Hotuba ya rais Kikwete Bungeni Julai 16 - Full Text

Kwa takwimu zangu nilizonzo ni nchi moja tu Afrika ambayo haichukui hata senti tano toka mataifa ya nje katika bajeti yake ya Serikali. Nayo ni nchi ndogo iitwayo Eritrea. Ulaya hawaipendi kabisa kwasababu imetafsiri uhuru katika vitendo, na kwa maana hiyo wanashindwa kuibana kwa kutumia mbinu yao ya misaada.

Wakati Tanzania ikipata 44% ya pesa ya bajeti toka wafadhili, hii inamaanisha kuwa ukiwaudhi wafadhili basi hata mishahara ya watanzania haitakuwepo. Sasa utawaambia nini wanajeshi wakati hawajapata mshahara wao!

Usipoliona hilo kama ni hatua kubwa sana sijui nini kwako kitakuwa kikubwa. Wasalaam!

Zawadi je serikali imekopa shilingi ngapi kufidia nakisi ya bajeti yake. Tusije tukadanganywa kuwa tumepunguza utegemezi wa wafadhali wakati huo huo fuko la deni la taifa linapanda exponetialy. Denmark wakitataa kukupa msaada ukaenda kukopa kwa Libya kufidia ule msaada uliotegemea hakuna cha kufurahisha hapo.Hata hao Eritrea unaowasifu sio kuwa bajeti yao inajitosheleza.kiasi kikubwa chanakisi ni mikopo ambayo nadhani unajua masharti yake. Na sababu ya eritriea kukataliwa misaada ni bajeti yao kubwa ku fund jeshi.

Nitaungana na wewe kupongeza hili la kupunguza utegemezi wa misaada kwenye bajeti kama hakuna mikopo nyuma yake.
 
Hapo kabla sikujua kama Wizara ya Mifugo na Uvuvi inaitwa Wizara ya kitoweo, hadi alipotamka hivyo!
 
Amesamarise hotuba(summarize??) , vinginevyo ingechukua masaa 10 na wabunge wangesinzia.

La msingi ni kutaja mafanikio ya kiutendaji na ukuaji wa uchumi.

Kituko ninachokiona mimi ni kwa nini jambo la Lowassa kujiuzulu lisiwemo kwenye hiyo summary ya mheshimiwa wakati ni tukio kubwa la kitaifa lakini la kuwapa wasanii studio iliyogharimu milioni 50 liwemo. Yaani nyie mnavyofanya shortlist mnaacha mambo ya maana na kuchukua ya kijinga!!
 
Huyo ndo Kikwete muigizaji na si mchezaji halisi.

Mie naona kwamba sisi watanzania ni waburuzwaji hata kama hatutaki tutaambiwa tunataka.
 
Zawadi je serikali imekopa shilingi ngapi kufidia nakisi ya bajeti yake. Tusije tukadanganywa kuwa tumepunguza utegemezi wa wafadhali wakati huo huo fuko la deni la taifa linapanda exponetialy. Denmark wakitataa kukupa msaada ukaenda kukopa kwa Libya kufidia ule msaada uliotegemea hakuna cha kufurahisha hapo.Hata hao Eritrea unaowasifu sio kuwa bajeti yao inajitosheleza.kiasi kikubwa chanakisi ni mikopo ambayo nadhani unajua masharti yake. Na sababu ya eritriea kukataliwa misaada ni bajeti yao kubwa ku fund jeshi.

Nitaungana na wewe kupongeza hili la kupunguza utegemezi wa misaada kwenye bajeti kama hakuna mikopo nyuma yake.

Nakubaliana nawe kabisa kuhusu hili la mikopo, si tu kwa vile ulivyoliweka bali binafsi nilishangazwa na Rais ambaye amejaza takwimu nyingi za uchumi na kutosema lolote kuhusu mikopo ya nje 2005 na sasa hivi 2010.

Hata hivyo nipo njiani kuichanganua hotuba nzima ambayo nitaiandika hapa JF baada ya masaa 7. Katika uchanganuzi huo nitaandika juu ya yale ninayomuunga mkono na yale ambayo sikubaliani naye (critics).
 
