Hotuba ya Rais Kikwete 30.6.2012

Hotuba ya Rais Kikwete 30.6.2012

ataondoka tena kwa aibu sana...anakuja na hotuba yenye kutaka huruma ..hkuna haja ya kuunda jeshi limuondoa ataondoka yeye tu

Vumilia hadi 2015; nimekupa the easiest root maana naona unajipendekeza kwa US; unda jeshi tu watakuunga mkono haraka ..anzisha na daily hatred kwa waarabu, wairan na waislamu utapata pesa za kufa mtu..mkuu
 
Mkuu tuachane na mishahara kuna la uboreshaji wa huduma kwenye vifaa mbona hajajibu na hilo ndo linatuhusu sana watz!

Hilo ndilo linalotakiwa kuanyika, si uboreshaji wa mishahara tu, ila vitendea kazi mahospitalini ni kitu kinachoingia akilini mwangu, maana gharama za matibabu nje zitapungua.
 
Kazi ya muda mfupi ni tofauti na kazi ya masiaha inayochukua maelefu ya watumishi, jaribu kutofautisha kdigo utaona.
nikikuuliza wametumia criteria gani kuwalipa namna hiyo utanijibu?na kuna ulazima wa kuwalipa hela yote hiyo?hivi tanzania ni ya kwanza kutengeneza katiba mpya?wengine walofanya hivo wametumia gharama kama za kwetu?...na kumbuka kakupa mfano mmoja tu ya matumizi mabaya ya kodi zetu.....
 
Tarehe 26 Juni, 2012, Dkt. Mkopi alifika Mahakamani ambapo alikana kuwa yeye hahusiki na kuitisha huo mgomo lakini hakumtaja aliyehusika. Pamoja na rai hiyo, Jaji alimuamuru Rais wa MAT aka
watangazie wanachama wake kusitisha mgomo. Dkt. Namala Mkopi hajafanya hivyo hadi leo na mgomo umekuwa unaendelea kinyume cha Sheria.
Natambua kuwa Serikali nayo inatajwa katika orodha ya wanaotiliwa shaka. Mimi nimeshangazwa sana na hisia hizo kwani siioni sababu ya Serikali kufanya hivyo. Dkt. Ulimboka alikuwa mmoja wa kiungo muhimu katika mazungumzo baina ya Serikali na Madkatari.
Ni kweli kwamba yeye si mtumishi wa Serikali, hivyo hakustahili kuwa sehemu ya majadiliano haya. Kulikuwa na rai ya kutaka asiwepo, lakini nilisema wamuache maadam Madaktari wanamuamini kuwa anaweza kuwasemea vizuri zaidi kuliko wao wenyewe walioajiriwa na Serikali.

There you have it! Mnahitaji ushahidi zaidi?

 
he is a failure leader hafai hata kidogo analete bifu za mtaani kwenye jambo lamaana kama hili anafikiri ni bongo movie wanaetafuta sterling, hata nchi kubwa kama marekani wasingethubutu ku treat madaktari wao tena wa public sector kama huyu mtu anavyotaka kuonesha, hiii kw amtu mwenye akili anajua kwamba with or without kumuua ulimboka inatosha tena sana kuondoa serikali yake madarakani, na hapa ndipo napomuona lowasa muoga let him come out now atangaze kutokubaliana na serikali inavyohandle swala la madaktari, hata mimi nisiyekkubaliana na wizi wake ntakua upande wake, maana pesa alizoiba zinaweza kurudi lakini sio wagonjwa wanaotiririka kufa kama sisimizi mahospitalini na sisi tunamuangalia tu huyu ****** akicheza makida makida, mapinduzi yanataka uongozi, na huu ndi muda wa lowasa kutuonyesha tofauti ya yeye ni huyu boys to men, tulipofika Tanzania inataka kiongozi jasiri, Lowassa haihitaji CCM isipokua CCM inamuhitaji lowasa huu ndio ukweli, hakuna amri ya kukamata itakayotekelezeka juu ya Lowasa come out now Morani man ili Tanzania ipone humiuhitaji kikwete wewe kutafuta urais, show us the difference today, tunataka action kwa sasa toka i am telling you utakua musa wa Tanzania leo, Ulimboka could be fred wako ama any of those young people unaojua hawana makosa wanaingizwa kwenye haya kwa kuwa JK hana uwezo ni DHIFUEST MARA ELFU, come out now I am challenging you uone mungu atakavyokuinua na jeshi kubwa la wananchi litakavyokupokea huhitaji chama kuwa kiongozi,na huhitaji urais kuwa shujaa, do it now historia itakuandika soma hii hotuba ya kuandikwa na wakina michuzi na premy na Kim Kimbanga ndio utaelewa tuna deal na kituko gani

