuamua kujificha chini ya kichaka akisubiri usiku mwingine uingie ndio aendelee.

“Nitatembea kila siku usiku kama Bundi na asubuhi nitajificha vichakani hadi nifike ninakokwenda, ninajua ninasakwa sana lakini hawatanikamata hata siku moja!” Bibi Nyanjige aliongea peke yake huku akitetemeka kwa baridi ndani ya kichaka alichojificha.

Alikuwa bado hajakata tamaa na hakutaka kufanya hivyo, alikuwa na matumaini ya kujinasua kutoka mikononi mwa kifo kilichokuwa kimemzunguka! Usiku ulipoingia alitoka kichakani na kuendelea na safari yake, hiyo ndiyo ikawa staili yake ya safari!

Kwa siku kama tatu alitembea usiku na mchana alijificha kichakani.Njaa haikumsumbua sana kwani alishazoea maisha ya porini, alikula matunda na majani ya miti.
 
Tutaonana kesho.......
 
  • Thanks
Reactions: Lee
SEHEMU YA 38...

“Hii hapana! Tunakwenda nayo Dar es Salaam makao makuu ni lazima tuipelekea hospitali kuu ya Jeshi ili wakubwa waione tena usiku wa leo hii hii! Maana huyu bibi aliisumbua sana dunia!”
“Sasa wataamimi vipi bila kichwa?”

“Alama zote zipo, hii cheni yake imeandikwa jina lake si unaona!” Alisema askari mmoja na akamwonyesha askari mkufu ulioandikwa neno Nyanjige walioukuta shingoni mwa maiti!
“Na hata hizi nguo alizovaa ndio zake kabisa!” Alisema askari huyo.

Magari yote yaliondoka moja likiwa kimbeba maiti zote kuelekea hospitali ya Tumbi na gari jingine la polisi likiwa limebeba maiti moja lilielekea Dar es Salaam! Gari hilo la polisi halikusimama Chalinze lilinyoosha moja kwa moja kuelekea jijini Dar es Salaam ambako lilifika baada ya kama dakika arobaini na tano!

Maiti ilipelekwa moja kwa moja hadi chumba cha maiti cha hospitali ya jeshi ambako usiku huohuo wakuu wa jeshi walifika na kuanza kuikagua maiti hiyo.
“Jamani mna uhakika huyu mliyemleta ni bibi Nyanjige kweli?”

“Ni yeye afande si mnaona hata huu mkufu wake afande!!”
“Hebu niuone!” Afande Mwita Mitiro aliuomba mkufu huo, alipokabidhiwa alianza kuukagua, alipoliona jina la Nyanjige kwenye mkufu huo hata yeye aliamini ulikuwa ni mwili wa bibi Nyanjige.
Mbona fupi sana hii
 
SEHEMU YA 22...

Huku akitetemeka bibi Nyanjige alinyata taratibu na kuizunguka kwa mara ya pili kabati kuelekea upande mwingine ili kumkwepa muuguzi akapanda kwenye ngazi na kulala katikati ya maiti mbili bila muuguzi kugundua, alimwona muuguzi akiendelea kufagia kuizunguka kabati, bibi alijua kama angebaki nyuma ya kabati ni lazima angekamatwa.


“Mungu amesaidia swali ni kwamba
nitatokaje humu ndani?” Alijiuliza bibi Nyanjige bila kupata jibu.
Alitaka sana kutoka chumba cha maiti mapema kabla maiti za wanajeshi hazijakaguliwa asubuhi hiyo jambo ambalo kwa uhakika alijua lingehatarisha usalama wake! Kwa idadi kubwa ya vifo vya wanajeshi alivyosababisha alikuwa mtu aliyesakwa kuliko hata gaidi Carlos!


Baada ya kumaliza kufagia muuguzi alitoka nje na kuufunga mlango wa chumba cha maiti nyuma yake na giza likarejea tena! Bibi Nyanjige aliutumia muda huo kuvua nguo za kijeshi alizokuwa nazo mwilini mwake na kubaki na gauni lake la kawaida, alizitupa nguo hizo sakafuni na kuendelea kulala katikati ya maiti akizidi kutafakari njia ya kujiokoa na kifo kilichokuwa mbele yake.

Mara mlango ulifunguliwa safari hii hakuingia muuguzi peke yake aliongozana na kundi la wanaume kumi na mbili.
“Maiti yenu ipo palee kwenye zile ngazi pembeni ya kabati!” Alisema muuguzi huku akizionyesha maiti ambazo bibi Nyanjige alilala katikati yake! “Hapa lazima nijikaushe vinginevyo mtu mzima nitaabika!” Aliwaza bibi wakati wanaume wale wakizidi kuikaribia ngazi aliyolala.

“Nyie wanaume hebu mmoja wenu aje atie kwanza saini kwenye kitabu cha kuchukulia maiti yenu!” Muuguzi aliwaeleza na wanaume wote walisita na mmoja wao alikwenda hadi kwenye meza na kutia saini kwenye kitabu!
“Haya nendeni mkachukue zipo maiti mbili moja ndiyo yenu!”
“Sawa!”

Wanaume hao waliondoka kuelekea kwenye ngazi na walipozifikia walishangaa kuona kukuta kuna maiti tatu moja ya mwanamke ikiwa imelala katikati ya maiti mbili na sakafuni kukiwa na mavazi ya kijeshi!
“Nesi!”
“Mnasemaje?”
“Mbona kuna maiti tatu wakati wewe umesema ni mbili?”
Njaa je?
 
Shunie baby, hebu shusha nondo usinilazimishe niende msata kilingeni niombe msaada wakukaushe usingizi ili ukeshe unashusha nondo tu
 
Back
Top Bottom