Nakubaliana nawe kabisa kuhusu hili la mikopo, si tu kwa vile ulivyoliweka bali binafsi nilishangazwa na Rais ambaye amejaza takwimu nyingi za uchumi na kutosema lolote kuhusu mikopo ya nje 2005 na sasa hivi 2010.

Hata hivyo nipo njiani kuichanganua hotuba nzima ambayo nitaiandika hapa JF baada ya masaa 7. Katika uchanganuzi huo nitaandika juu ya yale ninayomuunga mkono na yale ambayo sikubaliani naye (critics).
Safi sana Zawadi, hivi ndivyo inavyohitajika... Nilidhani utafumba macho kutoangalia issue ya MIKOPO ambayo hakuigusia. Inapendeza kuyaangalia masuala haya kwa mapana sana maana yanatugharimu, baadae ikigundulika taifa linadaiwa mabilioni ya pesa tutabaki kuduwaa, vyanzo ni hivihivi, rais anajigamba sana, anadai mafanikio lukuki bila kusema WAPI alichemka kama rais... Too sad, walau hata wale wanaomuunga mkono wanaweza kuona 'usanii' ulikofanyika!

It's not like we hate him, ila asituchuuze...!
 
Mie nimechoka na Rais anapojimegea kwamba amefanikisha sana suala la kupata mikopo kwa wanafunzi wa elimu ya juu wakati wanafunzi hawa wamekuwa wakipata mikopo hii kwa shida sana,mara boom lichelewe kuingia,means testing yenyewe ni bomu,wengine wanapata mara mbili mbili.wengine wanapata nje ya utaratibu,Migomo ya hapa na pale ilikuwa mingi katika kipindi chake. Sioni cha kujifagilia hapa.
 
In 2007 RITES ltd of India won a contract from the Parastatal Sector Reform Commission (PSRC) to operate passenger and freight services on a concession basis for 25 years. The concession agreement was signed on September 3 2007, and was to begin on October 1 2007. The railway will be run as Tanzania Railway Ltd, with the government owning a 49% stake
 
Nilitarajia Mzee mzima atasema amesafiri mara ngapi kwenda nje ya nchi lakini niliambulia patupu.
 
Nilitarajia Mzee mzima atasema amesafiri mara ngapi kwenda nje ya nchi lakini niliambulia patupu.
Haikuwa hotuba ya kuongelea ALIKOCHEMSHA! Inaelekea hakuna serikali ilikoenda kombo, au angepagusa tu....

Inaelekea serikali ya Mkapa ilikuwa na makosa mengi sana lol
 
Wakulima waziponda Power Tiller

na Joseph Malembeka, Morogoro

MPANGO wa serikali kuboresha kilimo kwa kuwawezesha wakulima kuondokana na jembe la mkono na kutumia zana mpya ya matrekta madogo ‘Power Tiller’ umeelezwa kuwa hauna manufaa kwa wakulima kama ilivyokusudiwa.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti, baadhi ya wakulima Morogoro vijijini walisema wazo hilo linaonekana kuwa la kisisa kutokana na uingizwaji wa matrekta hayo kutozingatia tafiti juu ya uwezo wa kuyaendesha, mahali pa kuyapeleka, utendaji kazi wake na hata faida na hasara zinazoweza kujitokeza.

“Ni afadhali kutumia jembe la ng'ombe kuliko haya matrekta, kwanza yana gharama ya mafuta na matengenezo, halafu yameletwa hadi huku milimani, unadhani yatafanya kazi gani....haya yanafaa kwenye maeneo chepechepe (oevu) huku kwetu ni pakavu labda wangeleta matrekta makubwa,” alisema Selemani Kibwana wa Bwakila juu. Waliitaka serikali kufanya tafiti za kina juu ya mahitaji muhimu kwa wakulima badala ya kukaa na kuanzisha miradi ambayo manufaa yake kwa jamii ni madogo ikilinaganishwa na gharama zinazotumika. Uchunguzi uliofanywa na Tanzania Daima katika baadhi ya vijiji wilayani humo na manispaa, umebaini kuwa matreta hayo yanafanya kazi tofauti na matarajio ya serikali kwa kusomba vitu kama mkaa, kuni kutoka mashambani na kusafirisha watu kutoka sehemu moja hadi nyingine

Tayari Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Luteni Kanali mstaafu, Issa Machibya, ameagiza kuwachukulia hatua watu wanaotumia matrekta hayo madogo kinyume cha matumizi yaliyokusudiwa.
 