Umefanya kosa kuchukulia nchi kama Marekani kuwa kielelezo cha migomo ya madaktari hapa Tanzania. Marekani madaktari hawagomi na kuna sheria kali kwani ikitokea mgonjwa anakufa kwa uzembe huo wa daktari ikiwa ni pamoja na migomo anashtakiwa kwa kosa la kusababisha kifo kosa linaloangukia second degree murder. Usicheze na Marekani wewe, vingienevyo kama hukubaliani na mafao kazini acha kazi nenda kafanye kwa unayeona atakupa mafao stahiki lakini si kuwekea rehani maisha ya wagonjwa.
 
Madaktari sasa ni kusuka au kunyoa. Asiyekubali mshahara uliopo NJIA NYEUPEEE....kwenda kusaka mwajiri atakayewalipa 3,500,000/=. Andaeni njia pia kwa ajili ya WALIMU wanaodai nyongeza ya 100% ya mshahara wa sasa na wametangaza kugoma kuanzia mwezi huu wa Julai. WAIRAN wanakuja ku-replace nafasi za madokta na nyie WALIMU wapo vijana mitaani wale f4 & f6 bila shaka watatwaa nafasi zenu, ikishindikana walimu toka CHINA watakuja nchini.
 
Vumilia hadi 2015; nimekupa the easiest root maana naona unajipendekeza kwa US; unda jeshi tu watakuunga mkono haraka ..anzisha na daily hatred kwa waarabu, wairan na waislamu utapata pesa za kufa mtu..mkuu

sina haja ya kumwaga damu kama anayomwaga huyo headless chicken!!! na kwa mkwara aliopigwa ma wamarekan lazima afyate...
 
nikikuuliza wametumia criteria gani kuwalipa namna hiyo utanijibu?na kuna ulazima wa kuwalipa hela yote hiyo?hivi tanzania ni ya kwanza kutengeneza katiba mpya?wengine walofanya hivo wametumia gharama kama za kwetu?...na kumbuka kakupa mfano mmoja tu ya matumizi mabaya ya kodi zetu.....

Kwa madai ya Madaktari na wabunge kama kila mtumishi ajipangie mshahara nini kitawezekana? Ndio maana tuna idara ya utumishi ambayo kwa kushirikiana idara ya hazina hufanya tathmini ya pato la taifa vs matumizi ya umma, hapo unaweza kupata kima sahihi ambacho mtumishi anatakiwa alipwe. Kwa mtazamo huo wako unaweke egemeo la wenzo upande mmoja na wakati upande mwingine nyumba inazidi kuanguka.
 
Mwisho wa hotuba yake anaonekana kukiri kwamba kuna mtu/watu wa serikali wamehusika ktk huu ujambazi. Mimi nampa ushauri wahusika watolewe kafara,wakamatwe na kupelekwa mahakamani kulinda heshima ya nchi yetu. Hata kama aliyetoa amri ni Pinda,akamatwe na kushitakiwa.
 
