Hotuba za Rais kila mwezi

Hotuba za Rais kila mwezi

Je unaridhika na hotuba za Rais Kikwete?

  • Ndio

    Votes: 13 15.5%
  • Hapana

    Votes: 71 84.5%
  • SIJUI

    Votes: 0 0.0%
  • Sina jinsi

    Votes: 1 1.2%

  • Total voters
    84
  • Poll closed .
Swali la msingi hapa sio Rais kutumia sheria gani kusamehe wezi/wahujumu uchumi (bila hata ya kufikishwa mahakamani), bali nani kamtuma akasamehe watu hao......
80% ya wapiga kura walimtuma Mkuu labda? Au niamini (kwa dhati) amejisamehe?
 
Sheria ya msamaha maalum wa Rais a.k.a Amnesty...

hivi ni chombo gani ambacho kilitoa hukumu kwamba watuhumiwa wamekosa?
utamsameheaje mtuhumiwa? naamini nje ya chombo cha kisheria mtuhumiwa anaweza kusamehewa (kufutiwa mashitaka) na mkosewaji (katika hali hii wananchi).
kwa kweli mimi bado nashangaa kwa mazingaombwe yanayoendelea.
 
Kikwete ameamua kuyafanya siri majina ya mafisadi wa EPA. Watanzania hatujui hao walioiba pesa hizo ni akina nani na waliiba kesi gani. Hivyo basi kwa kuwa majina ya wezi hao yamefanywa siri hatuwezi hata kutathmini je ni nani na nani waliorudisha kiasi chote cha fedha walizoiba toka EPA.

Kwa hiyo kuna uwezekano kabisa kwamba kuna wegine labda wamerudisha 20% tu au less than that, lakini kwa kuwa 'wamerudisha' pesa basi Kikwete kaamua kuwasamehe.

Ni lazima majina ya wote waliohusika na wezi huo wa mabilioni ya EPA yawekwe hadharani na kiasi gani kilichoibiwa na kila mmoja wa mafisadi hao na pia kujua ni kiasi kipi kimerudishwa na hao inaosemekana waliorudisha pesa hizo.

Kikwete kaingia madarakani kwa kutumia pesa za mafisadi ndiyo maana anaogopa kuwafikisha mbele ya sheria. Kama hawezi kuwashighulikia mafisadi ni bora ajiuzulu na kumpisha Rais ambaye atakuwa ni msafi na hana woga wa kupambana na mafisadi.

Pia Watanzania tungependa kujua pesa hizo zimewekwa kwenye bank ipi na account number ili tufuatilie kama kweli pesa hizo zipo au ni usanii tu.
 
Leaders react furiously on EPA scam

2008-11-02 11:31:05
By Rodgers Luhwago

Opposition leaders yesterday reacted irritably to the way the head of state has handled the EPA scam which cost the nation Sh138.195billion, saying it has proved that the nation was losing the battle against grand corruption.

Among other things, the opposition leaders challenged the move to grant amnesty to the EPA suspects who have returned a total of Sh69.3billion which they obtained fraudulently from the Bank of Tanzania (BoT).

Addressing the nation on Friday, President Kikwete said the Attorney General-led task force has done a tremendous job, managing to recover about 76.7 percent of the Sh90billion which Ernst and Young established was paid fraudulently to 13 local companies.

The head of state also ordered those who failed to return the looted billions to be prosecuted by the Director of Public Prosecutions (DPP), a decision that indicated that other suspects who managed to pay back the money will not be charged.

Speaking to the Guardian on Sunday on separate occasions, opposition leaders said the billions returned by EPA suspects were clear evidence that could have been used to prosecute the culprits before the court of law.

Tanzania Labour Party (TLP) National Chairman Augustine Mrema said the President should have made public the names of suspects who returned the monies, including the amount of money that each one swindled instead of making blanket statements in his speech.

``How do we know that the money has been returned or the names of people who paid back to me this is a just another nightmare that has clouded this nation in fighting grand corruption.

``The President just told us about the money that has so far been recovered. Worse still he never mentioned individuals who owned the companies as if the companies had no owners,`` Mrema angrily reacted.


According to Mrema, it was important for the President to reveal names of individuals who returned the money for the public to know. ``We are stressing this because it is obvious that the money was returned by people, not animals or trees,`` he added.

The once outspoken home affairs minister said pressing charges against companies that have failed to return the money is a joke because owners of the companies are likely to have registered the companies, using either fake individual names or names of people who did not really benefit from the stolen money.


Civic United Front (CUF) National Chairman Prof. Ibrahim Lipumba said he was disappointed by the President.

``It is very disappointing to see criminals going free in a country that brags to be adhering to the principle the of rule of law. Besides returning the money they should also be taken to court to face charges,`` said Prof Lipumba.

According to Prof Lipumba, President Kikwete should have waited for court action before granting an amnesty to them (EPA suspects).

The CUF leader explained that by asking the office of the Director of Public Prosecutions (DDP) to decide whether or not to try those who failed to return the money is another hindrance for the legal measures to be instituted against them.


