Uchaguzi 2020 Hotuba ya Tundu Lissu kuwania Urais: Neno wajumbe limepata maana mpya 2020

View attachment 1526252
Kabla siajaenda mbali sana, ninaomba nianze kwa kusema kwamba nimepata fadhaha kubwa jinsi ya Kuwaita nyinyi wote mliokusanyika hapa katika ukumbi huu kama baraza kuu la Taifa la chama chetu. Katiba yetu ya chama inawaita wote wajumbe wa baraza kuu la taifa. Hata hivyo,
tangu kura za maoni zianze kwenye Chama cha Mapinduzi na wajumbe kuwapiga spana wale wagombea wajasiliamali wa kisiasa was aliosaliti harakati za kiukombozi ambazo ziliongozwa na chama chetu na kuunga mkono juhudi. Hali ilikuwa mbaya kwa wajasiliamali hao wa kisiasa, kiasi kwamba mmoja wao alisikika akisema kwamba wajumbe si watu. Kwasababu ya maana hii mpya ya neno wajumbe ninaomba mniuie radhi na mnirushisu nisitume ni neno wajumbe. Badala yake ninaomba niwaite nyinyi wote viongozi, ili niweze kujinusuru kutoka katika masahibu ya kupigwa spana na wajumbe kama wale waliokimbilia CCM.

Wheshimwa vioongozi, nilipotangaza nia yangu ya kugombania u Rais wa Jamhuri ya Muungano kwa niabaya Chama Chetu, mnamo tarehe 08/06/2020. Nilieleza kwa kirefu kidogo ajenda mahususi za uchaguzi mkuu huu na kwanini ninaamini kwamba ninafaa kupewa dhamana huyo na Chama Chetu.

Watia nia wengine pia walishatoa maelezo yao kuhusu jambo hili. Leo mbele yenu viongozi wa barazakuu la Taifa, ninaomba nisirudie yale niliyoyasema 08/06/2020. Maswala hayo yote na mengine mengi yamefafanuliwa kwa kirefu katika ilani yetu ya uchaguzi mkuu ambayo tutaipitisha leo.

Na ilani hiyo na agenda zake zote ndiyo itayokuwa agenda mahsusi ya kwangu ambapo mtanipa ridhaa ya kupeperusha bendera ya chama chetu leo.

Ninaomba mniruhusu viongozi nielezee aina ya uchaguzi mkuu tutakao kuwa nao mwaka huu. Na aina ya mgombea wa Chadema anaehitajika kukabiliana na uchaguzi huo. Ili kukiletea chama chetu ushindi.

Waheshimiwa viongozi, uchaguzi mkuu huu utakuwa mgumu kuliko uchaguzi mkuu mwingine wowote katia historia ya mfumo wa vyama vingi vya siasa katika nchi yetu. Mheshimwa Mwenyekiti, katika mazingira haya halisi. mgombea au kiongozi wetu atakaegombea anatakiwa kuwa mgombea wa aina gani.

1. mgombea wa Chadema lazima awe mwenye historia ndani na nje ya chama ya kuaminika kwa msimamo wake.

2. Pili ndugu mwenyekiti, mgombea Uraisi wa Chadema awe ni yule mwenye uwezo wa kuunganisha nguvu kubwa ya umma inayohitajila ili kushinda uchaguzi mkuu huu. Hatutashinda kwa mvua za kawaida za masika ya kiuchaguzi, tutashinda kwa kutengeneza kimbunga cha wapiga kura a umma wa Watanzania. Amacho yeyote atakaejaribu kukizuia kitamsomba na yeye mwenyewe. Kimbunga hicho cha kisiasa hakiwezi kutengenezwa na mgombea asiye kuwa na hitoria yeyote ya mapambano ya kidemokrasia. Asiyekuwa na msimamo unaoeleweka na ambae uwaminifu wake ni wa mashaka.

3. Waheshimiwa viongozi, tunahitaji mgombea atakae we za kwainua wagombea ubunge na udiwani wa chama chetu. Mgombea asiye weza kuamsha hisia za wapiga kura hataweza kuingiza watu wetu barabarani. Kwa idadi inayohitajika pale kura zetu zitakapoibiwa au pale ambapo wagombea wetu walioshinda watakapodhurumiwa.
Kipengele No. 3 ndicho hasaa!
 
Don't forget that it's a LOW - MIDDLE INCOME COUNTRY
It is a Threshold Low-Middle Income Stage meaning it would have taken Kikwete about one year of Magufuli's five to reach meaning it will take decades under Magufuli to reach Threshold Upper-Middle Income Stage meaning we have a long way to go to become a Middle Income Country. We need change!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom