jamani nani anawatetea kcmc?,huyo anayetetea uoza wa pale inawezekana ni mtumishi wa pale au ana ndugu yake pale,
hebu nenda hata leo pale kcmc kuanzia hapo casuality pameoza,ni kweli wagonjwa wanafikishwa pale wakiwa mahututi unaona kabisa manesi wanapishana tu wala hawaangalii cha mgonjwa mahututi wala nini,kcmc ya sasa si ile ya zamani ambako huduma zilikuwa nzuri sana,leo kama huna ndugu yako pale kcmc inaweza kukuchukua siku nzima bila kupata huduma.
kuna huu mfumo wa watumishi kubeba mafaili ya wagonjwa,hapo ndo kasheshe ya kufa mtu.
ukifika medical record,unaonyehsa kadi yako,mpaka faili lipatikane ni mwendo wa saa moja na zaidi,likipatikana mpaka lipelekwe sehemu ya malipo inakuchukua mwendo wa saa moja na ushee,ukishalipia faili linapelekwa kwa daktari mpaka ufikiwe ni mwendo wa zaidi ya saa moja.
sasa fikilia kama unamgonjwa anahitaji matibabu ya haraka hawezi kufa kabla ya kumuona daktari?.
nenda kwenye wadi za wagonjwa,watu wamelazwa chini utafikili ni maiti wa ajali wanaosubiri kutambuliwa na ndugu zao,hapo bado mnasema huduma ni nzuri kcmc?,tusifanye ushabiki kwenye masuala yanayogusa uhai wa binadamu,wateteeni kcmc lakini ukweli unabaki pele pale kwamba huduma ni mbovu tena ile mbayaaaaaaaaaaaa.haina tofauti na mawenzi ambayo sasa inaitwa hospital ya rufaa ya mkoa,huu ni upuuzi kweli kweli.
Hospital ya rufaa ya mkoa isiyokuwa na dawa,isiyokuwa na huduma ya X-Ray,isiyoweka dawa kidonda cha mtu aliyeumia.
sasa hivi wana mradi wa kuuza dawa,zile dawa za bei ghali zinauzwa nje ya hospital kwenye duka la dawa la kilimani,na hawana hata haya wanakwambaia nenda kanunue hizi dawa kilimani,je kwa nini isiwe sehemu nyingine?,hapo kilimani wana ubia gani hao madaktari wa hospital ya mawenzi?,lakini atatokea kichaa mwingine akatetea huduma nzuri mawenzi kama wanavyotetea kcmc,ajabu na kweli.