``This case is straightforward. We do not need any considerations of the DPP. All this proves that President Kikwete is not serious. He has proved his weakness before the public,`` he said.

Prof Lipumba further said the decision to protect EPA looters would set a bad precedent in the country.


United Democratic Party (UDP) John Cheyo criticised the President for being an obstacle to the practice of the rule of law. He said since no individual is above the law, EPA suspects were supposed to be taken to court to defend themselves.

``The President should stay aside and let the law take its course. We are not ready to see the President setting a bad precedent in this country.

This is very unfortunate,`` said Cheyo, who is scheduled to hold a press conference today, to speak about the matter at length.

He said returning the stolen money should not be taken as an excuse of not appearing before the court law.
On his part, Chama Cha Deemokrasia Na Maendeleo ( Chadema) Secretary General Willibrod Slaa strongly criticised the President for breaking the law.

He said by granting an amnesty to the EPA suspects the President showed the world that he was above the law.

``The President has no powers to forgive a person who has committed a criminal offence. Since any criminal offence is administered by a law enacted by the legislature, violating such a law also becomes a serious offence,`` he said.


He added: ``I would like to tell Tanzanians that if we (the Opposition) were the majority in the Parliament, we could cast a `Vote of No confidence` in Parliament against the President.

Addressing the nation on Friday, President Kikwete said over Sh 69.3 billion out of Sh90.billion which is equivalent to 76.7 per cent stolen from EPA account has been recovered.

The money was swindled by 13 companies using forged documents. In the address, the President said an investigation into nine other companies that pocketed Sh43 billion were still going on.

He said he directed the head of an investigation team, the attorney general, to hand over to the DPP files of suspects who failed to return the stolen money.

SOURCE: Sunday Observer
 
" you can be a fool even you go to school"


ni hivi jamani alikuwa na maana ya kujisamehe kwanza yeye

tuwe na akili

jk ni mwizi namba moja wa epa!!!!pesa za epa ndizo zilizo mfikisha ikulu,,wakati ridhiwani akipita na pesa kwenye lile landcruiser kuelekea dodoma!!!mkafikiri pesa za mabibo
kule bagamoyo!!!

Na nyie wanafiki wabunge na hao wa (nwec)!!!!wakati mnachotea mafungu mbona hamkuuliza zimetokea wapi habari ndio hiyo

nafikiri swala la epa!!tupige magoti kwa mungu amshushie moto kila aliehusika kimwili mtakutana na haya majina kule mahakamani

rama salehe

john makoyi

mwanakijiji mie

invisc
na wenzangu mie mama hundred!!!!!

Ukija wenye bank m jeetu patel na wengineo wapi na wapi!!!

Mungu ikoe tanzania
 
EPA auditing cost Sh1.1bn, claims BoT

2008-11-02 11:25:08
By Rodgers Luhwago

As the nation ponders the future of EPA scandal, the Bank of Tanzania is finally coming out revealing how much it cost to investigate the scam that has rocked the fourth phase regime.

Speaking exclusively to The Guardian On Sunday this week, Bank of Tanzania (BoT) governor Prof Benno Ndullu revealed that Ernst and Young, was paid a total of Sh1.1billion to investigate EPA accounts.

The Central Bank governor defended the payments adding that the auditing firm deserved such huge payment because the task to investigate the looted billions was daunting, and needed to be done professionally.

He was speaking about the news that Ernst and Young, was paid a whopping Sh6.5billion to investigate the EPA accounts.

However, reliable information that reached this newspaper earlier this week had it that Ernst and Young Company received around Sh 6.5 billion as the payment for auditing EPA account after which a loss amounting to Sh 133 billion was discovered.


``The company was paid close to Sh 1.1 billion for doing the job not Sh 6.5 billion and mind you the same money covered costs of bringing in the firm`s experts from outside Tanzania,`` said Prof Ndullu who was very cooperative.

The cost that EPA suspects have caused to this nation is what makes the public feel that the President should have no mercy on them.

However, after the President�s speech issued on Friday, it is quite clear that the issue is still very complicated despite the recovery of Sh69billion.

If one decides to work on the confirmed figure the conclusion that is likely to be drawn is that such huge amount of taxpayers` money could have been directed to support other sectors, especially in social amenities.

Commenting on the cost that the government incurred in hiring the auditing firm Karatu legislator Dr Willibroad Slaa said lack of good governance in the country is what has brought the nation to such a point.

He said reports of embezzlement of public funds had been in the public domain since mid nineties but the government turned a blind eye to them.

He said there were other international auditing firms, including Coopers and Lybrand and Deloite & Touche that raised the alarm but nothing was done.

``Sh 1.1 billion is nothing to a country that embraces and protects people who loot billions of shillings from public coffers.

When a country reaches such a horrible stage spending Sh 1.1 billion would not surprise me. However, still that remains as embezzlement of public funds,`` he said.

Dr Slaa said in the first place there was no need for the government to invite any auditing firm to look into the BoT�s books of accounts last year since everything known some years back .

