Huduma bora za afya: Mbona bado wakina mama wanaojifungua wanalazwa hadi watatu kitanda kimoja?

Bushmamy

JF-Expert Member
Aug 18, 2019
8,848
15,252
Serikali yetu kupitia wizara ya Afya naona ipo busy na kampeni za chanjo za Uviko19 huku ikijisahaulisha huduma muhimu huko kwenye Hospital za serikali.

Jana nilienda kutembelea mama mmoja jirani yangu Alieenda kujifungulia Mt Meru hosp,na mtoto kuwekwa chumba cha joto kwa muda wa wiki mbili maana mtoto alizaliwa kabla ya Umri.

Nikiwa pale wodini naona wakina mama wamelala kwenye kitanda kimoja wengine wawili vitanda vingine hadi watatu pamoja na watoto wao wachanga ikabidi nimuulize yule mama jirani yangu nilienda kumsalimia, hapa mnalala Vipi wanawake wawili na watoto wenu ilhali vitanda ni vidogo? Akasema ndo hivyo hivyo hamna namna.

Basi nikiwa pale akaletewa Bill ya Hospital ambayo ilikuwa Tsh. Laki 300,000.
Nilivofika nilimkuta yupo na mumewe Na walikuwa tayari kuondoka ila baada ya bili kuja ikabidi waghairi kuondoka ili kesho aje amtoroshe mke wake maana hana namna kabisa ya kupata hiyo pesa.

Baada ya bili kuja alienda kuomba apunguziwe maana yeye ni kibarua tu mjini hapa hana Kazi na. Mkewe ni mama wa nyumbani.

Ombi hilo lilivogoma mwamba uamuzi aliouchukua ni kutoroka kukimbia bili.

Wizara ya afya tunaomba mfuatilie huko kwenye Hospital zenu boresheni huduma zenu na pia muweke viwango rafiki vya gharama kwa ajili ya wananchi wenu tafadhali
 
Ili uachane na kadhia hiyo... Pambana upate mshiko ukatibiwe Agha Khan.

Serikali haiwezi kukufanyia kila kitu. Serikali ni maskini kuliko wewe. Ina madeni kibao.... achana na ule uhuni wa "hela za ndani zipo". Ukinielewa utanishukuru
 
Ili uachane na kadhia hiyo... Pambana upate mshiko ukatibiwe Agha Khan.

Serikali haiwezi kukufanyia kila kitu. Serikali ni maskini kuliko wewe. Ina madeni kibao.... achana na ule uhuni wa "hela za ndani zipo". Ukinielewa utanishukuru
Ni wangapi wenye huo uwezo?
 
Serikali yetu kupitia wizara ya Afya naona ipo busy na kampeni za chanjo za Uviko19 huku ikijisahaulisha huduma muhimu huko kwenye Hospital za serikali.

Jana nilienda kutembelea mama mmoja jirani yangu Alieenda kujifungulia Mt Meru hosp,na mtoto kuwekwa chumba cha joto kwa muda wa wiki mbili maana mtoto alizaliwa kabla ya Umri.

Nikiwa pale wodini naona wakina mama wamelala kwenye kitanda kimoja wengine wawili vitanda vingine hadi watatu pamoja na watoto wao wachanga ikabidi nimuulize yule mama jirani yangu nilienda kumsalimia, hapa mnalala Vipi wanawake wawili na watoto wenu ilhali vitanda ni vidogo? Akasema ndo hivyo hivyo hamna namna.

Basi nikiwa pale akaletewa Bill ya Hospital ambayo ilikuwa Tsh. Laki 300,000.
Nilivofika nilimkuta yupo na mumewe Na walikuwa tayari kuondoka ila baada ya bili kuja ikabidi waghairi kuondoka ili kesho aje amtoroshe mke wake maana hana namna kabisa ya kupata hiyo pesa.

Baada ya bili kuja alienda kuomba apunguziwe maana yeye ni kibarua tu mjini hapa hana Kazi na. Mkewe ni mama wa nyumbani.

Ombi hilo lilivogoma mwamba uamuzi aliouchukua ni kutoroka kukimbia bili.

Wizara ya afya tunaomba mfuatilie huko kwenye Hospital zenu boresheni huduma zenu na pia muweke viwango rafiki vya gharama kwa ajili ya wananchi wenu tafadhali
Moumt Meru iko Arusha mjini. Mi nashauri msipeane mimba kama mnadhindwa kulipia bill ya laki 3 wakati sote tunajua hali halisi ya matibabu

Uzembe mwingine ni kwamba hiyo laki 3 ingetosha kabisa kulipia bima ya afya na tatizo hilo lisingetokea.

