Kweli usilolijua litakusumbua.
Una maana gani unaposema hakuna madaktari,au madaktari wanafunzi? Unafahamu ranking ktk kada hii,au basi tu umeamua kupost?
Kule kuna madaktari wanafunzi wa degree ya kwanza(hawa bado hawajawa madaktari kamili). Wako kwenye masomo,na ili uwe daktari kuna wakati unafundishwa ukiwa darasani na kuna wakati unafundishwa ukiwa hospitali mbele ya wagonjwa.Hawa hawaruhusiwi kutoa matibabu kwa mgojwa.
Kuna madaktari wanaosomea ngazi ya udaktari bingwa kama vile wa watoto,wa akina mama,upasuaji nk.Hawa tayari ni madaktari kamili na walishafanya kazi miaka kadhaa.Hawa ndio tunaokutana nao ktk hospitali za mikoa na mara chache ktk za wilaya. Mbona hulalamiki ukiwakuta huku mikoani? Kwa mfano KCMC hawa wanasoma miaka minne,kwingine wanasoma miaka mitatu tu. Wanafanya kazi kama madaktari wengine unaowajua wewe. Ni vema ukatambua tu kwamba,hawa ni wanafunzi tu wanapokuwa darasani na mwalimu wao,ila wanapokuwa eneo la kazi wanafanya kazi kwa mujibu wa taratibu za kikazi nchini.Na kwa taarifa yako,popote utakapoenda hawa ndio wanaofanya kazi za dk.bingwa sio KCMC. Kwa ukubwa wa hospitali ile sio rahisi kujitosheleza kila sehemu kwa na madaktari bingwa.Hata muhimbili ukienda utakuta wanaofanya kazi za madk.bingwa ni hawa unaowaita hapa wanafunzi.
Kuna madaktari wanaofanya kazi chini ya uangalizi wa madaktari bingwa(interns),hawa tayari wana degree ya kwanza lkn kwa mujibu wa taratibu zilizopo,ni sharti kwanza wafanye kazi kwa mwaka mmoja chini ya uangalizi wa mabingwa kabla hawajapewa kibali cha kufanya kazi katika hospitali zetu. Hawa ndio waliogoma mwaka jana. Unakumbuka huduma zilivyozorota? Tulikuwa tunawaitaje,wanafunzi?? Kazi yao inaonekana na ndio maana ktk mgomo kilitokea kile ulichokiona.
Kwa hiyo basi ungetwambia ni madaktari wa type gani ambao wewe ukiwaona ndio roho yako inaridhika.Lkn vile vile,ungesema ikiwa hapo kabla hawa unaowaita wanafunzi walikuwa hawatoi huduma hapo hospitali.Pia ungesema mapungufu yaliyopo hapo hospitali kwa kukosekana hao madak.unaowataka.
Napenda pia kukukumbusha kuwa,ufanyaji kazi wa kitabibu hopitali unafuata protocal. Mganga wa kwanza kumwona mgojwa anaposhindwa kutambua/kutibu anamrefer mgonjwa kwa dk.ambaye yuko juu yake kitaalam,naye huyu anaposhindwa anamsogeza mbele kwa mwingine wa juu yake,nk...nk...nk. Labda utuambie huko KCMC utaratibu huo haupo? Kama upo,ni lazima hao unaoita wanafunzi wanauzingatia,na hapo point yako inakuwa imekosa mashiko.
Ni vema watu wakajua kwamba huduma mbaya sio tu kukosa madk.peke yake.Madaktari wanaweza kuwapo na bado ukakosa huduma nzuri vile vile. Kama ndugu yangu umekosa huduma zuri hapo hospitalini sio kwa sababu umehudumiwa na hao unaoita wanafunzi. Hospitali ile imekuwa ikijiendesha hivyo kwa kipindi kirefu sana tu,na imekuwa ikivutia wagonjwa wengi sana kutoka maeneo mbali mbali kutokana na huduma inayotolewa pale(na hao wanafunzi).
Ushauri: Kisheria mgonjwa ana haki ya kuchagua dk.anayehitaji amtibu. Kama unadhani hao wanafunzi hawakidhi vigezo vya kukuhudumia una haki ya kuomba kuonana na daktari unayemwamini,atakusaidia.Hakuna haja ya kuja hapa kulalamika,kwa sababu kuna hospitali nyingi sana wagonjwa wanapoteza maisha kwa kukosa hapo unaoita wanafunzi.
Binafsi ningekuunga mkono ikiwa ungesema labda umeombwa rushwa,au umekataliwa kutibiwa,au labda mgonjwa wako amechelewa kupata matibabu bila sababu ya msingi,au pengine wamekosea dawa nk...nk...nk. Kwa kweli pale KCMC wanajitahidi sana,na kusema limebaki jina tu,mimi nakukatalia kabisa. Binafsi hospitli ile naijua sana tu,na mara kwa mara nakwendaga pale. Kiukweli uwepo wa wanafunzi pale hospitali unarahisisha sana utoaji wa huduma kwa wagonjwa.Huwezi kutambua urahisi wa huduma za pale ni hadi utakapopata bahati ya kutembelea hospitali zingine kubwa ndio utakapopata jibu.Na pengine utarudi hapa kuwaomba radhi jamaa!