Hotuba ya Rais Kikwete 30.6.2012

Hotuba ya Rais Kikwete 30.6.2012

Hana jipya lolote ni mzushi tu,anaomba madaktari warudi kazini wakati tayari zaidi ya madaktari 200 walishapewa barua za kufukuzwa kazini zaidi ya siku 2 zilizopita.
 
Huna hoja.

Waliyokubaliana kayasema na ambayo serikali imekataa na hayo kayasema waziwazi na ambayo hawajakubaliana kayasema waziwazi na kasema asiyeyataka hayo ambayo serikali imeyakataa aache mwenyewe kazi. Nini zaidi usichokielewa?Kama huna hoja kaa kimya kama wenzako.


Uamsho mnataka madaktari wa Iran waje ili baadae nao watake kulipwa fadhila ili ianzishe mahakama ya 'hedhi' na sharia za kishetani ndani ya Tanzania kwaajili ya kusuluhisha ndoa, talaka na kukatana viungo. Kwa hilo mmefeli jaribuni strategy nyingine.
 
Umefanya kosa kuchukulia nchi kama Marekani kuwa kielelezo cha migomo ya madaktari hapa Tanzania. Marekani madaktari hawagomi na kuna sheria kali kwani ikitokea mgonjwa anakufa kwa uzembe huo wa daktari ikiwa ni pamoja na migomo anashtakiwa kwa kosa la kusababisha kifo kosa linaloangukia second degree murder. Usicheze na Marekani wewe, vingienevyo kama hukubaliani na mafao kazini acha kazi nenda kafanye kwa unayeona atakupa mafao stahiki lakini si kuwekea rehani maisha ya wagonjwa.

C s, kuna mwandishi mmoja aliandika kitabu "Duniani kuna Watu" Na hapa JF kuna Watu: mradi kuna huo uhuru wa maoni basi watu hujiandikia tu. Kuna wale wasiojua nini kinaendelea Duniani au hata hapa nchi wana mifano ya Ajabu.
Wengi wao wanadhani Demokrasia ni Ruhusa ya kufanya chochote Unachotaka bila kujali sheria na taratibu zilizopo na hii Inawagusa hata Waandishi mahiri hapa JF wamekuwa ni washabiki na wakwepa ukweli.
 
Kikwete ahsante sana.

Sasa ondokeni mkafanye kazi zenu za private au mrudi kazini, uamuzi ni wenu, na huko mahospitali tutaanza kuwawekea tathmini ya kujuwa ni nani anaefanya kazi na anastahili kulipwa na nani asiyefanya. Mnalo?
wewe ni nani mpaka utishe watu hata kama wewe uko jikoni hivi mnafikiri mpo hapo kwa kutisha watu p.......mbfu!
 
Baba mwanaasha kafika ukomo wa akili yake.
 
Mkuu hakuna anaetishiwa Nyau, kila jambo lazima liwe na Mstari wake, haliwezi kwenda/kuendeshwa bila kuwa na "Limitation" yake.
The so called dhaifu amefikia yake now its up to the Doctors, tha ball is in Doctors court!

Ok lets assume madaktari nao wanakomaa, watawafukuza kazi? watapata wapi wengine, Hakuna daktari aliye idol duniani, wote wana kazi, na kwa taarifa yako daktari anaeweza kufanya kazi kwenye mazingira ya kitanzania ni hawa wa kwetu tu ambao wakuwa trained kujua ugonjwa kutokana na historia ya mgonjwa, maana hawana vifaa kwa ajili ya uchunguzi, unakuta hata xray machine hazifanyi kazi katika hospitali kubwa kama Bombo. kwa hiyo tusijidanganye tutaleta madaktari kutoka nje hawataweza kufanya kazi, na watanzania wataendelea kuteseka. EE JK acha kutisha watu, najua hupendi kushindwa lakini kwa hili ungesurrender kuokoa maisha ya raia wako.
 
kamaliza kuisoma.
mbariki baba mwanaasha
 
Ndio maana nchi kama Marekani dactari akigoma na kusababisha madhara kwa mgonjwa anafunguliwa mashtaka, na kama mgonjwa akifa anafunguliwa kesi ya mauaji first or second degree murder. Lakin mfanyakazi mwingine wa sekta nyingine atakachofanyiwa ni kufukuzwa tu kazini. Je umeona tofauti ya viapo hivyo vya kazini kwa watumishi.