``When we, in the opposition, tirelessly spoke of embezzlement of public funds we had information of the findings of the work done by Deloite & Touche, Coopers and Lybrand and others.

The problem was that the government was sweeping the rot under the carpet,`` he added.

Dr Slaa explained that generally it was `improper` for the government to invite auditors and also form a presidential task force under the Attorney General to trail the suspects.

The government formally appointed Ernst & Young to audit BoT`s books of accounts on September 10 last year after opposition legislators raised an alarm on the massive theft of funds from the central bank.

The company was given 60 days to conclude the work.
The central findings released by the government in January 2008 showed that a total of Tsh133 billion (about $113 million) was paid under the EPA scheme during 2005/06 (July- June) to 22 local companies based on fraudulent documentation or without any supporting documentation.

Upon receiving the report, the governor of the BoT was dismissed before President Jakaya Kikwete announcing an immediate suspension of operations under the EPA scheme until proper control procedures were established.

SOURCE: Sunday Observer
 
Bilioni 1.1 au bilioni 6.5? Kitendawili kimeshaanza

Bado hatujaweka na pesa za gharama walizotumia kamati ya 'kukusanya' pesa za EPA toka kwa wahusika na uchunguzi wa mali za wezi hao ndani na nje ya nchi, na kamati hiyo bado haijamaliza kazi.
 
Bado hatujaweka na pesa za gharama walizotumia kamati ya 'kukusanya' pesa za EPA toka kwa wahusika na uchunguzi wa mali za wezi hao ndani na nje ya nchi, na kamati hiyo bado haijamaliza kazi.

Naona uchunguzi wa EPA nao umegeuka mradi wa kutajirisha watu!!!
 
Imetolewa mara ya mwisho: 02.11.2008 0006 EAT

• VUGUVUGU LA EPA:JK azongwa

*Wanasiasa wakuna vichwa
*Wanasheria washikwa butwaa
*Kilaini: Mambo haya mazito

Na Waandishi Wetu, jijini

HOTUBA aliyoitoa Rais Jakaya Kikwete juzi usiku hususan kuhusu ufisadi katika Akaunti ya Malipo ya Madeni ya Nje (EPA), imepokewa kwa hisia tofauti, huku watu wengi wakiwamo wanasiasa wakizidi kumkosoa kwamba anaongoza nchi bila kufuata katiba ya nchi.

Waliozungumzia na gazeti hili jana walisema walitarajia angetaja orodha ya majina ya mafisadi katika akaunti ya EPA na kufikishwa mahakamani, lakini kinyume chake amebaki kuwakumbatia na kumbebesha mzigo Mkurugezi ya Mashitaka ya Umma (DDP) ili awafikishe mahakamani.

"Tulitarajia Rais angetaja majina ya hao watu aliodai wamerejesha sh. bilioni 69 na kutoa maelekezo wafikishwe mahakamani badala ya kutuambia kuwa kampuni tisa hazijulikani zilipo," alisema mwanasheria CHADEMA, Bw. Tindu Lisu.

Alisema waliohusika kuchota fedha hizo wanakabiliwa na kosa la jinai, hivyo katika makosa ya aina hiyo haishitakiwi kampuni bali wamiliki na wakurugenzi wake.

Alisema inashangaza kusikia Rais akitaja kampuni zulizoshindwa kurejesha fedha hizo badala ya kutaka wamiliki na wakurugenzi wake. Alisema lengo la Rais Kikwete ni kutaka kugeuza kesi hiyo iwe ya madai ionekane kampuni ndizo zinazodaiwa badala ya kushitaki wamiliki wake na wakurugenzi ambao walihusika kughushi nyaraka.

Alifafanua kuwa DDP analindwa na sheria inayompa mamlaka ya kutekeleza wajibu wake bila kuingiliwa, lakini katika sakata hilo la EPA inaonekana wazi kuwa aliingiliwa. "Leo hii Rais anamwelekeza awafikishe mahakamani watuhumiwa wa EPA walioshindwa kurejesha fedha, ina maana alikuwa amemzuia?"alihoji na kuongeza:

"DPP hana uhuru gani kama anasubiri maelekezo kutoka kwa Rais Kikwete?," amehoji Lissu na kuongeza kuwa watuhumiwa wa ufisadi katika akaunti ya EPA walipaswa kushughulikiwa siku nyingi, lakini inavyoonekana yeye (Rais) ndiye alizuia.


Alisema kama kweli fedha hizo zimerejeshwa Rais Kikwete alipaswa kuwaeleza Watanzania zimerudishwa na akina nani na tarehe gani. " Kwa mazingira haya hatuna sababu yoyote ya kumwamini Rais Kikwete ikiwa hatawaambia Watanzania waliorejesha fedha hizo ni akina nani,"alisisitiza.

Dkt. Slaa: Nimekosa imani na Rais

Mbunge wa Karatu, Dkt. Wilbroad Slaa, alisema hotuba aliyoitoa Rais ni dalili za wazi za yeye kushindwa kuongoza nchi.

