Hoja ya haja: Kutoka Michuzi blog

Sumaku

Member
Feb 17, 2009
53
1
( Hii nimeinasa kule Michuzi blog, imepambisha mjadala. Kuna mwenye sehemu ya kwanza atumwagie humu ukumbini!)

HOJA YA HAJA

Mwibaji na watwana, mlifi ni mwungwana
(sehemu ya pili na ya mwisho)

Ilipopita awamu ya pili ikajiri awamu ya tatu (Awamu kati). Hii kwa hakika ilikuwa awamu ambayo iliingia katikati na kuyaangalia mapungufu na mafanikio ya awamu ya kwanza na awamu ya pili.


Awamu hii ikarudia pale pale kwenye awamu ya kwanza kuhusu swala la demokrasia, na kwamba viongozi wake wakawa wakali kwamba wanataka kurudisha tabia ile ile ya kuogopa watu wasisemeseme hovyo. Hakika viongozi wa awamu ta tatu walikuwa wakali sana na wakatengeza uga ambao ilikuwa si rahisi tu kupenyeza rupia hata penye udhia.

Awamu hii ilisheheni sifa za kujenga uchumi na kwamba pato la taifa likawa limedhibitiwa na ule uholela baada ya “RUKSA” haukuwepo tena, na zaidi ubinafsi sasa ukarudi na kujilimbikiza kwa hao viongozi wa awamu ya tatu. Kauli mbio hapa ilikuwa na “Uongozi Bora”. Hakika ulikuwa uongozi bora maana matokeo yake yalikuwa kwamba baadhi ya viongozi walikuwa bora haswaa katika kujizatiti ki-uchumi na kimaendeleo binafsi na siyo kwa kila mwananchi!.

Mengi yamesemwa na bado yataendelea kusemwa kuhusu maazimio yenye madhumini endelezi ya awamu zote tatu na hapatakosa kujiri kasoro zake ambazo baadhi nimezigusia hapo juu.

Haya sasa tupo kwenye awamu ya nne ambayo ilipokelewa kwa vishindo, shangwe na nderemo nah ii kweli iliingia kwa staili yake tofauti kabisa na awamu zote japo ikizingatia kabisa misingi muhimu iliyowekwa na awamu zote ambazo zilizopita. Hapa tukapata utawala wa kwanza kabisa wa uongozi wote wa juu kuwa na safu kubwa ya vijana ambayo wengi waliitafsiri kwa lugha ya kigeni “boys to men”. Hakika pailikuwa na faraja kubwa na hasa kwa vijana ambao ndiyo tumaini kubwa la maendeleo yeyote katika nchi yeyote.

Hapa pakatokea demokrasia ya uga mpana kabisa kwamba unaweza kusme chochote na hata jambo ambalo si zuri kulisema kwa kumtaja kiongozi yeyote yule wa kitaifa na bado hutafanywa lolote kama vile kupelekwa kuzuizini ama kuitwa muhaini.

Sasa ni hili ndilo limezaa yote haya ya watu kutumia vinywa vyao kusema yanayowakera binafsi na kuyafanya ya kitaifa, kujenga tabaka za makundi ya wafuasi wa kisiasa na mpaka kufikia kuleta makundi ambayo sasa ndiyo yamekuwa maarufu ndani ya serikali na vyama vyao vya kisiasa na hata mpaka kwenye dini!!!! Hakika chombo kinawenda mrama hapa!!!

Nani alisema kwamba unapokuwa na uhuru wa kusema basi unasimama kwenye majukwaa na kuanza kukashifu na kubeza viongozi wa kitafia eti tu kwa sababu nawe ulikuwa kiongozi wa nyadhifa fulani katika awamu zilizopita?


Mbona wapo ambao walikuwa na hata nyadhifa kubwa tu wamekaa kimya na ndiyo sasa wanatumika kama wapatanishi wa malumbano haya!!! Kwa nini hizi taasisi ambazo zina majina makubwa zisijitenge ili kujitofautisha na “taasisi shutumu” badala ya kuleta maneno ama makongamano ya kushutumu, kukashifu na kudhalilisha viongozi ziungane na waungwana ambao wamekuwa mstari wa mbele katika kuleta suluhu ya matatizo yanayojiri nchi yetu kisiasa na kiuchumi??
Bado ninadirki kusema serikali ya awamu ya nne ni shujaa maana imefungua milango yote ya uhuru na mpaka baadhi ya watu wanadirki sasa kufanya mashambulio ambayo dhahiri yanaonyesha kulenga mtu binafsi??? Kweli tumefikia hapo bila ya kujijua ama kwa makusudi?????


Tanzania, Tanzania, Nakupenda kwa moyo wote!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
 
Hawa watu wana laana ya aina fulani.. sitaki kuwajibu lakini wananitibua mweh!
mabadiliko hayajaletwa na Awamu ya nne bali watu na nyakati! Kama kuna watu wa kupongezwa na haya mabadiliko basi ni wanahabari (japokuwa wapo wale wanaopotosha jamii pia kwa maslahi ya Ufisadi).

Kwanza huyo Michuzi mwenyewe ni mnafiki nikipeleka article zangu za kusema uozo ndani ya Serikali ya JK huwa ha-publish ndo hawa tunawaita vibaraka! lakini huwa mstari wa mbele kutoa zile zinazompamba Rais na serikali yake! Halafu anadai ati blog ya Jamii!
 


Bado ninadirki kusema serikali ya awamu ya nne ni shujaa maana imefungua milango yote ya uhuru na mpaka baadhi ya watu wanadirki sasa kufanya mashambulio ambayo dhahiri yanaonyesha kulenga mtu binafsi??? Kweli tumefikia hapo bila ya kujijua ama kwa makusudi?????


Huyu kaandika kwanza kwa kujikomba kwa Michuzi ambaye ni CCM damu na mnafiki mkubwa sijui kwa nini hajifunzi kwa akiNa Lusekelo

Au kaandika kweli kwa ujinga akijua kuwa kusema sana kama yeye allivyoandika sana sio kipimo cha mafanikio..

Kila mtu leo angemsifia JK hata hao waliosema wasingesema kama tu JK angewapeleka jela na mali zetu kurudishwa.

mwaka wa tano nyimbo zile zile, bado mtu anakaa na kumsifia JK?
 
