HOJA MBADALA: Tuhamasishe CCM imsimamishe Membe 2015?

HOJA MBADALA: Tuhamasishe CCM imsimamishe Membe 2015?

Hivi unaposema hayo maneno hapo ktk red huwa una maana gani? Aaaaaaggggggg
Mkuu Nsanu, jf was meant for ma gt, ila hata sisi watu wa kawaida tusio ma great thinkers pia tupo, utakapo kuwa kuwa mkubwa zaidi kidogo kiakili, nawe utakuwa great thinker hivyo nawe ndio angalau utanielewa namaanisha nini!.
P.
 
Hiki kinachoitwa kashfa ya fedha za Libya tumeisubiri muda mrefu lakini nafikiri huyo producer wa hiyo filamu mitambo yake imeungua na umeme wa Tanesco. Niwaambie hivi, and you can take this to the bank, Membe has what it takes to be the next President na kama kuna wanaodhani uadilifu siyo sifa ya uongozi basi labda mnazungumzia uongozi wa Freemasons au kwa TB Joshua. For once Mwanakijiji umeona mbali!
Time will tell,siku utakaposikia kuhusu huyu jamaa ndio utajua kuwa Tanzania ni nchi ya maajabu saba ya duniani.
 
Membe pekee ndiye anajipambanua safi katika wana CCM wanaouota Urais! hana kashfa na unafki kama Lowassa na Sitta
 
MM naomba nichakachue thread yako kama inavyoendelea kuchakachuliwa.
Mara nyingi natatizika sana kila ninaposoma habari za fulani ni best candidate.
Hapa ndipo nakubaliana na Mkandara kuwa elimu ya uraia bado ni tatizo kubwa sana.

Wenzetu wanaojua kuchagua viongozi huangalia kigezo kimoja hadi kingine:
Maadili ya mtu, misimamo yake kisiasa, anasimamia nini, mahusiano na wenzake, mahusiano na chama chake, ushiriki katikashughuli za kijamii, maadili yake, mahusiano kati yake na wananchi, mtazamo wake kuhusu nchi, historia ya utendaji wake, maamuzi aliyowahi kuayafanya huko nyuma, uthubutu katika kusimamia anachokiamini n.k.

Tunatakiwa twende mbali zaidi ya hapa pa kusema fulani atatusaidia.
Labda nitoe mifano kidogo, ni Membe aliyetuambia kuwa tumeibiwa katika Radar, ni Membe aliyekataa kutuambia nani ni wezi. Alichotaka ni ku-score political point kuwa pesa zimerudi! Sasa huyu mtu kimaadili unamweka kundi gani?
Nina nani miongoni mwetu anayejua misimamo ya Membe kuhusu masuala ya kitaifa?

Mfano wa pili, ni Lowasa huyu aliyetuambia hakuna wizi Richmond, ni Lowasa huyu aliyejiuzulu kwa dhambi anayosema hakuitenda, ni Lowasa huyu anayesema alifanya hivyo kuilinda serikali, ni Lowasa huyo asiyetuambia nani alibofoa Richmond hadi leo tunapata hasara. Ushujaa wa kusema huyu ni best candidate unakuwa katika misingi gani?
Ni nani anayeweza kunishawishi kuhusu uadilifu wa Lowasa hadi apewe ofisi kubwa kiasi hicho?Ni nani anayeweza kutumia vigezo ilivyoweka kumpa pasi Lowasa japo 60%?

Kama ni suala la kusema tu fulani anafaa basi mimi nasema Sophia Simba anafaa kama best candidate.
Msiniulize kwa vigezo gani kwasababu lengo ni kutaja tu.

kwa mantiki ya MM mimi naona LUSINDE ndio anafaa.. Ndugu nguruvi3 znachakuongeza ww ni noumaaa
 
...Kama ni suala la kusema tu fulani anafaa basi mimi nasema Sophia Simba anafaa kama best candidate.
Msiniulize kwa vigezo gani kwasababu lengo ni kutaja tu.

