Mkuu ebandio! sikuwa na jinsi ya kuchukua hatua wakati ule ili hali mgonjwa wangu alikuwa hoi pale hospitalini..
Hatua yoyote ile kwa pale ingehatarisha uhai wake!
Ilifikia hatua yakutaka kumzaba nesi vibao, baada ya yeye kunijibu kwa kejeli!
Kama system ya uongozi haipo sawa, hakuna hatua ambayo ingeleta mashiko kwa wakati ule!
Ni udhaifu kwa upande wangu..
Na hatua ndogo niliyochukukua yakuacha maoni yangu pale juu ya utendaji kazi wa hosp..
Thanks to dr. Makule of mt.meru hospital he tried alot to serve a life of my beloved grandma..may her soul rest in peace!!
Mkuu ebandio hakika umenikumbusha mbali..hasa kuchukua hatua!
Pole ndugu yangu, ila ni muhimu kuchukua hatua maana kwa hatua yako moja utaokoa roho za wengi. Najua usingeweza kuokoa roho ya Bibi yako lakini hujui ya baadaye maana sisi wote tungeweza kuangukia kwenye mkono wa muuguzi huyo. Kumzaba kibao wala kusingekusaidia maana ungeishia kufunguliwa kesi, na nafikiria kama muuguzi angelikuwa mwanamke.
Hata hivyo bado mimi nasisitiza kuchua hatua ya kutoa taarifa kwa uongozi, maana mara nyingi sisi tuna tabia ya kutotoa taarifa halafu tunafikiri uongozi unajua, mara nyingi hawajui. Mpendwa wetu Ntabaye hawezi kuwa kila sehemu kwa wakati mmoja. Viongozi wa sehemu mara nyingi hufichwa uovu labda kama wanakula sahani moja kwa uovu, jambo hili ni gumu kulieleza kwa mtu asiye kwenye mtandao huo. Naomba nikupe hadithi fupi ya jambo hilo ili uone linalojificha, "mathalani mgonjwa alienda kwa rafiki yake ampeleke kwa Daktari bingwa kwa kuwa aliona mpango wa appointment ni mgumu na mrefu, huyu rafiki akamwambia kwa ubize wa yule daktari leta 200,000/=, yule bwana akajikamua akapata 100,000/=, kufika kwa daktari (kwa kuwa walikuwa wawili) akamuomba amtibie kwa ukamilifu sana (kwa kuwa aliambiwa kwa kutoa nusu unaweza usipate matibabu yenye maana), kwa kuwa pesa iliyobaki ataleta baadaye. Daktari katika kushangaa, na kujiuliza akamwita yule jamaa, kwa kuwa yeye alimwambia kuwa yule ni ndugu yake naye akataka kumsaidia, si mfanyakazi mwenzake, baada ya kuulizwa akabaki mdomo wazi, baadaye Daktari alimtaka yule bwana ampe ile pesa yake, na kumrudishia mgonjwa (hii si hadithi bali ilitokea Muhimbili), kama mgonjwa asingejitetea kwa upungufu wa hela, uovu ule usingejulikana. Uongozi haukujua na hata daktari mwenye we hakuwa na habari. HIVI NDIVYO JINA ZURI LA HUDUMA HUHARIBIKA. Taabu zote tunasababisha sisi tunaoamua kutotoa taarifa ili kukomesha uovu. Naomba nisistize kuwa hujachelewa kumtolea taarifa muuguzi mwovu ili asiue wengine. Mungu akutangulie katika hilo.