Hongera Maulid Kitenge

Hongera sana Maulid wa Kitenge, wewe ni Miongoni mwa wanahabari bora kabisa Tz, Tunajivunia sana kwako
 
Hata mimi nimeshangaa sana wanausalama gani silaha zimekaa kama bongo movie wako location kiasi kwamba akitokea mtu aliyejichokea anamalizana nao hapo hapo
Bongo movie yenyewe wanayaigiza hayohayo yaliyoko kwenye idara hii kama ilivyo kwa kina 007 kuigiza kile wanachokifahamu juu ya idara yao
 
Siku ya leo kumetokea tukio la kustaajabisha ktk tasnia ya siasa nchini tanzania. Tukio hilo limetokea dar es salaam wakati aliyekuwa waziri wa michezo na tamaduni Nape nauye akitaka kuongea na waandishi wa habari baada ya kuondolewa katika nafasi yake ya uwaziri. Nape ameondelewa leo hii katika nafasi yake baada ya mh rais kufanya marekebisho madogo katika wizara mbili.

Baada ya mh Nape kuwasili maeneo ya Pritoria hotel kulitokea tafrani baada ya watu walitambuliwa kuwa ni maafisa usalama kumzuia asiongee na waandishi na kumtaka arudi ndani ya gari. Wakati sakata hilo likitokea mmoja wa maafisa usalama alitoa bastola na kumtishia Mh Nape ambaye naye hakustuka . Afisa huyo aliirudisha silaha hiyo kiunoni kisha kuanza kumsukuma Mh nape kumrudisha ndani ya gari. Pasipo kutarajiwa kijana mmoja mtanashati aliyevaa koti jekundu alionekana kujongea kujua kinachoendelea baada ya kuona tafrani ikitokea.

Kijana huyo aliweza kutambuliwa kuwa ni mtangazaji maarufu Maulid Kitenge. Kijana huyoo aliweza kuingilia kati na kumtoa afisa usalama kwa nguvu eneo la tukio huku akimsukuma bila kuogopa. Hakika alifanikiwa akamuondoa eneo hilo na afisa huyo alitii bila shurti. Wengi tumeona na kustaajabu na hatuna budi kumpa hongera maulidi kitenge kwa ujasiri aliouonesha.

ILA
Nimejaribu kujiuliza kwa hali ya kawaida kuna raia wa kawaida anaweza kuwa na ujasiri wa namna hiyoo. Nikapata jibu inawezekana na yeye ni wale watu wanaovaa suti nyeusi(mashushu).mpaka sasa bado sijapata jibu sahihi .

Waungwana ninyi mnaonaje nawasilishaView attachment 485865View attachment 485866View attachment 485867View attachment 485868
Kuna kale kachalii nilikaona kwenye hiyo prukushani kalivoona bastola kalitoka nduki,yani ni kaoga kama jicho..,teh,,teh...
 
Kitenge kakuta bastola imesharudishwa kiunoni, kakuta malumbano ndio akayaingilia, pia alitumia kauli za busara kumtoa yule kijana na kumuomba kuacha kutumia nguvu kwa mh nape ambae ni kijana mwenzao. Nimeongea nae jana anasema alikua mbali hakuona tukio la bastola ila kama sifa na pongezi anafurahi sana kuzipokea
 
...Kama ukifatilia Vizuri hiyo clip...Kitenge katoa wapi ujasiri wa kumzui huyo jamaa huku anamuambia unaharibu mambo...
Kama isingelikuwa na yeye usalama asingesema chochote..

Nahisi kitenge mtu wa usalama!
Kwani watu wa usalama peke yao ndo wajasiri?
 
Ni walewale. Maana alisikika akimwambia huyo jamqa... mkuu umeharibu na inawezekena kitenge ni bosi wake
 
Kitenge anapiga nondo balaa, jamaa kapigwa kibega akapepesuka mita kumi, hapo hajakatwa mtama.

Wale manjagu kitenge alikuwa na uwezo wa kukomaa nao wote, shezea kijana wa fumagila wewe.
 
Back
Top Bottom