Hotel kubwa Morogoro kubomolewa

Hotel kubwa Morogoro kubomolewa

hivi inakuwaje kama ana legally documents zote za kiwanja?inabidi serikali iwajibike
 
Utwambie kabisa hotel ni ya nani make kuna huyu POPOMA mmoja anajiita GENTAMYCINE ametuhabarisha kuwa eti ni ya Babaake DogoJembe... sasa wengine tukajiongeza pengine familia imeponzwa na ile mikatuni yake anayorusha kutwa kuchwa mitandaoni kumkashfu Rais wa mioyo ya Watanganyika Mheshimiwa saaana Dr.JJP Magufuli.
Hoteli ni ya jitu la TRA lakini limeijenga miaka mingi yawezekana limedunduliza
 
Last edited by a moderator:
hivi inakuwaje kama ana legally documents zote za kiwanja?inabidi serikali iwajibike
Hawa watendaji wa serikali wanahitaji maombi!si umeona mbwembwe za makontena yaliyokamatwa Tegeta....
 
Imejengwa juu ya bomba LA mafuta LA TAZAMA no lazima ibomorewe tu

gorofa kama hili nondo zake zitakuwa meter kumi chini ya ardhi ndo msingi wake uliko sasa hilo bomba liko umbali gani?
 
Kwa taarifa kutoka kwa watu wakaribu wammiliki anasema sehemu iliyoingilia eneleo la wazi nisehemu ilipojengwa chumba cha jenereta na sehemu ya fensi
 
Imejengwa juu ya bomba LA mafuta LA TAZAMA no lazima ibomorewe tu

Wewe unajua msingi Wa ghorofa? Haiwezekani kuchimba msingi ukute bomba kubwa kama la tazama halafu uendelee kujenga. Hao watu wa tazama, ardhi, maji, halmashauri,mkoa walikuwa wapi hadi ghorofa likaisha na kutumika? Si haki hata kidogo
 
Ndio maana hii nchi haiendelei. Wachawi kila kona, Mtu unaweza ukadhani wachawi ni wale wanaoruka na ungo usiku, kumbe wengine wanatembelea Kilimo kwanza. Unaanzaje kubomoa jengo kama hilo. Kwani wao walikuwa wapi tangu msingi unaanza kuchimbwa?

Ili tujifunze kuheshimu utawala wa sheria, bora lianguke chini/ Utajengaje kwenye bomba kubwa la mafuta ta Tazama ukasema huo ni uchawi????
 
Hii serikali ya awamu ya 5 tusipokuwa makini itakuwa ya kibabe na kikatili sn!
Busara zinahitajika kwa suala la kujenga juu ya Bomba la Mafuta (Tazama) na eneo la wazi.
Mf. Kuna kuhamisha bomba kwa gharama za mjenzi au kujenga Handaki ardhini kwa ajili ya repair and Maintenance.

Ujinga mwingine wa serikali tusishabikie hovyo hovyo, walikuwa wapi wakati anajenga?
Acha siasa wewe! Watanzania lazima walazimishwe kufuata sheria ndipo maendeleo yatakuja. Enzi za pesa kuongea kwisha. Kutekeleza sheria Ubabe unatakiwa sio kuleta s?asa. Livunje ili wengine wajifunze. Hizi sio enzi za ser?kali kuogopa wanyepesa.
 
Mbona mnatetea ufisadi!!! Naamini mwenye hiyo hoteli alipata kiwanja kiujanjaujanja na inawezekana pia hana kibali cha ujenzi wa Hoteli ya aina hiyo kwa sehemu kama hiyo, kwa wale wanaoijua vizuri Msamvu ya Morogoro. Imekula kwake ba watu wa aina hiyo.

Tuwe makini kuweka "assets" za kudumu kwenye maeneo yasiyo na uhakika.

TAFAKARI CHUKUA HATUA

Simtetei mvunja sheria asilani, ila afisa ardhi na mipango miji wasiachwe. Ni dhahiri wame-bank mlungula kupindisha mambo.
 
Hoteli ni ya jitu la TRA lakini limeijenga miaka mingi yawezekana limedunduliza

Sasa mkuu mbona unaendeleza speculation? tutajie jina la huyo afsa wa TRA hujui kuwa wameamriwa kutaja mali zao na madeni? Tumbua jipu wewe au unaogopa usaha??
 
Huyo mmriki nae boya tu atafanyaje uwekezaji mkubwa namna hii bila kufanya upembuzi yakinifu? hotel kubwa namna ile unaijenga juu ya bomba la mafuta?? no wonder pesa ya uwekezaji huo itakuwa ni dirtyMONEY

Hujui mmiliki? Haitabomolewa hiyo
 
Hiyo hotel ni kweli imejengwa karibu sana na lilipopita bomba la Tazama hakiwanja chenyewe hakieleweki kipo kama eneo la wazi vile.hata wakibomoa poa tu wakome ni pesa zetu wa TZ zilitumika kuja hiyo hotel.
 
Sheria huwa zinafuatwa vizuri kwenye nchi zenye mipango, huwez kubomoa mali za watu kwenye nchi ambayo asilimia 80 haijapimwa, bongo hata leo hii ukinunua kiwanja mwaka kesho utaambiwa ni eneo la makaburi
Kwa hyo we unapendekeza tuendelee kuishi kienyejienyeji? Nyie ndo mlinufaika na system ya kifisadi. Libomolewe iwe funzo kwa majinga na majizi yote
 
Back
Top Bottom