Kabla ya ajira kuna mkataba ambao unasaini, iwe nchi za Ulaya, Marekani na hapa Tanzania, na kila aina ya kazi ina mikataba yake, huwezi kufananisha mkataba wa daktari wa binadamu na mkulima au mwalimu.
Mkuu madaktari hawaruhusiwi kugoma kama wanatimiziwa mahitaji yao muhimu ikiwa ni mishahara, marupurupu na mazingira mazuri ya kufanyia kazi, hii ni taaluma nyeti na pia lazima iangaliwe kwe unyeti wake. hakuna haki bila wajibu. serikali ina wajibu wa kuwaangalia vizuri madaktari wake na madaktari wana wajibu wa kuitumia vyema serikali yao. kwa tanzania daktari anafananishwa na sociologist (samahani sociologists) na haivyo hathaminiwi, katika mazingira kama haya anaruhusiwa kugoma. Kaulize marekani madaktari wanalipwa kiasi gani na mazingira yao ya kufanyia kazi yakoje ndio ulinganishe na Tanzania
 
""Kama kuna mtu wa Serikali kafanya, itakuwa kwa sababu zake binafsi na siyo za Serikali au kwa kutumwa na Serikali."""

Aisee..kwa hiyo kama JK/PINDA ameagiza kama JK/PINDA ana sababu zake binafsi?.
Hapa DHAIFU amesound kama anamjua vile aliyefanya hiki kitu.

Si kwamba aliyefanya ana yake kama Rais navyotaka tufahamu. Aliyefanya ana hakika baba mwenye nyumba hana muelekeo.

Baba mwenye nyumba ukiwa mlevi ukashindwa kuongoza familia, ni kawaida kila mtoto kujitungia njia ya kuishi. Wengine watakuwa malaya, wengine walevi, wengine wabakaji, nk. Hiyo ni kuonyesha hakuna central command.


 
Spring of mikosi, mabalaa yaja....yani litatoka hili linakuja lile na huo ndo mwanzo wa mapinduzi kwa Tanzania
 
Kikwete bado anatumia advantage ya watu kutojua mengi kuhusu mgomo.Dr anasoma miaka kibao na kazi ya udaktari si kazi ya furaha kihivyo kama huna wito.Ni kazi ambayo huwa unaifanya mpaka unakuwa addict na hata ukianzisha kahospital kako bado kama wewe ni mmojawapo ya madaktari tegeo bado utashinda huko. Mil hata 4 si big deal kihivyo.Nchi inayo hela ila ipo allocated katika ujinga na wizi.

Dr. anakosa vifaa hadi anaamua kuwa mbunifu katika mwili wa binadamu?Tabia ya kufanya kitu cha tofauti katika operation ili ufanikishe zoezi si nzuri kwani kufanya majaribio.Madactari, pilots, jamaa wa rockets, huwa hawatakiwi buni kitu kipya.Huwa wanatakiwa wafuate established and proven procedures.Wakitoka nje halafu kikaharibika kitu huwa mahakama inawahusu.Sasa km hawana vifaa vinavyotajwa katika procedures, itabidi waingie katika utendaji wa kinyume cha sheria ambao unawahatarisha.Sijui rais haoni hilo?Kuwa blah blah zake ndio si halali.Mgomo ni halali kama ilivyo kwa bima kabla ya kuingia mazingira hatarishi.
 
Ok lets assume madaktari nao wanakomaa, watawafukuza kazi? watapata wapi wengine, Hakuna daktari aliye idol duniani, wote wana kazi, na kwa taarifa yako daktari anaeweza kufanya kazi kwenye mazingira ya kitanzania ni hawa wa kwetu tu ambao wakuwa trained kujua ugonjwa kutokana na historia ya mgonjwa, maana hawana vifaa kwa ajili ya uchunguzi, unakuta hata xray machine hazifanyi kazi katika hospitali kubwa kama Bombo. kwa hiyo tusijidanganye tutaleta madaktari kutoka nje hawataweza kufanya kazi, na watanzania wataendelea kuteseka. EE JK acha kutisha watu, najua hupendi kushindwa lakini kwa hili ungesurrender kuokoa maisha ya raia wako.