Kama ni hivyo, naunga mkono hoja, sasa ni zamu ya kina mama na Sophia Simba anafaa zaidi kuliko wengine waliopo, ila niende mbali zaidi kidogo na kupendekeza kwamba Job Ndugai awe ndio running mate, halafu washauriane vizuri ili Waziri Mkuu ajae awe Lazaro Nyalandu;
 
Nenda kawahamasishe ndugu zako wa kule mtama-lindi,hatutaki tena rais ajaye awe chinga, kama yule bwana ake na mama wa kichaga
 
Mimi nadhani tunapoteza tu muda wetu mwingi sana kujadili majina ya wagombea wa CCM wakati ni dhahiri kwamba hata asimamishwe nani kwa tiketi ya CCM, chini ya kanuni ya sasa ya Mshindi ni Mshindi, atakayeshinda Uchaguzi Mkuu ngazi ya Urais 2015 ni CCM, kwa mfano hata mgombea wa CCM akipata 50.01% dhidi ya mgombea wa Chadema 49.99%, mshindi atakuwa ni CCM, labda kama katika kipindi kilichobakia Chadema watafanya juhudi za ziada katiba mpya ibadili Uchwara huu;

Vinginevyo ushindi wa Chadema utakuwepo zaidi majimboni. Ni muhimu tu katika kipindi hiki (hasa iwapo kanuni ya mshindi ni mshindi itabakia intact):


  • Chadema wakaanza kujiandaa kisaikolojia juu ya uwezekano wa kualikwa kuunda serikali ya Umoja kutokana na Chadema kushinda viti vingi sana vya Ubunge, huku ikijua wazi kwamba itakuwa ni kula matapishi yake kwani ndoa ya Vyama Chadema imeikataa kama vile ni ndoa ya Jinsi Moja;


  • Huku nao CCM waanze kujiandaa pia kisaikolojia kuwa na Rais ambae atapita uchaguzi mkuu kwa just above 50%, kwa mara ya kwanza katika historia ya chama hiki;

Ni muhimu pia Chadema isijidanganye na matokeo ya uchaguzi Zanzibar 1995, 2000, 2005, 2010 ambapo CUF inasemekena ilishinda mara zote; Hii ni kwa sababu kama ilivyokuwa kwa uwepo wa mabaki ya TANU bara, yapo mabaki ya ASP Zanzibar, na CCM ni ndoa tu ambayo Suala la yupi ni mke na yupi ni mume baina ya TANU na ASP, is very much open to debate;
 
ni Membe tu ambaye anaonekana kulindwa na mlolongo mkubwa wa kashfa mbalimbali na japo - kama nilivyosema wiki kadhaa nyuma - hajajiandaa kuwa Rais ni wazi miaka hii miwili iliyobakia inaweza kumsaidia kujitengenezea na kuwa a true "presidential candidate"


The weight of the thread in what is manifested in red + bold! This Mwanakijiji is contemptuously and ambivalently expressing himself in sarcasm.

Bahati mbaya sana wachache huwa wanafumbuliwa kufumbua mafumbo!
 
Magamba wasahau 2015

Kwa tume hiihii na police hawahawa, Magamba wana kila sababu ya kushinda mwaka 2015. Mbona tunasahau mambo mapema hivi jamani wakati sote tunajua nini kilitokea 2010?? nini kitazuia history kujirudia tena?
 
Siasa zetu zipo njia panda vibao vya kuelezea wapi pa kwenda vimeibiwa, basi limejaa abiria raia wakitanzania na dereva wa sasa ajielewi wala hajui njia ya mafanikio hipo upande gani. Yeye mwenyewe nafasi kaikwaa kutokana na umaarufu wake dhidi ya madereva wenzake aina maaana alikuwa ndio dereva bora, isipokuwa alikuwa the most likable character.

Options of the next candidates are based on trying of the unknown, therefore who is qualified the most on this trial-bases? no one knows. And only god knows of this tryst if s/he has enough experience.

