Hotuba za Rais kila mwezi

Hotuba za Rais kila mwezi

Je unaridhika na hotuba za Rais Kikwete?

  • Ndio

    Votes: 13 15.5%
  • Hapana

    Votes: 71 84.5%
  • SIJUI

    Votes: 0 0.0%
  • Sina jinsi

    Votes: 1 1.2%

  • Total voters
    84
  • Poll closed .
Pia tusishangae akiamua kuingia mitini tena mwa mwezi wa tatu mfululizo.
Mungu ibariki Tanzania

Nina uhakika kabisa JK hatatoa hotuba na akitoa nitashangaa sana, maana anayotakiwa kuongelea ni mengi mno na hana majibu yake, na akiyaibua tu atashindwa kuyahimili. Huyu mkuu nchi tayari imeshamshinda na sijui kwanini CCM hawaanzi kuandaa mtu mwingine wa kuchukua 2010.
 
sijui anajisikiaje kutufanyia anayotufanyia...one day baada ya miaka mingi atajuta anachotufanyia,inatia uchungu kweli kweli!
 
hatoongea ila akiongea ataongelea kuhusu kupanda kwa mafuta duniani na jinsi gani watanzania tunavyopaswa kustahamili shida inayotupata kama wanavyostahamili watu wengine duniani kote.
 
oh Ya!, Alikuwa Very Goood Kwenye Interviews Lakini Akashindwa Kujenga Hata Nyumba Kwao Masasi, Na Hata Baada Ya Kustaafu Akajenga Lushoto Tanga Kwa Marafiki Zake Kina Ngwiliz Na Kigoda,

Badala Ya Kujenga Kwenye Mizimu Ya Mababu Zake, Masasi, Je Tulitegemea Nini Kutoka Kwa Huyu Msomi As Far As Taifa Is Concerned?

Mkuu Mkapa Kwao Ana Nyumba Hivyo Ni Vema Ukaendelea Na Hoja Zingine Tu Za Maana, Hili La Nyumba Halitusaidii Kabisa Ktk Mjadala Huu.
 
Yeye Ndiye Mwenye Nchi Wakuu, Kwani Huko Mikoani Hazungumzi? Kama Anazungumza Basi Ni Vema Sisi Jf Tuzichukulie Hizo Nazo Kama Sehemu Muhimu Za Ujumbe Wake Kwa Watanzania.
 
Utaratibu huu aliuanzisha mtangulizi wake. Umekaa Kikatolikitoliki hivi. Anahutubia kwa kurekodiwa na hakuna maswali. Kwa kuwa yeye ni SEHEMU ya BUNGE, labda ile nafasi ya PM ya kila Alhamis apewe RAIS angalau mara moja kwa mwezi.
 
July ndiyo inayoyoma hiyo, JK atalonga au ataendelea na ububu wake kuhusu maswala muhimu yaliyoigubika nchi.
 
July ndiyo inayoyoma hiyo, JK atalonga au ataendelea na ububu wake kuhusu maswala muhimu yaliyoigubika nchi.

Siku hizi naona kaamua kufanya kazi ya waziri wa jinsia na watoto, kukataza wababa waache kutongoza binti wadogo na kuwaelekeza wawafate wamama wazima ambao ni saizi yao!!

Hizo ndo hotuba alizobaki kutoa muheshimiwa raisi wetu!
 
Nimehatika kusikiliza kipindi cha Bunge cha asubuhi hii Waziri Mkuu akijibu maswali ya Wabubge moja kwa moja. KWa bahati nzuri Mbuge mmoja ameuliza swali ambalo nimekuwa najiuliza bila kupata majibu. Mbunge alitaka kujua ni muda gani Mh. Rais hajazungumza na wnanchi kwa mujibu wa utaratibu aliojiwekea.

Waziri Mkuu amethibitisha kuwa Rais hajaongea na Wananchi kwa miezi miwili sasa ati kwa kuwa majukumu yamemzidi- Mwenyekiti wa EU na safari zimekuwa nyingi!

Mimi nilikuwa najifariji pengine sijafuatilia tu maana ukweli ni kuwa nimeshachoshwa na maneno bila matendo na nadhani hata JK amegundua kuwa Wanachi hawafuatilii tena hotuba zake maana sijasikia wakilalamika kuzi-miss hizo hotuba za kila mwezi!

Lakini ajabu nyingine ni ukimya wa Serikali na Ikulu? Yaani miezi miwli inapita bila hotuba kama tulivyozoeshwa lakini Slava Rwey kauchuna! Kwani Kazi ya Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu si pamoja na kutoa ufafanuzi wa namna hiyo? AU wanataka kutuambia kuwa hizo hotuba si muhimu tena? Ingawa ukweli ni kuwa JK azungumze au asizungumze to me it does not make any difference (nimechoshwa na porojo!).

Hata hivyo nategemea mwezi huu JK ataongea hasa kutokana na maswala ya Muungano ambayo yame-hit sana mwezi huu na pia kuhusu hatma ya Uchunguzi wa pesa za EPA ambao haileweki eleweki kama peza ni za Serikali au Wafanyabiashara wamejiibia wenyewe!
 
majibu ya waziri mkuu ni ya upeo wa chini. huyu bwana aligombea kuwaongoza watanzania, hayo majukumu ya AU siyo yakumfanya ashindwe kuongoza wananchi wake. AU kuna commission ina watu makini yeye ni chairman anapangiwa ya kufanya, ila hapa yeye ndo mkuu wa kaya. ni aibu tunafikia kuhoji kupitia BUNGE raisi haongei tena na wananchi wake!!!!!!!!!!!!!!!!!!!! lazima kuna more than a PROBLEM. Salva hajui anachokifanya yeye kuongelea minor and useless issues tuuuu.
 
Hata mimi jambo hli limekuwa likini intrigue sana.Kwakweli sikuelewa kwanini. Lakini rohoni kunakitu kikawa kinaniambia ni kwa sababu yale mambo ya msingi ambayo yanagusa maslahi ya wananchi hayuko tayari kuyazungumzia,kwahiyo anaona aibu.Na nadhani huu ndiyo ukweli !Lakini aibu mpaka lini ?Ningekuwa mimi ningepiga moyo konde,nikawaomba wananchi msamaha,nikawaeleza hali halisi, nikaahidi kutorudia makosa ya nyuma,halafu nikawaomba tusonge mbele.Nadhani hii ingesaidia kupunguza hasira yao.Kwa bahati mbaya viongozi wetu wanajiona wao kama miungu watu,kwahiyo kuwaomba wananchi msamaha ni jambo ambalo haliko katika ajenda zao na nadhani wamefika mahali ambapo sasa wanajiona kwamba wao hawakosei kabisa.Kiongozi mwadilifu ni yule anayekubali kukosolewa.Kwa mantiki hiyo ndugu yangu, tusitegemee hotuba kutoka ikulu,na kama ikiwepo itakuwa ni hotuba ambayo ni kwa ajili ya kulinda maslahi yao, na wala sio maslahi ya wananchi walala hoi.
 
Ndugu Yangu Tujaribu Kidogo Kuwa Fair...kwani Hata Wewe Ungekuwa Ndio Jk Ungeongea Nini Na Hao Watanzania Ambao Ni Wananchi Wako Wenye Kiu Na Shauku Kubwa Ya Kuona Ukitoa Hatua Za Utekelezaji Wa Matatizo Makubwa Yanayo Wakabili Ikiwemo Epa, Richmond, Zanzibar Sio Nchi, Mfumuko Wa Bei, Uduni Wa Maisha N.k...kwa Ufupi Ni Kkwamba Kijana (j.k) Hana Jipya La Kutueleza Watanzania..au Hata Kama Analo Anajuwa Fika Halitokuwa Na Manufaa Au Mabadiliko Yoyote Kwa Haya Matatizo Yanayowasumbua Watu Wake Aliowaahidi Maisha Bora...na Inamuwia Vigumu Kusimama Mbele Ya Watu Wake Waliomuaminia Kuwa Mkombozi Wao Ilihali Anafahamika Kuwa Na Uswahiba Wa Karibu Sana Na "wafavu Wote" Waliolitia Taifa Lake Matatizoni...kwa Ufupi Anaona Aibu...na Hatokaa Aongee Na Watu Wake Kwa Sababu Atakuwa Anawasaliti Anaokunywa Na Kula Nao...anaogopa Hata Kivuli Chake Sasahivi...sanasana Watanzania Tuwe Wastaarabu "tumsamehe" Na Tumruhusu Atuombe Radhi Ya "ki-utu Uzima" Kwa Kukubali Kuingia Kwenye Guiness Book Of Records Kwa Kuwa Rais Wa Kwanza Tanzania Kuongoza Kwa Kipindi Kifupi Cha Miaka Mi-5....inapendeza Hiyo. Zaidi Ya Hapo Naona Kama Utafika Wakati Watanzania Watamtolea Uvivu Na Kumfuata Mjengoni Pale Magogoni Wambebee Mabango Kuwa Hawafai Tena.
 
Hii habari haistahili kuwa breaking news!!!!!!!!!!!!!!!

Anyway, Jamaa hakujuwa kuwa hii kazi ni kubwa kuliko yeye. Hana jipya, ndiyo maana kila siku yuko kwenye ziara. Ni mtu wa kumuonea huruma tu.
 
Hotuba hizi zitakuwa na maana na umuhimu unaokusudiwa endapo zitakuwa LIVE na mbele ya waandishi makini au Bungeni na kisha aruhusu maswali. Vinginevyo hazina tofauti na zile tunazoziona kwenye taarifa za habari. Akina Bush wanaweza karibu kila wiki. Yeye anashindwa nini?
 