Huyu kaandika kwanza kwa kujikomba kwa Michuzi ambaye ni CCM damu na mnafiki mkubwa sijui kwa nini hajifunzi kwa akiNa Lusekelo

Au kaandika kweli kwa ujinga akijua kuwa kusema sana kama yeye allivyoandika sana sio kipimo cha mafanikio..

Kila mtu leo angemsifia JK hata hao waliosema wasingesema kama tu JK angewapeleka jela na mali zetu kurudishwa.

mwaka wa tano nyimbo zile zile, bado mtu anakaa na kumsifia JK?


Safi!!!!!

Nadhani watu wanatakiwa kujua swala mmoja ndio kweli JK anafanya kazi hatukatai hilo, ila swala la kufanikisha barabara fulani ambazo zilikuwa zimeisha wekewa fungu lake awamu iliyopita hatuna shaka nalo hata uduchu.

Kuna haya mambo ya UFUSADI, MIKATABA YA MADI(ambayo leo nimesikia kwa gazeti ati Ben Mkapa anatetea iyo mikataba aliyo isimamia yy na kuibinafsisha)RICHMOND,KAGODA na mengineyo huko ndiko Rais anapimwa uwezo wake wa kikazi na kujua dhamila yake iko kwa maslahi ya nchi au? Tizameni hata Aljazera au CNN mkaone wakina OBAMA wanavyo pimwa utendaji wao wa kazi iwe leo Tanzania tu Rais kuhojiwa au kusemwa kuwa kuna tatizo katika uongozi wako imekuwa nongwa jamani? hata hao wakina REDET wasiji kombea hapa, msitufanye sie wandanganyika jamani kuwa hatuoni kuwa kuna mapungufu huko IKULU. swala hapa watu pia wanajiuliza kama Mwl JKN aliweza kuwakemea watu na kuwashughurikia iweje yeye MJK katika izi enzi za zama za UWAZI na UKWELI anashinda kutoa matamko kama Rais? msituletee msemo wenu wa "mnyonge mnyongeni laki haki yake mpe" wao hao viongozi walipokuwa wakipitia mikataba walikuwa hawaoni miaka ijayo ya watanzania wataishi vipi? Viongozi walio kosolewa wasiji tafutie visingizio ati hao wazamani walifanya nini?kweli kama kiongozi wa nyakati hizi unataka kufanya comparison of those ages na sasa we nikiongozi kweli? kama wataka kuleta changes ndio wakati mwafaka wa kuwaonyesha wanao kukosoa kuwa unaweza and prove them right na your a strong leader period
 
Siamini kwamba mabadiliko ya uhuru wa maoni yameletwa na awamu ya nne.ukweli ni kuwa times change.Huu ni wakati ambao mabadiliko yanadai ni lazima yatokee na siyo serikali iliyoyaleta.
Kwa ufupi kama hawa jamaa wangeliweza, wangetaka kuona tuko kimya hatuongei chochote ila vichwa vyetu tu ndio vionekane. Wameacha mambo yalivyo baada ya kugundua athari za watu kutembea na dukuduku moyoni.
 
nadhani kuna hoja. tujadili na sio kuanza kumshambulia mtoa hoja nasi tutakuwa punguani kama tunavyomwona yeye.

Kwamba awamu ya kwanza ilikuwa na udikteta na kuzuia watu kusema ni kweli na hata watu waliwekwa vizuizini. Lakini awamu hii ilikuwa na jukumu la kujenga taifa moja na ilifanikiwa. Uchumi ilishindwa licha ya kupata misaada mingi kutoka benki ya dunia na nchi za skandinavia. mmesahau tulivyokuwa tunatuma watoto kupanga mistari maduka ya ushirika?

Kwamba awamu ya pili ilikuwa na uholela ni kweli. Lakini awamu hii ilipanua demokrasia na kufungua njia za uchumi na bidhaa kuwa madukani na hivyo hali ya maisha ya watu kuwa bora. Hata hivyo awamu hii haikuweza kabisa kudhibiti na kuongoza uchumi vizuri na hata mfumuko wa bei kufikia 35%

Kwamba awamu ya tatu ilijenga misingi imara ya uchumi ni kweli kabisa. nyie wasomi mnaita fundamentals of the economy. Hii kazi ilifanyika na pato la taifa kukua zaidi ya maradufu na sekta mpya za uchumi kutokea na kutengeneza ajira nyingi sana kulko wakati wowote toka nchi ipate uhuru. Hata hivyo awamu hii iliajaa rushwa kiasi kwamba rushwa zote tunazozungumza leo hii, ukiacha richmond, ni rushwa za awamu ya tatu.

Awamu ya nne imepanua uhuru. watu wapo huru kusema bila woga. Hata hivyo imeshindwa kutafsiri ukuaji wa uchumi wa awamu ya tatu kutoka juu kwenda chini kwa watu na hata mfumuko wa bei umefikia asilimia 13 kutoka 4 alizoacha mkapa. Pia umeshindwa kuchukua hatua kwa mafisadi wa awamu ya 3 ambao wengine wapo awamu ya nne.

Sasa kosa la mtoa hoja kule michuzi lipo wapi au tunataka kusikia tunayoyapenda?
 
Bado ninadirki kusema serikali ya awamu ya nne ni shujaa maana imefungua milango yote ya uhuru na mpaka baadhi ya watu wanadirki sasa kufanya mashambulio ambayo dhahiri yanaonyesha kulenga mtu binafsi??? Kweli tumefikia hapo bila ya kujijua ama kwa makusudi?????

Tatizo la ushabiki ni upofu!
Mtu binafsi ninani huyo? Yule alieomba ridhaa yetu na tukampa? Kwaiyo akiboronga tusimseme eti sababu alileta uhuru?
Hii campaign ya kusafisha waliejichafua kwa matendo yao wenyewe inaonekana imepamba moto kwetu. Uzuri wengi wetu hatudanganyiki!
 
Mwibaji na watwana, mlifi ni mwungwana

(sehemu ya kwanza)

Hizi lawama tutatupiana mpaka lini? Umahiri wa kusemana umekuwa ndiyo utamuduni wetu sasa na haswa kwenye duru la siasa. Baya zaidi hakuna yeyote kati ya hawa wasemaji anakuwa muelimishaji, bali, anakuwa mkosoaji ama mlalamikaji ambaye huongeza na kurudia kauli mbiu “Nchi itafikia ama inaelekea pahali pabaya”, ama kweli sumu ya neno ni neno.

