Hotuba ya rais Kikwete ya kufunga mwaka 2010

Hotuba ya rais Kikwete ya kufunga mwaka 2010

Thanks to CDM, CUF, NCCR na wote walioshiriki kushinikiza, ishu ya katiba ni mwanzo na ni mafuriko Kikwete asingeweza kupingana nayo (upo hapo wewe topical?) zaidi ya kujiunga na mkondo wa upepo wa kimbunga, sasa ishu ni dowans lazima kieleweke
 
Sasa Jaji Werema wakati anatoa maoni yake kuhusu katiba alikuwa ame base wapi? au alikuwa hajui ofisi yake imemshauri nini Rais? au Ikulu imeamua nini kuhusu ushauri alioutoa? Sielewi vizuri haya mambo yanavyokwenda
  1. Celina Kombani -- Serikali haina pesa wala bajeti ya kuandaa katiba mpya
  2. PM Pinda: Serikali inalipokea swala la katiba mpya, italifanyia kazi kwa kumshauri Rais
  3. AG Werema: Katiba mpya hapana, tuweke viraka kwenye hii iliyopo kama ni lazima
  4. President: Anakubali katiba mpya ni muhimu, na ataunda tume kushughulikia hilo
Haya yote ni ndani ya siku 60 baada ya uchaguzi.
 
Kombani na Werema tuwakabidhi kwa Ocampo kwa kujaribu kuchochea machafuko. Bila kauli zao mbaya CUF wasingekuwa na sababu ya kuandamana
 
KIMEELEWEKA!... Kikwete amehofu kupingana na sauti ya umma. Attorney General Frederick Werema na Waziri wa Sheria na Katiba Celina Kombani wajiuzulu au wafukuzwe kazi kwa kupinga katiba mpya.

Inawatosha kwa sasa, mmeshatuliza mzuka. Kimeeleweka, duh!
 
Nadhani walimwonya Makamba safari hii. Hata naye amesema, mwenyekiti wake atalitolea tamko, nandilo litakuwa tamko la chama cha mapinduzi. Na hicho ndicho kimetokea leo hii.

Kikwete asingeweza kuitolea nje hoja ya katiba mpya kwa kuwa he has nothing to lose kwa sasa. Ameshaiba kura, amekuwa Rais wa magendo kwa uporaji wa haki za watanzania. May be atasimamia kipengele kimoja tu cha Rais kutoshitakiwa mahali popote kutokana na maamuzi na utendaji wake akitekeleza kazi yake ya Urais, na Uamiri jeshi mkuu.
 
Nadhani walimwonya Makamba safari hii. Hata naye amesema, mwenyekiti wake atalitolea tamko, nandilo litakuwa tamko la chama cha mapinduzi. Na hicho ndicho kimetokea leo hii.
Kikwete asingeweza kuitolea nje hoja ya katiba mpya kwa kuwa he has nothing to lose kwa sasa. Ameshaiba kura, amekuwa Rais wa magendo kwa uporaji wa haki za watanzania. May be atasimamia kipengele kimoja tu cha Rais kutoshitakiwa mahali popote kutokana na maamuzi na utendaji wake akitekeleza kazi yake ya Urais, na Uamiri jeshi mkuu.

Unaonaje kama tungeenda kwa mrengo wa kuongelea issues kuliko mtu/watu.
 
Sure,Viongozi wetu wengi wanapenda kurukia hoja hata ambazo sio zao.mbaya zaidi wanaongea km sio viongozi.yaani mara nyingi wanaongea wanatoa mawazo binafsi bila kujali systerm waliyomo. Ni tatizo kweli.

kwenye red si hivyo mkuu wakubwa huwa wanawatanguliza kwanza hao akina kombani kuangalia hali ya hewa mfano hapa kina mkwele waliona hali ni mbaya halafu ndio wanakuja wao HIZI NI STRATEGY ohooo
 
Kombani na Werema wajiuzulu. Wameropoka uongo ambao haukuwa na baraka kutoka juu! Vinginevyo washushwe vyeo.
 
Huyu werema nashindwa kuelewa ameokotwa wapi?hana kariba ya kuwa mwanasheria utafikiri mvuta bangi yeye kila kitu anatumia maguvu kama askali,hoja za kulazimisha...
 
Unaonaje kama tungeenda kwa mrengo wa kuongelea issues kuliko mtu/watu.

Kwa akili yako ya kawaida kabisa, tunawezaje kujadili mada hii, bila kumtaja Kombani,Werema, Pinda na Kikwete. Pia na wengine wengi waliojitokeza kuzungumzia issue hii muhimu?
 
Kwa akili yako ya kawaida kabisa, tunawezaje kujadili mada hii, bila kumtaja Kombani,Werema, Pinda na Kikwete. Pia na wengine wengi waliojitokeza kuzungumzia issue hii muhimu?

Kwa akili yangu kabisa naweza kumtaja Kombani kasema katiba mpya is a big no, issue ya kudiscuss ni kwamba kwa nini katiba mpya ni a big no, kifungu gani kimekiukwa etc, Sio koongelea watu, ooh Kombani hana akili kwa kusema katiba ni a big no, huu ni mfano tu msinimalize na mundu.
 
