Ndugu yangu umenikumbusha mbali. Ukifika Butiama, nyumbani kwa Baba wa Taifa, sehemu inaitwa Stendi, hapo saa 12 asubuhi tayari kuna ugali na nyama vinakuwa vimeshaiva. Hicho chakula wenyewe utasikia wanasema, "Lete rungu kwa kichuri". Maana yake ni ugali wa mtama uliochanganywa kwa mhongo kwa nyama ya mbuzi. Pembeni lazima kuwe na pilipili.
Ndugu yangu umenikumbusha mbali. Ukifika Butiama, nyumbani kwa Baba wa Taifa, sehemu inaitwa Stendi, hapo saa 12 asubuhi tayari kuna ugali na nyama vinakuwa vimeshaiva. Hicho chakula wenyewe utasikia wanasema, "Lete rungu kwa kichuri". Maana yake ni ugali wa mtama uliochanganywa kwa mhongo kwa nyama ya mbuzi. Pembeni lazima kuwe na pilipili.
Kaka yangu hapo hali maana ana Vidonda vya tumbo...... Hahahaaa umenivunja mbavu Mkuu.
Tajen majina ya hizo hotel tukajikumbushe pande za mara na mwanza
charminglady unamuona huyu mdogo wako anazungumzia JJ CLUB, ukimwambia Makaranga Disko atashangaa.we marura ni noma asikwambie mtu, pale JJ CLUB napo kulikuwa dogo langu moja lilikuwa linapika supu ya ukweli ile noma
Kwangu imekuwa news baada ya kukuta mgahawa mmoja jijini Dar wateja wake wakila ugali mida ya saa mbili asubuhi. Je hii ni kawaida?!
Maoni yako ni yapi ikiwa karibia hotel kadhaa zikaamua kupika saubuhi chakula kinacholiwa mchana,bila kujali ni ndizi,wali ama ugali na maharage
Arusha,Manyara,Singida ugali asubuhi tena majogoo ndo mlo wetu. Mh Dr W.P. Slaa,Mh Tundu Lisu,Mh L.Nyalandu wanajua vizuri utaratibu huu wa lishe.Hata mimi wakati niko single nilikuwa nagonga zege asubuhi jijini DSM.
Wazee wetu zamani ndo mtindo wao wa kula,chakula cha asubuhi kiliheshimiwa sana,hasa kwa wanaume.Babu yangu aliwahi kunieleza kuwa wanaume hukung'oli wanawake majogoo,hivyo asubuhi ni vizuri ushibe.Chai asubuhi sio mpango kabisa.
aliokwambia ugali unaliwa mchana tu ni nani?
Mkuu tunaangalia tamaduni zetu waTz kwa kawaida ni mchama ama usiku ila hii ya asubuhi itawashangaza wengi
Na maeneo yanayokaliwa na wakurya kwa wingi.Hii ipo zaidi Nairobi
kuna hotel ngapi mji uaoishi wanapika ugali asubuhi? na kama ni chache kwanini?
fika hotel yoyote ile na hasa kwa migahawa yote apo tarime mjini,ila ya butiama ni baraa