Nampongeza kikwete amefanya uamuzi mgumu tuliotazamia, tunataka watu wenye kujali uhai wa binadamu kuliko wanaotanguliza masilahi yao kwa kuwekea rahani uhai wetu.

Nashaa unampongeza kw kushindwa kkutoa maamuzi. Alichokifanya ni kuwachongea kwa wananchi. Alichotakiwa kukifanya ni kuwafukuza wote waliogoma na si kuwapa options. Hayo ndiyo maamuzi magumu ambao hawezi kufanya na huo ndiyo udhaifu unaozungumziwa na Mnyika. Kama kweli serikali haina uwezo huo basi ingekuwa kila sekta pamoja na wabunge
 
Tarehe 26 Juni, 2012, Dkt. Mkopi alifika Mahakamani ambapo alikana kuwa yeye hahusiki na kuitisha huo mgomo lakini hakumtaja aliyehusika. Pamoja na rai hiyo, Jaji alimuamuru Rais wa MAT aka
watangazie wanachama wake kusitisha mgomo. Dkt. Namala Mkopi hajafanya hivyo hadi leo na mgomo umekuwa unaendelea kinyume cha Sheria.
Natambua kuwa Serikali nayo inatajwa katika orodha ya wanaotiliwa shaka. Mimi nimeshangazwa sana na hisia hizo kwani siioni sababu ya Serikali kufanya hivyo. Dkt. Ulimboka alikuwa mmoja wa kiungo muhimu katika mazungumzo baina ya Serikali na Madkatari.
Ni kweli kwamba yeye si mtumishi wa Serikali, hivyo hakustahili kuwa sehemu ya majadiliano haya. Kulikuwa na rai ya kutaka asiwepo, lakini nilisema wamuache maadam Madaktari wanamuamini kuwa anaweza kuwasemea vizuri zaidi kuliko wao wenyewe walioajiriwa na Serikali.

There you have it! Mnahitaji ushahidi zaidi?


Tuna mifano kadhaa ambayo vyombo vya usalama vinajichukulia sheria mkononi. Kama yaliyotokea kwa Zomba kuua wafanyabiashara wa madini kule msitu wa Louis Mbezi aliagizwa na serikali au ilikuwa ni mipango yake binafsi kuwachomowa waathirika?
 
Hakuna lolote hapo! Ameweka kwenye blog! Ana ogopa kuwaangalia watanzania, hana lolote. Eti ana sikitishwa kwa kile kilicho mkuta ulimboka.

Unafiki mtupu

Hapa Jombaa wewe ndio MNAFIKI sasa; maana jana waliitwa baadhi ya waandishi wa Habari kwa ajili ya kurekodi hotuba hii; na aliyetoa hapa kwenye Blog sio JK bali ni moja ya waandishi waloalikwa jana tunategemea pia kuiona kwenye TV zetu usiku wa leo kama ilivyo kawaida; sema JF tumeweza ipata mapema na kuijadili
 
Wote wawili mnalinganisha mbingu na ardhi!
Umefanya kosa kuchukulia nchi kama Marekani kuwa kielelezo cha migomo ya madaktari hapa Tanzania. Marekani madaktari hawagomi na kuna sheria kali kwani ikitokea mgonjwa anakufa kwa uzembe huo wa daktari ikiwa ni pamoja na migomo anashtakiwa kwa kosa la kusababisha kifo kosa linaloangukia second degree murder. Usicheze na Marekani wewe, vingienevyo kama hukubaliani na mafao kazini acha kazi nenda kafanye kwa unayeona atakupa mafao stahiki lakini si kuwekea rehani maisha ya wagonjwa.
 
Tarehe 26 Juni, 2012, Dkt. Mkopi alifika Mahakamani ambapo alikana kuwa yeye hahusiki na kuitisha huo mgomo lakini hakumtaja aliyehusika. Pamoja na rai hiyo, Jaji alimuamuru Rais wa MAT aka
watangazie wanachama wake kusitisha mgomo. Dkt. Namala Mkopi hajafanya hivyo hadi leo na mgomo umekuwa unaendelea kinyume cha Sheria.
Natambua kuwa Serikali nayo inatajwa katika orodha ya wanaotiliwa shaka. Mimi nimeshangazwa sana na hisia hizo kwani siioni sababu ya Serikali kufanya hivyo. Dkt. Ulimboka alikuwa mmoja wa kiungo muhimu katika mazungumzo baina ya Serikali na Madkatari.
Ni kweli kwamba yeye si mtumishi wa Serikali, hivyo hakustahili kuwa sehemu ya majadiliano haya. Kulikuwa na rai ya kutaka asiwepo, lakini nilisema wamuache maadam Madaktari wanamuamini kuwa anaweza kuwasemea vizuri zaidi kuliko wao wenyewe walioajiriwa na Serikali.

There you have it! Mnahitaji ushahidi zaidi?


mi nishasema kuwa huyu ndo mtuhumiwa namba moja ..kisha pinda namba mbili....
 
sina haja ya kumwaga damu kama anayomwaga huyo headless chicken!!! na kwa mkwara aliopigwa ma wamarekan lazima afyate...

Kumbe unapiga mkwara tu..JK anajua namna ya ku-deal na hiyo mikwara wewe..

Nilikuwa nakupa namna itakayokupa easiest money..endelea kuwa na hatred kwa waarabu, wairan na waislamu wa Tanzania na nje..utakuwa darling wa US..na watakupa support umwondoe huyu JK muislam mbaya sana anaharibu Tanganyika aliyoiasisi st. nyerere..ok
 
Katika hotuba yake ya jana, ya kila mwisho wa mwezi aliyotoa mheshimiwa Rais na kusema kama kuna daktari anayeona hawezi kufanya kazi bila malipo wanayotaka atafute mwajiri mwingine awezaye kulipa hivyo. Kwa kauli hiyo natafsiri kwamba anataka wafukuza kabisa na kuleta hao wa kigeni na kama si hao wa kigeni sijui ana option gani? Kwa mtazamo wangu sasa naona huyu rais wetu sasa amechemka kwa kiwango kilichopitiliza na inabidi afikirie sana juu ya matamshi ayatamkayo na azipitie vizuri hotuba anazoandaliwa. Sasa nadhani amejimaliza mwenyewe! Hivi anadhania akifukuza madaktari option nyingine ya madaktari atapata wapi? Serikali imetumia fedha nyingi sana kusomesha hawa madaktari CREAM OF THE NATION halafu kirahisi tu kwa kutumia dhamana aliyopewa anasema watafute mwajiri mwingine! Inamaanisha ni sawa na ku invest katika biashara ya kiwanda halafu una invest fedha nyingi kukiandaa kiwanda hicho na kiwanda kinapotaka anza zalisha na kukurudishia fedha unasema sioni faida ya hichi cha ndani, naachana nacho nakifunga kiwanda hichi cha ndani ntakuwa na import bidhaa toka viwanda vingine vya nje zenye gharama kubwa kuliko zile ambazo zingezalishwa na kiwanda hicho cha ndani. Je, vipi ile fedha iliyo invest na muda iliyotumia kuwasomesha na vyuo tulivyofungua kwa fedha nyingi. Hana uchungu kabisa na rasilimali zilizotumika kuwa invest hao madaktari anataka kuwatisha kwa divide and rule. Embu afukuze madaktari wote halafu tuone wengine atawatoa wapi na kwa fedha zipi? Labda kama atawakodi kwa pesa zake za mfukoni na si kuchezea fedha za walipa kodi!

