Huu Wimbo wa "Kuchapiwa ni SIRI ya Ndani"

Huu Wimbo wa "Kuchapiwa ni SIRI ya Ndani"

Hakika hata mimi hayo maneno huwa siyaelewi kabisa sijui ni kwa vile sikukaa na wazee wanieleze misemo ya kikubwa kama huo.
 
HAYA MANENO MBELE ZA WAKWE LAZIMA UJIFANYE KIKOHOZ KIMEKUSHIKA ILI YASISIKIKE!

'Ai haya maneno walinena wazee wa zamani ii…..
Ukiwa Mjanja kuchapiwa ni siri ya ndani
Haya maneno walinena wazee wa zamani ii…..
Ukiwa Mjanja kuchapiwa ni siri ya ndani'
 
Mimi naona kinachowaudhi ni ile thought ya kuchapiwa; maana kuna nyimbo far worse than this hamlalamiki.

kuna nyimbo zimeimbwa na wanamuziki wazee wa zamani zina maneno machafu kuliko hili la kuchapiwa.....
 
Wimbo hauna maana hata kidogo sina mke ila ulinifanya nimfukuze ndani mpenzi wangu maana kwa ufahamu wa kawaida hakuna anayeweza kuvumilia na kuona ni siri ya ndani kuchapiwa.
Msingi kiuno→→ unamjibu nini mtu juu ya usemi huu kiuno kinakuwa vp ili kiweze kukupa mtaji hapa mjini kama siyo ku promote zinaa
 
Sio kwa approach hii ya kubomoa mkuu

Kusema ukweli ndiyo kubomoa? Kwani ni siri wake za watu hawachapwi nje ya ndoa zao? Rate imekuwa kubwa kiasi ya kwamba kuliko kutoa siri ni bora kuvumilia kama wanawake wanavovumilia wanaume zao wakichapa nje!
Mavoko anataka kufundisha wanandoa usiri wa ndani wa ndoa zao kuepusha kuvunjika kwa ndoa lukuki!
 
Naomba nieleweshwe vizuri
  1. Ni kweli haya maneno walisema wazee wa zamani?
Hajatuambia ni wazee gani! Inaweza kuwa kweli kuna wazee walisema hivyo. Si ni kama wale waliosema "kitanda hakizai haramu" tu?

2.Huu wimbo una maadili hasa kuimbwa na watoto?
La hasha! Hatutegemei watoto wazungumzie habari za "kuchapa" na "kuchapiwa". Waimbaji wa wimbo huo ni watoto?

..Ni kweli kuchapiwa ni SIRI ya Ndani? kivipi?
Sasa kama ukichapiwa (say "mkeo") unaenda kuutangazia ulimwengu kuwa umechapiwa/unachapiwa? Labda kama umeamua kutoa talaka pia!

4.Wapi mamlaka?
Sio rahisi kuchukua hatua kwa kuwa neno lililotumika tayari lililenga kupunguza ukali wa neno halisi la kitendo ambacho mtunzi alikusudia. Au pengine mtunzi anataka kutuambia umuhimu wa kuvumiliana na kutunza siri katika mahusiano/ndoa?
 
Mimi naona kinachowaudhi ni ile thought ya kuchapiwa; maana kuna nyimbo far worse than this hamlalamiki.

naona hapo umegongea msumari haswa. ningekiona kitufe cha like ningekugongea.
huu wimbo unachoma watu haswa! hilo wazo la kuchapiwa limekuwa msumari haswa.
mbona wimbo wa mwana fa "bado nipo nipo" watu hawakulalamika?
wimbo wa ali kiba na jay dee "single boy" mbona watu walikaa kimya"

huu wimbo unafundisha watu ndoani uvumilivu. siku hizi unakuta watu wanafumania wenzi wao wanaita na wapiga picha ili stori itoke na shigongo auze. hivyo mnakumbushwa ukichapiwa fanya siri uyamalize na mwenzi wako. "muungwana akivuliwa nguo huchutama".
 
naona hapo umegongea msumari haswa. ningekiona kitufe cha like ningekugongea.
huu wimbo unachoma watu haswa! hilo wazo la kuchapiwa limekuwa msumari haswa.
mbona wimbo wa mwana fa "bado nipo nipo" watu hawakulalamika?
wimbo wa ali kiba na jay dee "single boy" mbona watu walikaa kimya"

huu wimbo unafundisha watu ndoani uvumilivu. siku hizi unakuta watu wanafumania wenzi wao wanaita na wapiga picha ili stori itoke na shigongo auze. hivyo mnakumbushwa ukichapiwa fanya siri uyamalize na mwenzi wako. "muungwana akivuliwa nguo huchutama".

Well said! na Mimi natafuta kitufe cha like nikupe BIG LIKE! Muungwana akivuliwa nguo....... = kuchapiwa ni top secret!
 
Wana JF idara husika zimekufa siku nyingi sna, nyimbo nyingi za sasa hazina maadili kbs, mbali na kuchapiwa siri ya ndani, je mnasemaje kuhusu video ya nyimbo ya FA na AY cheza bila kukunja godi, huyu mdada amevaa boxa alafu design yake imetengeneza bonde kati ya ---- na ----, huwezi angalia na watoto kbs
 
Mimi naona kinachowaudhi ni ile thought ya kuchapiwa; maana kuna nyimbo far worse than this hamlalamiki.

you are right my dear! wamechukizwa na neno kuchapiwa ni siri ya ndani, maana wanaogopa sana hiyo kitu ya kuchapiwa.
kama ni maadili, kuna nyimbo nyingi zipo nje ya maadili, pengine kuliko hata huu

ila pia ukiangalia kwa maisha ya zamani, ni kweli hakukuwa na maugomvi watu hawana mtoto, hayo mambo yalikuwa yanamalizwa kwa kwenda kuchuma dawa kwa mganga tu, tena mume ndio anampeleka mkewe, afu mke na mganga wanaenda chimba dawa wanakaa kama wiki/ mwezi porini wakirudi huko mama mjamzito
 
naona hapo umegongea msumari haswa. ningekiona kitufe cha like ningekugongea.
huu wimbo unachoma watu haswa! hilo wazo la kuchapiwa limekuwa msumari haswa.
mbona wimbo wa mwana fa "bado nipo nipo" watu hawakulalamika?
wimbo wa ali kiba na jay dee "single boy" mbona watu walikaa kimya"

huu wimbo unafundisha watu ndoani uvumilivu. siku hizi unakuta watu wanafumania wenzi wao wanaita na wapiga picha ili stori itoke na shigongo auze. hivyo mnakumbushwa ukichapiwa fanya siri uyamalize na mwenzi wako. "muungwana akivuliwa nguo huchutama".

pokea like yangu.. hilo neno kuchapiwa siri ya ndani ndilo linalowasumbua watu wengi. lkn wimbohauna tatizo. si kila unapohisi kuna kuvunjwa kwa uaminifu unatakiwa umwambie kila mtu... wenye busara huyamaliza kihekima, ndio maana haswa ya siri ya ndani, a wazee wa zamani walifanya hivyo.
 
Back
Top Bottom