Chiya Chibi
JF-Expert Member
- Jul 6, 2011
- 484
- 110
Imebadilika pale serikali iliamua kuchangia huduma, na ukwel ni kwamba serikal inachelewa sana kutoa inachoahidi na pengine kutokutoa kabisa
Labda upande huo wako vizuri!
kwa hiyo na serikali inahusika? bad government if they are concerned...
dr Riwa umejibu vyema sana lkn nina swali moja dogo sana ninalotaka kuuliza hivi hospitali ya mkoa ya iringa, madaktari wake hawana ugumu ambao huko kcmc na kwingine wana upata? je manesi wake nao wanalipwa tofauti na huko kcmc kiasi kwamba hawa wanaweza kuuza bidhaa wodini??Ukiangalia kijuu-juu unaweza dhani tatizo hapo ni manesi...lakini ukiangalia kwa upeo mkubwa zaidi utagundua tatizo ni system. Sitegemei nesi anayelipwa hela ya kutosha kukimu maisha yake na familia yake atafanya biashara ICU badala ya kuconcentrate na wagonjwa.
Penda usipende...wahudumu wa afya mahospitalini (wakiwemo madaktari na manesi) ni binadamu, wana mahitaji kama binadamu wengine. Na hayo mahitaji yasipotimizwa, ni dhahiri ufanisi wa hao wahudumu hautakuwa wa kiwango cha kuridhisha...and this is true for every other sectors, wafanyakazi hawako makini na kazi zao wala hawajitumi wasipopata kipato cha kuweza kukimu mahitaji yao. Na wengine wataengage kwenye vibiashara mbali mbali ili kufill hiyo gap inayomiss..sababu watoto lazima waende shule, nyumbani paliwe, kodi ya nyumba ilipwe, watu wavae, akiba kwa huduma mbali mbali kama afya, na nauli ya kwenda kazini.....natimizaje hayo yote kama mshahara wangu haunitoshi hata kwa wiki 1?!
You expect 100% from people....pay them accordingly, in short of that...expect less!
Another issue ni vifaa vya kufanyia kazi (kugundua magonjwa, kutolea tiba na ufuatiliaji wa matibabu) as well as vya kujikinga na maambuki kwani kila siku unadeal na wagonjwa wengi tu na kuna risk kubwa ya kuambukizwa magonjwa mbali mbali...and funny thing is...you dont even afford hizo huduma za afya ambazo wewe mwenyewe unazitoa. Tuliwahi kumchangia hela daktari mwenzetu kununua dawa za kansa ya damu (chemotherapy) kwa mwanae aliyekuwa akiugua kansa ya damu...wakati mwenyewe anatibia watoto wa watu wenye tatizo hilo..can you imagine!?
Usikurupuke tu na kubebesha lawama zote wahudumu wa afya wakati mfumo wenyewe wa utoaji huduma hizo ni mbovu umekufa kwisha kabisa, hasa katika hospitali za level ya chini kama dispensaries, health centres and district hospitals. Bajeti ya wizara ya afya haikidhi hata for service delievery tu, sahau prevention part...tunategemea kuomba omba kwa wafadhili...unategemea manesi wasiuze sabuni? unataka wauze nini....wawe dada poa usiku?!