Mkuu Asante Tusubiri yatakayojiri: Who will blink First!
 
kawajibu vuzuri madaktari....kama muajiri wa sasa hawezi kukulipa unachotaka ai unachostaili huitaji kugoma ....ni kuacha kazi ns kumfuata muajiri anayekulipa vizuri.....madaktari acheni kusumbua vichwa vyetu.....labda mtubainishie kuwa pesa hizo zipo mahala mmeziona...after all mlipwe m 3.5 kea lipi?....

Hiyo ni kufanya serikali kama nyumba yake binafsi. Raia hawezi kuambiwa asuse ajira ya serikali eti tu Rais hataki.
 
(Soma kauli yake kwenye sehemu ya hotuba yake) Kutokana na ukweli huo basi kama daktari anayeona kuwa hawezi kufanya kazi Serikalini bila ya kulipwa mshahara huo awe huru kuacha kazi na kwenda kwa muajiri anayeweza kumlipa kiasi hicho. Nasi tutamtakia kila la heri. Hana sababu ya kugoma ili ashinikize kulipwa mshahara huo. Asisumbuke, hatalipwa mshahara huo. Isitoshe, hana sababu ya kuendelea kuwa na mgogoro na mwajiri ambaye hana uwezo wa kumlipa anachokitaka. Huna sababu ya kumpa usumbufu mwajiri wa kukuandikia barua ya kujieleza au kukuachisha kazi. Kwa nini upate usumbufu wa kupata barua hizo na kuzijibu. Kwa nini upate usumbufu wa kuachishwa kazi na kutakiwa kuondoka kwenye nyumba ya Serikali ndani ya saa 24. Jiepushe na yote hayo kwa kujiondoa mwenyewe. Usipofanya hivyo, mwajiri anakuwa hana jinsi bali kukuondoa kazini maana unakwenda kinyume na sheria za kazi na maadili ya kazi ya udaktari."
 
Mkuu madaktari hawaruhusiwi kugoma kama wanatimiziwa mahitaji yao muhimu ikiwa ni mishahara, marupurupu na mazingira mazuri ya kufanyia kazi, hii ni taaluma nyeti na pia lazima iangaliwe kwe unyeti wake. hakuna haki bila wajibu. serikali ina wajibu wa kuwaangalia vizuri madaktari wake na madaktari wana wajibu wa kuitumia vyema serikali yao. kwa tanzania daktari anafananishwa na sociologist (samahani sociologists) na haivyo hathaminiwi, katika mazingira kama haya anaruhusiwa kugoma. Kaulize marekani madaktari wanalipwa kiasi gani na mazingira yao ya kufanyia kazi yakoje ndio ulinganishe na Tanzania

Mkuu nimerudi Nakukumbusha tu tuko Tanzania 7,000,000/= Kila ilivyo ni lazima kuwe na Uwiano. kwa hiyo Waalimu, Polisi, Magereza ,Jeshi, Maliasili nk wote watataka sio 7m lakini Uwiano wa hizo. Think!
 
wewe ni nani mpaka utishe watu hata kama wewe uko jikoni hivi mnafikiri mpo hapo kwa kutisha watu p.......mbfu!

Usiogope, hakuna anaekutisha wala aliyepo jikoni. Huo ndio ukweli, soma hotuba ya Kikwete kwa umakini, utanielewa nakwambia nini.
 
Mkuu madaktari hawaruhusiwi kugoma kama wanatimiziwa mahitaji yao muhimu ikiwa ni mishahara, marupurupu na mazingira mazuri ya kufanyia kazi, hii ni taaluma nyeti na pia lazima iangaliwe kwe unyeti wake. hakuna haki bila wajibu. serikali ina wajibu wa kuwaangalia vizuri madaktari wake na madaktari wana wajibu wa kuitumia vyema serikali yao. kwa tanzania daktari anafananishwa na sociologist (samahani sociologists) na haivyo hathaminiwi, katika mazingira kama haya anaruhusiwa kugoma. Kaulize marekani madaktari wanalipwa kiasi gani na mazingira yao ya kufanyia kazi yakoje ndio ulinganishe na Tanzania

Tusichukua mambo juu juu tu na katika kujalidili haya tuisome vizuri hotuba hiyo, tuifahamu, tuifahamu serikali na mpango wa shughuli zake za kila siku, kwani serikali haipo kwa ajili ya madokta tu, ipo kwa ajili ya umma mzima wa watanzania.