Huyo ndo Kikwete muigizaji na si mchezaji halisi.

Mie naona kwamba sisi watanzania ni waburuzwaji hata kama hatutaki tutaambiwa tunataka.

Naona tutumie neno Sisi watanzania au wengi wa watanzania wana kiherehere cha kuchagua viongozi wabovu/mafisadi hakuna haja ya kumchagua kiongozi yoyote yule mara ya pili kama mara ya kwanza hakutimiza tulicho tegemea kwake, mtu achaguliwe mara ya pili ni yule aliye onyesha uwezo wa kufanya kitu na si porojo
 
Pg 4 Ninapoangalia mafanikio makubwa tuliyoyapata katika kipindi hiki na kulinganisha na changamoto tulizokabiliana nazo, huwa nastaajabu na kujiuliza tumewezaje? Mimi siyo Sheikh na wala siyo mwanazuoni wa dini yangu. Ni mcha Mungu wa kawaida tu hivyo naamini kuwa ni rehema za Mwenyezi Mungu ndizo zilizotuwezesha kupata mafanikio tunayojivunia sote hii leo.

Ni kweli Muheshimiwa rais kipenzi chetu anamaanisha kutumia neno mafanikio tena makubwa au ni kuongeza hicho kivumishi ili kupanba hotuba.? Ni kweli rais anataka watanzania tuamini target zake na kile alichpenda kiwe kimefanikiwa kwa asilimia japo 80%?

Hoja yangu nyingine ni kuhusu chngamoto. Nadhani kila wizara na mkoa ina watu waliojaiwa kama maafisa wa sera na mipango. Je hawa moja ya kazi zao sio kuforecast risk, challenges na kupendekeza counter measures ili tifike kule tunakotaka kwa haraka. Kwa njaa kweli tushukuru hatukuomba msaada nje kama wenzetu wakenya lakini kwa suala la Nishati/ umeme hapa nampa below avarage

Ukiondoa Changamoto wa mdoororo wa uchumi wa dunia wich was new , changamoto za njaa, ukame, mgawo wa umeme hazitakiwi kuwa changamoto kwa CCM. hizi zinaweza kuwa changamoto kwa serikali kama ya CUF au ya CHADEMA. Wananchi tunaichagua CCM kwa kuwa tunajua ina experince of past mistake/sucess.Yet rais anatoa hotuba ya excuse za changamoto kama vile CCM imekamata madaraka miaka mitano iliyopita. JK anatakiwa awabane watendaji wake asikubali hizi excuses kirahisi.

Inawezekana wajanja wachache wanamuandikia JK hatuba ambazo sio hisia zake halisi.

Kwangu mimi JK nampa credit kwa serikali yake kuonyesha dhana ya utawala bora na kuwajibika kiasi fulani japo inaweza kuwa sanaa.au ni kutoka na ppressure ya wafadhili walau tumeonyeshwa mazingaombwe ya mramba , yona kufikiswa kwa pilato. walau tumeona EL kujiuzulu. Sanaa au Mazingaombwe haya Mkapa hakutuonyesha. Lakini inanishangaza yeye mwenyewe JK halioni hili
 

2. Yote kumi lililonipendeza katika hotuba yote ni upunguzaji wa tegemezi katika bajeti toka (2005,) 44% hadi (2010), 28%. Hapa ndipo aliponifikisha.
Kwa sababu hili lilikuwa linaniuma sana tena sana, tena sana. Maana kwa upande wangu ilikuwa kama kujidanganya ukaeleza eti uchumi unapanda kwa asilimia 7, lakini bajeti yako kila mwaka inaongezeka kwa kutegemea misaada toka nje.

Nategemea hali hii ya kupungua itaendelea kila mwaka wa bajeti mpaka ifikie 10% ndio moyo wangu utatulia.

Sijui kama unafuatilia kwa karibu mambo ya nchi hii? kama jibu lako ni ndiyo, basi unafahamu kwamba hilo unalojivunia, Kikwete na serikali yake wanasikitika kunyimwa misaada. Bajeti ya mwaka huu walinyimwa msaada dakika za mwisho kabla ya bajeti na ndo maana walitangaza kukopa benki.