Kama umepewa option ya bima ya afya ambayo ni nafuu sana ukaipuuzia basi usimpe mimba mtoto wa watu kwa kukosa laki 3. Sasa kama huna laki 3 huyo mtoto utamtunzaje?

Kupata mtoto ni hiari... kumtunza ni lazima. Tujipange
 
kweli ni za serikali. wanaojifungua kawaida wanakaa watatu kitanda kimoja. wa upasuaji wawili kitanda kimoja
Sio.kweli my dear. Labda kama ulimaanisha hospital za serikali. Kuna private hospital wagonjwa wanatamani wabakie wodini mpaka wapone kuliko kwenda kuponea nyumbani
 
kweli ni za serikali. wanaojifungua kawaida wanakaa watatu kitanda kimoja. wa upasuaji wawili kitanda kimoja
Serikali yetu tunaijua. Hivi sasa ukitaka kupata mtoto lazima ukae mezani kupanga bajeti. Sasa kama unaamua kuzaa kea kutafuta umaarufu tatizo ndo linaanzia hapo.

Kuna bwege mmoja alishangaa nina watoto wawili (wale wanaofahamika) yeye anao sita. Nikamwambia ndo uwezo wangu.

Juzi kati hapa anaombea mwanae mmoja aje afikie kwangu kwakuwa gharama za hostel ni kubwa. Nikamwambia sima room ya mgeni... Niache kufurahia maisha kufurahisha wengine?

Wakati maisha ni hayahaya?

Enjoy maisha my dear Numbisa
 
Babuuu kwenye mabano nimeelewa hasa.

Same too you Babuu,maisha yenyewe haya hayaeleweki. Ishi unavyopenda
Serikali yetu tunaijua. Hivi sasa ukitaka kupata mtoto lazima ukae mezani kupanga bajeti. Sasa kama unaamua kuzaa kea kutafuta umaarufu tatizo ndo linaanzia hapo.

Kuna bwege mmoja alishangaa nina watoto wawili (wale wanaofahamika) yeye anao sita. Nikamwambia ndo uwezo wangu.

Juzi kati hapa anaombea mwanae mmoja aje afikie kwangu kwakuwa gharama za hostel ni kubwa. Nikamwambia sima room ya mgeni... Niache kufurahia maisha kufurahisha wengine?

Wakati maisha ni hayahaya?

Enjoy maisha my dear Numbisa
 
Moumt Meru iko Arusha mjini. Mi nashauri msipeane mimba kama mnadhindwa kulipia bill ya laki 3 wakati sote tunajua hali halisi ya matibabu

Uzembe mwingine ni kwamba hiyo laki 3 ingetosha kabisa kulipia bima ya afya na tatizo hilo lisingetokea.

Kama umepewa option ya bima ya afya ambayo ni nafuu sana ukaipuuzia basi usimpe mimba mtoto wa watu kwa kukosa laki 3. Sasa kama huna laki 3 huyo mtoto utamtunzaje?

Kupata mtoto ni hiari... kumtunza ni lazima. Tujipange
Huyo mtoto alivyozaliwa aliwekwa chumba cha joto. Hiyo Bima mtoto anakatiwa akiwa tumboni? Na bili iliyokuja ni pamoja na gharama za chumba cha joto kwa mtoto.
 
Huyo mtoto alivyozaliwa aliwekwa chumba cha joto. Hiyo Bima mtoto anakatiwa akiwa tumboni? Na bili iliyokuja ni pamoja na gharama za chumba cha joto kwa mtoto.
Dah... nasikitika kumbe hata hujui bima ya afya ya mama mjamzito inacover matibabu ya kichanga chake...

Alijisemeaga Lowassa... Elimu, Elimu, Elimu...
 
Dah... nasikitika kumbe hata hujui bima ya afya ya mama mjamzito inacover matibabu ya kichanga chake...

Alijisemeaga Lowassa... Elimu, Elimu, Elimu...
Hapana mkuu labda kama wamebadilisha siku hizi, mimi hiyo ilinitokeaga natumia Bima lakini mtoto yupo chumba cha joto nalipia cash,lakini mimi Bima inanihudumia
 
Back
Top Bottom