"Hizi ni dalili za wazi za Rais Kikwete kushindwa kuongoza nchi kwa sababu wezi wanajulikana yeye anawasamehe," alisema na kuongeza kuwa: "Rais hana mamlaka ya kusamehe watu ambao hawajahukumiwa."

Dkt. Slaa alisisitiza kuwa kwa kauli ya jana tayari Rais Kikwete kwa mara nyingine tena ametangaza kuwasamehe watuhumiwa wa ufisadi waliorejesha sh. bilioni 69.

"Hii inaonyesha kuwa wapo watu walio juu ya sheria, makosa yote waliyotenda yanajulikana isipokuwa hawafikishwi mahakamani kwa sababu wanalindwa,"alisema. Alisema Rais Kikwete ameonesha jinsi anavyoongoza nchi kwa upendeleo, ubaguzi na kujenga matabaka.

"Kama anaweza afungue magereza yote ili wanaotumikia kifungo waweze kutoka," alisema. Dkt. Slaa alisema ni jambo la kushangaza kwa Rais Kikwete kufumbia macho vigogo wa Serikali walioidhinisha fedha hizo na badala yake anataka makampuni aliyochota kiasi hicho cha fedha kuzirejesha.


Kuhusu kauli ya Rais Kikwete kuwa kuna kampuni tisa ambazo hadi sasa Kamati aliyoiunda ikiongozwa na Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Bw. Jonhson Mwanyika, haijui yalipo, Dkt. Slaa alisema hiyo inaonesha wazi kuwa Rais Kikwete hatulii ofisini na kusoma.

Alisema wataalamu washauri wote waliochunguza sakata la EPA waliishaweka wazi kuwa kampuni hizo tisa zimetafutwa na imethibitika kuwa zote ni hewa na hazijulikani zilipo duniani kote.

"Kwa nchi masikini kama Tanzania inayotumia kiasi cha asilimia 34 ya misaada ya wahisani inaendelea kutumia fedha nyingi kutafuta kampuni ambazo inajulikana hazipo, ni aibu na inaonesha jinsi gani Rais asivyotulia ofisini kwake na kujisomea,"alisema.

Dkt. Slaa alisema kwa jinsi Rais Kikwete alivyoshindwa kulishughulikia suala la EPA, kama wabunge wa upinzani wangekuwa wengi wangeeda mbali zaidi na kuomba apigiwe kura ya kutokuwa na imani naye.

"Mimi kuanzia sasa sina imani naye, kama wabunge wa upinzani tungekuwa wengi tungeenda mbali zaidi na kuangalia uwezekano huo," alisema. Alisema kama hotuba yake ingejadiliwa kwenye kikao cha Bunge kinachoendelea wangetumia nafasi hiyo kuwasilisha maombi hayo.


Hata hivyo alisema kama hotuba hiyo itajadiliwa kikao kijacho cha Bunge bado atakuwa na nafasi ya kuwasilisha ombi hilo. Hata hivyo alisema kwa sasa ni vigumu kuwasilisha pendekezo hilo kwa kuwa ipo kanuni inayozuia kutajwa kwa jina la Rais.

Mrema: Anafuata nyayo zangu

Mwenyekiti wa Tanzania Labour Party (TLP) Augustino Mrema,alisema inavyoonekana Rais Kikwete ameanza kuiga utaratibu kama aliokuwa nao ambapo alikuwa kiwataka watu wote walioiba fedha kuanza kuzirejesha.

"Nilikuwa na utaratibu uliojulikana kama Tajirika na Mrema, naona Rais Kikwete ameanza kufuata nyayo zangu," alisisitiza Bw. Mrema.

Rais Kikwete katika hotuba yake ya jana alisema suala hilo ameliacha kwa DPP ili aweze kuwachukulia hatua za kisheria.

Naye Mwenyekiti wa TPP-Maendeleo, Bw. Peter Mziray, alimshauri Rais Jakaya Kikwete, aache kuendelea kuzungumzia suala la EPA kwani Watanzania wameishamuelewa ni nini anakisema, hivyo wasingependelea kuzidi kupoteza muda.

"Watanzania wamemuelewa Rais Kikwete ni mtu wa aina gani, kinachotakiwa ni wao kuanza kujiandaa kwa mabadiliko kwani CCM haiwezi kupambana na mafisadi," alisema Bw. Mziray.


Alisisitiza kuwa kwa mara nyingine Rais Kikwete ameweza kutoa hotuba ambayo haina jipya ndani yake na hiyo imedhihirisha kuwa fedha hizo zilitumiwa na CCM kwenye kampeni kama ambavyo imekuwa ikidaiwa.

Profesa Baregu: Serikali ijiuzulu

Kwa upande wao wasomi Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) wamesema kitendo cha Serikali kushindwa kuwachukulia hatua watuhumia hao wa ufisadi inatosha kuilazimu Serikali kujiuzulu.

Mhadhiri wa Kitivo cha Siasa za Sayansi, Profesa Mwesiga Baregu, aliliambia gazeti hili muda mfupi kabla ya Rais Kikwete kulihotubia Taifa juzi, kuwa kushindwa kuwachukulia hatua watuhumiwa wa ufisadi kunageuzwa suala hilo kuwa la kisiasa.


