Hussein Tuwa vs Eric Shigongo (Riwaya)

well hata mimi nimesoma hadithi mbili tu za Tuwa lakini nyingi sana za Shigongo. Mara ya mwisho kusoma hadithi hizo ilikuwa 2002, za shigongo ninazozikumbuka kama 'escape from rwanda', 'before i die the world should forgive me' na moja ya yule bibi aliyekuwa na uwezo wa kuongoza jeshi la wanyama na wadudu, ile novel yake ya kwanza, hiyo ya 'rais anampenda mke wangu sikuimalizia, kuna ile ya yule msichana mwenye mzimu wa lutego, kuna ya yule dogo aliyekuwa na akili akawa anagombaniwa na marekani na tz, kuna ya kolo na yule binti wa balozi, na nyinginezo nyingi.

Shigongo alikuwa(nadhani bado) anaandika hadithi nyingi sana katika magazeti yake(nafikiri kila siku ya wiki ana gazeti) kwa hiyo kufuatilia si jambo rahisi.

Kingine sisi Waswahili hatupendi kusoma vitabu/riwaya yaani ni wavivu mno. Kama Shigongo angeweza kuchapisha riwaya moja USA or UK angefika mbali sana kwani naona anawazidi kiuwezo wakina Rene Bravan Robinson(James H Chase), Sydney Sheldon, John Grisham, Jeanne Rowling, Danielle Steel, Jilly Cooper, Dan Brown. Kwani yeye novel zake haziko typecast sio za aina moja kwani kwa Sydney Sheldon mara nyingi kunakuwa na mwanamke ambaye anakuwa na nguvu sana, hapo hapo anakuwepo mwanaume ambaye yuko naye karibu ingawa ana malengo mabaya naye na mwisho wa novel mwanamke yule anaanguka au kushindwa katika jambo fulani, ingawa baadhi ya novel ziko tofauti na muundo huu kama 'are you afraid of the dark','the other side of me' na 'nothing last forever'. John Grisham novel zake zote ni zinahusiana na sheria zaidi. JK Rowling ni Harry Potter pekee(magic).

Shigongo ana kipaji cha kuelezea(story telling) lakini sidhani kama huwa anafanya utafiti wowote kabla ya kuandika novel yake. Kama angeweza angekuwa anafanya utafiti hata mwaka mzima kabla ya kuandika novel yoyote hizo za magazetini aachie watu wengine watumie jina lake kama pen name, yeye aandike moja ikiwezekana kwa kiingereza atafute publishers wa UK or USA. Kama atatengeneza jina ataweza kufikia mbali sio kukaa kugombana na kina chameleon.

Binafsi niliacha kusoma hadithi zake kwa sababu hazikuwa na quality kama zile za bestsellers wa nje, halafu alikuwa hatoi novel ya pamoja mpaka ukasome gazeti sasa unakuta j3-Ijumaa kila siku hadithi tofauti tofauti ufaitiliaji unakuwa mgumu.

Kwa upande wa Tuwa anajua sana storytelling bila haja ya kutaja vitu vigumu vigumu au sehemu za nje ya nchi, lakini ameandika hadithi chache kushindanisha na shigongo kwa hiyo labda alibahatisha au amekosa platform ya kuonesha kazi zake. Kwa hiyo kwa upande mmoja naona si sahihi kumlinganisa Tuwa na Shigongo ni kama vile kumlinganisha Dean Ashton na Wayne Rooney
Mkuu! Uthibitisho wa ubora wa utunzi wa vitabu Si sawa Na football player kwamba huwezi kuthibisha ubora wake kwa mechi moja, mtunzi bora WA story utamuona Tu toka anavyokushawishi uendelee kusoma toka page ya kwanza, Tuwa mpaka sasa Ana zaidi ya Novel 5 ambazo nimezisoma, kweli unashindwa kujua uwezo WA Mtunzi ambaye Ana Novel tano sokoni, Tuwa Ni bora kuliko Shigongo, hadithi zake ukiwa unasoma muda wote anamweka msomaji roho juu, Na style yake ya uandishi sio level za Shigongo!
 
hussein Tuwa ni mkali, hadithi zake zimetulia na ametumia akili, shigongo hana jipya hadithi zake zote zinafanana, hazihamasishi kusoma, na ukianza kusoma tu unapredict itakuaje maana matukio yafanana
Sometime akijua kuwa umejua itakavyoisha anabadiri gia angani, bas story inakuwa ya kusadikika
 
Acha kabisa Tuwa mzee wa taharuki ni habari nyingine kabisa. Shigongo anasubiri sana kwa Tuwa . Mkimbizi kuna huyu dada wa kuitwa TIGGA kila siku kwake ilikuwa taharuki mpaka unatamani hadithi isiishe.Namkubali sana Tuwa kuliko Shigongo though financially Shigongo yupo juu.
 
yani Hussein Tuwa ni mkalii alinifanya niache kusoma hadithi za shigongo.
Soma Mkimbizi, Mtuhumiwa na utata yani ni noma jamaa anajua sana sana.
Hivi willy Gamba aliishia wapi??
Alikufa mkuu aristabus elvis musiba.
 