Jaribu kuwa analytical ili uweze kuona illogical statements za mtu kama huyu. Hata hivyo haitawezekana hata siku moja nchi isiyoweza kukusanya kodi, yenye wafanyabiashara walio na immunity ya kulipa kodi, yenye wabunge wasiolipa kodi ikajiendesha yenyewe bila misaada!
 
Hotuba ya Raisi JK ina sura mbili, ya Kisiasa na ya maendeleo halisi ya kiuchumi. Kama Rais anayeingia katika uchaguzi ninakubaliana naye kuwa na sura hizo mbili kwani kila mwamba ngoma huvutia kwake. Hata hivyo ni bora kukaa kimya pale ulipoharibu kuliko kuwadanganya wananchi kwa kuleta takwimu za kupika, kwani ukimya kimsingi ni jibu tosha kwa watanzania.

Bila kupoteza muda napenda kuichambua hotuba huku nikija na nukuu za mara kwa mara.

Nitaanza na lile lililonifurahisha sana la kupunguza tegemezi katika bajeti. nukuu, "Aidha, tumeendelea kupunguza utegemezi wa wafadhili katika bajeti ya Serikali kutoka asilimia 44 mwaka 2005/2006 hadi asilimia 28 mwaka huu, 2010/2011"
Hili kwangu ni fanikio kubwa sana, na matarajio yangu hali iende chini mpaka 10%. Pamoja na kwamba Rais ameficha deni la Taifa ambalo ni 5.3 bilioni, kitu ambacho ilikuwa ni lazima akiseme. Hata hivyo deni ni tofauti na msaada, deni ni pesa yako ambaye utairudisha, lakini ile pesa ya msaada ni sawa tu na omba omba. Kila Nchi ina deni, siijui hata nchi moja hapa duniani isiyo na deni. Kwa mfano jirani zetu Kenya wana deni la 6.3 bilioni. Hata hivyo ni lazima angelisema hilo.

"wakati ule Ndugu Lawrence Masha... kuitazama upya mikataba ya madini. Kutokana na ushauri wa Kamati, niliagiza kufanyike majadiliano kati ya Serikali na makampuni ya madini kuhusu kipengele cha nyongeza ya asilimia 15 kwenye mtaji wa awali ambao haujarejeshwa. Kuwepo kwa kipengele hicho kulifanya makampuni yasilipe kodi ya mapato, hivyo kuifanya nchi isipate chochote mpaka mwisho wa uhai wa mgodi. Lengo letu ilikuwa kuondoa kipengele hicho. Nafurahi kusema kuwa tulifanikiwa katika mazungumzo yetu na makampuni......."
Hili nalo ni fanikio kubwa sana. Nashindwa kuelewa utasaini vipi mkataba na kampuni ambayo haitalipa kodi mpaka mwisho wa uhai wa mgodi! Hapa sitomuelewa Mkapa hata siku moja, kwani hizo nchi zenye hayo makampuni zimeweka mbele kodi. Kama safari zake ndio zimeleta mafanikio haya, basi watanzania tunayo haja ya kukubaliana naye maana zinalipa. Piga mwenyewe hesabu ya kodi ya miaka yote iliyobaki mpaka uhai wa mgodi uishe!

"Pato la Taifa liliongezeka kutoka shilingi 15.9 trilioni mwaka 2005 hadi shilingi 28.2 trilioni mwaka 2009 kwa bei za miaka husika."
Hapa sina maoni, kwani matarajio ya kila mtanzania ni kuongezeka kwa pato la Taifa ili tuukimbie umasikini uliobobea. Sasa kuongezeka mara mbili kwa kipindi cha miaka mitano sishawishiki sana kama ni kasi nzuri ukizingatia umasikini tulionao na changamoto ya majirani zetu EAF. Matarajio yangu pato lingeongezeka angalau mara 4 kwa miaka mitano.

