Huyu jamaa ni kilaza kabisa! Anatia aibu sana! Zote pumba tupu. Nimehamaki apa ile mbaya, hajui hata motion za watu. We MS ndo umeandika speech mbovu kama hii-toa taka hizi?
Hivi huyu ni raisi au bomu maana hajui kukubali kupanda kwa gharama za umeme ni kuongeza hali ngumu kwa mwananchi nawashangaa hata hao wanaofurahia hii hotuba au mnadhani mtapewa ukuu wa mikoa tuwe Positive tuache UNAFIKIIIIIIII!!!!!
Wewe una matatizo maana sidhani kama hii speech ni mbovu.
Sasa Jaji Werema wakati anatoa maoni yake kuhusu katiba alikuwa ame base wapi? au alikuwa hajui ofisi yake imemshauri nini Rais? au Ikulu imeamua nini kuhusu ushauri alioutoa? Sielewi vizuri haya mambo yanavyokwenda
Haya yote ni ndani ya siku 60 baada ya uchaguzi.
- Celina Kombani -- Serikali haina pesa wala bajeti ya kuandaa katiba mpya
- PM Pinda: Serikali inalipokea swala la katiba mpya, italifanyia kazi kwa kumshauri Rais
[*]AG Werema: Katiba mpya hapana, tuweke viraka kwenye hii iliyopo kama ni lazima- President: Anakubali katiba mpya ni muhimu, na ataunda tume kushughulikia hilo
Mh! tusubiri tuone tume ya uchaguzi itakuwaje, nina mashaka mengi.
JK ana sehemu yake na taratibu zake, vyombo vya dola, taasisi zoote zina taratibu zake, Bunge ambapo ndipo kwenye uwakilishi wetu kuna taratibu zake, na bado serikali kupitia mwanasheria mkuu wana taratibu zao. Hawa wote ni mihimili ya mchakato mzima wa uundwaji wa katiba.
La Mnyika litaendelea bungeni na la rais litaendelea au yatakutana mahali. Ila ikumbukwe la msingi sote na hao wengine angalau tunatambua na kukubaliana juu ya umuhimu wa katiba mpya. Mikakati itaainishwa, itachanganuliwa, itaratibiwa na kufikia kinachohitajika. Mungu ibariki Tanzania HASA WATU WAKE
NAOMBA NISAHIHISHE KICHWA CHA HABARI ILI ANGALAU KINGESOMEKA "Kiwete aonyesha msimamo, akubali katiba mpya" Hakuwahi kutoa kauli ya kukinzana au kupigana kuhusu katiba hadi asalimu amri. Tuwe fair
Rais wetu syo makini hta kdgo! Just imagine ktk speech hiyohiyo anasema gharama za shughuli/bidhaa mbalimbali zmepanda as justification ya kupanda kwa bei ya umeme, then anasema inflation imeshuka more than halfly! Mi apa sjaelewa wadau, plz nijuzeni?