Mlengo wa Kati
JF-Expert Member
- Feb 16, 2011
- 2,730
- 492
Polisi kamateni viongozi wa CHADEMA ni wahaini na wachochezi. Slaa anadai kuwa polisi mnatumiwa na CCM na amewahusisha na kukatwa mapanga na wabunge wa CHADEMA. Mnyika amesema hatuna serikali na kuwataka wananchi kushiriki kufanya mapinduzi kwa nguvu ya umma. Mbowe amesema watu waingie barabarani kutaka mafisadi wachukuliwe hatua. Huu wote ni uchochezi kinyume na utawala wa sheria.
.ndiyohiyo
kwa mtizamo wangu inaonekana dr slaa amewazoea sana polisi na kuwachukulia kama mashemeji zake eti tu kwa vile nae na chama chake cha chadema wanavaa makombati ya mgambo basi nao wanajiona kama polisi! siku moja nilikua dodoma hotel nasikia vijamaa vya chadema vinajiita eti kamanda! sasa nikamwangalia mnyika ukamanda kautoa wapi hata jeshi la mgambo hajawahi pata mafunzo! ndio maana dr slaa anaona polisi wako sawa kisa manguo yake ya khaki anayo vaaa!