Haiingii akilini gharama kubwa serikali itakayoingia na gharama ya kuwahudumia hao wageni na matatizo ya lugha/communication watakayoyapata hao madaktari wageni! Sidhani kama wabunge wa nchi hii wataridhia upuuzi huo wa kuzidi kuitia serikali katika gharama kubwa namna hiyo wakati ilikwisha invest kwa hawa wazawa! Sijui kama wanaomshauri wamefanya cost-benefit analysis na kujua faida na hasara ya hatua anayotaka kuichukua. Washauri wa rais na serikali acheni kushauri vibaya jamani!

Mimi namshauri rais atumie hekima na busara kutatua hili suala! Kwanza akae na hao madaktari atekeleze matakwa yao yote angalau kwa awamu. Madaktari ni watu waelewa sana, angalau angeanza na kununua vifaa tiba na madawa kwa awamu kwa kuongeza budget ya vitu hivyo. Pili angeongeza mishahara yao kwa kiasi fulani na si lazima iwe milioni 3.5. Kama kima cha chini kilikuwa ni shilingi laki 9 why asiongeze kufika angalau milioni 1.5 kwa kufanya comparison na nchi jirani na za Afrika na kuona viwango vya chini vya mishahara vinavyolipwa madaktari wa nchi nyingine angalau kuwe na uniformity na nchi jirani na hizo nyingine? Unadhania madaktari wangekataa? Anasingizia madaktari wanataka mishahara 3.5m na zaidi, je serikali imejaribu kuongeza kidogo toka hiyo laki tisa ya sasa mapaka angalau hata 1.5m halafu ndo iseme kama madaktari wamekataa? Hizo gharama za kununua vifaa, madawa na kuwaongeza mishahara pamoja na matakwa yao mengine kama na nyumba na risk allowances, green cards n.k unadhania zitakuwa kubwa kuliko kuwakodi madaktari wa nje wenye masharti magumu kuliko hawa wazalendo wa hapa ndani?

Angalia hapo Mh. Rais sio unataka kujimaliza wewe mwenyewe na serikali na chama chako! Hivi unadhania ukijishusha na serikali yako ukawatimizia matakwa yao madaktari (na watumishi wote wa sekta ya afya) kwa awamu/portions unadhania hili tatizo litaendelea? Hivi ukijishusha ukaonyesha kutimiza matakwa ya madaktari ambayo yako genuine utaonekana wewe ni dhaifu? Amini nakwambia utaonekana dhaifu sana Mh. Rais kama utatunisha misuli na hali kuendelea kutotimiza matakwa yao! Amin nakwambiwa utaonekana una hekima na busara kama utatekeleza matakwa yao yote kumi kila moja kidogo kidogo na madaktari wakaendelea na kazi na kutoa huduma kuliko hilo unalolifanya la kutunisha misuli.

Nadhani pia hao washauri wako wasipokushauri kama ninavyokushauri naomba wachukulie hatua mapema especially huyo waziri mpya wa afya na washauri wengine wote wakushaurio kuhusu hilo. Haiwezekani ku-substitute madaktari wazaedha wa kwa madaktari wageni wenye gharama? Ni gharama kubwa sana na jambo hili halitekelezeki na competency ya hao watu sijui kama inajulikana vizuri na pia compatibility kwa mazingira ya hapa bongo na vitendea kazi feki vya hapa pamoja na mawasiliano ya lugha sijui kama wataweza kuperform. Au ndo unaendelea kuwafanya watanzania na fedha zao za kodi vichwa vya wendawazimu? Si vizuri kufanyia majaribio yasiyo na tija fedha za watanzania!

