Asalam,
Msiopenda utaratibu wa mimi kufuatilia na kusoma kwa makini hotuba za Rais wangu Mpendwa mtanisamehe.
Mwaka 2021 Fatma Karume (Shangazi wa Taifa ) aliandika andiko moja muhimu sana juu ya namna ya kumfahamu vema Rais wetu, naomba kumnukuu "Ukitaka kumwelewa Rais Samia na Hotuba Zake sikiliza anapoongea yale ambayo hayako katika hotuba rasmi anayoisoma, msikilize yale anayotupia katikati ya hotuba lakini nje ya yaliyoandikwa"
Tokea hapo nimekuwa makini sana kumsikiliza Rais kila ninapopata muda ajiwa mubashara na kama sina muda basi naitafuta recorded na maandishi. Huwa ninapita pia katika vyanzo mbali mbali kujaribu kuelewa alichosema, hasa kama sikumsikiliza mubashara.
Leo Asbh nimeamka na kupitia hotuba na maongezi ya Rais akiwa Arusha kwenye kikao cha wakuu wa mashirika ya Umma na Wenyeviti wa Bodi wa Mashirika husika. Kwa ujumla Mh. Rais ameongea mambo mazuri sana, amekemea sana matumizi mabaya ya mali za Umma katika mashirika ya Umma. Lkn katika hotuba na maongezi yake mengi, kuna kipengelee kimenigusa, anasema
"NAONA (nawaonea) AIBU KUWACHUKULIA HATUA WALIONIZIDI UMRI"
Ktika maongezi hayo wanaonekana Wazee wengi wastaafu wakifurahi na kutabasamu.
Sasa, Maongezi haya ya Rais dhidi ya wanaotapanya mali za umma yanatuweka katika muktadha gani dhidi ya mapambano ya Rushwa, Uongozi Bora, Uzalishaji na nidhamu katika kusimamia maendeleo ya Taifa.
Je, kama Rais anaona AIBU, anawatazama na kuwaacha TAKUKURU, POLISI, WATAWAWEZA KWELI HAWA?
Kesho nitapitia hotuba zake nyingine. Asalam
Msiopenda utaratibu wa mimi kufuatilia na kusoma kwa makini hotuba za Rais wangu Mpendwa mtanisamehe.
Mwaka 2021 Fatma Karume (Shangazi wa Taifa ) aliandika andiko moja muhimu sana juu ya namna ya kumfahamu vema Rais wetu, naomba kumnukuu "Ukitaka kumwelewa Rais Samia na Hotuba Zake sikiliza anapoongea yale ambayo hayako katika hotuba rasmi anayoisoma, msikilize yale anayotupia katikati ya hotuba lakini nje ya yaliyoandikwa"
Tokea hapo nimekuwa makini sana kumsikiliza Rais kila ninapopata muda ajiwa mubashara na kama sina muda basi naitafuta recorded na maandishi. Huwa ninapita pia katika vyanzo mbali mbali kujaribu kuelewa alichosema, hasa kama sikumsikiliza mubashara.
Leo Asbh nimeamka na kupitia hotuba na maongezi ya Rais akiwa Arusha kwenye kikao cha wakuu wa mashirika ya Umma na Wenyeviti wa Bodi wa Mashirika husika. Kwa ujumla Mh. Rais ameongea mambo mazuri sana, amekemea sana matumizi mabaya ya mali za Umma katika mashirika ya Umma. Lkn katika hotuba na maongezi yake mengi, kuna kipengelee kimenigusa, anasema
"NAONA (nawaonea) AIBU KUWACHUKULIA HATUA WALIONIZIDI UMRI"
Ktika maongezi hayo wanaonekana Wazee wengi wastaafu wakifurahi na kutabasamu.
Sasa, Maongezi haya ya Rais dhidi ya wanaotapanya mali za umma yanatuweka katika muktadha gani dhidi ya mapambano ya Rushwa, Uongozi Bora, Uzalishaji na nidhamu katika kusimamia maendeleo ya Taifa.
Je, kama Rais anaona AIBU, anawatazama na kuwaacha TAKUKURU, POLISI, WATAWAWEZA KWELI HAWA?
Kesho nitapitia hotuba zake nyingine. Asalam