Mara zote panapotokea jambo ambalo linahitaji marekebisho ama mtazamo chanya wa kuboresha hilo jambo, basi ada ya mja ni kunena na siyo kulaumu, kukashifu, ama kudhalilisha na kuwafanya wengine waonekane si bora na labda wapo kwenye nyadhifa walizokabidhiwa na umma kimakosa!!! Kamwe huu si uungwana!!! Ninaandika haya makala kwa makusudi ya kulenga na kukemea tabia mpya ambayo imejitokeza hivi karibuni ya “malumbano bayana” kwa staili ya kuwaita waandishi wa habari ama kuitishia kongamano - na hili linajiri hasa kwa viongozi wa juu wa serikali waliyopo madarakani na wale ambao kwa nyakati fulani walikuwa viongozi katika serikali hii hii.

Kwa matatizo ya kisiasa na kiuchumi ambayo yanamgusa kila mtanzania hayana haja ya yote haya bali zaidi yanahitaji kutafutiwa ufumbuzi na siyo malumbano ambayo mara nyingine watu wameyafananiisha na mtindo maarufu wa nyimbo za mafumbo yaani “Taarab”. Sasa haya mafumbo tumamfumbia nani wakati watanzania takriban wote hivi sasa ni waerevu!!! Kw kurudia lugha yeti ya mtaani ningesema huu si wakati wa “longolongo” kinachotakiwa na kuyanusuru maisha ya watanzania wengi ambao mpaka leo hii wanasuasua katika kujikimu ki-maisha.

Uongozi wa aina yeyote ile huwa mgumu, na siku zote hapatakuwa na asilimia 100 ya makubaliano ama kutokubaliana kwa maamuzi katika uongozi. Hayumkiniki kukubali kwamba yale ya makubaliano ndiyo yenye mafanikio na yasiyo makubaliano ndiyo mapungufu. Awamu zote tatu za Serikali ya Muungano, Tanzania, zilitenda mema mengi na mapungufu hayakukosekana. Sasa bado tungali kwenye awamu ya nne ambayo bado ipo madarakani na kwa hakika nayo ipo katika mchanganuo huo huo wa kuyatazma mema ambayo imetenda na mapungufu yanayojitokeza. Ni ukweli usiyopingika kwamba awamu zote hizi nne zimekuwa na madhumuni ya makusudi ya kuendeleza na kufanya mambo mema kabisa kwa ajili ya wananchi wake maana awamu zote hizi na wananchi wake hawana desturi ama tabia ya kujipaa makaa wenyewe kama pweza.

Katika makala haya nisingependa nami nijitiye katika umahiri wa kusema na kuwa sawa na hao wasemaji wengi ambao sasa ndiyo wamekuwa vichwa vya habari na wahamasishaji wa habari kwa kutenga muda na kuwaita waandishi wa habari wasikilize yaliyotangia mawazoni mwao kana kwamba ni jambo geni na jipya kusikika na dhahiri wanakuwa mithili ya bata akili kwa watoto, ilihali wakijuwa wazi kabisa linalojiri ni yarabi nafsi yangu – (ubinafsi). Kama kweli tunakubali na kusema kwamba penye wazee haliharibiki neno, basi nina hakika kwamba bado tuna wazee ndani ya uongozi na hata nje ya uongozi sasa lipi linaloshindikana kuweza weka mambo sahihi? Kusema tu isitoshe maana tonga si sawa na tui na si kila mwenye makucha huwa simba. La muhimu zaidi ambalo ndiyo pungufu kwetu sisi watanzania ni UZALENDO!! Ni kweli upo UZALENDO lakini si UZALENDO wa tamaa ya kuwa na maendeleo ya kiujumla kiuchumi na kisiasa na mara zote painamapo ndipo painukapo.

Ukitazama kwa uyakinifu katika mambo yote ambayo yanaleta malumbano bayana, utaona kwamba kubwa zaidi linaloelekezwa kwetu sisi wananchi ni katiak kuambiwa kwamba serikali iliyopo madarakani ina matatiozo ya uongozi na ndiyo maana ya matatizo mengi ambayo yamejiri katika nchi hivi sasa.

Hakika, kila awamu ya serikali ilikuwa na mambo yake ambayo yalitukuzwa na kuonekana bora nay ale ambayo yalekebehi ni kuonekana si bora. Inahitaji muda mrefu kuandika makala ambayo ingechambua awamu za serikali zote zilizopita mpaka kufika sasa, lakini kwa makusudi y aujumbe wa makala hii nitarahisisha kwa mifano michache ambayo yote ikiashiria namna gain demokrasia ilivyo ongeza wigo wa uhuru kwetu sisi watanzania.

Ilikuwa si jambo rahisi katika awamu ya serikali ya kwanza ya kizalendo Tanzania watu kusema lolote lile ambalo lingeonekana kama ni jambo kinyume na uongozi wa wakati ule na yeyote yule aliyethubutu kufanya amd kusema kinyume basi aliitwa “Muhaini” na adhabu yake ilikuwa kutiwa kuzuizini na wlae ambao walikuwa na uwezo kidogo waliponyoka kwenye adha hii na kukimbilia kusihi nje ya nchi ama hata nje ya bara la Africa. Watu hawa ambao walikimbia nje walitengenezewa mazingira ambayo yaliwaweka pahala pagumu hata kujitetea maana tukingali wadogo nyakati zile tulifundishwa hat anyimbo za kuimba za kuwadhalilisha hawa “mahaini” na hata kufikia kusema kama atatokea basi “mchinje”!!!! Na hizi hasa ndzio zilikuwa mbinu za propaganda za kisiasa wakati huo ambazo kwlei zilifana na hasa kwa matumizi ya vyombo vya habari na njia zote za mawasiliano ambazo zilikuwa zote zipo mikononi mwa serikali tawala.