Well according to Plato, in a ship turmoil sailors tend to look for the popular character to guide the course instead of the experienced one ( read Plato's philosophy The Republic Study Guide : Summary and Analysis of Book VI | GradeSaver). But then how do you know of the experienced one if s/he doesn't advertise himself and his knowledge. CCM ndipo hipo hapo amna cha 'Membe' wala nani as the best available presidential candidate, so far hawaongelei matatizo ya taifa bali yao binafisi na ya kichama tu. Ni sawa kwa kweli kwa sisi kuwanadi watu hawa, halafu ndio tusubiri waongelee matatizo yetu?

On the other hand tusisahau the philosophy of the golden mountain yaani ahadi mbadala za walio nje ya CCM maana hawaelezei watafikia vipi hapo lakini mara nyingi hutukumbushia hizi ahadi za mlima wa dhahabu je ni kutumia ignorance yetu au wanao uwezo huo wa kutupatia huo mlima kupitia sera mbadala. Or may be they are just exploiting our ignorance for their gain. Hivi kweli wanae huyo mtu wa kutuletea huo mlima kwa mbinu sahihi na zaidi ya kutumia uozo wa sasa ndio njia ya kuupata huo mlima. (read hume on this SparkNotes: An Enquiry Concerning Human Understanding: Sections II and III)

Siasa zetu bado sana, mtaji ni elimu dhaifu ya asilimia kubwa ya watanzania blame it on JKN trust me.
 
Ukiangalia sana kati ya viongozi wengi wa CCM na walioko serrikalini Membe ndiye anayeonekana kuja kuweza kumudu kuwa mgombea wa kiti cha Urais kupitia chama hicho. Ukimlinganisha na wagombea wengine (hasa Lowassa aliyejiuzulu kwa kashfa) ni Membe tu ambaye anaonekana kulindwa na mlolongo mkubwa wa kashfa mbalimbali na japo - kama nilivyosema wiki kadhaa nyuma - hajajiandaa kuwa Rais ni wazi miaka hii miwili iliyobakia inaweza kumsaidia kujitengenezea na kuwa a true "presidential candidate"

CCM ikimsimamisha Membe kama mgombea wake inaweza kuwa na nafasi ya kushinda tena kiti cha Urais; wakimsimamisha mtu mwingine yeyote itakuwa ni mwisho wa utawala wa CCM.

Ni kweli?
Enzi za uchaguzi ule wa picha ya mgombea mmoja upande mmoja na sehemu nyingine kuwekwa kivuli, hapo angeweza kuuchukua ki-urahisi kabisa. lakini katika siasa za sasa hivi zilizojaa uana harakati nafikiri amepoa sana hana mvuto hata wa kushawishi. Labda kura za kupikwa tu.
 
Siasa zetu bado sana, mtaji ni elimu dhaifu ya asilimia kubwa ya watanzania blame it on JKN trust me.
Why blame in on one only?, kwa nini waliofuatia AHM, BWM na JMK nao wasipate sehemu yao ya blame?!. Usitumie kisingizio cha msingi dhaifu, hivyo nyumba dhaifu!, kama JKN aliacha msingi dhaifu, hao waliompokea kwa nini waliendelea kujenga kwenye ule ule msingi dhaifu na kuachwa hivi hivi, wakati walipaswa kwanza kubomoa huo msingi dhaifu ndipo wajenge msingi mpya imara ili nyumba yetu isimame imara?!.
P.
 
Mimi nadhani tunapoteza tu muda wetu mwingi sana kujadili majina ya wagombea wa CCM wakati ni dhahiri kwamba hata asimamishwe nani kwa tiketi ya CCM, chini ya kanuni ya sasa ya Mshindi ni Mshindi, atakayeshinda Uchaguzi Mkuu ngazi ya Urais 2015 ni CCM, kwa mfano hata mgombea wa CCM akipata 50.01% dhidi ya mgombea wa Chadema 49.99%, mshindi atakuwa ni CCM, labda kama katika kipindi kilichobakia Chadema watafanya juhudi za ziada katiba mpya ibadili Uchwara huu;

Vinginevyo ushindi wa Chadema utakuwepo zaidi majimboni. Ni muhimu tu katika kipindi hiki (hasa iwapo kanuni ya mshindi ni mshindi itabakia intact):