Ndugu Wananchi;

  • Mwaka 2004/2005, mshahara wa kuanzia wa daktari ulikuwa shilingi 178,700/=,
  • mwaka 2005/ 2006 tuliupandisha na kuwa shilingi 403,120/=. Tuliendelea kuupandisha
  • mwaka hadi mwaka mpaka kufikia shilingi 957,700/= wanazolipwa sasa.
  • Kiasi hicho ni mara mbili ya mishahara ya watumishi wa taaluma nyingine wenye shahada ya kwanza wanaoanza kazi ambao kwa wastani hupata shilingi 446,100/=.

Tunafanya hivyo kwa kutambua na kuthamini nafasi maalum ya madaktari katika jamii na ukweli kwamba bado tunayo safari ndefu ya kuziba pengo la madaktari nchini. Lakini inaonekana juhudi zetu zote hizo hazithaminiwi.

Ndugu Wananchi;
Sina budi kusisitiza kwamba tunapofanya hivyo tunaongozwa na uwezo tulio nao wa kulipa.


  • Kwa sasa hatuwezi kuwaahidi kuwa tunao uwezo wa kuwalipa mshahara wa kuanzia wa shilingi 3,500,000/= na posho zote zile.
  • Tukifanya hivyo malipo ya daktari anayeanza kazi yatakuwa shilingi 7,700,000/=. Kwa hakika kiasi hicho hatutakiweza. Si vyema kutoa ahadi hewa kwa watu tunaowaheshimu na kuwathamini kama walivyo madaktari.


Kutokana na ukweli huo basi kama daktari anayeona kuwa hawezi kufanya kazi Serikalini bila ya kulipwa mshahara huo awe huru kuacha kazi na kwenda kwa muajiri anayeweza kumlipa kiasi hicho. Nasi tutamtakia kila la heri.

  • Hana sababu ya kugoma ili ashinikize kulipwa mshahara huo. Asisumbuke, hatalipwa mshahara huo.
  • Isitoshe, hana sababu ya kuendelea kuwa na mgogoro na mwajiri ambaye hana uwezo wa kumlipa anachokitaka.
  • Huna sababu ya kumpa usumbufu mwajiri wa kukuandikia barua ya kujieleza au kukuachisha kazi. Kwa nini upate usumbufu wa kupata barua hizo na kuzijibu. Kwa nini upate usumbufu wa kuachishwa kazi na kutakiwa kuondoka kwenye nyumba ya Serikali ndani ya saa 24.


Jiepushe na yote hayo kwa kujiondoa mwenyewe. Usipofanya hivyo, mwajiri anakuwa hana jinsi bali kukuondoa kazini maana unakwenda kinyume na sheria za kazi na maadili ya kazi ya udaktari.

Mamlaka za ajira zimeanza kuchukua hatua hizo na wataendelea kufanya hivyo kwa wote wanaoendelea kugoma. Najua baada ya hatua hizo kuchukuliwa kuna manun’guniko ya kuonewa. Hivyo, mlitegemea mwajiri afanyeje? Ni bora kufanya hivyo ili ajue hana daktari aweze kufanya utaratibu wa kuziba hilo pengo na huyo ajae awe na mahali pa kuishi. Vinginevyo atakuwa anajidanganya kuwa anae daktari ambae hayupo kazini na wala hataki kufanya kazi.