"Vilevile, tumetimiza ahadi yetu ya kuimarisha ushirika nchini kama nguzo kuu ya kuunganisha nguvu za wanyonge kujiletea maendeleo. idadi ya Vyama vya Ushirika vya aina mbalimbali nchini imeongezeka kutoka 5,730 mwaka 2005 hadi 9,501 mwaka 2010. Vyama vya Akiba na Mikopo (SACCOS) kwa mfano, vimeongezeka kwa karibu mara tatu kutoka vyama 1,875 mwaka 2005 hadi 5,344 mwaka 2010. Aidha, akiba na amana za wanachama zimeongezeka zaidi ya mara tano kutoka Shilingi 31.4 bilioni mwaka 2005 hadi shilingi 174.6 bilioni mwaka 2010."
Suala la kuwaangalia wanyonge ni la muhimu sana. Mimi si mwanachama wa chama chochote kile cha ushirika, kwa hiyo nashindwa kuelewa kama njia hii ni bora zaidi katika kuwasaidia wanyonge au ndio tarumbeta kubwa lenye matokeo hafifu. Natarajia sana kuwasikia watafiti wa uchumi vyuo vikuu (UDSM, Mzumbe n.k) waje na takwimu za mafanikio/kufeli kwa mwelekeo huu. Kama unasaidia basi ni hatua kubwa.

"Tumeendeleza sera ya kutokuwepo na ushuru wa forodha kwa matrekta. Kwa sababu hiyo, idadi ya matrekta yaliyoingia nchini katika kipindi cha 2006-2009 ni 1,737; yakiwemo makubwa 362 na madogo (power tillers) 1,379. "
Huu ni utani kwa nchi ambayo imetangaza sera za 'KILIMO KWANZA'. Isitoshe 65 % ya wananchi wamejiajiri katika sekta hii ya kilimo, iweje leo katika watu zaidi ya mil 20 uzungumzie matrekta 1737. Hii ni sifuri lazima juhudi zaidi ifanyike.

"Aidha, katika kipindi hiki pia juhudi za kupambana na uvuvi haramu ziliongezwa. Kati ya mwaka 2006 – 2009 tulivuna samaki wenye thamani ya shilingi 783.3 bilioni na kuuza nje ya nchi samaki wenye thamani ya shilingi 597.5 bilioni."
Serikali imepoteza fedha nyingi sana hapa, ndio maana hata takwimu hazikutajwa kabisa. Tukiwa makini sekta hii ya uvuvi inaweza ikatuingizia pesa mara 50 ya hii inayotajwa na haya ndio maeneo ya kuongeza pato la taifa mara 4 kwa miaka 5. Bado wizi ni mkubwa na ni lazima ukomeshwe na wananchi wataarifiwe.

"2010 tumefanikiwa kupima na kutoa hati kwa jumla ya vijiji 6,129. Kwa sababu hiyo idadi ya vijiji vilivyopimwa na kusajiliwa vimefikia 10,682. Hii ni sawa na asilimia 97 ya vijiji 11,000 nchini. Mtakubaliana nami kwamba haya ni mafanikio makubwa." Wakati tunaingia katika soko la pamoja EAF, hatua hii ni muhimu sana kwani ni lazima tuondokane na dhana kuwa utaratibu wetu wa miliki ya ardhi bila stakabadhi. Na serikali lazima iwe na takwimu kuwa ni ardhi kiasi gani iko huru. Upimaji wa vijiji 6129 kwa kipindi cha miaka 5 ni mafanikio makubwa. Nina imani kuwa asilimia 3 ilyobaki itamalizwa kwa mwaka mmoja. Na wananchi popote pale walipo wajitahidi kupima ardhi wanayoikalia au wanayoimiliki kijadi.

"Kwa kushirikiana na wananchi, katika kipindi cha miaka mitano hii, tumeweza kujenga shule za sekondari 2,171 ikilinganishwa na shule 1,202 zilizojengwa toka uhuru mpaka mwaka 2005. .....Ongezeko hili limewezesha idadi ya wanafunzi wanaosoma sekondari kuongezeka toka 524,325 mwaka 2005 hadi 1,638,669 mwaka 2010."

Hapa nashindwa kuelewa kabisa ni miujiza gani aliyoifanya mpaka akaweza kuhamasisha ujenzi wa shule za sekondari 2,171 kwa kipindi cha miaka 5 na wanafunzi 1.6 mil.