Awamu hii ilipita na tukaona hata wale “wahaini” na waliyokuwa kizuizini wamerudi na wakaingia tena katika duru la siasa ambapo hawakufua dafu maana tayari walikuwa wamechoka sana ama kwa umri ama maradhi ama taabu zingine zozote za kutokuwa karibu na jumuiya ambayo wangependa kuchangia japo kidogo walichokuwa nacho!!! Haya yote yalikuwa ni mateso na bugudha ambazo baadhi ya watu walizipata kutoka kwenye serikali ya kipindi hicho, na hata waliporejea hapakuwa na kushitakiwa ama kusukumwa sukumwa tena maana tayari walikuwa wanaonekana tofauti ndani ya jamii ambayo waliipoteza takriban zaidi ya miaka ishirini na zaidi!!.

Demokrasia ikwa kidogo sasa inapenya baada ya ruhusa ya kuwaingiza “wahaini” na kuwafutia makosa wale waliyotiwa kizuizini kwa kutofautiana na uongozi wa juu wa serikali ya kipindi hicho.

Awamu ya pili ikafungua ukurasa mpya ambao ulikuja kuzaa uhuru wa biashara na kuweka na uwezo mwingi tu wa baadhi ya wananchi kujiweka pahala panono ki mapato, jambo ambalo lili zaa kauli mbio “RUKSA”. Kweli baadhi ya wananchi wakapat “ruksa” ya kuwa matajiri na hata wawekezaji ama wabia. Ilikuwa furaha isiyo kifani na hapa ndipo utajiri uliyo zaa ubinafsi ulipoanzia.

Ikumbukwe kwamba hii awamu ya pili nayo iliingia na staili yake ya uongozi na viongozi ambao walikuwa ndiyo chaguo la awamu hiyo.

Ndipo hapa tulipoanza kuwa na kipima joto cha uongozi maana sasa tunalo jingine la kufananisha. Mambo mengi yakasemwa kuhusu awamu ya kwanza na ugumu wa maisha ambao ulionekana kuwepo katika serikali ya awamu ya kwanza, sasa tumepewa “RUKSA” hivyo ilikuwa ni umahiri wako wewe mwananchi kwamba ni kiasi gani unaweza “kujichanganya”, “Bongo” imezaliwa.


Awamu ya pili ikapita kwa vishindo na visa vingi tuu na hata pakatokea kwamba uongozi wa awamu ya mwanzo kuwa na “malumbano bayana pekee” ninaposema malumbano bayana pekee nina maananisha kwamba haya malumbano yaliweza kutolewa upande mmoja tuu na upande ambao unashambuliwa ulikuwa butu kujibu haya labda kwa hofu ile ya kwamba unaweza kuwekwa “kizuizini” ama kuitwa “muhaini”, maana bado uongozi wa awamu ya kwanza ulikuwa bado na wafuasi wake wngi ambao bado walikuwa watendaji sehemu nyeti za serikali ya awamu ya pili!!!! Lakini pakatokea njia na namna ya kuwaopunguzia makali hawa viongozi waliyokuja toka awamu ya mwanzo nayo ilikuwa ni kuyabatilisha baadhi ya maamuzi na maazimo muhimu yaliyopitishwa awamu ya mwanzo.!!!!

Awamu hii ya pili tulisikia watu wakibezwa kuendesha nchi kwa kuwasikiliza wake zao na wengine waliitwa “wahuni” basi ili mradi kuna jambo la kukosoa lilipenyeza, nab ado watu wakastahimili na kukaa kimya bila ya majibu na mambo yakawa swhari maana ilikuwa “RUKSA”.

usikose kesho (inshaallah panapo majaaliwa) sehemu ya pili na ya mwisho ya hoja nya haja hii




QUOTE=Sumaku;707612] ( Hii nimeinasa kule Michuzi blog, imepambisha mjadala. Kuna mwenye sehemu ya kwanza atumwagie humu ukumbini!)

HOJA YA HAJA

Mwibaji na watwana, mlifi ni mwungwana
(sehemu ya pili na ya mwisho)

Ilipopita awamu ya pili ikajiri awamu ya tatu (Awamu kati). Hii kwa hakika ilikuwa awamu ambayo iliingia katikati na kuyaangalia mapungufu na mafanikio ya awamu ya kwanza na awamu ya pili.


Awamu hii ikarudia pale pale kwenye awamu ya kwanza kuhusu swala la demokrasia, na kwamba viongozi wake wakawa wakali kwamba wanataka kurudisha tabia ile ile ya kuogopa watu wasisemeseme hovyo. Hakika viongozi wa awamu ta tatu walikuwa wakali sana na wakatengeza uga ambao ilikuwa si rahisi tu kupenyeza rupia hata penye udhia.

Awamu hii ilisheheni sifa za kujenga uchumi na kwamba pato la taifa likawa limedhibitiwa na ule uholela baada ya “RUKSA” haukuwepo tena, na zaidi ubinafsi sasa ukarudi na kujilimbikiza kwa hao viongozi wa awamu ya tatu. Kauli mbio hapa ilikuwa na “Uongozi Bora”. Hakika ulikuwa uongozi bora maana matokeo yake yalikuwa kwamba baadhi ya viongozi walikuwa bora haswaa katika kujizatiti ki-uchumi na kimaendeleo binafsi na siyo kwa kila mwananchi!.

Mengi yamesemwa na bado yataendelea kusemwa kuhusu maazimio yenye madhumini endelezi ya awamu zote tatu na hapatakosa kujiri kasoro zake ambazo baadhi nimezigusia hapo juu.

Haya sasa tupo kwenye awamu ya nne ambayo ilipokelewa kwa vishindo, shangwe na nderemo nah ii kweli iliingia kwa staili yake tofauti kabisa na awamu zote japo ikizingatia kabisa misingi muhimu iliyowekwa na awamu zote ambazo zilizopita. Hapa tukapata utawala wa kwanza kabisa wa uongozi wote wa juu kuwa na safu kubwa ya vijana ambayo wengi waliitafsiri kwa lugha ya kigeni “boys to men”. Hakika pailikuwa na faraja kubwa na hasa kwa vijana ambao ndiyo tumaini kubwa la maendeleo yeyote katika nchi yeyote.

Hapa pakatokea demokrasia ya uga mpana kabisa kwamba unaweza kusme chochote na hata jambo ambalo si zuri kulisema kwa kumtaja kiongozi yeyote yule wa kitaifa na bado hutafanywa lolote kama vile kupelekwa kuzuizini ama kuitwa muhaini.