''Sisemi warudishe fedha, Serikali ieleze ni kwa nini inashindwa kuwafikisha mahakamani kwa sababu wanakabiliwa na kosa la jinai," alihoji Profesa Baregu na kuongeza kuwa: "Walitakiwa wafikishwe mahakamani ili utolewe uamuzi kulingana na makosa yao na si vinginevyo."

Alisema yeye hapendi kuona sheria inazimwa au kupindishwa kwani bila uamuzi wa busara kuchukuliwa Serikali itakuwa inahalalisha watu kuhujumu uchumi.

Alitoa mwito kwa kila mtu kuhakikisha anatimiza wajibu wake ili kuepusha matukio ya aina hiyo kujirudiia.

"Tusipotatua hili tutakuwa tukiidhinisha vurugu kwani tayari watu wengi wameanza kujichukulia sheria mkoni, na kujaribu hata kurushia mawe msafara wa Rais jambo ambalo ni kosa la jinai," alisema na kuongeza"

"Tumeona wazee wailiokuwa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) wakifunga barabarna kuzua magari." Kwa upande wake Dkt Benson Bana, alisema watu kurudisha fedha hizo sio mwisho, kwani wao ndio wanaopaswa kuisadia mahakama kuweza kutoa uamuzi wake.

Kwa upande wake Askofu wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Methodius Kilaini, alipoulizwa alijibu; "Haya ni mambo mazito, siwezi kutoa maoni yangu labda Rais wa Baraza la Maaskofu au Katibu Mkuu," alisema.

Mkuu wa Idara ya Itikadi na Mafunzo wa NCCR-Mageuzi na Mhadhiri wa Kitivo cha Elimu UDM, Bw. George Kahangwa, alisema kinachoonekana sasa ni Rais Kikwete kushindwa kuchukua hatua dhidi ya wezi wa fedha za akaunti ya EPA.

"Unajua hapa linatumika neno mafisadi, lakini ukweli hawa ni wezi,walitakiwa kufikishwa mahakamani kama wezi wengine," alisema na kuongeza kuwa suala hilo litazidi kuwaumiza Watanzania.

Alisema pamoja na Rais kumwelekeza DPP awachukulie hatua, lakini hakuna muda maalum ambao amempa awe ametekeleza agizo hilo kama yeye alivyokuwa amewapa Otoba 30, mwaka huu.

Alisisitiza kuwa wale ambao wamerejesha fedha hizo na ambao hawajazirejesha wanatakiwa kufikishwa mahakamani kwa sababu ni wezi kama walivyo wezi wengine.

Profesa Safari: Amevunja katiba

Kwa upande wake gwiji wa sheria Profesa Abdallah Safari, alisema kitendo cha Rais Kikwete kushindwa kutangaza kuwachukulia hatua watuhumiwa wa ufisadi kimethibisha wazi jinsi anavyokiuka katiba.

"Ameshindwa kabisa kujisahihisha, tatizo hapa hatuna upinzani wa kweli, kama ungekuwepo ungemlazimisha hata kujiuzulu," alisema Profesa Safari na kuongeza kuwa tangu mwanzo Rais Kikwete alikuwa akingilia uhuru wa DPP kuweza kuwafikisha mahakamani.

"Kwa kweli inasikitisha, binabsi hii naiona kama Kikwete style...Watanzania wamesikitika sana lakini hawana cha kufanya kwa sababu hawana upinzani imara,"alisisitiza.

Akitoa maoni yake binafsi Katibu Mkuu wa Baraza la Maaskofu Tanzania, Bw. Antony Makunde, aliwataka Watanzania wavute subira na kuwa na imani na Rais wao.
 
wana JF najua kwa wale walioisikiliza hotuba ya mh raisi wetu wa jamhuri ya muungano wa tanganyika walihuzunika sana baada ya kutolewa hukumu
ya baadhi ya wahusika wa EPA kabla hawafikishwa mahakamani!!
Ni mambo ambayo wengi walishaandika hapa na wengine kuapa kwa majina ya wazazi wao hakuna kitakachoofanyika zaiidi ya kuumwa nyuki wadogo hilo ndilo lililowekwa jana bayana nini kinaendelea!!!!
natumani wote wenye akili zao timamu wanajua pesa za EPA ndizo zilizotumiwa kuwahonga wananchi wa tanga-nyika kumchagua raisi wao na viabaraka wake kuingia pale kivukoni!!!!na kwa hili si shaaka wengi wameonja neema yake!!!na ndio maana kuna mtu aliniuliza mbona ikulu haina heshima tena wanaingia watu wa a ajabuajabu!!!!sikuwa na jibu la kuwapa kuogpa mwisho ntataja epa nikalie mlango wa sheria!!!
Hakika ni hotuba iliyojaa mahaba ya mwimbaji yussuf na nduguze kana kwamba wale walioiba pesa nyingi na kuweza kulipa kwa wakati hakuna atakaeshugulikiwa!!!inantia wasiwasi basi pale BOT kuna mchezo mchafu mkubwa ambao watu wengi hawaujui na inaezekana kuna watu wakiongozwa na huyu mh sana kuchukua pesa zetu na kwenda kuzilimbika huko uswiss akishaondoka anazirudisha bila inte!!1