  • Chadema wakaanza kujiandaa kisaikolojia juu ya uwezekano wa kualikwa kuunda serikali ya Umoja kutokana na Chadema kushinda viti vingi sana vya Ubunge, huku ikijua wazi kwamba itakuwa ni kula matapishi yake kwani ndoa ya Vyama Chadema imeikataa kama vile ni ndoa ya Jinsi Moja;


  • Huku nao CCM waanze kujiandaa pia kisaikolojia kuwa na Rais ambae atapita uchaguzi mkuu kwa just above 50%, kwa mara ya kwanza katika historia ya chama hiki;

Ni muhimu pia Chadema isijidanganye na matokeo ya uchaguzi Zanzibar 1995, 2000, 2005, 2010 ambapo CUF inasemekena ilishinda mara zote; Hii ni kwa sababu kama ilivyokuwa kwa uwepo wa mabaki ya TANU bara, yapo mabaki ya ASP Zanzibar, na CCM ni ndoa tu ambayo Suala la yupi ni mke na yupi ni mume baina ya TANU na ASP, is very much open to debate;
Mchambuzi ndiyo maana tumekuwa tunakemea mambo ya kufanya siasa ''unilaterally'.

Watu hawajifunzi kutokana na makosa. Mwaka 1995 NCCR mageuzi ilikuwa moto sana ikisheheni wanachama, personalities n.k. Mikutano ikijaa mashariki hadi magharibi, kaskazini hadi kusini. Postmorterm ya uchaguzi ilionyesha kuwa wakati NCCR wakijipanga katika nafasi za uwaziri n.k. CCM ilikuwa bize huko vijijini na ndiko walikopata ushindi.

Chadema hawaonekani kujifunza kutokana na hayo. Tulidhani operesheni Sangara na M4C vingebadilisha mtazamo wa kisiasa, badala yake tunaona mbio za kugombea na kuendelea kuugawa umma.

Kwa sasa chama kama CUF wanajua wazi kuwa hawana uwezo na wamepoteza imani ya kupewa dola.
Wanachokifanya ni kutaka kubaki na kitu ili waendelee kuwemo ndani ya ndoa.
Kwa kufanya hivyo watagawa kura za Chadema siyo CCM.
Mgawanyiko wowote ndani ya CDM utakiumiza chama sana kwasababu 'maadui; sasa ni zaidi ya mmoja.

Mchambuzi, watu hawakumbuki kuwa baada ya 1995 CCM walipeleka haraka mswada wa 'winner takes all'' na ndiyo bakora iliyowamaliza CUF hadi kuuingia katika ndoa ya mkeka.
Mara zote CCM ilikuwa ina mahesabu ya 50.001% na kuibuka kidedea. Bakora hiyo sijui kama itawanusuru CDM.

Mchakato walioukabali CDM unaendelea, na wao wamekaa pembeni bila kutoa maoni. Wamekaa pembeni wakati CCM ikifanya vitu vyao. Hili jambo unalozungumzia siyo popular miongoni mwa wengi, muhimu ni ukweli usemwe bila kuvikana vilemba vya ukoka.
Tume ya uchaguzi nayo ni mtego mwingine usioonekana.

Kinachoshangaza katika siasa zetu ni hili jambo la kutaja majina bila kuwa supporting data, evidence etc.
Makosa hayo yamefanyika miaka 7 iliyopita.
Wakati wenzetu jirani wakikimbia sisi tumebaki kusikia hadithi hakuna lolote la maana, nchi imekwama!
Bado tumejikita katika kutafuta viongozi kwa kuangalia majina tena hata yale machafu yanayomlazimu shetani kuona aibu yakitajwa

Tumekuwa sensitive kwa majina zaidi ya mkakati,thread hii wala haikulenga majina ukiisoma kwa makini ina mantiki zaidi iliyokusudiwa na pale chini kuna neno ''ni kweli''?
neno ni kweli limeachwa katika mjadala sasa ni majina na wala si mikakati ya kupata kiongozi bora.
Elimu ya umma inahitajika sana!
 