Huyu jamaa yuko pagumu sasa, amejitahidi kunyamaza kwa muda sasa juu ya issue zote nyeti. Akitokea popote kwa sasa, wanachosubiri wananchi sii lingine zaidi ya mambo nyeti yanayotukabili, asipoongea hayo anaelewa ni wazi atakuwa ameifukia "credibility" yake kwenye kaburi ambalo wananchi wameshachimba wanamsubiri aitumbukize mwenyewe halafu wao wafukie.

Kibaya hata mtandao masilahi umejichukulia nafasi ya kujiweka imara zaidi na kupanga mengi zaidi kwa nafasi ya prezidaa kunyamaza, mwenyewe yuko kwenye list ya kuchafuliwa na kuharibiwa umaarufu wake kisiasa.

Kwa sasa anatapatapa sana maana muda wa kujitetea kwa kugeukia popote ni kama hakuna, amejitega mwenyewe na atajitegua mwenyewe. Wananchi ni wavumilivu sana na wanamwangalia tu JK atarusharusha miguu mpaka wapi.
 
Hotuba hizi zitakuwa na maana na umuhimu unaokusudiwa endapo zitakuwa LIVE na mbele ya waandishi makini au Bungeni na kisha aruhusu maswali. Vinginevyo hazina tofauti na zile tunazoziona kwenye taarifa za habari. Akina Bush wanaweza karibu kila wiki. Yeye anashindwa nini?
Usanii wake wala nguvu zake hazimfikii mtu kama Bush, mambo yeshamzidi nguvu na kwa sasa atavyoropoka mara nyingi ndio atavyofupisha njia zake za uongo maana mwisho wa uongo utakuwa karibu kupita kiasi.
 
Namuonea huruma sana Rais wetu maana yeye kama utashi wake ulivyo alitaka awe Rais tuuu......si vinginevyo..hayo mengine yatajiendesha kilongox2 tu...hakuwa na ile JKN alivyokuwa anawauliza "utawafanyia nini watu wako"Jk hana lolote la kutufanyia zaidi ya kuandikwa kuwa TZ imeshawahi kupata Rais Mkwere...ndio raha yake....anakatisha tamaa...Rais si ujanja ujanja na kuweka ma best zako kila kona....uwaridhishe...no way...
 
Katika muda wote ambao Rais Mstaafu BW Mkapa hakuwahi kuacha kutoa hotuba yake kwa Wananchi kila mwezi hata alipokuwa nje ya nchi bado aliweza kuacha hotuba yake ikisubiri muda wa kuicheza kweny TV na Radio na tena Wanachi (mimi miongoni mwao) nilikuwa naisubiri kwa hamu siku zote!

Ni huyu Rais wetu JK ndiye aliyeiomba kazi ya Urais kwa hiyari yake tena bila kushawishiwa, na ni Mh. JK mwneyewe aliyetuatangazia na kutuahidi kuwa atakuwa akitoa hotuba zake kuzungumza na Wananchi kila mwezi na ni naamini kabisa Mh Rais wetu JK alijua wingi wa majukumu na kazi zilizo mbele yake kabla hajatuahidi kuzungumza nasi kila mwezi iweje leo Waziri Mkuu Mh. Pinda atuambie kuwa Rais ametingwa na kazi nyingi na safari ambazo baadhi ya Watanzania wanalalamika kuwa zimekuwa nyingi mno ashindwe kutoa hotuba zake za mwezi kwa vizingizio hivyo? Yaani Mh. Pinda anataka kutuambia kuwa wetu anafanya kila kitu yeye mwenyewe? Kuandika hotuba yeye! Kutembelea ndani na nje ya nchi yeye! Kujibu barua na malalamiko ya Wananchi yeye! Kila yeye, yeye!

Hapana, kuna jambo; la sivyo ndo tusubiri utimilifu wa ile methali ya Kiswahili-KIMYA KINGI KINA MSHINDO MKUU?
 
Kama hadi hii leo Raisi hajasema chochote kuhusu habari za Mauaji ya Albino hapa Tanzania ,wakati habari zimeanza kutangaa kwenye vyombo vya Kimataifa nimeona BBC nimeona Internationa Jazira na Channel France kuna hatari Kikwete akahusishwa na mauaji haya kutokana na principle za United Nation ,mkimuona mpeni salamu kuwa ajitahidi asije akakumbwa na balaa hapo baadae ,yaani akemee japo mara moja ,kukaa kimya chake wachunguzi wa Kimataifa na Haki za Binadamu wanampigs jicho ,kwa tahadhari nendeni mkazitazame principle za Umoja wa Mataifa Kikwete kama kiongozi wa Nchi hawezi kuvuka ikiwa jamii iliyopo itapanda katika viriri vya United Nation kitengo cha Haki za Binadaamu ,saa ingine naona Mheshimiwa anatamani kufa kwani Nchi inaonekana kumshinda na kusema hawezi anakufa kiungwana..
 
Back
Top Bottom