nirudi kwenye ujumbe maalum ni kwamba kama ulisikiliza utaona rais akiwa mhusika mkuu wa EPA aliamua kujipa msmaha na marafiki zake kwa kuweza kulipa kiasi cha fedha za EPA!!!leo hii ndugu zetu wanateswa na ajira pale BANK M kisa muhindi anataka penzi kinyume na maumbile ukiuliza naitwa rajesh J.patel, ninaamaana wapi WAKINA JEETU PATEL

WAPI YULE KIJANA ALIEAMUA KUWEKA OFISI ZAKE PALE REGENCY KARIBU NA NYUMBA YA RAIS KIKWETE!!!!NA NDIO HUYO ALIELETA ZILE VOG 2 NA BA!!!

Mhh hhhh RAISI wacha msamaha wakupe watanzania uichofanya natumaini si watanzania wala nchi za nje zitakazokaa kimya na katika hili nakuhakikishia nchi itabadilika na watu wataamua kutafuta haki zao kwa hali yoyote ile

mh rais embu omba mungu akupe utisho wa kiroho uoni aibu wale wazee wanalala pale barabarani kuzuia vigogo wenzako wasipite je unafikiri walikuja kuona ikulu ikoje!!!!uhoni lile ziwa la yule mama uliloonyeshwa kwenye gazeti litakudai na familia yako mpaka mwisho wa maisha yako!!!huogopi wale vijana wako wanawapiga wale wazee kisa wamepewa amri toka kwa KOVA na wenzake!!!

mh Rais husikii hata hawa watu wanaotufanya na wengine tunajua kubonyeza kwenye komputer leo hii(WALIMU) wanavyodai haki zao kwa shifda lini mtawaeshimu na kuwakumbuka hawa ni binadamu kama wanao wanavyokuja kudai pesa za shule na kadhalika

,mh Rais Huoni haya mashirika yetu ya kila siku wafanyakazi wanaishi kwa migomo na mengineo!!!huoni ama hamakuona aibu walimu na wazazi wetu wanakufa na njaa pale kivukoni kudai hakizetu na huku mkiwawapa wale wahindi wa RAILWAY million 370?????????y? raisi

leo hii mashirika yote halizao ni mbovu tunashindwa hata kuyainua matokeo yake tunakimbilia kwenye kuyabinafsisha baada ya kujua tumeliwa na then tunaamua kuwalipia na mishahara yao jamani!!!!!!!jamani wewe mh raisi unatupeleka wapi

Mwisho hongera kwa kujpa msamaha mwenyewe kwa wizi na udanganyifu wa EPA!!!!!
 
Naona uchunguzi wa EPA nao umegeuka mradi wa kutajirisha watu!!!

Itaundwa tume nyingine kuchunguza kama Ernst & Young wamelipwa shilingi bilioni 6.5 au 1.1 billion na wakati huo mafisadi wakiendelea kupeta tu. 🙁
 
teh teh teh teh, wadanganyika mtalia hadi xmas!
 
teh teh teh teh, wadanganyika mtalia hadi xmas!

MAMA

MI SITAKI!!!!!
 
JK apingwa

na Happiness Katabazi
Tanzania Daima~Sauti ya Watu

WATU waliotoa maoni kuhusu hotuba iliyotolewa juzi na Rais Jakaya Kikwete, wamezipinga hatua zilizochukuliwa dhidi ya watu wanaotuhumiwa kuchota mabilioni ya fedha kutoka katika Akaunti ya Malipo ya Madeni ya Nje (EPA).

Waliliambia gazeti hili kuwa hatua hizo zilizochukuliwa na rais, zinamfanya aonekane amevunja Ibara ya 13 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977, kwa kitendo chake cha kuwasamehe watu walioiba na kurejesha fedha za EPA.

Akizungumza na Tanzania Daima jana, Mhadhiri Mwandamizi wa Kitivo cha Sheria cha Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Dk. Sengondo Mvungi, alisema Ibara ya 13 ya Katiba ya nchi inatamka usawa mbele ya sheria, hivyo kitendo cha rais kuwasamehe waliorejesha fedha hizo si sahihi na kusema inashangaza kwa nini rais anawakingia kifua watu hao.

"Rais Kikwete amekosea kutoa msamaha kwa hao mafisadi waliorejesha fedha hizo kwa sababu hao waliozirejesha wamekiri kosa na ushaidi wa wizi huo umepatika, kinachotakiwa, mafaili ya waliorejesha na ambao hawajarejesha yapelekwe kwa DPP ili awafungulie kesi mahakamani," alisema Dk. Mvungi ambaye ni mwanasheria kitaaluma.