Hivi unataka uniambie kada ya madaktari na watumishi wengine wa afya sio cream of the Nation? Hivi kada hiyo kweli serikali haijainvest pesa nyingi kusomesha hao madaktari n.k. Hivi hao wanaosema kuwa sijui wamdaktari wasiringe na wasideke je, wao waseme kiukweli wanaweza waka compare uwezo wao kitaaluma na wa madaktari? IQ za madaktari ziko juu sana na hivyo thamani yao haiwezi kulinganishwa na watu wengine. Sikatai kuna watu ambao sio maktari wana IQ kubwa pia. Lakini majority ya madaktari wana IQ kubwa ukilinganisha na za watu wa kada nyingine nyingi. Ni watu wachachea mbao sio madaktari wamepita huo uwezo na ndio maana kwa kuelewa hilo nchi nyingi sana Duniani zinawathamini na kuwalipa fedha nyingi kutokana na ugumu wa elimu waipatayo, ugumu wa kazi zao na pia kwa ajili ya kiwango cha akili kitumikacho katika kazi hiyo na ugumu wa kazi yenye na risk kubwa iambatanayo na kazi hiyo. Nasema ugumu wa elimu hiyo kwa kuanza kumchambua daktari toka alipoanza shule mpaka anapofikia kufuzu. Muda wote ana kazi ya kuongoza darasani kuanzia elimu ya msingi, sekondari mpaka chuo kikuu anapokutana na wakali wenzake ambao ukiwa lele mama shule ya chuo hauimalizi. Sasa itakuwaje madaktari walipwe mishahara sawa na hao waliokuwa wakiwaongoza? Mimi kwa kweli nawaheshimu sana madaktari na wanasayansi wengine kwa uwezo walionao na bidii juhudi na maarifa waliyojaaliwa na mwenyezi Mungu na ugumu wanaoupitia katika shule zao. Mimi binafsi sistahili kupata kiwango sawa na wao nikijilinganisha uwezo wangu mimi na wa madaktari. Naunga sana mkono haki wanayoidai, na wale wanaopinga nadhani ni suala la wivu wa kipuuzi baadhi ya Watanzania tulionao. Kama unauwezo na akili ya kama daktari aliyonayo na unaweza kufanya afanyayo daktari kajaribu leo kidogo kukaa darasa moja na daktari halafu mpewe pepa uone utakachopata na daktari utakachopata halafu ndo utathmini kama unastahili kuwa sawa na daktari kimaslahi.

Nchi zilizopiga hatua kimaendeleo zili invest sana kwenye sayansi na wanasayansi wake. Lakini sisi watanzania tuna invest kwenye siasa na porojo kuliko uhalisia. Sijui kama tutaendelea? Jamani serikali iwathamini madaktari wake badala ya hao wa nje. Iwape value fo money madaktari wake iliogharamia kuwasomesha. Kama kila solution ya kila kitu ktk nchi nchi hii ni ku-import basi serkali yetu haina uhalali wa kuitwa serikali kwani itakuwa imekosa ubunifu na kutegemea akili za nje. Tunakopa nje, misaada toka nje, malighafi toka nje n.k. Hivi kweli hatuna vya kwetu? Na kama tunavyo je tunavithamini?

Embu fikiria hao madaktari wa nje wakija watakavyothaminiwa na watakavyosikilizwa kwa kupewa kila wakitakacho kuanzia magari, nyumba nzuri, anasa nyingine, mishahara mikubwa, n.k na bado ufanisi wao unaweza usiwe kama wa hawa wa kwetu! Kwanini serikali ni rahisi kuwasikiliza wataalamu wa nje kuliko wa hapa kwetu?

Serikali itumie busara katika hili ama sivyo itakosa uhalali wa kuitwa serikali na pia kukosa kura 2015 au vurugu kutokea. Pia serikali iwaadhibu watu wachache ndani ya serikali waliohusika na kutaka kumuua dr. ulimboka na wale wanaoishauri vibaya! Isichezee ovyo fedha za wananchi wa Tanzania wakati solution zipo hapa ndani na ni rahisi kutekelezeka.

Imagine mikoa yooote na wilaya zote zipate madaktari toka nje! Je jambo hili linawezekana? Liyumba na akina mramba wameshtakiwa kwa maamuzi/matumizi mabaya yaliyoiingizia seriakli hasara je, ni kwanini na huyo asemaye ataleta madaktari nje na huyo asemaye atafukuza madaktari nje asishtakiwe kwa kuiingiza serikali hasara ya kutotumia ilicho invest badala ku import na kuiingizia serikali hasara?