. Upanuzi wa mafunzo ya walimu katika vyuo vikuu umeongeza walimu wanaohitimu kutoka
500 mwaka 2005 hadi 5,339 mwaka 2009.
Haya ni mafanikio makubwa sana. Kama kasi ni hii katika elimu basi tuntaondokana na tatizo lililopo la shule za sekondari zilizojaa bila walimu. Hata hivyo ni lazima ni kubali kuwa sielewi ni vipi JK ameweza kufanikisha hayo ukilinganisha na uchumi wetu ambao unasuasua. Elimu ni kitu muhimu, wahenga wanasema ni bora mwalimu mmoja kuliko vitabu 1000.

kandanda: "Tanzania imepanda kutoka nafasi ya 172 Desemba 2005 hadi nafasi ya 108 Aprili 2010."
Unapoahidi ni lazima utekeleze, hapa ahadi yake imetimia. Ni wakati wa vijana kutafuta ajira katika kandanda, ni muhimu kutumia nafasi hiyo.

"Jumuiya ya Afrika Mashariki imekuwa na manufaa makubwa ya kiuchumi kwa Tanzania kuliko vile tulivyotazamia wote. Mwaka 2005 Tanzania iliuza katika soko la Afrika Mashariki bidhaa zenye thamani ya dola za Kimarekani milioni 161. Mwaka 2008 iliuza bidhaa za dola milioni 353.1, na mwaka 2009 mauzo yalipungua hadi dola milioni 272.1 kutokana na mtikisiko wa uchumi. Na, ukweli ni kwamba bado hatujatumia ipasavyo uwezo wetu na fursa zilizopo."
Ni utani gani huuuu!!! Milioni 40 ya watanzania muuze EAF $ 161, $353, $272. hAPA HAKUNA EXECUSES, NI MBAYA MBAYA MABAYA ZAIDI. Si kabla ya mtikisiko wa uchumi wala wakati wa mtikisiko wa uchumi, namba ni ndogo sana. Juhudi ni lazima zifanyike kama tuko makini, vinginevyo tutatumiwa tu. Hii ni changamoto kwa kiongozi yeyote yule ajayo. Matarajio yangu ni 1000MIL $ MINIMUM. wAKE UP JK!!!!


Maeneo yafuatayo yanaongoza kwa kufanya vibaya
, Mheshimiwa Rais anasema "Serikali ya Awamu ya Tatu iliamua kutafuta kampuni ya uendeshaji wa reli ije isaidie kuendesha Reli yetu ya Kati. Hivyo ikapatikana kampuni ya RITES ya kutoka India." Sio tu serikali ya awamu ya tatu bali hata serikali ya JK bado haijafanya lolote katika kutatua adha hii. Huu ni usafiri mkubwa kwa mikoa zaidi ya mitano, iweje leo serikali ichezee shilingi kwa kipindi cha miaka mitano? JK hawezi kuwa na sababu yeyote ya kujikosha eti kwa vile si yeye aliysaini mkataba. Kwanini ameweza kufanikisha lile tatizo la madini na ashindwe hili? Ukweli kwa siku zijazo Wahindi wasipewe kontract yeyote nyeti kama hii.

"Tumeboresha utendaji wa Halmashauri zetu kimuundo, kifedha na kiutumishi ili ziweze kuchochea kasi ya maendeleo ya watu wetu. Katika kipindi cha miaka mitano iliyopita tumeongeza ruzuku kwa Halmashauri kwa zaidi ya mara tatu kutoka shilingi bilioni 780 mwaka 2005 hadi shilingi bilioni 2,728 mwaka huu."
Uchumi mzuri wa nchi unategemea sana uchumi mzuri wa Halmashauri. Halmashauri zimeoza na ni lazima zipewe changamoto ili ziweze kujiendesha na si kutegemea ruzuku. Tatizo kubwa hapa lipo katika elimu na maadili, kwani wafanyakazi wa halmashauri hawafahamu kabisa kuwa wanafanya kazi kuleta maendeleo ya watu katika halmashauri zao. Aidha uchaguzi wa madiwani lazima uwe makini. Hapa ninamaanisha kuwa ni muhimu kuweka vigezo vya elimu katika uchaguzi wa madiwani, na si kuwatoa wagombea toka vijiweni.

"Tumeunda upya chombo cha kuzuia na kupambana na rushwa (TAKUKURU). Sasa TAKUKURU ina ofisi katika kila wilaya na tumeiongezea uwezo wa kibajeti na rasilimali watu na vitendea kazi."
Hii ni bu-sh-it, sioni mafanikio yeyote hapa. Chombo hiki bado kinahtaji mabadiliko makubwa sana ili kiwe na ufanisi. Rushwa bado inapepea, na hatuwezi kufanikisha juhudi za kutetea haki za raia, utoaji wa haki na ukuzaji wa uchumi katika mazingira haya.