Sasa ni hili ndilo limezaa yote haya ya watu kutumia vinywa vyao kusema yanayowakera binafsi na kuyafanya ya kitaifa, kujenga tabaka za makundi ya wafuasi wa kisiasa na mpaka kufikia kuleta makundi ambayo sasa ndiyo yamekuwa maarufu ndani ya serikali na vyama vyao vya kisiasa na hata mpaka kwenye dini!!!! Hakika chombo kinawenda mrama hapa!!!

Nani alisema kwamba unapokuwa na uhuru wa kusema basi unasimama kwenye majukwaa na kuanza kukashifu na kubeza viongozi wa kitafia eti tu kwa sababu nawe ulikuwa kiongozi wa nyadhifa fulani katika awamu zilizopita?


Mbona wapo ambao walikuwa na hata nyadhifa kubwa tu wamekaa kimya na ndiyo sasa wanatumika kama wapatanishi wa malumbano haya!!! Kwa nini hizi taasisi ambazo zina majina makubwa zisijitenge ili kujitofautisha na “taasisi shutumu” badala ya kuleta maneno ama makongamano ya kushutumu, kukashifu na kudhalilisha viongozi ziungane na waungwana ambao wamekuwa mstari wa mbele katika kuleta suluhu ya matatizo yanayojiri nchi yetu kisiasa na kiuchumi??
Bado ninadirki kusema serikali ya awamu ya nne ni shujaa maana imefungua milango yote ya uhuru na mpaka baadhi ya watu wanadirki sasa kufanya mashambulio ambayo dhahiri yanaonyesha kulenga mtu binafsi??? Kweli tumefikia hapo bila ya kujijua ama kwa makusudi?????


Tanzania, Tanzania, Nakupenda kwa moyo wote!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
[/QUOTE]
 
Pumba!! awamu ya nne wamepewa misaada zaidi ya awamu zote za Utawala zilizopita, lakini cha ajabu wanaongoza kwa mifumuko wa bei, wanaongoza kwa kujenga barabara zisizo na viwango na ucheleweshwaji wa ujenzi huo, kisa wenye mtandao wanataka hizo projects wakiongozwa na RA! Pia safari zisizo na kichwa wala miguu zikifuatana na umati wa watu!

Nakuomba ukalale utuachie wenye uchungu na nchi hii! Ukiwa unachangia humu ndani jaribu kuweka facts sio kuoanisha ati serikali ipi ni nafuu zaidi! What if zote zilikuwa wendawazimu? When you are given over 80% of votes of confidence, know that comes at a price! the same percent will kick you out if you disappoint them! And this is what we are trying to do! Mobilizing mass to see uozo! this jamaa TOSHA SASA na akachekee huko alikotoka yaani mtandaoni!

Hawa jamaa wanaimba ati kilimo Kwanza ukiangalia nchi hii ina Big Five Regions as food Baskets! sasa tujiulize Pwani ni one of them? Jibu ni hapana sasa ni kwanini kila barabara inajengwa pwani sasa? Project nyingi zinaamishiwa huko? Kama 48% ya uchumi wetu inategemea kilimo kwanini zisijengwe huko kwenye big five regions? kuna economic activities gani Pwani?

Na migodini napo? Kama over 30% of GNI inatokana na migodi kwanini leo hii hatuna barabara na umeme wa uhakika? matokeo yake kila siku tunawapa tax cuts hawa wenye migodi kwa vijisababu ati production cost kubwa! Humo humo watu wanaingiza mafuta ya magendo tunapoteza makusanyo ya kodi na tunauza madini yetu bei ya kutupwa! Wakati tungekuwa na umeme wa uhakika tungeuza umeme plus tax collection inge-improve plus more job creation.

Huu muda si wa kuacha watu wenye kuchekacheka madarakani ati? Kupendelewa kwetu na US na EU kwenye misaada comes once in a life time! If we mess the chance now hatutakaa tena tupate uliza Kenya na Uganda wakwambie! wamepita huku tulipo sasa! So get the point wakubembea apime na kujua kama yuko nasi wananchi au yuko na EL na RA na other wanamtandao?

Wewe kalagha bao!

Mwibaji na watwana, mlifi ni mwungwana

(sehemu ya kwanza)

Hizi lawama tutatupiana mpaka lini? Umahiri wa kusemana umekuwa ndiyo utamuduni wetu sasa na haswa kwenye duru la siasa. Baya zaidi hakuna yeyote kati ya hawa wasemaji anakuwa muelimishaji, bali, anakuwa mkosoaji ama mlalamikaji ambaye huongeza na kurudia kauli mbiu "Nchi itafikia ama inaelekea pahali pabaya", ama kweli sumu ya neno ni neno.

Mara zote panapotokea jambo ambalo linahitaji marekebisho ama mtazamo chanya wa kuboresha hilo jambo, basi ada ya mja ni kunena na siyo kulaumu, kukashifu, ama kudhalilisha na kuwafanya wengine waonekane si bora na labda wapo kwenye nyadhifa walizokabidhiwa na umma kimakosa!!! Kamwe huu si uungwana!!! Ninaandika haya makala kwa makusudi ya kulenga na kukemea tabia mpya ambayo imejitokeza hivi karibuni ya "malumbano bayana" kwa staili ya kuwaita waandishi wa habari ama kuitishia kongamano - na hili linajiri hasa kwa viongozi wa juu wa serikali waliyopo madarakani na wale ambao kwa nyakati fulani walikuwa viongozi katika serikali hii hii.

Kwa matatizo ya kisiasa na kiuchumi ambayo yanamgusa kila mtanzania hayana haja ya yote haya bali zaidi yanahitaji kutafutiwa ufumbuzi na siyo malumbano ambayo mara nyingine watu wameyafananiisha na mtindo maarufu wa nyimbo za mafumbo yaani "Taarab". Sasa haya mafumbo tumamfumbia nani wakati watanzania takriban wote hivi sasa ni waerevu!!! Kw kurudia lugha yeti ya mtaani ningesema huu si wakati wa "longolongo" kinachotakiwa na kuyanusuru maisha ya watanzania wengi ambao mpaka leo hii wanasuasua katika kujikimu ki-maisha.