Sure,Viongozi wetu wengi wanapenda kurukia hoja hata ambazo sio zao.mbaya zaidi wanaongea km sio viongozi.yaani mara nyingi wanaongea wanatoa mawazo binafsi bila kujali systerm waliyomo. Ni tatizo kweli.
Tatizo ni kiongozi wao mkuu aliyewaweka pale walipo na wanafanya kwa niaba yake na yeye anasoma upepo unakoelekea.
 
Kwa akili yangu kabisa naweza kumtaja Kombani kasema katiba mpya is a big no, issue ya kudiscuss ni kwamba kwa nini katiba mpya ni a big no, kifungu gani kimekiukwa etc, Sio koongelea watu, ooh Kombani hana akili kwa kusema katiba ni a big no, huu ni mfano tu msinimalize na mundu.

Nimekupata mkuu. Kumbe kwa akili yako ya kawaida, Celina Kombani sio mtu.
 
Swali dogo la kujiuliza ni kuwa, je kwa tamko hili la Kikwete, ile hoja binafsi ya Mnyika, haina nguvu tena Bungeni?
 
Naona akili yangu iko fixed haiko mkao wa kuelewa. Endelea na uelewavyo.

Samahani kama nimekukwaza ndugu. Hebu tuendelee na mada bila kuchoka,kwani ndio kwanza ngoma iko kilingeni. Je Mnyika na hoja yake Bungeni ina haja ya kusikilizwa?
 
([FONT=Palatino Linotype, serif]Ndugu Wananchi;[/FONT]
[FONT=Palatino Linotype, serif]Natambua[/FONT][FONT=Palatino Linotype, serif] kuwepo kwa mazungumzo, katika jamii kuhusu uamuzi wa EWURA wa kukubali ombi la Shirika la Umeme (TANESCO) kuongeza bei ya umeme. Wakati mwingine mazungumzo yamekuwa na hisia kali na hata jazba kutawala. Wizara, TANESCO na EWURA wameeleza kwa ufasaha misingi iliyotumika mpaka kufikia uamuzi huo. Sina maelezo mazuri zaidi ya hayo. Ninachotaka kusema mimi ni kuwaomba Watanzania wenzangu kutokukubali suala hili la kibiashara na kiuchumi kugeuzwa kuwa la kisiasa na kutafutiwa majawabu ya kisiasa. [/FONT]

[FONT=Palatino Linotype, serif]Naomba tuamini [/FONT][FONT=Palatino Linotype, serif]na kukubali maelezo ya TANESCO na EWURA kwamba katika miaka minne hii gharama za uendeshaji, uzalishaji, usafirishaji na usambazaji wa umeme zimepanda kama zilivyopanda katika shughuli nyingine. Hivyo basi, kutaka bei ya umeme ibaki kama ilivyokuwa miaka minne iliyopita hautokuwa uamuzi sahihi kiuchumi na kibiashara kwa TANESCO. EWURA imefanya kazi nzuri ya kuchambua maombi ya TANESCO na kuyakubali yanayostahili na kuyakataa yasiyostahili kuwa sehemu ya bei. Kwa kufanya hivyo, watumiaji wa umeme wamelindwa wasibebeshwe mzigo usiostahili na Shirila la Umeme limewezeshwa ili lisiendeshe shughuli zake kwa hasara. [/FONT])



Mkulu JK hivi hujui kwamba gharama za uendeshaji za Tanesco zimetokana na mikataba ya kinyonyaji iliyoingia na makampuni feki na makampuni ya kinyonyaji? Kuwapa watanzania adhabu ya kulipa unyonyaji huu ni kuwaonea, mkulu tafuta namna ya kudhibiti malipo ya kinyonyaji yanayofanywa na Tanesco ili bei ya umeme ibaki kama ilivyokuwa. Heri ya Mwaka mpya.
 
JK ana sehemu yake na taratibu zake, vyombo vya dola, taasisi zoote zina taratibu zake, Bunge ambapo ndipo kwenye uwakilishi wetu kuna taratibu zake, na bado serikali kupitia mwanasheria mkuu wana taratibu zao. Hawa wote ni mihimili ya mchakato mzima wa uundwaji wa katiba.

La Mnyika litaendelea bungeni na la rais litaendelea au yatakutana mahali. Ila ikumbukwe la msingi sote na hao wengine angalau tunatambua na kukubaliana juu ya umuhimu wa katiba mpya. Mikakati itaainishwa, itachanganuliwa, itaratibiwa na kufikia kinachohitajika. Mungu ibariki Tanzania HASA WATU WAKE

NAOMBA NISAHIHISHE KICHWA CHA HABARI ILI ANGALAU KINGESOMEKA "Kiwete aonyesha msimamo, akubali katiba mpya" Hakuwahi kutoa kauli ya kukinzana au kupigana kuhusu katiba hadi asalimu amri. Tuwe fair
 
hizi ni geresha na sarakasi tu za CCM. Kama hawako organized kutoa tamko unison, tutawaaminije kwa hili. Anyway hapa wanajaribu kupoza mambo tu na mpaka nitakaapoona hatua za msingi zinachukuliwa ndipo nitaamini. Huyu si ndiye aliahidi mambo lukuki yasiyotekelezeka?

Mtakao kuamini aminini, but I'm still very skeptical. I will move with no president as a person till 2015.
That is!
 
Ananzidi kutuchefua tu. Tulitaka kumwona shujaa kwa kuanzisha mchakato wa katiba lakini tuko gizani hata hotuba yake hatuioni.
 
Back
Top Bottom