mwanaharakatihalisi1
Senior Member
- Apr 26, 2013
- 107
- 25
Naona hata aibu. Serikali inatakiwa iimarishe hospitali zake. serikali tegemezi ni serikali dhaifu
Kwa wale mliofika siku za karibuni hapa kcmc mtakubaliana na mimi, hospital hii kubwa na maarufu haitoi tena huduma za kueleweka, wanaofanya kazi sasa kama madaktari ni wanafunzi..Hili ni tatizo kwani linazorotesha sana huduma..tabu tupu
Kweli usilolijua litakusumbua.
Una maana gani unaposema hakuna madaktari,au madaktari wanafunzi? Unafahamu ranking ktk kada hii,au basi tu umeamua kupost?
Kule kuna madaktari wanafunzi wa degree ya kwanza(hawa bado hawajawa madaktari kamili). Wako kwenye masomo,na ili uwe daktari kuna wakati unafundishwa ukiwa darasani na kuna wakati unafundishwa ukiwa hospitali mbele ya wagonjwa.Hawa hawaruhusiwi kutoa matibabu kwa mgojwa.
Kuna madaktari wanaosomea ngazi ya udaktari bingwa kama vile wa watoto,wa akina mama,upasuaji nk.Hawa tayari ni madaktari kamili na walishafanya kazi miaka kadhaa.Hawa ndio tunaokutana nao ktk hospitali za mikoa na mara chache ktk za wilaya. Mbona hulalamiki ukiwakuta huku mikoani? Kwa mfano KCMC hawa wanasoma miaka minne,kwingine wanasoma miaka mitatu tu. Wanafanya kazi kama madaktari wengine unaowajua wewe. Ni vema ukatambua tu kwamba,hawa ni wanafunzi tu wanapokuwa darasani na mwalimu wao,ila wanapokuwa eneo la kazi wanafanya kazi kwa mujibu wa taratibu za kikazi nchini.Na kwa taarifa yako,popote utakapoenda hawa ndio wanaofanya kazi za dk.bingwa sio KCMC. Kwa ukubwa wa hospitali ile sio rahisi kujitosheleza kila sehemu kwa na madaktari bingwa.Hata muhimbili ukienda utakuta wanaofanya kazi za madk.bingwa ni hawa unaowaita hapa wanafunzi.
Kuna madaktari wanaofanya kazi chini ya uangalizi wa madaktari bingwa(interns),hawa tayari wana degree ya kwanza lkn kwa mujibu wa taratibu zilizopo,ni sharti kwanza wafanye kazi kwa mwaka mmoja chini ya uangalizi wa mabingwa kabla hawajapewa kibali cha kufanya kazi katika hospitali zetu. Hawa ndio waliogoma mwaka jana. Unakumbuka huduma zilivyozorota? Tulikuwa tunawaitaje,wanafunzi?? Kazi yao inaonekana na ndio maana ktk mgomo kilitokea kile ulichokiona.
Kwa hiyo basi ungetwambia ni madaktari wa type gani ambao wewe ukiwaona ndio roho yako inaridhika.Lkn vile vile,ungesema ikiwa hapo kabla hawa unaowaita wanafunzi walikuwa hawatoi huduma hapo hospitali.Pia ungesema mapungufu yaliyopo hapo hospitali kwa kukosekana hao madak.unaowataka.
Napenda pia kukukumbusha kuwa,ufanyaji kazi wa kitabibu hopitali unafuata protocal. Mganga wa kwanza kumwona mgojwa anaposhindwa kutambua/kutibu anamrefer mgonjwa kwa dk.ambaye yuko juu yake kitaalam,naye huyu anaposhindwa anamsogeza mbele kwa mwingine wa juu yake,nk...nk...nk. Labda utuambie huko KCMC utaratibu huo haupo? Kama upo,ni lazima hao unaoita wanafunzi wanauzingatia,na hapo point yako inakuwa imekosa mashiko.
Ni vema watu wakajua kwamba huduma mbaya sio tu kukosa madk.peke yake.Madaktari wanaweza kuwapo na bado ukakosa huduma nzuri vile vile. Kama ndugu yangu umekosa huduma zuri hapo hospitalini sio kwa sababu umehudumiwa na hao unaoita wanafunzi. Hospitali ile imekuwa ikijiendesha hivyo kwa kipindi kirefu sana tu,na imekuwa ikivutia wagonjwa wengi sana kutoka maeneo mbali mbali kutokana na huduma inayotolewa pale(na hao wanafunzi).
Ushauri: Kisheria mgonjwa ana haki ya kuchagua dk.anayehitaji amtibu. Kama unadhani hao wanafunzi hawakidhi vigezo vya kukuhudumia una haki ya kuomba kuonana na daktari unayemwamini,atakusaidia.Hakuna haja ya kuja hapa kulalamika,kwa sababu kuna hospitali nyingi sana wagonjwa wanapoteza maisha kwa kukosa hapo unaoita wanafunzi.
