Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,478
- 39,997
Nipashe
Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Selemani Kova, amesema miongoni mwa vitu vinavyomkosesha usingizi ni vitendo vya uhalifu, biashara ya dawa za kulevya na suala la wapiga debe na vibaka, lakini amedai kuwa amepunguza uhalifu huo kwa asilimia 50.
Alisema hayo jana ikiwa ni siku 100 tangu ashike wadhifa huo wenye changamoto nyingi akitokea mkoa wa Mbeya.
Alikuwa akizungumza na Nipashe katika mahojiano maalumu kuhusu mipango yake ya sasa na ya baadaye katika kupambana na uhalifu na suala la wapiga debe.
Alisema hivi sasa uhalifu uliopo ni wa kuvizia lakini sio kama ilivyokuwa huko nyuma ambapo wahalifu walikuwa wakitamba.
Alitoa mfano kwamba kuanzia Jumatatu wiki hii hakuna tukio lolote la uhalifu lililoripotiwa kwake, jambo ambalo anaamini kwamba kazi ya kupambana na uhalifu imefanikiwa.
Akitoa takwimu, Kova alisema, jumla ya vibaka 3120 walikamatwa katika msako maalumu jijini, wapiga debe 1586, watuhumiwa wa dawa za kulevya watu 3109, wauzaji wa bangi 1537 na pombe haramu ya gongo 1490.
Alisema takwimu hizo ni mpaka jana na kwamba bado mkakati wake wa kupambana na uhalifu uko pale pale.
Alifafanua kuwa kilichomsaidia kufikia malengo yake ni mbinu ya kuwashirikisha wananchi ambao anawatumia kufichua wahalifu katika maeneo wanayoishi.
Kova alisema, ameandaa kompyuta maalumu ambayo wananchi wanapomtumia ujumbe mfupi kupitia kwenye simu zao za mkononi kufichua uhalifu hufikia humo na kuhifadhiwa na baadaye anaufanyia kazi haraka.
Alisema ujumbe huo unatakiwa kutumwa kwenda namba ya simu 0785034224 na kwamba kila mwananchi anayetoa siri za uhalifu anahifadhiwa jina lake.
Kwa upande wa nidhamu kwa askari wake alisema, wale wenye mchezo wa kuwabambikia kesi wananchi siku zao zinahesabika.
Alisema enzi za kubambikia wananchi kesi zimepitwa na wakati na yule atakayebainika atajuta kwa nini alifanya hivyo ili mradi wananchi wampatie taarifa sahihi.
Kuhusu uhalifu, alisema watu wenye ndoto za kufanya uhalifu kama njia ya kupata utajiri wamechelewa na hivi sasa hawatafanikiwa.
Aliwataka watu wa namna hiyo kubuni na kufanya kazi za halali zenye kuwapatia riziki badala ya kuendelea kuwabugudhi wananchi.
Aidha, Kova alisema amebaini njia inayotumiwa na vibaka wanaoandamwa ambapo wanavizia wananchi kwenye purukushani za kugombea daladala na kuwaibia mali zao.
Alisema kutokana na hali hiyo, jeshi la polisi kanda ya Dar es Salaam, linatarajia kuanzisha utaratibu wa wananchi kupanda daladala wakiwa kwenye mstari.
Kamanda Kova alisema, hilo linawezekana kwani hata nchi jirani ya Kenya inafanya hivyo na kwamba hatua hiyo itasaidia kuondoa wizi wa simu na fedha kutoka mifukoni.
Aliwashukuru wananchi kwa kutoa ushirikiano kwa polisi katika kufichua uhalifu na kwamba kila askari atakayejituma kupambana na majambazi kwa ujasiri atapata zawadi anazotoa kila mwezi.
My Take:
Uongozi si maneno tu bali ni vitendo pia. Na vitendo vinaweza kupimwa. Kwa mtindo huu nampigia debe Kova. Kwa wanaokumbuka tulizungumza na Kamanda huyu akiwa kule Mbeya mara baada ya soko la Mwanjelwa kuungua. Ni mtu anayetoa ushirikiano mkubwa sana kwa waandishi. Swali je, upele umepata kucha Dar? Only time will tell. Lakini kupunguza uhalifu kwa asilimia 50 ndani ya siku mia moja, si utani!!
Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Selemani Kova, amesema miongoni mwa vitu vinavyomkosesha usingizi ni vitendo vya uhalifu, biashara ya dawa za kulevya na suala la wapiga debe na vibaka, lakini amedai kuwa amepunguza uhalifu huo kwa asilimia 50.
Alisema hayo jana ikiwa ni siku 100 tangu ashike wadhifa huo wenye changamoto nyingi akitokea mkoa wa Mbeya.
Alikuwa akizungumza na Nipashe katika mahojiano maalumu kuhusu mipango yake ya sasa na ya baadaye katika kupambana na uhalifu na suala la wapiga debe.
Alisema hivi sasa uhalifu uliopo ni wa kuvizia lakini sio kama ilivyokuwa huko nyuma ambapo wahalifu walikuwa wakitamba.
Alitoa mfano kwamba kuanzia Jumatatu wiki hii hakuna tukio lolote la uhalifu lililoripotiwa kwake, jambo ambalo anaamini kwamba kazi ya kupambana na uhalifu imefanikiwa.
Akitoa takwimu, Kova alisema, jumla ya vibaka 3120 walikamatwa katika msako maalumu jijini, wapiga debe 1586, watuhumiwa wa dawa za kulevya watu 3109, wauzaji wa bangi 1537 na pombe haramu ya gongo 1490.
Alisema takwimu hizo ni mpaka jana na kwamba bado mkakati wake wa kupambana na uhalifu uko pale pale.
Alifafanua kuwa kilichomsaidia kufikia malengo yake ni mbinu ya kuwashirikisha wananchi ambao anawatumia kufichua wahalifu katika maeneo wanayoishi.
Kova alisema, ameandaa kompyuta maalumu ambayo wananchi wanapomtumia ujumbe mfupi kupitia kwenye simu zao za mkononi kufichua uhalifu hufikia humo na kuhifadhiwa na baadaye anaufanyia kazi haraka.
Alisema ujumbe huo unatakiwa kutumwa kwenda namba ya simu 0785034224 na kwamba kila mwananchi anayetoa siri za uhalifu anahifadhiwa jina lake.
Kwa upande wa nidhamu kwa askari wake alisema, wale wenye mchezo wa kuwabambikia kesi wananchi siku zao zinahesabika.
Alisema enzi za kubambikia wananchi kesi zimepitwa na wakati na yule atakayebainika atajuta kwa nini alifanya hivyo ili mradi wananchi wampatie taarifa sahihi.
Kuhusu uhalifu, alisema watu wenye ndoto za kufanya uhalifu kama njia ya kupata utajiri wamechelewa na hivi sasa hawatafanikiwa.
Aliwataka watu wa namna hiyo kubuni na kufanya kazi za halali zenye kuwapatia riziki badala ya kuendelea kuwabugudhi wananchi.
Aidha, Kova alisema amebaini njia inayotumiwa na vibaka wanaoandamwa ambapo wanavizia wananchi kwenye purukushani za kugombea daladala na kuwaibia mali zao.
Alisema kutokana na hali hiyo, jeshi la polisi kanda ya Dar es Salaam, linatarajia kuanzisha utaratibu wa wananchi kupanda daladala wakiwa kwenye mstari.
Kamanda Kova alisema, hilo linawezekana kwani hata nchi jirani ya Kenya inafanya hivyo na kwamba hatua hiyo itasaidia kuondoa wizi wa simu na fedha kutoka mifukoni.
Aliwashukuru wananchi kwa kutoa ushirikiano kwa polisi katika kufichua uhalifu na kwamba kila askari atakayejituma kupambana na majambazi kwa ujasiri atapata zawadi anazotoa kila mwezi.
My Take:
Uongozi si maneno tu bali ni vitendo pia. Na vitendo vinaweza kupimwa. Kwa mtindo huu nampigia debe Kova. Kwa wanaokumbuka tulizungumza na Kamanda huyu akiwa kule Mbeya mara baada ya soko la Mwanjelwa kuungua. Ni mtu anayetoa ushirikiano mkubwa sana kwa waandishi. Swali je, upele umepata kucha Dar? Only time will tell. Lakini kupunguza uhalifu kwa asilimia 50 ndani ya siku mia moja, si utani!!