Dk. Mvungi alimtaka Rais Kikwete asichanganye mtu kukiri kosa na kurudisha alichoiba na madaraka yake ya kusamehe.

Akifafanua, alisema kuwa Ibara ya 145 ya Katiba inampa mamlaka rais kusamehe mtu ambaye ameshahukumiwa na mahakama, baada ya mahakama kumkuta na hatia, na si kumsamehe mtu ambaye hajafikishwa mahakamani na kukutwa na hatia.

"Rais asiwageuze Watanzania mambumbumbu wa sheria… nasisitiza rais amevunja Katiba ya nchi na ninawataka Watanzania tusimame kidete kuitetea Katiba yetu," alisema Dk. Mvungi.


Kwa upande wake Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe, alisema kuwa, juzi rais Kikwete aliwathibitishia wananchi kwamba ana mkakati wa makusudi wa kuwalinda wezi wa EPA.

"Kama Kikwete kwenye hotuba yake aliweza kutaja jina la Rais wa Chama cha Walimu (CWT), alishindwaje kutaja hata jina la fisadi mmoja aliyeiba fedha nyingi BoT? Nasema hivi, rais ana urafiki wa karibu na hawa mafisadi, ndiyo maana anapatwa na kigugumizi cha kutaja majina yao na hata kueleza Kampuni ya Kagoda Agriculture ni ya nani," alisema Mbowe.

Hata hivyo, naye alisisitiza kuwa rais amevunja Katiba ya nchi na kwamba kinachoendelea kujidhiirisha ni ombwe la uongozi katika taifa.

Alisema rais hana mamlaka ya kumsamehe mtu ambaye hajahukumiwa na mahakama kama alivyofanya kuwasamehe waliorejesha fedha bila ya kufikishwa mahakamani.

Naye Mwenyekiti wa Chama cha Tanzania Labour (TLP) Augustine Mrema, alisema ameshangazwa kwa kitendo cha rais kuutangazia umma kwamba hadi juzi mchana zilikuwa zimerejeshwa sh bilioni 69.3, lakini akashindwa kutaja majina ya watu waliozirudisha fedha hizo.

Aidha, Mrema alisema rais alipaswa kusema fedha hizo zimerejeshwa kwenye benki gani.

Mrema alisema kitendo cha rais kuagiza kamati ya uchunguzi wa wizi huo kuorodhesha majina ya makampuni yaliyoshindwa kurejesha fedha hizo na kuyawasilisha kwa Mkurugenzi wa Mashitaka, ni mbinu nyingine ambayo imelenga kuyashitaki makampuni mahakamani badala ya kuwashitaki watu waliohusika, na kuwaomba wananchi wawe macho na hali hiyo.

"Kama rais anataka wananchi wamuelewe na kuendelea kumheshimu ni vyema ataje majina ya hao waliokwapua fedha hizo na si kuorodhesha makampuni, kwa sababu mwisho wa siku watakaofikishwa mahakamani ni makarani wa makampuni hayo badala ya wahusika wakuu… awataje kwa sababu tutakuwa tumewajua wabaya wetu na hiyo ndiyo itakuwa zawadi ya Krismasi kwa sisi wananchi wake, tutafurahi sana.

"Rais asiwakingie kifua mafisadi hata kama walimsaidia kitu fulani… basi iwe siri yake moyoni na awatose na wananchi tutamlinda. Na ninamtaka aelewe kwamba hotuba yake haina maana, kwa sababu haijataja majina ya mafisadi," alisema Mrema.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF), Profesa Ibrahim Lipumba, alisema amesikitishwa na kupoteza imani ya Rais Kikwete kwa jinsi alivyolishughulikia suala hilo la EPA.

"I am totally disappointed' (nimesikitishwa sana)… nilidhani rais angeamuru wale waliorejesha hizo fedha nao wakamatwe na wafikishwe mahakamani, kumbe mwenzetu ameamua kuvunja sheria za nchi kwa makusudi kabisa na kuwaruhusu watuhumiwa hao warejeshe fedha kisha waendelee kutanua mitaani.

"Nasema nimesononeshwa na nimepoteza imani na utawala wa rais, sijui nchi hii anaipeleka wapi," alisema Profesa Lipumba kwa masikitiko.

Alisema mtindo huo wa kiongozi mkuu wa nchi kupindisha sheria kwa sababu walioiba fedha hizo ni maswahiba zake, utakuja kuleta machafuko nchini, kwani anaamini watu ambao ndugu na jamaa zao wapo rumande kwa makosa ya wizi watajisikia vibaya na kuanza kutaka nao ndugu zao wapewe nafasi za kurejesha kile walichoiba ili wafutiwe kesi zinazowakabili.

Naye Mwadhiri Mwandamizi kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Profesa Mwesiga Baregu, alisema ameshindwa kumuelewa Rais Kikwete ana mpango gani na taifa kwa sababu wizi wa fedha za EPA ni makosa ya jinai, lakini anashangaa ni kwa nini amekuwa na kigugumizi kuwachukulia hatua waliorejesha fedha hizo.

