Hongereni Mabasi ya Kilimanjaro Express

Hongereni Mabasi ya Kilimanjaro Express

Hata hizi Happy Nation mpya ziko vizur zina AC na usb charging system nikarudi Moshi na Hai Express full AC kutoka Dar ila tulivyofika same wakazima AC
Hata mimi Kuna siku nilipanda hai express ac wamekuja kuwasha kimara toka arusha. Niliapa siji kupanda tena.
 
Kila siku mnyama anaruka dar to mombasa dar to tanga dar to nairobi dar to arusha,mombasa to nairobi ,mombasa to lamu,mombasa to malindi,mombasa to kisumu,mombasa nakuru ,mombasa eldoret,monbasa kampala,mombasa kigali,mombasa to kisii etc
Mkuu samahani kama nitakukwaza.. mimi nipe ratiba ya basi za Arusha ili niache kukariri hiyo ya saa tatu.
 
Kilimanjaro ni wasikivu mno na ndiyo maana wamekuwepo tangu mimi nikiwa mtoto kabisa enzi hizo zilikuwa zinaitwa KBS enzi mzee Maeda akiwa hai..

Mkuu Kilimanjaro hii si ile KBS ya yule mama mbabe wa Arusha. Hii ya sasa ilikuwa inaitwa Sawaya those days.
 
Nimepanda tahmèed arusha -Dar full AC tatizo hotelini Liverpool kuchafu sana.

Mkuu pale ni kwamba Mabasi yote ya Waarabu lazima yaingie Liverpool. jaribu kuchunguza, wakimna Hood, Islam, abood, Spider, taqwa, Clasic, Sumury na nyinginezo za Waarabu lazima watie timu pale,
Kuna day nilipanda Abood ya Moro nikamuuliza Konda akanimbia Tajiri wao ana mkataba na jamaa wa Liverpool na hata basi lao likiharibikia mitaa ya korogwe, mombo na maeneo ya jirani basi wale liverpool hutengeneza bure yaani gharama huwa ni za kwao
 
Nimepanda tahmèed arusha -Dar full AC tatizo hotelini Liverpool kuchafu sana.
Mkuu hapo umenimaliza nguvu zote. Hii hotel ya Liverpool hata bure huwa sili. Chakula kibovu mno. Tahmeed kama basi wako vizuri ila hotel kama ni hiyo wajirekebishe.
 
Wakuu juzi nimekata mzizi wa fitna baada ya kupanda Tahmeed LIVE from Tanga to Dsm. Jamaa wako vizuri mno. Ni waungwana hakuna ujanjaujanja. Safari ilikuwa nzuri kupitiliza. Nimeamua kwa safari zangu zote za Tanga au kokote Tahmeed inapopita niwe naipanda.
 
Wakuu juzi nimekata mzizi wa fitna baada ya kupanda Tahmeed LIVE from Tanga to Dsm. Jamaa wako vizuri mno. Ni waungwana hakuna ujanjaujanja. Safari ilikuwa nzuri kupitiliza. Nimeamua kwa safari zangu zote za Tanga au kokote Tahmeed inapopita niwe naipanda.
Nami nina mpango wa kusafiri na Tahmeed soon...
 
Toa evidence na uwe mkweli kabisa kwa kumuogopa mungu lini umesikia tahmeed imeanguka au kuwaka moto,halafu nipm namba yako nikutumie mamia ya picha za ajali za kilimanjaro na dar express, mbaya zaidi kwa uongo wako wiki iliyopita kilimajaro imeanguka na kuua wiki iliyopita ikitoka stand arusha

Bro jipange vizuri lasivyo nitakuona hujawahi hata kuipanda hiyo kilimanjaro,maana hapa unatia aibu tu
Tahmeed imeungua jana, una swali lingine?
 
Sasa lililoungua moto kama halikuua inabidi warudie tena maana lengo huenda halijatimia! biashara zilizo jikita kwenye mazingaombwe tabu!
 
Back
Top Bottom