...Hoja hii so ya chama chochote cha siasa, ni hoja kwa manufaa ya uwajibikaji ndani ya Serikali, na imepata nguvu kwa sababu ya mwelekeo wa Wabunge wa vyama vyote kuunga mkono hatua za kuwawajibisha Mawaziri...
...Mwenye akili yoyote na anayeiunga mkono hoja hii kwa manufaa ya mama Tanzania, hataihusisha kamwe hoja hii na chama chochote cha siasa, kwani kufanya hivyo ni kuwatenganisha wabunge na kupelekea kuiua hoja hii kabla haijakamilisha kusudio lake, na hii ni hekima...
...Zitto yupo juu ya siasa za vyama bungeni, na tunahitaji Wabunge wengi zaidi bungeni wanaoweza kusimamia maslahi ya nchi bila kujali manufaa ya vyama vyao, Ebu tumwache Zitto mwenyewe aseme....
LUKAZA: Hoja ya Zitto ya kutaka Waziri Mkuu Pinda apigiwe Kura ya Kutokuwa na Imani naye yakwama kutokana na kanuni za Bunge
...Amesema wabunge wa vyama vyote wamesaini ispokuwa UDP na kwamba, uongozi wa CUF umetoa maelekezo maalumu kwa wabunge wake kusaini.
...Zitto amesema hoja hiyo ni ya wabunge wote bila kujali itikadi za vyama na lengo ni kutengeneza Bunge la utendaji badala ya kulalamika.
Iwapo hoja hiyo itapitishwa na Bunge, Pinda atakuwa Waziri Mkuu wa kwanza kupigiwa kura ya kutokuwa na imani naye.
Zitto amesema kuwa wanatarajia kuwasilisha hoja hiyo kwa Spika wa Bunge, Jumatatu kwa ajili ya hatua zaidi....