"Hivi hao waliorejesha fedha walizikopa kwenye EPA au kwenye Saccos… kwa sababu unapokopa fedha lazima uzirejeshe lakini hawa tumeambiwa waliiba na kama wanazirejesha ni kidhibiti tosha cha kuwaburuza mahakamani… Watanzania tumpinge rais katika hili, kwani amevunja sheria za nchi," alisema.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Vijana wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), John Mnyika, akizungumza kutoka Mwanza, alisema Rais Kikwete ameendelea kuligawanya taifa kwa kuwalinda mafisadi na kugeuza suala lao kuwa la madai badala ya jinai.

Alisema hata mjadala wa OIC umeendelezwa na serikali yake yenyewe (Kikwete).

"Nimeshangaa. Lakini nikashangaa zaidi kwa Rais Kikwete kutofautiana wazi wazi na Waziri wake wa Mambo ya Nje, Bernard Membe, ambaye Rais Kikwete amemuita kuwa ndiye ana dhamana ya suala hilo. Wakati rais anasema kwamba utafiti wa suala hilo bado haujakamilishwa na Waziri Membe, waziri mwenyewe wakati anahutubia Bunge Agosti 22 mwaka huu alitangaza kwamba wizara yake imeshakamilisha utafiti. Nani mkweli kati yao, Mungu ndiye ajuaye.

"Lakini Mwalimu Nyerere, katika kitabu cha Uongozi wetu na hatma ya Tanzania, alizungumza vizuri kuhusu serikali. Mwalimu aliweka wazi, mkusanyiko wa mawaziri wasiokuwa na dira ya pamoja na uwajibikaji wa pamoja, wanabaki kuwa serikalini kwa mujibu wa sheria tu, lakini kimaadili na kimantiki; hakuna serikali," alisema.

Juzi usiku Rais Kikwete alihutubia taifa pamoja na kuzungumzia mambo mengine, aliiagiza Kamati ya Uchunguzi ya Wizi wa fedha za EPA kuwasilisha majina ya makampuni yaliyoshindwa kurejesha fedha hizo kwa DPP, ili hatua za kisheria zichukuliwe.

Kikwete alitangaza uamuzi wake huo uliokuwa ukisubiriwa kwa shauku kubwa na Watanzania walio wengi, akitekeleza ahadi aliyoitoa wakati alipohutubia Bunge mjini Dodoma Agosti 21 mwaka huu.

Akizungumzia urejeshwaji wa fedha hizo, Kikwete alisema taarifa alizoletewa juzi mchana zilikuwa zikionyesha kuwa kiasi cha sh bilioni 69.3 kati ya sh bilioni 90.3 zilikuwa zimerejeshwa kutoka katika akaunti ya EPA, kiasi ambacho ni asilimia 76.7 ya fedha zote.

Akizungumzia kuhusu mzozo unaozingira uamuzi wa Tanzania kujiunga katika Jumuiya ya Kiislamu duniani (OIC), alieleza hali hiyo inayogawa watu katika tofauti zao za kiimani kuwa isiyofurahisha na kwamba unaweza kulipeleka taifa pabaya.

Hata hivyo alisema hadi hivi sasa serikali bado haijaamua iwapo Tanzania ijiunge au isijiunge katika jumuiya hiyo, kutokana na ukweli kwamba, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa iliyopewa kazi ya kutafiti inaendelea na kazi ya kulifuatilia suala hilo, hivyo haijawasilisha serikalini matokeo ya utafiti wao pamoja na mapendekezo na kuamuliwa ipasavyo.
 
teh teh teh teh, wadanganyika mtalia hadi xmas!

MAMA

MI SITAKI!!!!!


utajiju mama mia, shangilia ushindi wa mafisadi hadi hapo utakapoamua kuacha kufuata upepo unapoelekea kama bendera...hiyo ndiyo tafsiri ya ushindi wa kishindo
 
Je, kutakuwa na hotuba ya mwisho wa kila mwezi toka kwa JK mwezi huu? Watanzania tunaisubiri kwa hamu hotuba hiyo kusikia atasema nini.
 
Wana JF, mara nyingi imekuwa vigumu kujua kama Rais wa Jamhuri alihtoa hotuba ya mwezi au la na mara nyingine wengine huwa tunashindwa kupata/kusoma hotuba hizo ambazo huwa zina mambo muhimu kwa Taifa.

Bubu ataka kusema huwa ni hodari sana kutuletea habari mbalimbali kama zilivyoandikwa na magazeti ya TZ.

Napenda kushauri kuwa tuwe na thread maalum ambayo haitaondolewa kwa jina la "Hotuba ya Rais mwezi huu" ili tuweze kufuatila na kusoma hotuba hizo kila mwezi na ili tuweze kufanya marejeo ya hotuba za Mkuu wa nchi.

MAPENDEKEZO


Napendekeza Bubu ataka kusema na Moderator ndio wawe wawekaji wa hotuba hizo kila mwezi na sisi wengine tuwe Wachangiaji.
Naomba kuwasilisha
 
Back
Top Bottom