Baada ya haya yote napenda kusema kuwa kuna mengi mazuri yamefanyika na kuna mengi yaliyojificha ambayo si mazuri kwa mipango endelevu
. Licha ya upungufu wa niliyoyataja huko awali, napenda kusema kuwa mafanikio yaliyopatikana kwa kipindi cha miaka mitano yanatia moyo. Na napenda kuchukua nafasi hii kuwapongeza wote waliofanikisha maendeleo hayo.

Ni wakati huu wa uchaguzi ambao mwananchi anayonafasi ya kutathmini kama Mbunge au Rais amefanya ya kutosha katika eneo lake. Kuwa mbinafsi kidogo na angalia katika kata yako, wilaya, jimbo kwanza, sahau hata mkoa, kumefanywa nini katika kipindi hiki cha miaka mitano kabla hujaamua kumpigia nani. Achaneni na maneno, vuateni vitendo, na wala msiogope ku-risk kwani hiyo nayo ni sehemu ya maisha. Hakuna biashara isiyo na hasara.


Kwa kuhitimisha, nawaomba wananchi popote pale mlipo MFUKUZENI KIONGOZI YEYOTE YULE ALIYEKUWA MADARAKANI KWA KIPINDI HIKI CHA MIAKA 5 ATAYEOMBA KURA BILA KUTOA TAKWIMU (NAMBA) KWA KIPINDI ALICHOKUWEPO MADARAKANI.
 
Je sababu ya kupungua asilimia ya wafadhili haiwezi kuwa wao ndio wametukatia na sii ridhaa yetu wenyewe kupunguza tegemezi?.
 
Zawadi Ngonda, Ni rahisi sana kuchukulia takwimu kama hizi kama ni maendeleo ikiwa hufahamu ni kiasi gani kimepotezwa au ni kiasi gani cha ujazo kilitakiwa.

Nitakupa mfano mmoja mfdogo sana ktk Elimu.

Mwaka 1975 wanafunzi wa elimu ya msingi nchini waliweza kufikia asilimia 99 waliokuwa darasani pamoja na kuwepo shule chache kuliko leo hii. Na watu waknalaani mfumo mzima wa UPE kuwa unatazama zaidi quantity badala ya Quality..

Leo tunafuata mfumo ule ule isipokuwa chini ya bendera tofauti na hakika tumefikia asilimia hizo hizo 99 za watoto kuwa shuleni. Je, hizi takwimu za leo kweli zinakidhi haja na malengo ya maendeleo ya elimu nchini..
 
Namnukuu:
Mheshimiwa Spika,
Kwa upande wa wasanii hasa wa muziki, katika miaka mitano hii tumeshuhudia kukua na kustawi kwa muziki wa kizazi kipya na uigizaji wa filamu. Nasikitishwa sana na hali ya wasanii kutokupata malipo ya haki kwa kazi zao. Niliamua nijaribu kusaidia. Nilipokutana na baadhi ya wana muziki wa kizazi kipya wakanieleza haja ya wao
kuwa na mastering studio yao ili waweze kumiliki kazi zao. Nimeshawanunulia mtambo huo uliogharimu shilingi 50 milioni. Hivi sasa tumelipia mtaalamu mshauri kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam asaidie kutengeneza njia bora ya kusambaza kazi za wasanii wa muziki na filamu ili wapate malipo halali kwa jasho lao. Mafanikio ya zoezi hili yatatufundisha namna ya kuwasaidia wasanii wa fani nyingine pia.

Mheshimiwa kweli kafanya kazi kubwa sana, ni mfano wa kuigwa :smash:
Invisible
Despite a lot of shortcoming in JK's tenure but your quoting just a para of the speech and ridiculing his achievements is hitting below the belt.

Tuzungumzie mapungufu na wakati huo huo tusherehekee mafanikio. Hivi huyu jamaa kama kweli ameboronga sana kwenye kipindi chake cha urais angekuwa popular kama alivyo sasa???