Uongozi wa aina yeyote ile huwa mgumu, na siku zote hapatakuwa na asilimia 100 ya makubaliano ama kutokubaliana kwa maamuzi katika uongozi. Hayumkiniki kukubali kwamba yale ya makubaliano ndiyo yenye mafanikio na yasiyo makubaliano ndiyo mapungufu. Awamu zote tatu za Serikali ya Muungano, Tanzania, zilitenda mema mengi na mapungufu hayakukosekana. Sasa bado tungali kwenye awamu ya nne ambayo bado ipo madarakani na kwa hakika nayo ipo katika mchanganuo huo huo wa kuyatazma mema ambayo imetenda na mapungufu yanayojitokeza. Ni ukweli usiyopingika kwamba awamu zote hizi nne zimekuwa na madhumuni ya makusudi ya kuendeleza na kufanya mambo mema kabisa kwa ajili ya wananchi wake maana awamu zote hizi na wananchi wake hawana desturi ama tabia ya kujipaa makaa wenyewe kama pweza.

Katika makala haya nisingependa nami nijitiye katika umahiri wa kusema na kuwa sawa na hao wasemaji wengi ambao sasa ndiyo wamekuwa vichwa vya habari na wahamasishaji wa habari kwa kutenga muda na kuwaita waandishi wa habari wasikilize yaliyotangia mawazoni mwao kana kwamba ni jambo geni na jipya kusikika na dhahiri wanakuwa mithili ya bata akili kwa watoto, ilihali wakijuwa wazi kabisa linalojiri ni yarabi nafsi yangu – (ubinafsi). Kama kweli tunakubali na kusema kwamba penye wazee haliharibiki neno, basi nina hakika kwamba bado tuna wazee ndani ya uongozi na hata nje ya uongozi sasa lipi linaloshindikana kuweza weka mambo sahihi? Kusema tu isitoshe maana tonga si sawa na tui na si kila mwenye makucha huwa simba. La muhimu zaidi ambalo ndiyo pungufu kwetu sisi watanzania ni UZALENDO!! Ni kweli upo UZALENDO lakini si UZALENDO wa tamaa ya kuwa na maendeleo ya kiujumla kiuchumi na kisiasa na mara zote painamapo ndipo painukapo.

Ukitazama kwa uyakinifu katika mambo yote ambayo yanaleta malumbano bayana, utaona kwamba kubwa zaidi linaloelekezwa kwetu sisi wananchi ni katiak kuambiwa kwamba serikali iliyopo madarakani ina matatiozo ya uongozi na ndiyo maana ya matatizo mengi ambayo yamejiri katika nchi hivi sasa.

Hakika, kila awamu ya serikali ilikuwa na mambo yake ambayo yalitukuzwa na kuonekana bora nay ale ambayo yalekebehi ni kuonekana si bora. Inahitaji muda mrefu kuandika makala ambayo ingechambua awamu za serikali zote zilizopita mpaka kufika sasa, lakini kwa makusudi y aujumbe wa makala hii nitarahisisha kwa mifano michache ambayo yote ikiashiria namna gain demokrasia ilivyo ongeza wigo wa uhuru kwetu sisi watanzania.

Ilikuwa si jambo rahisi katika awamu ya serikali ya kwanza ya kizalendo Tanzania watu kusema lolote lile ambalo lingeonekana kama ni jambo kinyume na uongozi wa wakati ule na yeyote yule aliyethubutu kufanya amd kusema kinyume basi aliitwa "Muhaini" na adhabu yake ilikuwa kutiwa kuzuizini na wlae ambao walikuwa na uwezo kidogo waliponyoka kwenye adha hii na kukimbilia kusihi nje ya nchi ama hata nje ya bara la Africa. Watu hawa ambao walikimbia nje walitengenezewa mazingira ambayo yaliwaweka pahala pagumu hata kujitetea maana tukingali wadogo nyakati zile tulifundishwa hat anyimbo za kuimba za kuwadhalilisha hawa "mahaini" na hata kufikia kusema kama atatokea basi "mchinje"!!!! Na hizi hasa ndzio zilikuwa mbinu za propaganda za kisiasa wakati huo ambazo kwlei zilifana na hasa kwa matumizi ya vyombo vya habari na njia zote za mawasiliano ambazo zilikuwa zote zipo mikononi mwa serikali tawala.

Awamu hii ilipita na tukaona hata wale "wahaini" na waliyokuwa kizuizini wamerudi na wakaingia tena katika duru la siasa ambapo hawakufua dafu maana tayari walikuwa wamechoka sana ama kwa umri ama maradhi ama taabu zingine zozote za kutokuwa karibu na jumuiya ambayo wangependa kuchangia japo kidogo walichokuwa nacho!!! Haya yote yalikuwa ni mateso na bugudha ambazo baadhi ya watu walizipata kutoka kwenye serikali ya kipindi hicho, na hata waliporejea hapakuwa na kushitakiwa ama kusukumwa sukumwa tena maana tayari walikuwa wanaonekana tofauti ndani ya jamii ambayo waliipoteza takriban zaidi ya miaka ishirini na zaidi!!.

Demokrasia ikwa kidogo sasa inapenya baada ya ruhusa ya kuwaingiza "wahaini" na kuwafutia makosa wale waliyotiwa kizuizini kwa kutofautiana na uongozi wa juu wa serikali ya kipindi hicho.

Awamu ya pili ikafungua ukurasa mpya ambao ulikuja kuzaa uhuru wa biashara na kuweka na uwezo mwingi tu wa baadhi ya wananchi kujiweka pahala panono ki mapato, jambo ambalo lili zaa kauli mbio "RUKSA". Kweli baadhi ya wananchi wakapat "ruksa" ya kuwa matajiri na hata wawekezaji ama wabia. Ilikuwa furaha isiyo kifani na hapa ndipo utajiri uliyo zaa ubinafsi ulipoanzia.

Ikumbukwe kwamba hii awamu ya pili nayo iliingia na staili yake ya uongozi na viongozi ambao walikuwa ndiyo chaguo la awamu hiyo.

Ndipo hapa tulipoanza kuwa na kipima joto cha uongozi maana sasa tunalo jingine la kufananisha. Mambo mengi yakasemwa kuhusu awamu ya kwanza na ugumu wa maisha ambao ulionekana kuwepo katika serikali ya awamu ya kwanza, sasa tumepewa "RUKSA" hivyo ilikuwa ni umahiri wako wewe mwananchi kwamba ni kiasi gani unaweza "kujichanganya", "Bongo" imezaliwa.