Siasa zetu bado sana, mtaji ni elimu dhaifu ya asilimia kubwa ya watanzania blame it on JKN trust me.
My answer to your question and quote is entirely based on this this sentence of my post. Kwa maana hiyo nitajibu kuzingatia kipengele hicho tu or else correct me.
Why blame in on one only?, kwa nini waliofuatia AHM, BWM na JMK nao wasipate sehemu yao ya blame?!. Usitumie kisingizio cha msingi dhaifu, hivyo nyumba dhaifu!, kama JKN aliacha msingi dhaifu, hao waliompokea kwa nini waliendelea kujenga kwenye ule ule msingi dhaifu na kuachwa hivi hivi, wakati walipaswa kwanza kubomoa huo msingi dhaifu ndipo wajenge msingi mpya imara ili nyumba yetu isimame imara?!.
P.

Issue hapa is not who followed JKN, issue hapa who initiated the exploitation of the ignorance masses. Embu umeshawahi kujiuliza kwanini leo hii watanzania hawachagui watu ambao wenye huwezo wa kuwaletea maendeleo au hata kama walimjua huyo mtu wa kuwaletea maendeleo anafananaje,?

Huwezi kutetea uozo huo la sivyo CDM leo wasingekuwa wana angaika kwenda vijijini kuwa julisha hawa watu haki zao na ni nini hasa athari za kuwachagua viongozi wabovu.

Sasa embu jiulize tumepata uhuru lini na kwanini hawa watu hawajui nini hasa maana ya haki zao. Nyerere hakuwapa raia elimu ya uraia kwa sababu ya kutaka kulazimisha policies zake ambazo hazikuwa na economic justification bali ni utopia yake yeye tu.

Him being a great philosopher pawned a majority of Tanzanians for his economical ambitions, by that he had to deprive them of their understanding of democracy and the right to choose on what they thought would benefit them independently.

Waliofuata wametumia ulemavu aliouwacha to advance their courses for their selfish purposes. Na sasa we have to pay the price, by motivating the young ones for the large part to see uozo wa CCM for what it is.
 
Waliofuata wametumia ulemavu aliouwacha to advance their courses for their selfish purposes. Na sasa we have to pay the price, by motivating the young ones for the large part to see uozo wa CCM for what it is.
Wakati anaaga, alisema wazi, "kutenda kosa, sii kosa, kosa kurudia kosa!".

Yeye katawala kwa miaka 23, by 2015 tutatimiza miaka 30!, hivi kweli, is fair mtoto anazaliwa mpaka anatimiza miaka 30, amekosa haki zake za msingi toka kwa baba yake na mama yake ambao wako hai, na kuja kutupia lawama kwa babu yake aliyemwachia baba yake kila kitu miaka 30 iliyopita?!.
 
Wakati anaaga, alisema wazi, "kutenda kosa, sii kosa, kosa kurudia kosa!".

Yeye katawala kwa miaka 23, by 2015 tutatimiza miaka 30!, hivi kweli, is fair mtoto anazaliwa mpaka anatimiza miaka 30, amekosa haki zake za msingi toka kwa baba yake na mama yake ambao wako hai, na kuja kutupia lawama kwa babu yake aliyemwachia baba yake kila kitu miaka 30 iliyopita?!.
Ndio maana wenzake wazalendo wa vyama vyote wanajaribu kurekebisha makosa yake, kwani makosa aliyoyafanya hayakuwa madogo wachilia mbali kutowapa elimu ya haki zao za msingi watanzania.

Kumbuka ni wanagapi waliokuwa wana elimu ya hadhi yake wakati Tanganyika inapata uhuru, kuwa mkweli na wangapi leo wana elimu ya hadhi yake. Point hapa ni kwamba viongozi wengi leo wenye madaraka wamepata elimu yao chini ya mwalimu, chini ya chama kimoja na wakijengwa kutetea sera za chama kimoja. Walichojifunza hawa watu ni kutumia miguvu ya kujilinda chini ya mwalimu wao 'JKN' lakini si uzalendo wa taifa lao ambao aliufikiria yeye.

Since walikuwa chini ya uongozi wake it says he did not just fail the social but his future leaders, unaona ndipo hapo kazi yetu ya kurekebisha makosa yake ambayo ni mengi, dont let me go into his economical policies, the guy failed us miserably.

usiku mwema
 
Elimu ya umma inahitajika sana!
Mkuu Nguruvi3, hapa ndipo mimi ninalia napo!. Hizi nondo mnazozimwaga humu ni darasa tosha, niko kwenye mchakato wa kurudi rasmi hewani na program ya elimu kwa umma kwa njia ya "vox pop" ili baadhi ya hoja zinazomwagwa humu, ziwafikie watu wa mbali zaidi, hata wale wasio na access ya mitandao au magazeti.

Kiukweli kama tunataka ukombozi wa kweli, nyinyi wenye ufahamu kama wewe, Mchambuzi, Mzee Mwanakijiji etc, zaidi ya kujitolea kumwaga elimu hii humu jf bure, nashauri mjitolee kuvisaidia hivi vyama not only to to the right things, but to do do the right things the right way at the right time!.

Moja ya matatizo makubwa kabisa ya vyama vyetu hivi vidogo vidogo, ni lack of communication strategy for reaching out the masses!. Gharama ya gari moja tuu 4x4 kama zile za M4C, inatosha kabisa kununulia vifaa vyote vya broadcast station, badala ya kutegemea tuu mikutano ya hadhara. Chama kubwa kina gazeti, redio and you never know by 2015 kitakuwa na TV yake!. Tuwasaidie hawa wadogo ku set priorities, zile umati kubwa za watu kwenye mikutano sio kura zile, we need to educate ili kuwahamasisha watu kujiandikisha, na wakisha jiandikisha kuhakikisha wanajitokeza kupiga kura!. 2012 inakatika, bado zijaona juhudi za makusudi za mass communications kwenye baadhi ya vyama!.
P.
 
Ndio maana wenzake wazalendo wa vyama vyote wanajaribu kurekebisha makosa yake, kwani makosa aliyoyafanya hayakuwa madogo wachilia mbali kutowapa elimu ya haki zao za msingi watanzania.

Kumbuka ni wanagapi waliokuwa wana elimu ya hadhi yake wakati Tanganyika inapata uhuru, kuwa mkweli na wangapi leo wana elimu ya hadhi yake. Point hapa ni kwamba viongozi wengi leo wenye madaraka wamepata elimu yao chini ya mwalimu, chini ya chama kimoja na wakijengwa kutetea sera za chama kimoja. Walichojifunza hawa watu ni kutumia miguvu ya kujilinda chini ya mwalimu wao 'JKN' lakini si uzalendo wa taifa lao ambao aliufikiria yeye.

Since walikuwa chini ya uongozi wake it says he did not just fail the social but his future leaders, unaona ndipo hapo kazi yetu ya kurekebisha makosa yake ambayo ni mengi, dont let me go into his economical policies, the guy failed us miserably. usiku mwema
Kama baba yako yupo, naye hakusomesha wewe eti kwa vile na yeye hakusomeshwa na baba yake ambaye ndie babu yako!, kumlaumu babu yako marehemu, kwa makosa ya kutomsomesha baba yako, na kujustify ndio sababu ya wewe kutosemeshwa, doesn't help!. Wewe mtoto unatakiwa ubanane na baba yako!, leave your late grand alone!. Umenikumbusha story ya Kalumekenge aliyekataa kwenda shule!.

NB. Kuwalaumu the dead ambao wamefanya makubwa kwa taifa hili genuinely, sio kuwatendea haki!. We live in the present!, let the past be the past!. Kuhusu JKN, mimi huwezi kuniambia chochote nikakuelewa, bora ujilalie zako!.

Angalizo tuu: Tuko kwenye mchakato wa kumtangaza JKN "Mwenye Heri", hivyo nguvu ya ki Mungu iko juu yake!, jiulize ni nini kilimfika FaizaFoxy kwa kumbeza huyu Mzee au yule Mzee Mohammed Said!, kwa vile hukijui, na mimi naomba nisikuambie chochote only nakushauri "respect the dead fallen heroes"!. Yakikukuta ya kukuta, usije kujilaumu kuwa hukuambiwa!. "Let the dead heroes rest in peace"!.

P.
 
Back
Top Bottom