Me nshatumia sana ikakataaa wewe
tatizo linasababisha ikatae ni kwakuwa hukujua steps za kuinstall.
ngoja tushare kwa faida yetu sote ambao tumechoka kubamizwa na Dstv.
hatua ya kwanza unahitaji kuwa na stable internet,binafsi natumia vodacom 4G inanitendea haki iko speed japokuwa inakula bundle kwelikweli,hatua ya pili download bluestacks katika computer yako halafu ui install,then download mobdro kwenye computer yako inaitwa Mobdro for window PC baada ya kudownload Mobdro nenda kwenye bluestacks.
jambo la kufahamu ni kuwa bluestacks kazi yake kubwa ni kuifanya computer yako ionekane kama android PC na hili file la mobdro bila app kama bluestack au mfano wa hizo haliwezi kucheza kwakuwa ni APK file format hivyo sasa fungua app yako ya bluestacks then upande wa kushoto kuna list ya icon nyingi huko chagua icon ya APK.
ukiiclick hiyo icon itaenda moja kwa moja kwenye computer yako na kutafuta APK file kule itaikuta hiyo Mobdro apk na kuinstall. Baada ya kuwa installed hatua ya kawaida ni kuidouble click hiyo app ya mobdro ambayo itaonekana ndani ya bluestacks na kuanza kuenjoy mamia ya channel kuanzia sports,news,cartoon,movies nk.
kwa muonekano mzuri chomeka waya wako wa HDMI kwenye computer yako kwenda kwenye HD TV yako then mambo yatakuwa murua,au wakati mwingine me naweza fanya mirror cast kwa TV kutoka katika simu yangu.