Microgynon
JF-Expert Member
- May 16, 2015
- 853
- 1,068
Nimeshakuja na huku
Cc.shunie
Cc.shunie
NzuriSEHEMU YA 03...
Ilikuwa si rahisi kumwona bibi Nyanjige kwa ulinzi mkali uliokuwepo nyumbani kwake porini, nyumba yake ilizungukwa na Tembo wasiopungua kumi, waliomlinda usiku na mchana! Wazungu wengi waliojaribu kumfikia ili kupata picha yake waliuawa kwa kunyangwa na Tembo!
Mzungu mmoja aliyekwenda porini kwa helkopta alifanikiwa kuipata picha ya bibi Nyanjige akiwa katikati ya tembo!
Ni picha hiyo iliyoleta matatizo kwani ilipochapishwa katika magazeti na majarida mbalimbali nchini Uingereza na Marekani serikali ya Tanzania ilishtuka na kuamini kuwa mtu aliyekuwa akitafutwa alikuwa porini nchini Kongo.
Bila kuchelewa ilituma wanajeshi wapatao ishirini waliopewa msaada na askari wengine kumi wa Kongo! Walifika hadi msituni lakini hawakufanikiwa kumkamata bibi Nyanjige na pia hawakufanikiwa kurudi salama nyumbani! Wote walikufa kifo hichohicho cha kukanyagwa na Tembo!
Mpaka mwezi moja baada ya askari hao kuondoka hapakuwa na mawasiliano yoyote kutoka msituni, simu zao za upepo ziliendelea kuita bila majibu! Hilo lilionyesha wazi watu hao hawakuwa hai!
Ilibidi serikali za Tanzania na Kongo kwa kushirikiana ziandae jeshi kubwa lenye askari wasiopungua elfu tano waondoke kwenda msituni kumsaka bibi Nyanjige!
Maaskari wote 5000 walilizunguka pori wakiwa na silaha kali mikononi mwao na ndege za kivita zilipita angani!
Askari ndani ya ndege hizo walipoangalia chini ka kutumia viona mbali waliziona maiti za askari wenzao zikiwa ardhini na tembo wengi wakiwa wamezunguka kibanda kidogo kilichoonekana kuwa kama nyumba.
Ghafla mamia kwa maelfu ya ndege walionekana angani, hawakujulikana walikotokea! Wengi walitua kwenye vioo vya mbele vya ndege hizo na kuwafanya marubani washindwe kuendesha ndege zao vizuri kwa sababu hawakuona mbele.
“Tufanya nini sasa?”
“Turudi tukatue kwanza, vinginevyo hawa ndege watasababisha tuangushe ndege ni wengi mno na sielewi wametoka wapi!”
“Sawa geuza basi!”
Wakati wanageuza ndege nyingine ilishafika karibu yao ikipita katikati ya makundi ya ndege, zote mbili ziligongana na kuwaka moto zikiwa angani! Askari waliokuwa wakitembea kwa miguu walishangaa kuona ndege zikigongana.
Inaendelea.
Asante shunie. Ila huyu bibi sitaki akamatwe kwanza. Maana ana vituko
Love youAbeeh
Njoo mamii kuna kitu nataka unisaidieAbeeeh babe
Nakuja unipe namba uwe unanipa wasapa ila Juliana ndo naikubali fanya kweli naisubiri Mama!Ungekuja tu jaman