Binafsi ningekuunga mkono ikiwa ungesema labda umeombwa rushwa,au umekataliwa kutibiwa,au labda mgonjwa wako amechelewa kupata matibabu bila sababu ya msingi,au pengine wamekosea dawa nk...nk...nk. Kwa kweli pale KCMC wanajitahidi sana,na kusema limebaki jina tu,mimi nakukatalia kabisa. Binafsi hospitli ile naijua sana tu,na mara kwa mara nakwendaga pale. Kiukweli uwepo wa wanafunzi pale hospitali unarahisisha sana utoaji wa huduma kwa wagonjwa.Huwezi kutambua urahisi wa huduma za pale ni hadi utakapopata bahati ya kutembelea hospitali zingine kubwa ndio utakapopata jibu.Na pengine utarudi hapa kuwaomba radhi jamaa!
Dah mkuu shukrani kwa kuleta hii mada hapa,ni kweli kabisa KCMC ni kwishine mie nilimpeleka mgonjwa wangu hapo yaani hamna kitu ni wanafunzi wanazunguka tu huko ndani huduma ni mbovu kupindukia,afadhali hospitali ya Mawenzi,kuna wagonjwa watatu ambao ninawafahamu walishawahi kuletwa pale kwa siku tofauti kwa kweli walifariki wote na ujue ukimlaza mgonjwa wako hapo kama anaugojwa complicated kidogo ujue umekwenda na maji na mgonjwa haudumiwi mpaka utoe hela
Kwakweli Hali ya hospitali hii ni ya kusikitisha mnoo.
Kwanza uchafu uliokithiri,ni aibu Sub ICU kuwa na Mende wengi kama jalalani.Ni aibu na fedheha Ma nurse wengi ni wakenya na wana lugha mbovu kwa wagonjwa.Ni aibu na fedheha Nurses wengi wa night hawafanyi kazi na wanalala ifikapo saa tatu.usiombe ukawa na drip watakacho fanya ni kutundika na kuifungulia hadi mwisho ndani ya dk 5 imeisha na hawajali umri.Dr aliyepo ni mwanafunzi ambaye hata prescription shida kuandika hadi amsubiri intern ambaye naye amsubiri resident.sasa mgonjwa atakuwa anasubiri tu?nimeyashuhudia kwa macho yangu bibi mmoja anamatatizo ya kupumua na kawekewa respiratory aid. oxygen imeisha na Nurse anasema amechoka atabadilisha asubuhi.naambiwa alijafariki!its so shame kuiita hospitali ya msamaria mwema!Malasusa amka toka usingizini!
my Mom died there...... sawa siku zake labda ndio zilifika ila maybe there was the doctors Fault : wahudumu wengi wa afya wanafanya kazi kwa mazoea..... yani unaweza kuwaona wahudumu wanapiga story wakiwa wanamhudumia mgonjwa aliepo serious mbaya..... au mtu akifa wakiwa wanambeba wanaweza pigiana story zenye kuchekesha mpaka wanamwachia maiti anaanguka chini ......mphuuu.
KCMC wanapata ruzuku kutoka hazina kulipa wafanyakazi na shughuli za Maendeleo (UNAUDITED) in billions
KCMC wanapata pesa kutoka kwa wagonjwa kwa malipo ya huduma
KCMC wanapata pesa za sadaka kutoka kwa wafadhili na waumini
Kama siyo ufisadi nipeni jina lingine
Ukiingia kcmc unanusa harufu ya kifo. Ukiangalia wagonjwa walivyolala koridoni na jinsi wanavyokuwa treated, oh my God! Its very scary. That place smells death.kuna mtu namfahamu alifanyiwa operation mara mbili, ya kwanza alifanyiwa na mwanafunzi alimkosea, ikabidi afanyiwe mara ya pili na daktari mzoefu, eneo lilelile.kama humfahamu mtu pale, umekwisha.
Nurse anasema amechoka hawezi kubadili oxygen, wewe unamwangalia unakimbilia kulipua kwenye JF ambapo hata haioni, je ulichukua hatua? si kuna uongozi, uliwaambia nini hao viongozi wake? Je ni haki kumuacha muovu aendelee na uovu wake bila kumwajibisha, natamani kusikia Mzee Kiwatengu umechukua hatua, vinginevyo hatuwezi kuendelea kwa kutumia JF pekee.
ninachoamini mimi ni mfumo au system mbaya ,maana ukiangalia mfano ukitaka kuchukua fail unawahi pale saa kumi na mbili ili ushike namba .unapewa namba mda wa saa moja .saa mbili wakitoka sala wanakutafutia faili unaitwa unaambiwa nenda kwenye malipo .
unaweza kukaa dirisha la malipo kwa muda usiopungua masaa matatu. usiposikia jina lako unawafuata makarani wanakutuma urudi dirishani uklikotoa namba au kadi ,fail unaweza kulipata mda wa saa sita na .mbaya zaidi kama unatumia bima utazunguka hadi uchoke kabla hujamuona daktari na baada ya kumuona daktari,utazunguka hadi uchoke hadi upate hiyo dawa.mimi natamani huu mfumo kwa wagonjwa wa nje urekebishwe