Nimeamka ck nyingi ndo maana nina ufahamu juu ya jambo hili, Mkuu njia ndo hiyo, hizo zingine unazosema zimeshindikana. Mgomo wa kada yoyote una athari, walimu wakigoma kunakuwa hakuna elimu, madereva wa mabasi nao kunakuwa hakuna safari, Daktari naye wagonjwa wanakufa hiyo ndo kada yake, we unataka agome kula? nani atamsikiliza.
Na hayo ndo malengo ya mgomo wowote ili haki husika inayodaiwa ipatikane. Huwezi kuwazuia kudai haki zao kwa kisingizio cha watu kufa halafu madai yao yanashughulikiwa kisiasa, eti tunaendelea na mazungumzo,mpaka lini? hadi kufikia watu wakaamua kugoma ni kwamba haya madai ni ya muda mrefu. Mliolala amkeni sasa msikubali kuwa foolled kila siku kuwa serk haina uwezo ili hali fedha zinalundikwa kwe akaunt za viongozi huko uswisi na kujinunulia makasri hapa nchini na nje ya nchi, vijana wetu wanasoma kwa shida vyuoni ili hali tuna rasilimali nyingi ambazo iwapo mikataba isingalifungwa ktk misingi ya rushwa na ubadhirifu yasingalitokea hayo.
Wakati umefika sasa Kila mmoja asimame pale alipo adai stahili yake(wakulima, wanafunzi,wafanyakazi) M/mungu atalipa juhudi InshaAllah.
mamayeyo usiogope kufa, wacha siye tufie wodini, lakini watoto na wajukuu zetu wanufaike hapo baadae na mgao sawa wa raslimali za Taifa letu.Hakuna anaye sapoti mauaji lakini fahamu kwamba hakuna kudai haki kwa lelemama, ikifikia hatua hii ni lazima watu wafe ili kupata mapinduzi ya kweli na ufumbuzi wa kudumu wa suala husika(watu wangapi walikufa South Afrika wakati wa kupinga ubaguzi wa rangi? lakini leo ni historia na kamwe ubaguzi ule haurudi tena mpaka kiama I swear, lakini kwa kuwa watu waliamua kukataa bila kujali watu wangapi watakufa) .
Kwa kuwa watawala tulionao wamekwisha fahamu watu wlionao ni wa aina ya
mamayeyo ndo maana wanatuburuza. Tubadilike sasa tuache uoga usio na msingi ambao ndo umetufikisha hapa tulipo,
Wanasiasa wanatuona waTZ kuwa ni watu mabongolala tusiojuwa haki zetu, tuziondoe hizi mindset kwenye vichwa vyao.