VS Madai ya madaktari

Ndugu Wananchi;
Kati ya tarehe 10 Aprili, 2012 na tarehe 30 Mei, 2012, vilifanyika vikao sita vya majadiliano kati ya Serikali na Chama cha Madaktari. Katika mazungumzo hayo hoja au madai 12 ya madaktari yalizungumzwa. Mambo hayo ni haya yafuatayo:

1.
Posho ya kuitwa kazini (on call allowance) iwe asilimia 10 ya mshahara.

2.Posho ya kufanya kazi katika mazingira hatarishi (Risk allowance) iwe asilimia 30 ya mshahara.
3.Madaktari wapatiwe nyumba grade A au posho ya makazi ambayo iwe asilimia 30 ya mshahara.
4.Posho ya kufanya kazi katika mazingira magumu iwe asilimia 40 ya mshahara.
5.Madaktari walipwe posho ya usafiri ya asilimia 10 ya mshahara au wakopeshwe magari.
6.Madaktari wanaoanza kazi walipwe mshahara wa shilingi 3,500,00/= kwa mwezi.
7.Madaktari wapatiwe Green Card za Bima ya afya.
8.Hatua za kinidhamu zichukuliwe dhidi ya Watendaji Wakuu wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii.
9.Viongozi wa Kisiasa kulazimisha kupewa rufaa nje.
10.Madaktari waliofukuzwa warudishwe kazini.
11.Huduma za afya ziboreshwe nchini.
12.Posho ya uchunguzi wa maiti iongezwe.

Serikali haijaridhia yafuatayo:
Ndugu Wananchi;
Mambo mawili hayakuwa na muafaka kabisa kati ya pande zetu mbili. Jambo la kwanza ni posho ya kuitwa kazini (on call allowance). Kwanza sina budi kueleza kuwa Serikali imekubali kuongeza posho hiyo. Tangu Februari, 2012 posho iliongezwa kutoka shilingi 10,000/= hadi shilingi 25,000/= kwa daktari bingwa (Specialist), shilingi 20,000/= kwa dakari mwenye usajili wa kudumu (Registrars) na shilingi 15,000/= kwa madaktari waliohitimu ambao wapo katika kipindi cha mafunzo kazini (Interns). Viwango hivyo vya posho vinatumika hivi sasa.

Ndugu Wananchi;
Jambo la pili ambalo muafaka haukufikiwa baina ya Serikali na madaktari ni kuhusu mshahara wa kuanzia kazi wa daktari. Madaktari wanataka uwe shilingi 3,500,000/= wakati Serikali inasema kiasi hicho hatukiwezi. Serikali imeeleza utayari wake wa kuongeza mshahara kwa kati ya asilimia 15 mpaka 20 kama ambavyo itafanya kwa watumishi wote wa umma katika mwaka huu wa fedha. Kwa kiwango cha sasa cha mshahara wao, daktari ataanzia kati ya shilingi 1,100,000/= na 1,200,000/= kutegemea kiwango kipi hatimaye kitaamuliwa. Madaktari wamekataa katakata na wameng’ang’ania shilingi 3,500,000/=.

Mgongano wa madai ya Madaktari na watumishi wengine:
Ndugu Wananchi;
Mwaka 2004/2005, mshahara wa kuanzia wa daktari ulikuwa shilingi 178,700/=, mwaka 2005/ 2006 tuliupandisha na kuwa shilingi 403,120/=. Tuliendelea kuupandisha mwaka hadi mwaka mpaka kufikia shilingi 957,700/= wanazolipwa sasa. Kiasi hicho ni mara mbili ya mishahara ya watumishi wa taaluma nyingine wenye shahada ya kwanza wanaoanza kazi ambao kwa wastani hupata shilingi 446,100/=.

Tunafanya hivyo kwa kutambua na kuthamini nafasi maalum ya madaktari katika jamii na ukweli kwamba bado tunayo safari ndefu ya kuziba pengo la madaktari nchini. Lakini inaonekana juhudi zetu zote hizo hazithaminiwi.

Ndugu Wananchi;

Sina budi kusisitiza kwamba tunapofanya hivyo tunaongozwa na uwezo tulio nao wa kulipa. Kwa sasa hatuwezi kuwaahidi kuwa tunao uwezo wa kuwalipa mshahara wa kuanzia wa shilingi 3,500,000/= na posho zote zile. Tukifanya hivyo malipo ya daktari anayeanza kazi yatakuwa shilingi 7,700,000/=. Kwa hakika kiasi hicho hatutakiweza. Si vyema kutoa ahadi hewa kwa watu tunaowaheshimu na kuwathamini kama walivyo madaktari.
 
Back
Top Bottom