Awamu ya pili ikapita kwa vishindo na visa vingi tuu na hata pakatokea kwamba uongozi wa awamu ya mwanzo kuwa na "malumbano bayana pekee" ninaposema malumbano bayana pekee nina maananisha kwamba haya malumbano yaliweza kutolewa upande mmoja tuu na upande ambao unashambuliwa ulikuwa butu kujibu haya labda kwa hofu ile ya kwamba unaweza kuwekwa "kizuizini" ama kuitwa "muhaini", maana bado uongozi wa awamu ya kwanza ulikuwa bado na wafuasi wake wngi ambao bado walikuwa watendaji sehemu nyeti za serikali ya awamu ya pili!!!! Lakini pakatokea njia na namna ya kuwaopunguzia makali hawa viongozi waliyokuja toka awamu ya mwanzo nayo ilikuwa ni kuyabatilisha baadhi ya maamuzi na maazimo muhimu yaliyopitishwa awamu ya mwanzo.!!!!

Awamu hii ya pili tulisikia watu wakibezwa kuendesha nchi kwa kuwasikiliza wake zao na wengine waliitwa "wahuni" basi ili mradi kuna jambo la kukosoa lilipenyeza, nab ado watu wakastahimili na kukaa kimya bila ya majibu na mambo yakawa swhari maana ilikuwa "RUKSA".

usikose kesho (inshaallah panapo majaaliwa) sehemu ya pili na ya mwisho ya hoja nya haja hii




QUOTE=Sumaku;707612] ( Hii nimeinasa kule Michuzi blog, imepambisha mjadala. Kuna mwenye sehemu ya kwanza atumwagie humu ukumbini!)

HOJA YA HAJA

Mwibaji na watwana, mlifi ni mwungwana

(sehemu ya pili na ya mwisho)

Ilipopita awamu ya pili ikajiri awamu ya tatu (Awamu kati). Hii kwa hakika ilikuwa awamu ambayo iliingia katikati na kuyaangalia mapungufu na mafanikio ya awamu ya kwanza na awamu ya pili.


Awamu hii ikarudia pale pale kwenye awamu ya kwanza kuhusu swala la demokrasia, na kwamba viongozi wake wakawa wakali kwamba wanataka kurudisha tabia ile ile ya kuogopa watu wasisemeseme hovyo. Hakika viongozi wa awamu ta tatu walikuwa wakali sana na wakatengeza uga ambao ilikuwa si rahisi tu kupenyeza rupia hata penye udhia.

Awamu hii ilisheheni sifa za kujenga uchumi na kwamba pato la taifa likawa limedhibitiwa na ule uholela baada ya "RUKSA" haukuwepo tena, na zaidi ubinafsi sasa ukarudi na kujilimbikiza kwa hao viongozi wa awamu ya tatu. Kauli mbio hapa ilikuwa na "Uongozi Bora". Hakika ulikuwa uongozi bora maana matokeo yake yalikuwa kwamba baadhi ya viongozi walikuwa bora haswaa katika kujizatiti ki-uchumi na kimaendeleo binafsi na siyo kwa kila mwananchi!.


Mengi yamesemwa na bado yataendelea kusemwa kuhusu maazimio yenye madhumini endelezi ya awamu zote tatu na hapatakosa kujiri kasoro zake ambazo baadhi nimezigusia hapo juu.

Haya sasa tupo kwenye awamu ya nne ambayo ilipokelewa kwa vishindo, shangwe na nderemo nah ii kweli iliingia kwa staili yake tofauti kabisa na awamu zote japo ikizingatia kabisa misingi muhimu iliyowekwa na awamu zote ambazo zilizopita. Hapa tukapata utawala wa kwanza kabisa wa uongozi wote wa juu kuwa na safu kubwa ya vijana ambayo wengi waliitafsiri kwa lugha ya kigeni "boys to men". Hakika pailikuwa na faraja kubwa na hasa kwa vijana ambao ndiyo tumaini kubwa la maendeleo yeyote katika nchi yeyote.

Hapa pakatokea demokrasia ya uga mpana kabisa kwamba unaweza kusme chochote na hata jambo ambalo si zuri kulisema kwa kumtaja kiongozi yeyote yule wa kitaifa na bado hutafanywa lolote kama vile kupelekwa kuzuizini ama kuitwa muhaini.

Sasa ni hili ndilo limezaa yote haya ya watu kutumia vinywa vyao kusema yanayowakera binafsi na kuyafanya ya kitaifa, kujenga tabaka za makundi ya wafuasi wa kisiasa na mpaka kufikia kuleta makundi ambayo sasa ndiyo yamekuwa maarufu ndani ya serikali na vyama vyao vya kisiasa na hata mpaka kwenye dini!!!! Hakika chombo kinawenda mrama hapa!!!

Nani alisema kwamba unapokuwa na uhuru wa kusema basi unasimama kwenye majukwaa na kuanza kukashifu na kubeza viongozi wa kitafia eti tu kwa sababu nawe ulikuwa kiongozi wa nyadhifa fulani katika awamu zilizopita?

Mbona wapo ambao walikuwa na hata nyadhifa kubwa tu wamekaa kimya na ndiyo sasa wanatumika kama wapatanishi wa malumbano haya!!! Kwa nini hizi taasisi ambazo zina majina makubwa zisijitenge ili kujitofautisha na "taasisi shutumu" badala ya kuleta maneno ama makongamano ya kushutumu, kukashifu na kudhalilisha viongozi ziungane na waungwana ambao wamekuwa mstari wa mbele katika kuleta suluhu ya matatizo yanayojiri nchi yetu kisiasa na kiuchumi??

Bado ninadirki kusema serikali ya awamu ya nne ni shujaa maana imefungua milango yote ya uhuru na mpaka baadhi ya watu wanadirki sasa kufanya mashambulio ambayo dhahiri yanaonyesha kulenga mtu binafsi??? Kweli tumefikia hapo bila ya kujijua ama kwa makusudi?????


Tanzania, Tanzania, Nakupenda kwa moyo wote!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
[/QUOTE]
 
Huyu kaandika kwanza kwa kujikomba kwa Michuzi ambaye ni CCM damu na mnafiki mkubwa sijui kwa nini hajifunzi kwa akiNa Lusekelo

Au kaandika kweli kwa ujinga akijua kuwa kusema sana kama yeye allivyoandika sana sio kipimo cha mafanikio..