Mmhh TUWA ni mtu matata sana .. Saana .. Ila shigongo anaonekana mkali kwa waswahili kwa kuwa ana miliki kampuni ya magazeti ambayo inampa nafasi ya kujitangaza zaidi
 
Kucompare watu maarufu si kitu kibaya, mara nyingi ni kuangalia mazuri na kuyaendeleza na yale mapungufu kuyarekebisha.

Kwenye suala la hadithi(riwaya) za magazetini, mimi nilijitahidi sana kufuatilia hadithi za Eric Shigongo(Ijumaa) na hadithi mbili tu za Hussein Hassan Tuwa(Mtuhumiwa na Mkimbizi).

Kwa maoni yangu, hadithi za Mr. Tuwa zilikuwa zina msisimko zaidi. Zilikuwa zinakupa nafasi ya muhusika kuwa kama ndiye uliyeko kwenye hadithi. Ilikuwa unapata picha kabisa.

Kwa maoni yangu naona Hussein Hassan Tuwa ni mtunzi mahiri na hodari kuliko Eric Shigongo.

Constructive comparison please!!

View attachment 66403
Mimi niliacha kisoma simulii za Erik shigongo pale lipotoa kitabu kikuuiuiibwa Cha rais anamtaa mke wangu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
well hata mimi nimesoma hadithi mbili tu za Tuwa lakini nyingi sana za Shigongo. Mara ya mwisho kusoma hadithi hizo ilikuwa 2002, za shigongo ninazozikumbuka kama 'escape from rwanda', 'before i die the world should forgive me' na moja ya yule bibi aliyekuwa na uwezo wa kuongoza jeshi la wanyama na wadudu, ile novel yake ya kwanza, hiyo ya 'rais anampenda mke wangu sikuimalizia, kuna ile ya yule msichana mwenye mzimu wa lutego, kuna ya yule dogo aliyekuwa na akili akawa anagombaniwa na marekani na tz, kuna ya kolo na yule binti wa balozi, na nyinginezo nyingi.

Shigongo alikuwa(nadhani bado) anaandika hadithi nyingi sana katika magazeti yake(nafikiri kila siku ya wiki ana gazeti) kwa hiyo kufuatilia si jambo rahisi.

Kingine sisi Waswahili hatupendi kusoma vitabu/riwaya yaani ni wavivu mno. Kama Shigongo angeweza kuchapisha riwaya moja USA or UK angefika mbali sana kwani naona anawazidi kiuwezo wakina Rene Bravan Robinson(James H Chase), Sydney Sheldon, John Grisham, Jeanne Rowling, Danielle Steel, Jilly Cooper, Dan Brown. Kwani yeye novel zake haziko typecast sio za aina moja kwani kwa Sydney Sheldon mara nyingi kunakuwa na mwanamke ambaye anakuwa na nguvu sana, hapo hapo anakuwepo mwanaume ambaye yuko naye karibu ingawa ana malengo mabaya naye na mwisho wa novel mwanamke yule anaanguka au kushindwa katika jambo fulani, ingawa baadhi ya novel ziko tofauti na muundo huu kama 'are you afraid of the dark','the other side of me' na 'nothing last forever'. John Grisham novel zake zote ni zinahusiana na sheria zaidi. JK Rowling ni Harry Potter pekee(magic).

Shigongo ana kipaji cha kuelezea(story telling) lakini sidhani kama huwa anafanya utafiti wowote kabla ya kuandika novel yake. Kama angeweza angekuwa anafanya utafiti hata mwaka mzima kabla ya kuandika novel yoyote hizo za magazetini aachie watu wengine watumie jina lake kama pen name, yeye aandike moja ikiwezekana kwa kiingereza atafute publishers wa UK or USA. Kama atatengeneza jina ataweza kufikia mbali sio kukaa kugombana na kina chameleon.

Binafsi niliacha kusoma hadithi zake kwa sababu hazikuwa na quality kama zile za bestsellers wa nje, halafu alikuwa hatoi novel ya pamoja mpaka ukasome gazeti sasa unakuta j3-Ijumaa kila siku hadithi tofauti tofauti ufaitiliaji unakuwa mgumu.

Kwa upande wa Tuwa anajua sana storytelling bila haja ya kutaja vitu vigumu vigumu au sehemu za nje ya nchi, lakini ameandika hadithi chache kushindanisha na shigongo kwa hiyo labda alibahatisha au amekosa platform ya kuonesha kazi zake. Kwa hiyo kwa upande mmoja naona si sahihi kumlinganisa Tuwa na Shigongo ni kama vile kumlinganisha Dean Ashton na Wayne Rooney
Usifananishe James A chase na watu wako wanaonunua riwaya

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hussein Tuwa kiboko...ile hadith ya mkimbizi, ilikuwa ukisoma Roh inakuwa juu juu....acha tu.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom