Hospitali ya KCMC Moshi! limebaki jina tu.

Hospitali ya KCMC Moshi! limebaki jina tu.

Bongo kila kitu kimebaki History even history yenyewe
 
Aisee serious mwenyewe ni shuhuda nimeacha sick sheet nikaenda Kilimanjaro hospital yaani jamaa kwanza ni wasumbufu! Hiyo kadi utailipia sehemu kama kumi hivi wanakuzungusha hadi unajiondoa mwenyewe. Mimi niliwahi saa kumi na mbili asubuhi hadi saa saba naachana nao sijamuona doctor, then kamlete ndio inachukua nafasi dah!
 
Unamaana gani kusema pesa za MUM?

naamisha pesa zinazotolewa na serikali kupitia Memorundum of Understanding kati ya kanisa na serikali ambazo tumeelezwa kusaidia kanisda ili litoe huduma kwa jamii na wakati huo bado huduma zinalipiwa katika hospitali hizo.sasa kama kuna matatizo hayo ya huduma ni je pesa hazitolewi na serikali?au management ya hizo pesa ni mbovu.na kama srikali haitoi pesa ule usemi wa kuwa kanisa liko mstari wa mbele kutoa huduma kumbe ni kwa ajili ya msaada wa srikali ndo wanaweza?
 
Bongo kila kitu kimebaki History even history yenyewe

Pale wakijipanga vizuri na kufanya mabadiliko ya kihuduma historia ya hospital hii inaweza kujirudia na ikawa bora zaidi..
 
Halafu nasikia kuna doctor mmoja mfupi sana mwembamba ndo mtaalam wa surgery. Kichekesho ni kwamba huwa ni mlevi kupindukia na mara kibao huwa anawachana wagonjwa akiwa mitungi nashindwa kuelewa how come KCMC wamtegee mlevi? Kwa mwenye taarifa hivi anaitwa nani vile yule doctor?
Ndio mkuu hata mimi ndugu yangu yamemkuta hayo hayo.
Huyo Doctor ni mlevi na malaya ile mbaya, ni mla rushwa mzuri sana.

*Jina lake la utani niliambiwa lakini sio busara kulitaja hapa.
 
mkuu shadhuly, hapa mi sidhani kama hyo pesa inafanya kazi, tatizo jingine hapa ni hawa watumishi (manesi na madokta) cjui ndiyo mshahara kidogo au ni kukosa ile commitment ya kufanya kazi! pia naona management ya hospital ni poor!
 
Kwa wale mliofika siku za karibuni hapa kcmc mtakubaliana na mimi, hospital hii kubwa na maarufu haitoi tena huduma za kueleweka, wanaofanya kazi sasa kama madaktari ni wanafunzi..Hili ni tatizo kwani linazorotesha sana huduma..tabu tupu

Shaka tuweke pembeni ile dhana ya maisha bora kwa kila mtanzania ndiyo iko ktk utekelezaji na itakapotimia ndipo tutalia na kusaga meno
 
Imebaki jina kwa kuwa uongozi uliopo hauwajali watumishi hasa hao manesi, kwani stahili zao hazilipwi kwa wakati. Je hapo unategemea nini?
Mkuu ndio kabisa, manesi wananyanyasika sana.

Yaani Daktari au watumishi wa ngazi ya juu wa hospitali kumtaka kimapenzi nesi ni jambo la kawaida kabisa.

Unyanyasaji wa kijinsia kwa manesi ni jambo la kawaida kabisa na hawana pa kulalamika kwani watafukuzwa kama mbwa.
 
Ndio mkuu hata mimi ndugu yangu yamemkuta hayo hayo.
Huyo Doctor ni mlevi na malaya ile mbaya, ni mla rushwa mzuri sana.

*Jina lake la utani niliambiwa lakini sio busara kulitaja hapa.

Umeona? KCMC is falling!!!
 
hata hivyo kcmc kuna upande wa serikali na upande wa msamaria mwema
hivyo inawezekana kimeharibika ni kile kitengo cha serikali.

kwa hiyo na serikali inahusika? bad government if they are concerned...
 
Mimi nilimwuguza mgonjwa ICU pale na nilitishwa sana. Manesi walikuwa busy na biashara zao za kuuza tauli na sabuni. Jikoni chakula kinatengenzwa kwa gharama ya walipa kodi, lakini utakifuata kantini. Nikajiuliza kama mtu aliye mahututi anaengojea kufa anauziwa tauli ya kunawa, bezeni, chakula n.k. Wale wenye nafuu wauziwa nini? Tanzania tumekosa maadili hadi mwisho. Madaktari ndiyo tena usiseme. Kila mtu anaiba na sasa tunaibia hadi maiti. Cha kusikitisha mno ni kuwa tuna watoto na ndiyo hayo tunayowafundisha. Je wao watakitendea nini kizazi chao na watoto wao? KCMC kwa sasa hata jina limeshaondoka kutokana na niliyoyaona kwa macho yangu pale ICU. Pumzika kwa amani kaka niliyekuuguza pale wiki nzima.

mkuu pole sana na haya yote yanatokana na uoga wa watz pamoja na kutothubutu na sijui tutaendelea na hii hali mpaka lini?
 
Shaka tuweke pembeni ile dhana ya maisha bora kwa kila mtanzania ndiyo iko ktk utekelezaji na itakapotimia ndipo tutalia na kusaga meno

ni watu wachache tu! wanaofanya maisha yaonekane magumu. watashindwa muda c mrefu.
 
hata hivyo kcmc kuna upande wa serikali na upande wa msamaria mwema
hivyo inawezekana kimeharibika ni kile kitengo cha serikali.

Please hebu niambie upande wa serikali ni upi? na upande wa Msamaria ni upi?
 
mkuu pole sana na haya yote yanatokana na uoga wa watz pamoja na kutothubutu na sijui tutaendelea na hii hali mpaka lini?

mkuu Shine ukiwa na mgonjwa hospitalin hutathubutu kufanya kitu kwa usalama wa mgonjwa wako...
 
Kwa sasa Hospitali ya KCMC ina huduma mbovu sana kuliko hospitali zote za rufaa za zamani(Muhimbili, Mbeya, Bugando)

Japokuwa ni taasisi bora sana kwa mafunzo kwa wataalamu mbalimbali wa afya lakini kwenye kutoa huduma huwezi kuamini kama hii ni Hospitali inayomilikiwa na Kanisa tena wanaiita taasisi ya Msamaria mwema!!

*Mambo kama haya ni ya kawaida kabisa kwa sasa pale KCMC

1/RUSHWA
(Kuanzia getini kwa walinzi, wafagiaji, Nesi, Wanafunzi, Madaktari mpaka chumba cha operation)

2/LUGHA CHAFU
(Ni jambo la kawaida kabisa mtumishi kumtukana mgonjwa au ndugu wa mgonjwa, Staff wa utawala wana lugha ya nyodo kama miungu wadogo)

3/USUMBUFU
(utaambiwa faili halionekani, Urudi kesho, fomu za bima hazipo, Muhusika hayupo kn)

4/UKABILA
(Pale ni uchaga kwenda mbele, kama wewe sio mchaga huna chako, wachaga wamefanya kama hospitali yao)

5/NGONO
(Ipo wazi wazi kuanzia kwa watumishi wao kwa wao au watumishi na wanafunzi lakini pia watumishi na wagonjwa au ndugu wa wagonjwa, sijui hali ya maambukizi ya Ukimwi upoje pale?)
 
hata hivyo kcmc kuna upande wa serikali na upande wa msamaria mwema
hivyo inawezekana kimeharibika ni kile kitengo cha serikali.

Nijuze tafadhali! kitengo cha serikali ni kipi? na cha msamaria ni kipi? Mamndenyi
 
mkuu Concrete, umeongea ukweli..hapo kwenye 3. naweka msisitizo! ni wasumbufu sana..unaweza kurudia x-ray mara kibao! ukiambiwa picha ya kwanza imepotea au haionekani na mgonjwa kashakaa kwa wiki moja wodini anarudishwa upya kwenye x-ray(mionzi) dah
 
kiwatengu, utakapoenda pale
jieleze bila shaka utapelekwa.

They are almost the same! msamaria mayb ni ule upande wa chuo. nadhani umeona alichoandka Concrete hapo juu, thats how KCMC is.
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom