Erythrocyte
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 117,730
- 218,305
Wema wa Sabodo si huu kiduchu wa kusaidia vyama vya siasa nchini Tanzania , Huyu mtu kifo chake ni pigo kuliko hata mapigo mnayoyajua , Kuna haja ya Hotuba ile ya Mbowe kuletwa hapa JF kwa njia ya Video (Naitafuta) , Ifike wakati sasa Bendera ziwe zinapepea nusu mlingoti kwa baadhi ya Wazalendo kama Sabodo wanapofariki , Ikiwezekana hata mizinga ivurumishwe hewani watu hawa wanapofariki , haiwezekani tunawaenzi wezi na makatiri lakini tunawaacha watu wema kama hawa .
Kumbe kuna wakati Sabodo alibeba dhamana ya Nchi kwenye uhaba wa Mafuta (nadhani ni diesel na Petroli) , cha kushangaza anasubiriwa Mbowe ndio ayaseme haya ! hivi viongozi wanaoficha historia hii hawaijui au hawataki ?
Iko haja ya viongozi wapya wachanga wa nchi hii kufundishwa kwanza walioifikisha hii nchi hapa ilipo badala ya kupewa vyeo kwa mtindo wa Koneksheni na Uchawa .
Uhakika ni kwamba over 90% ya viongozi wa nchi hii wakiwemo mawaziri na viongozi wa ccm hawajui Uzalendo wa Sabodo na ni Aibu kwao na Aliyewateua , Unateuaje watu wasioijua Nchi yao ?