Au tuseme wengi wa waTZ ni mbumbumbu???? Isije kuwa ile hadithi ya safari ya Aliyedaiwa kuwa mwendawazimu akiwa safarini na waliojidai wana akili ambapo walisafiri siku kadhaa bila ya chakula na njiani wakapita kwenye jalala la matunda ambayo mengine yalikuwa yameharibika ambapo wenye akili walimcheka sana yule mwendawazimu kwa akifakamia matunda yale lakini mbele ya safari baada ya siku kadhaa wale walidai kuwa na akili wakafa njaa na yule waliyemuona mwendawazimu akafika salama na mwenye afya.
 
Ilani ya CCM 2005 inasema:

25. Jambo la tatu la kipaumbele katika mchakato wa kujenga msingi wa uchumi wa kisasa wa taifa linalojitegemea ni mapinduzi ya viwanda na miundombinu ya kisasa. Viwanda ndivyo kiongozi wa uchumi wa kisasa. Dhana ya viwanda inakumbatia moja kwa moja dhana ya sayansi, teknolojia na uhandisi. Viwanda vina nafasi ya kimkakati katika mchakato mzima wa kujenga msingi wa uchumi wa kisasa wa taifa linalojitegemea. Mambo yafuatayo ni muhimu yazingatiwe:-

(i) Mapinduzi ya kilimo hayawezi kuwa endelevu bila ya mchango wa sekta ya viwanda; zana muhimu za kilimo hutengenezwa viwandani k.m. plau, trekta, mashine za kuvuna, mashine za kukoboa na kusagisha, n.k.

(ii) Mbolea na madawa hutengenezwa viwandani.
(iii) Mazao muhimu ya kilimo husindikwa na kutengenezwa viwandani na kuongezewa thamani.
(iv) Viwanda mama hutengeneza mashine, mitambo, injini mbalimbali, n.k
(v) Sekta ya viwanda ni sekta itoayo ajira zenye michepuo aina aina ya taaluma na ni uwanja wa kushamiri kwa sayansi na teknolojia.

JK baada ya miaka mitano anajisifia ifuatavyo:

Sekta ya Kilimo
Mheshimiwa Spika,
Ahadi tuliyoitoa ya kutoa kipaumbele cha juu kwa maendeleo ya kilimo tumeitimiza na matokeo yake yanaonekana. Mara baada ya kuingia madarakani tukatengeneza na kuanza kutekeleza Programu ya Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (Agricultural Sector Development Programme - ASDP). Aidha, ili kuipa Programu hiyo msukumo na kuwashirikisha kwa karibu wadau wa sekta binafsi mwaka 2009 tulibuni mkakati ujulikanao kama Kilimo Kwanza ili kutoa msukumo zaidi wa kuleta mapinduzi ya kijani nchini. Serikali imeongeza bajeti ya kilimo kutoka shilingi 233.3 bilioni sawa na asilimia 5.8 ya bajeti yote ya Serikali mwaka 2005/06 hadi shilingi 903.8 bilioni sawa na asilimia 7.8 ya bajeti yote ya Serikali mwaka 2010/2011. Ni dhamira yetu kuendelea kuongeza bajeti ya kilimo hadi kufikia asilimia 10 ya bajeti ya Serikali au hata kupita.

Mheshimiwa Spika,


Katika miaka mitano iliyopita, tumetimiza ahadi niliyoitoa hapa Bungeni ya kuhakikisha kwamba upatikanaji na matumizi pembejeo kwa wakulima unaongezeka. Tumeongeza fedha za ruzuku ya mbolea na pembejeo nyinginezo kutoka shilingi 7.5 bilioni mwaka 2005/06 hadi shilingi 143.8 bilioni mwaka 2010/11.


Mapinduzi ya uchumi hayaji bila mapinduzi ya viwanda. Je ni vingapi vimejengwa nchini ili kujenga uchumi wa kisasa wa Taifa linalojitegemea?


Zana za kilimo zinatengenezwa viwandani: ni ngapi tunatengeneza wenyewe mbona plau, trakta ndogo na kubwa zote tunaagiza nje – hata mbole hivyohivyo?

[FONT=AHIFFO+Tahoma]
Pimeni wenyewe ilani ilichosema na utekelezaji anaojisifia nao!
[/FONT]
 
Back
Top Bottom