Kila mtu leo angemsifia JK hata hao waliosema wasingesema kama tu JK angewapeleka jela na mali zetu kurudishwa.

mwaka wa tano nyimbo zile zile, bado mtu anakaa na kumsifia JK?


Michuzi hana uwezo wa kujifunza kwa waandishi mahili kama Lusekelo na Ngurumo; yeye utaalam wake ni kupiga picha TU!! Jakaya hajaleta uhuru wa watu kusema wazi wazi juu ya jinsi nchi inavyoyumbishwa; uhuru huo umeletwa na maendeleo ya jamii duniani!! Leo hii Kikwete ajaribu kuwaweka watu kizuizini tuone kama serikali yake itadumu hata siku moja!! Hata kuwafungulia kesi hao mafisadi wadogo haikuwa nia yake bali ni shinikizo la wenye nazo{ SO CALLED DEVELOPMENT PARTNERS}. Hao wenye nazo wanaofadhili budget yake hence safari zake za nje ndio hao hao walioshinikiza kuwepo kwa uhuru huu wa mawazo ambao unawaumbua CCM na mafisadi wao. Kikwete hawezi kurudisha enzi za kuwaweka watu kizuizini hata akitaka kufanya hivyo; huu ni wakati mwingine kabisa.
 
Maneno yanatakiwa kuwa mafupi, matendo ndio yawe marefu. Awamu zote zinazozungumziwa ni ccm ile ile tofauti inayojitokeza wazi kwa awamu ya nne ni ile staili ya kujifanya wao ni mvinyo mpya ndani ya kiriba cha kale(ccm) iliyopelekea kiriba kupasuka. Eeh SASA KIRIBA KIMEPASUKA TUNAHITAJI KIPYA NA MVINYO MPYA. HATUDANGANYIKIIIIIIIIIII!!
 
Ni uongo wa mchana kusema kuwa serikali ya awamu ya nne imefungua milango ya kuzungumza kwa uhuru. Hivi tumesahau jinsi wanamtandao wa serikali hii walivyotumia uhuru wa vyombo vya habari kuwachafua wale waliowadhania kuwa washindani wao katika kinyang'anyiro cha urais? Vyombo hivyo vilifanyiwa nini? Halafu kuna mtu hapa anataka eti tuzungumzie hoja. If I had a gun I would have shot the messenger for wasting our time.
 
mabadiliko hayajaletwa na Awamu ya nne bali watu na nyakati! Kama kuna watu wa kupongezwa na haya mabadiliko basi ni wanahabari (japokuwa wapo wale wanaopotosha jamii pia kwa maslahi ya Ufisadi).

Kwanza huyo Michuzi mwenyewe ni mnafiki nikipeleka article zangu za kusema uozo ndani ya Serikali ya JK huwa ha-publish ndo hawa tunawaita vibaraka! lakini huwa mstari wa mbele kutoa zile zinazompamba Rais na serikali yake! Halafu anadai ati blog ya Jamii!
Haijawahi kuwa blog ya jamii labda kama ana maana jamii ya magogoni!
 
Siamini kwamba mabadiliko ya uhuru wa maoni yameletwa na awamu ya nne.ukweli ni kuwa times change.Huu ni wakati ambao mabadiliko yanadai ni lazima yatokee na siyo serikali iliyoyaleta.
Kwa ufupi kama hawa jamaa wangeliweza, wangetaka kuona tuko kimya hatuongei chochote ila vichwa vyetu tu ndio vionekane. Wameacha mambo yalivyo baada ya kugundua athari za watu kutembea na dukuduku moyoni.
Watu wanapokosa hoja usema lolote hata lisilo na maana.
Kwani uhuru wa habari ni kitu cha hisani toka kwa kiongozi au ni haki yetu kikatiba?
Watu wengine bana?????? wapelekwe Milembe
 

Kwamba awamu ya kwanza ilikuwa na udikteta na kuzuia watu kusema ni kweli na hata watu waliwekwa vizuizini
. Lakini awamu hii ilikuwa na jukumu la kujenga taifa moja na ilifanikiwa. Uchumi ilishindwa licha ya kupata misaada mingi kutoka benki ya dunia na nchi za skandinavia. mmesahau tulivyokuwa tunatuma watoto kupanga mistari maduka ya ushirika?

Hakuna nchi ambayo haina watu ambao wako kizuizini kwa maslahi ya taifa husika. Marekani sasa hivi inashutumiwa kwa kuwaweka watu kizuizini kwenye gereza la Guatanamo huko Cuba!

Kimantiki Nyerere hakuwaweka kizuizini watu waliokuwa wanasema yeye hafai kuongoza, bali aliwaweka watu kizuizini waliokuwa wanadhani ni heri kutawaliwa na Mkoloni kuliko waafrika wenzao.

Mtei alipingana kwa hoja na Nyerere aliwekwa kizuizini au kutishiwa maisha yake? Sasa hivi ni wangapi wanapeperusha bendera za CCM kwenye biashara zao ili kulinda maslahi yao ya kibiashara?
 
Bado ninadirki kusema serikali ya awamu ya nne ni shujaa maana imefungua milango yote ya uhuru na mpaka baadhi ya watu wanadirki sasa kufanya mashambulio ambayo dhahiri yanaonyesha kulenga mtu binafsi??? Kweli tumefikia hapo bila ya kujijua ama kwa makusudi?????

Tatizo la ushabiki ni upofu!
Mtu binafsi ninani huyo? Yule alieomba ridhaa yetu na tukampa? Kwaiyo akiboronga tusimseme eti sababu alileta uhuru?
Hii campaign ya kusafisha waliejichafua kwa matendo yao wenyewe inaonekana imepamba moto kwetu. Uzuri wengi wetu hatudanganyiki!


Naachia wengine wakujibu huu upupu wako mie muda sina wa kuvutana nawe kwenye hili ............................
 
- Amewafungulia uhuru wanachi 70% wanaofuata upepo tu, inachekesha sana! Madaraka ya kupata kwa kutumia ndumba za Wa-Nigeria, ndio matokeo yake haya sometimes nasikia hizo ndumba huwa zina-expire!

Respect.


FMEs!
 
Back
Top Bottom