Wanafunzi wa chuo kikuu cha Mtakatifu Augustine wamekuwa wakishuhudia wizi mkubwa wanaofanyiwa na chuo hiki huku zaidi ya millioni 700 zikiliwa mbele ya macho yao.
Serikali ilianzisha mpango wa wanafunzi wa vyuo vikuu kuwa na Bima ya Afya kwa lengo zuri na kuwasaidia watoto wa wakulima kuweza kuapata huduma ya afya kwa unafuu kwa taratibu za NHIF ghalama za Bima kwa mwanafunzi ni Tsh 54,000 lakini SAUT wanawaibia hawa watoto wa masikini kwa kuwalipisha 100,000 kwa kila mtu kwa SAUT hii nafasi imekuchukuliwa kama nafasi ya kuwanehemesha baadhi ya wafanyakazi wa chuo hiki mwaka wa masomo 2017/2018 chuo chenye wanafunzi zaidi ya 8000 waliopata kadi za Bima hawakuzidi 1000 na wengine hawakupata huku wakiwa wamelipia kila mtu kiasi cha shilingi laki moja tena kwa lazima hata kwa ambao wanamiliki Bima za wazazi wao sijui huu mpango kama ni lazima au hiari ya mtu mbaya zaidi hata hao waliopata kadi hazikufanya kazi kutokana na kutolipiwa.
Katika mwaka huu wamasomo zoezi limeendelea vile vile watu wana kadi za bima za wazai wao ajabu wanalazimishwa kulipia tena bima huku wale ambao hawakupata mwaka jana wakilazimishwa kulipia tena huku pesa zao za mwaka jana zikiwa hazina majibu kuwa ziko wapi na zilifanya kazi gani?
PENALTY
Hapa pia kwenye penalty kumekuwa na wizi wa makusudi joining instruction ya SAUT inaonesha ulipaji wa Ada ni mara mbili kwa sermister lakini wadogo zetu wamekuwa wakifaniwa ndivyo sivyo Mdogo wangu karipoti chuo mwezi wa pili tu analazimishwa kulipa 911,000 ikipungua hata 100 anapigwa penalty ya laki moja na huu mchezo umekuwa endelevu jamani.
Baraza la Maaskofu sidhani kama alianzisha chuo hiki kuwaumiza watoto wa masikini bali ilikuwa kuwasaidia badala yake imekuwa ni maumivu mtu hana mkopo anajisomesha kwa kuungaunga halafu unampiga penalty huku ukimnyima hata kufanya mtihani.
Madogo wanatazamia kuanza mitihani Jumatatu lakini naambiwa wengi hawajapata kadi za mitihani sababu ikiwa ni penalty huku wengine system lao bovu likiwa linaonyesha wanadaiwa lakini hawadaiwi.
Jamani hebu tuhurumieni tunaosomesha tunaumia acheni hizi mambo.
Serikali ilianzisha mpango wa wanafunzi wa vyuo vikuu kuwa na Bima ya Afya kwa lengo zuri na kuwasaidia watoto wa wakulima kuweza kuapata huduma ya afya kwa unafuu kwa taratibu za NHIF ghalama za Bima kwa mwanafunzi ni Tsh 54,000 lakini SAUT wanawaibia hawa watoto wa masikini kwa kuwalipisha 100,000 kwa kila mtu kwa SAUT hii nafasi imekuchukuliwa kama nafasi ya kuwanehemesha baadhi ya wafanyakazi wa chuo hiki mwaka wa masomo 2017/2018 chuo chenye wanafunzi zaidi ya 8000 waliopata kadi za Bima hawakuzidi 1000 na wengine hawakupata huku wakiwa wamelipia kila mtu kiasi cha shilingi laki moja tena kwa lazima hata kwa ambao wanamiliki Bima za wazazi wao sijui huu mpango kama ni lazima au hiari ya mtu mbaya zaidi hata hao waliopata kadi hazikufanya kazi kutokana na kutolipiwa.
Katika mwaka huu wamasomo zoezi limeendelea vile vile watu wana kadi za bima za wazai wao ajabu wanalazimishwa kulipia tena bima huku wale ambao hawakupata mwaka jana wakilazimishwa kulipia tena huku pesa zao za mwaka jana zikiwa hazina majibu kuwa ziko wapi na zilifanya kazi gani?
PENALTY
Hapa pia kwenye penalty kumekuwa na wizi wa makusudi joining instruction ya SAUT inaonesha ulipaji wa Ada ni mara mbili kwa sermister lakini wadogo zetu wamekuwa wakifaniwa ndivyo sivyo Mdogo wangu karipoti chuo mwezi wa pili tu analazimishwa kulipa 911,000 ikipungua hata 100 anapigwa penalty ya laki moja na huu mchezo umekuwa endelevu jamani.
Baraza la Maaskofu sidhani kama alianzisha chuo hiki kuwaumiza watoto wa masikini bali ilikuwa kuwasaidia badala yake imekuwa ni maumivu mtu hana mkopo anajisomesha kwa kuungaunga halafu unampiga penalty huku ukimnyima hata kufanya mtihani.
Madogo wanatazamia kuanza mitihani Jumatatu lakini naambiwa wengi hawajapata kadi za mitihani sababu ikiwa ni penalty huku wengine system lao bovu likiwa linaonyesha wanadaiwa lakini hawadaiwi.
Jamani hebu tuhurumieni tunaosomesha tunaumia acheni hizi mambo.