heshima kwenu wanajamvi
for the first team nimepata ticket ya fast jet nikagundua ni wasanii bora precision air yetu tulioizoea japokuwa inatuzingua sana..
Nimekata ticket ya mwanza next week kwa kujua zile swaga zao za kibegi kidogo, hamna vinywaji zipo kwenye ticket za bei rahisi tu kumbe tofauti..
Nimelipishwa 198 roundtrip ticket ya dar mwz ya next wekend so nikaanza kusoma terms and condition kwenye ticket zao nikakuta ni vile vile kama umelipa 32,000, kwanza ndege haina classes, pili wote mnachukuliwa kama mmelipa bei moja hakuna kitu kilicho tofauti..
Nikamdodosa dada aliyenikatia ticket akanikandamizia kubeba samaki hairuhusiwi.. Nikajuta mara mbili zaidi maana precision yangu niliacha ticket juzi ya 179 online, begi unabeba size ya kutosha tu, kwenye fast jet kila kitu kununua hata ukate ticket ya bei gani,,,
halafu wanachokera zaidi bei wanazoweka kwenye website zao ni xcluding other charges ili wakuvutie unapofanya malipo unakuta imepanda mbaya tofauti na precision..
Ngoja nikaingie ndani nione huduma zao zikoje but kwa jicho la kwanza wameshanikera na nitatumia precision kama kawaida, naona ni wazuri kuliko huyu kasuku anaejiita low cost airline...
Kabla hamjakata fast jet kuweni makini wadau, ni pasua kichwa mbaya hawa watu kila kitu unalipishwa...
Nilitamani niikatae ticket sema tu sikuwa na jinsi