Pia nashauri jumuiya ya madaktari wamfiche dr. ulimboka na aende kwenye ubalozi wa marekani au nchi nyingine makini akahifadhiwe kwani popote alipo atafuatwa aangamizwe! Na wale wenye nyeti na ushahidi wa kuteswa kwake wajifiche wapiganie vita hii mafichoni na wauweke ushahidi wao kwa maandishi na kurekodi na wawape mawakili na wawakilishi wa vyama vya upinzani na jumuiya za kimataifa ushahidi wao kabla hawajawindwa na kuangamizwa.

Mungu ibariki Tanzanian, madaktari na Dr. Ulimboka.
 
mi nishasema kuwa huyu ndo mtuhumiwa namba moja ..kisha pinda namba mbili....

Ukipeleka kesi yako mahakamani utakuwa umewasaidia sana wananchi wa Tanzania

Unaweza pia kupeleka kesi yako US, Hague etc..
 
Nashaa unampongeza kw kushindwa kkutoa maamuzi. Alichokifanya ni kuwachongea kwa wananchi. Alichotakiwa kukifanya ni kuwafukuza wote waliogoma na si kuwapa options. Hayo ndiyo maamuzi magumu ambao hawezi kufanya na huo ndiyo udhaifu unaozungumziwa na Mnyika. Kama kweli serikali haina uwezo huo basi ingekuwa kila sekta pamoja na wabunge

Katika hili la madaktari ni sensitive, yataka busara, alichofanya ni kutoa mwanya kwa waliofuata mkumbo wabaki makazini na wale ambao hawako tayari na wameamua kuendelea na madai yao basi wajui hakuna la ziada ila kufukuzwa kama ilivyostokea Bugando na KCMC. Kwa hili hakuna option isipokuwa madaktari wasiokuwa flex-able basi waachie ngazi ili kunusuru maisha ya watanzania. Haiwezekani kuchezea uhai wa binadamu kwa kiwango hiki, mbona Dactari wao wanaonja sana na kumkimbiza nje ya nchi, je wananchi wangapi wanaofia hospitalini kwa uzembe wao?
 
Tuna mifano kadhaa ambayo vyombo vya usalama vinajichukulia sheria mkononi. Kama yaliyotokea kwa Zomba kuua wafanyabiashara wa madini kule msitu wa Louis Mbezi aliagizwa na serikali au ilikuwa ni mipango yake binafsi kuwachomowa waathirika?

Kwahiyo kwenye hii kesi as you stated "vyombo vya usalama" vilijichukulia sheria kwa maslahi ya nani? Mimi ninachoona ni clear contradiction kwenye hotuba nzima, achana na ya Zombe kwanza kwa suala hili itakuwa kazi sana kwa Kikwete and co kusafisha mikono yao, hawatamaliza hii ishu kama walivyozoea kwa kusema wacha ni upepo utapita..........the damage is already done mi friend
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Huna hoja.

Waliyokubaliana kayasema na ambayo serikali imekataa na hayo kayasema waziwazi na ambayo hawajakubaliana kayasema waziwazi na kasema asiyeyataka hayo ambayo serikali imeyakataa aache mwenyewe kazi. Nini zaidi usichokielewa?

Kama huna hoja kaa kimya kama wenzako.

Wewe ndio huna cha kuzungumza kazi kuitetea Serikali inayowaua raia wake wasio na hatia kila siku siku,mbona Serikali haikuzungumzia kuhusu uboreshwaji Wa mazingira ya kazi/vitendea kazi vinavyomuwezesha daktari kumtibu binaadamu mbona hii point Serikali inaikwepa sana na matokeo yake wanazungumzia mishahara na posho za madaktari?
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Back
Top Bottom